Nzega: Risasi zatumika kumuokoa Mbunge Kigwangalla

umeambiwa kapigwa kwa kuwatetea wachimbaji wadogo wewe unasema alikuwa anatetea wawekezaji? au hujui kusoma. Nenda gumbaru kajifunze a e i o u kwamnza.
 
huyu kingwangala ndo maana aliiba vyeti vya mwenzake kusomea maana hana akili hata kidogo...
 
Sidhani!...HATUJAFIKIA HUKO!
Kuna jambo hapa linafichwa!
Kuna thread ilianzishwa ilikuwa ikielezea yaliyojiri jana Nzega lakini huyo mbunge alipondwa sana kuwa ni ndumilakuwili na ndiyo maana alipibondwa! Halafu hebu cheki hii
Junior Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png



Join Date : 20th October 2011
Posts : 7
Rep Power : 0
Ametumwa kuja kumsafisha Kingwalala sijui jukwaani.
 
Ningesoma post yako ila ulivyoweka huyo mtoto kuwa uko naye nimeacha.
 
wana jf nipo nzega nikitoka mwanza katika ziara ya ndg ridhwani kikwete.

Usikuu huu nikiwa napata chakula nikasikia risasi zinalia mjini nikaamua kufatilia na kupata taarifa kuwa kuna mgodi ambao unaitwa isunga ngwanda ambao siku mbili zilizopita mbunge na wananchi waliungana kuufunga.

Leo kilicholeta vurugu ni pale mbunge wa nzega alipoenda kuwafata wananchi alioshirikiana nao kuufunga mgodi na kuwataka kuufungua mgodi na yeye akijiunga na polisi kuwataka wananchi wale waondoke wamuachie muwekazaji.

Wananchi walipandwa na hasira na kumvamia mbunge na kuanza kumpiga na kuvunja gari ya daktari wa wilaya ambayo aliazima naambiwa akiwa nzega huazima gari ya daktari wa wilaya na kuitumia.

Wananchi hao wenye hasira waliamua kumpiga mbunge kwa kitendo chake cha kuwasaliti wananchi hao na leo kuungana na polisi na wawekezaji.polisi ilibidi kutumia silaha za moto kumuokoa na na kuwakamata baadhi ya watu na kuwepeleka polisi jambo lilifanya wananchi kuandamana kwenda kuvamia kituo cha polisi na matokeo yake polisi kutumia risasi kuwatawanya wananchi wao.

Liliwaudhi wananchi nitukio la mbunge kigwangala kuwageuka wananchi na kujiunga na wawekezaji na polisi hivi sasa kunavurugu nzega mjini na maeneo ya isunga ktk mgodi huo.
riz mwekezaji
 
mkuu jana ulisema wewe ni mwalimu huko mwanza,umeamua kutembea na huyo rizone?mwenzio mtoto wa mjini huyo
Director huyo asikudanganye sisi tunamjua,LIJIDAI ETI ATAWATETEA WATU WA HAPO ISUNGANGWANDA kwenye kampeini fulani!!!!!!!!! Lakini hakufanya hivyo, hiyo ya Isungangwanda ni msg tosha kwa maghamba!!!!!!!! Wakiendelea kunyanayasa wananchi kama walivyofanya Dodoma watu watachukia na itakuwa ndio basi tena!!!!!!!
 
Kwa kuwa alisimama wazi wazi ndani ya Bunge kukemea wawekezaji kwa uwaazi pasipo woga wa Kiccm katika Bunge lla Tanzania basi logic ni kuwa thread hii inaasilimia sabini 70% za ukweli,kinachonikela ni watu jamvini kwa kuwa wengi uleta taarifa muhimu za matukio bila picha.Ni vyema kuwa na picha tupu pasipo ujumbe kuliko kuwa na ujmbe usio na picha.Tujifunze kwa wenzetu picha inasimamia ukweli haraka sana kuliko ujumbe pekee ambao unatupa shaka bali inasimama logic kuamua jibu.
 
Kingwangalla ni kigeugeu mwanzo mwisho. Kwa muda amekuwa anawasema CHADEMA kuwa wanataka nchi isitaliwake, kisa? kwa sababu wanafanya maandamano. Sasa week kala matapishi yake na kuandamana na wananchi kufunga mgodi. True to himself, siku mbili baadae anajitokeza na msimamo tofauti na aliokuwa nao wakati akifunga huo mgodi na wananchi!

