Kuzuia mikutano ya Chadema ni njia moja wapo ya kukifanya chama hicho kipendwe zaidi na wananchi wa Mbeya vijijini kwasababu, kitendo cha kuwazuia kitawapa shauku ya kutaka kujua kitugani ambacho CCm na serikali yake vinaogopa wananchi wasiambiwe na Chadema; wanarudia makosa yale yale ya Makamba kutaka kutumia uCCM wake kuzima mjadala wa EPA!! Mbinu za kuzuia mikutano ya Chadema zilishindwa Tarime na Mbeya pia zitashindwa hasa ukijua kuwa wanaMbeya wanausongo na serikali hii; sasa karibu mwezi mzima hawana umeme!!