Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Invincible,
Mkuu karibu sana hapa kijiweni maanake wewe huonekana tu pale jua linapokuchwa!..

Maneno yako yangekuwa sawa kama sasa hivi sote tungekuwa bado shule ya msingi.
Point yangu kubwa ni kwamba Mwalimu alikuwa mwalimu mkuu wa shule ya msingi na mengi mabaya/mazuri tulikutana nayo wakati ule ,lakini leo hii tupo shule za secondary na wengine vyuo vikuu wanafanya vibaya basi lawama zinarudi kule walikoanzia masomo yao ya msingi na sii majumbani kwa wazazi wao ama hawa walimu tuliokuwa nao huku secondary na vyuoni.

Nachokataa mimi ni kwamba pamoja na kwamba hawa walimu wetu wa sasa hivi ni kizazi cha Mwalimu haina maana kwamba mwalimu is responsible!...
Mwalimu atalaumiwa kwa wakati wake tulipokula unga wa Yanga, uji wa Bulga na kunywa maziwa ya kutengenezwa na hata vita vya kuikomboa Afrika kama mtapenda kutumia sababu hizo.
Hivyo hivyo Mkoloni atalaumiwa hadi siku ile tulipopata Uhuru wetu baada ya hapo lawama ni zetu wenyewe kwani tulipodai Uhuru tulifahamu fika umasini alotuachia na kwa furaha kubwa tulichagua kuwa Huru na umaskini kuliko kunendelea kutawaliwa..
Mwisho, hivyo hivyo tulipoamua kubadilisha mfumo wa kiuchumi na kuwa Mafisadi sioni sababu ya kumlaumu mwalimu kwani lawama zake zinaishia pale alipoachia kamba..
Matukio ya kutoendelea leo ktk darasa hili la secondary yapo ndani ya darasa hili yaani kama sio walimu wetu hawa kina Mkapa, JK na viongozi wote wanaokutana huko Butiama basi tatizo lipo ktk mfumo wa masomo ama sisi wenyewe wanafunzi!... tumeshindwa kabisa kuelewa somo hili la Ufisadi..Ndivyo Tulivyo ni pale tunapoendelea kutafuta sababu za kushindwa kwetu darasani wakati wanaohudhulia masomoni kila siku ni sisi sio Nyerere.
 
Bin Maryam,
Warusi na wachina walianza kwa Quarters. Wakulima vijijini walikuwa wanapangiwa kiasi cha kuzalisha. Na serikali inakuja kuchukua kile ulichopangiwa.

Kama ulipangiwa kutoa magunia matano ya ngano na kwa baada mbaya ukazalisha magunia sita basi magunia matano yanachukuliwa kwanza na serikali na wewe unabakia na gunia lako moja mpaka msimu mwingine wa chakula. Tuache utani, je ungekubali babu yako kule ujita atoe magunia ya mihogo kwa serikali kwanza kabla ya yeye kupata chakula?
Vilevile wao hawakukataa kuwa mtaji ni msingi wa maendeleo. Hivyo wapingaji ujamaa kama mimi walikuwa wanapelekwa Siberia kuchimba dhahabu na Uranium na kuliingizia taifa mapato bila malipo.
Hivyo miaka ya mwanzo ya Ujamaa kwa nchi kama China, Urusi au Vietnam haikuwa ya mchezo wala ngoma ya mganda. Urusi pekee yake ilipoteza millioni 7 hivi katika operasheni ya kuhamisha watu na uzalishaji wa vijiji vya ujamaa.
Kwa siasa hizo hizo waChina walipoteza kati ya 20 na 30 million. Na kwa mtaji huu maendeleo uyaonayo ya wenzetu kuweza kuendeleza siasa zao, hayakuja bila kuwa na gharama za maisha ya watu zilizokithiri.