Rewinding the tape, ni huyu huyu Kingwangalla aliyejiapiza huko nyuma kuwa angewahamasisha wananchi ili wafunge mgodi wa Resolute, lakini Kingwangalla being Kingwangalla akavamia ka-mgodi kadogo kabisa na sio Resolute. Kama kuna machafuko huko Nzega Kingwangalla atakuwa right in the middle of it kwa sababu ya kung'ata na kupiliza. Leo anasema hiki kesha anafanya the opposite. Kiongozi gani asiyesimamia anachosema?

Huyu bwana angeendeleza ujuzi wake wa kujitingaza jinsi alivyo 'msomi', lakini kwa muda huu mfupi amabapo amekuwa kwenye public eye anaonekana kuwa very immature in his thinking.

Nimekuwa nikisema hapa mara zote kwamba Kigwangala hana msimamo wala nia ya dhati ya kuwatetea wananchi wake. Kigwangala ametanguliza mbele ubinafsi na kutafuta sifa za kijinga na bahati mbaya sana jamaa ni kigeugeu. Nimekuwa nikimwambia hivyo mara zote hapa JF na hata habari ya kuufunga huo mgodi ilipokuja hapa kuna watu wakawa wanasema anastahili pongezi kwa kuwa jasiri na kuufunga huo mgodi mimi nilipingana nao moja kwa moja.

Ukweli unabaki pale pale kwamba Kigwangala anatafuta namna ya kujikubalisha kwa wananchi lakini hana ubavu wa kutunisha msuli ndani ya chama chake ambacho ndicho kinawakumbatia wawekezaji. Labda akitoka ccm naweza kufikiria kuamini kwamba anaweza kufanya kitu kwa ajili ya maslahi ya umma, lakini kuendelea kuwa ndani ya ccm hawezi kamwe kuwa na ujasiri wala uthubutu wa kusimamia maslahi ya umma.

Bila aibu mwakilishi wa wananchi anashirikiana nao kufunga mgodi laiki ndani ya siku mbili anawageuka wananchi wake na kuwataka waondoke na kumpisha mwekezaji. Sasa hapo ataaminikaje? ujasiri utaonekana wapi? jamaa ni msaliti, msaliti, msaliti!!
 
Wana Jf nipo nzega nikitoka Mwanza katika ziara ya Ndg ridhwani kikwete.

Usikuu huu nikiwa napata chakula nikasikia Risasi zinalia Mjini nikaamua kufatilia na kupata taarifa kuwa Kuna Mgodi ambao unaitwa Isunga Ngwanda ambao siku Mbili zilizopita Mbunge na Wananchi waliungana Kuufunga.

Leo Kilicholeta Vurugu ni Pale Mbunge wa Nzega alipoenda kuwafata wananchi alioshirikiana nao kuufunga Mgodi na kuwataka kuufungua mgodi na yeye akijiunga na Polisi.

Jamani jaribuni kujikumbusha wabunge wote ambao walijidai kupigania wananchi kwa kupambana na wenye migodi, wote sasa hivi wana Ma Vogue, Hummer na Ma crusher, msimshangae Kigwangala, anatafuta Hummer! Ndio wana siasa tulionao hao!
 
Hii habari haijakaa sawa, lazima kuna spinning ya kitoto hapa. Hao wawekezeji wako wangapi? Kuna uwekezekano Kingwangalla 'alikopa' watu toka eneo tofauti waje wapambane na wenjeji hapo ili ionekane wawekezaji wanapambana na mbunge?

Ni usanii ule ule kuanzia juu mpaka chini lao moja! usanii usanii every where!
 
Halafu hata hivyo ina maana kutokana na habari yenyewe wawekezaji nao walikuwa wanarusha mawe? Na kwa muonekano wa story yenyewe Kigwangwallah akawa kama mtu kati. Halafu hata hiyo gari inayotajwa mbona tofauti na iliyoelezewa awali? Mwanzoni ilionekana kama Range Rover lakini hapo inaongelewa gari ndogo Toyota Caldina.

Mwandishi wa habari hii Mustapha Kapalata sijajua anaandikia gazeti gani lakini nimewahi kumsikia mara kadhaa akiripotia RFA.
Ukiisoma hiyo habari unaiona jinsi ilivyofanbyiwa spinning, tena za kitoto kabisa.

