Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,106
Lipo tatizo ambalo linapaswa kufanyiwa utafiti. Tunaweza tukadhani tunaua vijana kisiasa kumbe tunafifisha viongozi wa kesho wa Tanzania.
Nikimwangalia Nassari akiwa Chadema na leo ndani ya CCM kuna utofauti mkubwa sana. Alipopewa na CCM hadi wakamnunua ila ameshindwa kabisa kukubaliana na hali iliyopo ndani ya chama tawala.
Nassari ameshindwa kuonyesha uwezo kama mkuu wa wilaya pote akiwa Mara na hata leo Monduli. Amekaa kimya sana, wananchi wamemkataa, amekosa mfariji kwa sababu ndani ya CCM hapewi platform ya kuonyesha utendaji na mtaani amepoteza marafiki wote aliokuwa nao.
Naamini amebaki na familia yake pekee; ndani ya CCM anaonekana kama mtu aliyekuja kuchukua nafasi zao za utawala. Mhe. Rais amejitahidi kumpa nafasi leo huko Arusha ameishia kusali hana mvuto tena.
Naamini bado anazo akili ila atazitumia wapi? Umri unakwenda kama ambavyo umri wa vijana wengi unakwenda; vipaji walivyopewa na Mungu wanashindwa kuvitumia kwa sababu wametekwa na watawala.
Tunahitaji brain za Nassari wa Chadema ili tuendelee kuliko tunavyohitaji brain za Nassari DC
Vijana amkeni mtapoteza nguvu nyingi kutumikia siasa kuliko kujitumikia. Bora kuishi maskini mwenye furaha kuliko tajiri wa mashaka.
Nikimwangalia Nassari akiwa Chadema na leo ndani ya CCM kuna utofauti mkubwa sana. Alipopewa na CCM hadi wakamnunua ila ameshindwa kabisa kukubaliana na hali iliyopo ndani ya chama tawala.
Nassari ameshindwa kuonyesha uwezo kama mkuu wa wilaya pote akiwa Mara na hata leo Monduli. Amekaa kimya sana, wananchi wamemkataa, amekosa mfariji kwa sababu ndani ya CCM hapewi platform ya kuonyesha utendaji na mtaani amepoteza marafiki wote aliokuwa nao.
Naamini amebaki na familia yake pekee; ndani ya CCM anaonekana kama mtu aliyekuja kuchukua nafasi zao za utawala. Mhe. Rais amejitahidi kumpa nafasi leo huko Arusha ameishia kusali hana mvuto tena.
Naamini bado anazo akili ila atazitumia wapi? Umri unakwenda kama ambavyo umri wa vijana wengi unakwenda; vipaji walivyopewa na Mungu wanashindwa kuvitumia kwa sababu wametekwa na watawala.
Tunahitaji brain za Nassari wa Chadema ili tuendelee kuliko tunavyohitaji brain za Nassari DC
Vijana amkeni mtapoteza nguvu nyingi kutumikia siasa kuliko kujitumikia. Bora kuishi maskini mwenye furaha kuliko tajiri wa mashaka.