ubarinolutu
JF-Expert Member
- Oct 22, 2012
- 1,974
- 3,909
Kwanza kabisa lazima tukubaliane kimsingi kuwa panya road ni school drop out hasa shule ya msingi na secondary, lakini wengi pia ni wale waliolelewa Kwa style ya single mothers hii nimeongea sio kukejeli lakini ni kutokana na mahojiano waliyofanya wenzao kituo Cha polisi.
Jana Tarehe 11.02.23 siku ambayo Simba ilifungwa huko Ugenini, Panya road walifanya matukio ya uvamizi na uporaji katika maeneo ya Bunju B.
Mimi najiuliza kwanini Hawa vijana wamekuwa wakatili kiasi hiki, yaani wakifanya uvamizi lazima wakuchororonge mapanga hata kama utakuwa mtiifu na kuwapa wanachotaka tofauti na majizi mengine.
Wao wakikufikia wanaanza na panga Halafu ndo wanadai Hela , simu, etc, pia wakishindwa kuchukua kitu wanakiharibu either Kwa kukipiga nyundo au kukikatakata.
Pia katika video hii hapa chini utaona Bado kuna Watanzania wachache wanakaa na hela ndani , mfano mmoja kuna mtu kakutwa na laki sita ndani, sijui ilikuwa ya matumizi ya kawaida sijui.
Pia najiuliza Hawa vijana walitumia mbinu gani kuweza kujikusanya wengi vile na kuunda timu yaani genge la wahalifu, hiyo sio kazi ndogo, huyo Kiongozi wao ana upeo fulani wa kipekee. Tunaita team building skills
Jana Tarehe 11.02.23 siku ambayo Simba ilifungwa huko Ugenini, Panya road walifanya matukio ya uvamizi na uporaji katika maeneo ya Bunju B.
Mimi najiuliza kwanini Hawa vijana wamekuwa wakatili kiasi hiki, yaani wakifanya uvamizi lazima wakuchororonge mapanga hata kama utakuwa mtiifu na kuwapa wanachotaka tofauti na majizi mengine.
Wao wakikufikia wanaanza na panga Halafu ndo wanadai Hela , simu, etc, pia wakishindwa kuchukua kitu wanakiharibu either Kwa kukipiga nyundo au kukikatakata.
Pia katika video hii hapa chini utaona Bado kuna Watanzania wachache wanakaa na hela ndani , mfano mmoja kuna mtu kakutwa na laki sita ndani, sijui ilikuwa ya matumizi ya kawaida sijui.
Pia najiuliza Hawa vijana walitumia mbinu gani kuweza kujikusanya wengi vile na kuunda timu yaani genge la wahalifu, hiyo sio kazi ndogo, huyo Kiongozi wao ana upeo fulani wa kipekee. Tunaita team building skills