Hao wawekezaji walikuwa wengi kiasi gani hadi waamue kupambana na wananchi? Hapa inaonekana Kigwangala alitaka kuwachuuza wananchi baada ya juzi kuungana nao kuufunga huo mgodi. Sasa atakuwa alirudi na wawekezaji hao baada ya yeye kuwekwa sawa akadhani itakuwa kazi nyepesi kuwarubuni wananchi waachie mgodi, ndio kastukia anapigwa mawe. Kwanini wananchi wasiponde mawe gari ya wawekezaji badala yake waiponde gari ya mbunge?? Kama wananchi hao walishirikiana na mbunge wao kuufunga huo mgodi, si jambo rahisi kiasi hicho kwa wananchi hao hao kushindwa kumlinda mbunge wao apigwe na wawekezaji, akili ya kawaida inakataa kabisa.
 
HTML:
Ndugu zangu wanaJF,
 
Tusiichezee nguvu ya wananchi hata siku moja, kwa usalama wa Taifa letu.  Toka juzi nimekuwa nikifanya jitihada mbalimbali za kutuliza munkari ya  wananchi wa kijiji cha Mwabangu. Watu wakichoka ni hatari sana.
 
Mimi sijawaangukia Resolute na wala siwezi kuwaangukia hata siku moja.  Wananzega wanachotaka ni maendeleo na haki yao ya kulipwa fidia kwa mali  yao iliyohodhiwa na ama kuvunjwa miaka 15 iliyopita, wananzega hawataki  mbunge mwehu anayeambiwa sasa tutawajengeeni shule kadhaa, maabara  kadhaa, tutawawekeeni lami, tutawalipeni fidia zenu n.k na mbunge huyo  akakataa akang'ang'ania maandamano tu! Tulichokifanya sisi ni kukubali  kwenda mezani na kuanza mazungumzo na mpaka sasa tupo katika hatua  mbalimbali, tukishindana tutaingia Barabarani mpaka mgodini. Nyie  subirini tu na mtaona!

kwa hiyo unatuambia baada ya kuandamana na kufunga mgodi ndo wawekezaji wakaamua kuwadanganya na ahadi feki? Sasa vurugu zimeanzia wapi mkuu? KIGEUGEU ,ANAWAGEUKIA
 
Na bado, ni vizuri wangemwachia alama yoyote mwilini kwake kama kumbu kumbu ambayo ingemsaidia kukumbuka jinsi serikali yake ilivyokaribisha mabepari wanaonyanyasa wananchi.
 
HTML:
Ndugu zangu wanaJF,
 
Tusiichezee nguvu ya wananchi hata siku moja, kwa usalama wa Taifa letu.  Toka juzi nimekuwa nikifanya jitihada mbalimbali za kutuliza munkari ya  wananchi wa kijiji cha Mwabangu. Watu wakichoka ni hatari sana.
 
Mimi sijawaangukia Resolute na wala siwezi kuwaangukia hata siku moja.  Wananzega wanachotaka ni maendeleo na haki yao ya kulipwa fidia kwa mali  yao iliyohodhiwa na ama kuvunjwa miaka 15 iliyopita, wananzega hawataki  mbunge mwehu anayeambiwa sasa tutawajengeeni shule kadhaa, maabara  kadhaa, tutawawekeeni lami, tutawalipeni fidia zenu n.k na mbunge huyo  akakataa akang'ang'ania maandamano tu! Tulichokifanya sisi ni kukubali  kwenda mezani na kuanza mazungumzo na mpaka sasa tupo katika hatua  mbalimbali, tukishindana tutaingia Barabarani mpaka mgodini. Nyie  subirini tu na mtaona!

kwa hiyo unatuambia baada ya kuandamana na kufunga mgodi ndo wawekezaji wakaamua kuwadanganya na ahadi feki? Sasa vurugu zimeanzia wapi mkuu? KIGEUGEU ,ANAWAGEUKIA
 
keli hata mi niko nzega niliskia risasi wakati napata mlo hapa ndasa. Nilijua wazee wa kazi wemevamia mahali....hapa hapa ndasa wakati ffu wamepaki risasi ilifyatukia hewani kidogo tutoke nduki.....ova
Mbona unachanganya habari Mkuu, Ndasa ipo Kahama, na iliypo Nzega ni Ngasa.
 
Aisee, huyu mbunge kama sikosei alikuwa ametupwa nje wakati wa kura lakini akabahatisha kuukwaa ubunge baada ya aliyekuwa anategemewa kuondolewa, kwa ufupi hao ni watu wasio na uwezo kutetea wananchi, inajidhihisha wazi kwa maamuzi ndumilakuwili wanayotoa kila wakati!!!!
 
Back
Top Bottom