Mkuu yote uliyoyaandika hayana ubishi hata kidogo lakini haikutokea Tanzania. Hata nchi za magharibi mbali na kutokuwa na siasa mbaya za kikomunist wao pia walipeleka vijana wao vitani ktk kushika makoloni ambako mamillioni walikufa!..
Hizi zilikuwa ni siasa zao ambazo sisi tulikaa pembeni kwani nchi zetu zilikuwa nyasi ktk vita ya hawa mafahari. Kifupi wakati ule nisingependa kuwa nchi yeyote kati ya hizo za magharibi ama za Mashariki kwani lolote lingetokea na pengine nisingekuwepo hapa leo hii kaburi lingekuwa Siberia, Vietnam, Kambodia ama Japan.
Now, tunaporudi ktk swala la Mwalimu kuna mabaya alofanya lakini kwa nia njema! .. naweza sema ni abuse ya baba kumpiga mwanae kwa sababu hakwenda shule!. Hivi ni vitu ambavyo siwezi kuvikataa wakati wa mwalimu isipokuwa kueleza umuhimu wa kwenda shule na sio machungu zile bakora, wakati wengi wenu mnazungumzia zile bakora mkipuuza umuhimu wa kwenda shule ili kuonyesha mabaya ya mwalimu. Na wengine wamezibeba hizo bakora na kusema pengine NDIVYO TULIVYO ni matunda ya fimbo zile za mwalimu...Yet, tunashindwa kutoa mfano hata mmoja ambao unaonyesha mwalimu alitumia bakora ktk kueneza siasa zake isipokuwa pale tu tulipokataa kwenda shule.
Russia,Korea, Vietnam, Ethiopia na China walifanya mabaya yote yanayopingwa hapa lakini mbona wao sii Ndivyo Tulivyo?..sisi tumepotea wapi.
Hapa ndipo ngoma ilipolala!
 
Now this brings us to a wider question of LEADERSHIP which is the main VOID in Tanzania. now the next question would be WHERE DO WE GO FROM HERE? surely we cant go back to UJAMAA and NYERERISM But still, just because we find ourself where we are today(economically) due to his mis calculations does not mean those who are elected to power should not have a vision and common sense.

My main arguement for bringing this debate is because Tanzania seem unable to make the switch from a Commodity based economy to one that is focused on manufacturing base economy simply because "MWALIMU ASINGEKUBALI HILI" etc etc

Look at Malaysia for instance. It has several ethnic groups that were bundled together by the colonialist, yet their prime minister who was MWALIMU's friend Dr. Mahathir Mohammed had a vision. Look at where Malaysia is today. Due to Mahathir's vision, today Malaysia is a leader in the Semiconductor industry, with a large Chemical processing industry. Furthermore it is now becoming a leader in the electronics industry, automobile manufacturing, textiles, and raw material processing. All this happening despite corruption taking place. Now how comes that our leaders in Tanzania have not done what the Prime Minister of Malaysia has done?

Malaysia successfully developed from a commodity-based economy to one focused on manufacturing. Today the Government of Malaysia seeks to make the leap to a knowledge-based economy. At independence, Malaysia inherited an economy dominated by two commodities--rubber and tin. In the 40 years thereafter, Malaysia's economic record had been one of Asia's best

Ohh lets not forget now they got smarter and have managed to fool our so called leaders in signing contracts without reading small prints...I am talking about IPTL contract of course

Dr Who or What ever it seems you don't know what u r talking about, that is why you a shifting the goal post from udini etc kuja kwenye Economics.
Sasa kukujibu kufuatana na ulivyoandika hapo juu, utaona kwa upo wrong kwenye Industrialisation Tanzania, (that is to shy away from ,commodity based economy,to industrial one) ndio maana tukawa na UFI, FISHNETS, MWATEX, MBEYATEX, NYUMBU etc, na ndio maana alijenga uhusiano na nchi zinazo endelea kwa kujenga Viwanda kama China, Malasyia,India, Cuba, Yogoslavia, ili na sisi tufaidike.
So kwa hilo naomba umpongeze.
Ukija kuhusu kumfanya Nyere kama Demi-GOD that is not true, kwa mfano mimi namfagilia Nyerere lakini simuoni ka ni Demi-God, au sikatai mapungufu yake either due to human error or hali ilivyokuwa wakati huo.
Kuhusu kuandaa viongozi wa kesho na kesho kutwa nafikiri, watu wazuri wapo kwa sasa, sema wakati ule alio kuwa nao au walioweza kujipenyeza, ndio hao machui kwanye ngozi ya kondoo, na jingine ni weakness za Taasisi zetu katika ku-control nchi ikiwa tuna kiongozi mpuuzi au kichaa , that is Mahakama ingekuwa kama wenzetu wa Pakistani na Bunge kama la Kenya Vile.
Maana tumeona Viongozi wetu wakishindwa kutawala wanaegamia kwenye Dini zao kama vile ni vita kati ya dini moja kwenda nyingine, kumbe sivyo, na sasa tumekwenda a step further, kutumia makabila yetu kama watu wa Lowasa wanavyo ona kumbe ni matatizo yao binafsi, mbona Ole sendeka asimtete Lowasa au Silaaa nae si wa huko?
 
Yes Tanzania at this very moment can develop like this Countries of East Asia known as the Tiger Economies. The first thing South Korea did in the 1960s is increase the nuber of schools and Universities from seven (7) to about forty seven (47) check fugures and numbers. They also opened many vocational training centers to train a skilled workforce. The government then encouraged private businesses and entrepenuership and they sponsored and gave credits to those companies that are doing good. In addition the government targeted and sponsored specific industries that are technology based such as electronics, automobile, aircraft and heavy industries.



At this very moment Tanzania has the capability to be another Japan or Singapore. The key is to develop both our human resource together with the natural resources coupled with GOOD LEADERSHIP. Good leaders with a vision and common sense equals a succesfull country like Japan.


and this is whats been missing in TANZANIA

Lakini hivi vitu Nyerere si amevifanya, mapaka cha mwisho, kabla Nyerere chini ya uongozi wa Nyerere ni cha Mbeya amacho kuna watu walipendekeza kiwe chuo kikuu, apart from that we have Dar Tech, Arusha Tech na vyuo vingine ambavyo labda havina big reputation kama hivyo vipo mwanza, ntwara tanga
 
Mwakilishi, mukombosi:

Mkiingiza kila kitu na udini tutaendelea kutawaliwa na matahira katika nchi hile ya mababu.

Inavyoonekana sasa hili amani iwepo na viongozi waendelee kunyonya basi kila mkoa ni lazima upate nafasi ya uwaziri na baraza la mawaziri liwe na watu wa dini mbalimbali.

Rais na Waziri mkuu atoke kwenye makabila madogo yaliochoka. Na makamu wa rais atoke Pemba.

Nchi ni lazima ikubali kuwa vurugu zitatokea lakini vyombo vya serikali ni lazima viwepo kutuliza vurugu hizo. Na kama vurugu zina ukweli wake basi zifanyiwe kazi hili jamii iweze kwenda hatua moja ya kimaendeleo.
 
Kadiri watanzania wanavyomwona Nyerere kiongozi bora; ndivyo Tanzania itakavyozidi kupata uongozi mbovu.

Sasa mafisadi wa CCM watafanya kikao huko Butiama ili kuwazuga wadanganyika.

JKN alikuwa mtu mwema,mpenda haki, mwadilifu; lakini hakuwa kiongozi bora. Mimi namlinganisha zaidi JKN na mwalimu mkuu wa shule ya msingi ambaye si mkali wala kwa walimu wenzake wala watoto wa shule. Wanajifanyia watakalo. Ila shule hiyo haifaulishi watoto kwenda sekondari.

Umerudi katika wimbo aliotunga ukitaka maendeleo unahitaji:
  1. Watu
  2. Ardhi
  3. Uongozi Bora
  4. Na siasa safi

Kuwa mwadilifu, mpenda haki, mtu mwema au kuwa mwanafalsafa haimfanyi mtu kuwa na performance nzuri katika uongozi. Na hiki ndio kitu kinacholeta conflicts kwa vipenzi wa Nyerere.
 
Lakini hivi vitu Nyerere si amevifanya, mapaka cha mwisho, kabla Nyerere chini ya uongozi wa Nyerere ni cha Mbeya amacho kuna watu walipendekeza kiwe chuo kikuu, apart from that we have Dar Tech, Arusha Tech na vyuo vingine ambavyo labda havina big reputation kama hivyo vipo mwanza, ntwara tanga

August:

Mbeya ilijengwa na Warusi, Dar Tech Mwingereza na Arusha Tech. Mjerumani. Hupati maendeleo kwa kutumia migongo ya watu.
 
Bin Maryam,
Mkuu ningependa sana kufahamu makosa yangu hasa napomkubali Nyerere kama Kiongozi bora.
Umetoa huo wimbo wetu kuwa ili tuendelee tunahitaji Watu, Ardhi, Siasa safi na Uongozi bora..
Ni kitu gani hapo juu kinachopingana na itikadi za nchi za magharibi ama elimu ya Uchumi!..
Naomba somo mkuu maanake nachoona mimi hao WATU ndio kina NDIVYO TULIVYO!.
 
Bin Maryam,


Mkuu yote uliyoyaandika hayana ubishi hata kidogo lakini haikutokea Tanzania. Hata nchi za magharibi mbali na kutokuwa na siasa mbaya za kikomunist wao pia walipeleka vijana wao vitani ktk kushika makoloni ambako mamillioni walikufa!..
Hizi zilikuwa ni siasa zao ambazo sisi tulikaa pembeni kwani nchi zetu zilikuwa nyasi ktk vita ya hawa mafahari. Kifupi wakati ule nisingependa kuwa nchi yeyote kati ya hizo za magharibi ama za Mashariki kwani lolote lingetokea na pengine nisingekuwepo hapa leo hii kaburi lingekuwa Siberia, Vietnam, Kambodia ama Japan.
Now, tunaporudi ktk swala la Mwalimu kuna mabaya alofanya lakini kwa nia njema! .. naweza sema ni abuse ya baba kumpiga mwanae kwa sababu hakwenda shule!. Hivi ni vitu ambavyo siwezi kuvikataa wakati wa mwalimu isipokuwa kueleza umuhimu wa kwenda shule na sio machungu zile bakora, wakati wengi wenu mnazungumzia zile bakora mkipuuza umuhimu wa kwenda shule ili kuonyesha mabaya ya mwalimu. Na wengine wamezibeba hizo bakora na kusema pengine NDIVYO TULIVYO ni matunda ya fimbo zile za mwalimu...Yet, tunashindwa kutoa mfano hata mmoja ambao unaonyesha mwalimu alitumia bakora ktk kueneza siasa zake isipokuwa pale tu tulipokataa kwenda shule.
Russia,Korea, Vietnam, Ethiopia na China walifanya mabaya yote yanayopingwa hapa lakini mbona wao sii Ndivyo Tulivyo?..sisi tumepotea wapi.
Hapa ndipo ngoma ilipolala!

Mwalimu alikuwa hapigi bakora hili watu waende shule. Hangekuwa anapiga bakora basi performance yake ingekuwa nzuri sana.

Yeye ni mfano na Mwalimu ambaye akitaka mtoto aende shule basi atampa mtoto hotuba ya masaa matatu ya umuhimu wa kwenda. Ingawaje hotuba yenyewe ina mambo muhimu, upeo wa mwanafunzi ni mdogo kuunganisha umuhimu wa yeye kwenda shule na matokeo yake ya baadaye.
 
Bin Maryam,
Mkuu ningependa sana kufahamu makosa yangu hasa napomkubali Nyerere kama Kiongozi bora.
Umetoa huo wimbo wetu kuwa ili tuendelee tunahitaji Watu, Ardhi, Siasa safi na Uongozi bora..
Ni kitu gani hapo juu kinachopingana na itikadi za nchi za magharibi ama elimu ya Uchumi!..
Naomba somo mkuu maanake nachoona mimi hao WATU ndio kina NDIVYO TULIVYO!.

Mkandara:

Kulikuwa na tofauti kubwa sana kati ya kiongozi wa nchi za magharibi na kiongozi wa nchi kama Tanzania asa baada ya kutangazwa kwa Ujamaa.

Nchi za magharibi kiongozi wa serikali kwa kiasa kikubwa ni REGULATOR.

Kwa Tanzania kiongozi alikuwa ni REGULATOR na wakati huohuo ni CEO wa shirika linaloitwa serikali. Serikali ya Tanzania ilikuwa ni mzalishaji kamili wa bidhaa mbalimbali.

Kwa public consumption tunaweza kusema kuwa tukitaka maendeleo tunahitaji:
  1. Ardhi
  2. Watu
  3. Siasa safi
  4. Na uongozi bora

Lakini tukienda kiuchambuzi, details za siasa safi na uongozi bora ni kubwa na zinatofautiana kutokana na kile wanachofanya. Kiongozi anayepanga sheria ya makampuni binafsi kushindana na kulipa kodi ni tofauti na yule anayeyapangia sheria za uzalishaji makampuni ya umma na wakati huohuo kuyaongoza japokuwa kwa mbali.
 
Mwakilishi, mukombosi:

Mkiingiza kila kitu na udini tutaendelea kutawaliwa na matahira katika nchi hile ya mababu.

Mimi sipendi udini,ila nimeuliza ni kwanini hapa zanzibar kuanzia vyama na serikali viongozi wooote ni waislamu?hakuna wakristo wasomi na wenye uwezo wa kuongoza zaidi ya hata hawa waliopo madarakani?Na inakuwa huko bara wakristo wakichaguliwa wengi kiaina ktk serikali ya jamhuri minong'onoinaanza?Naomba jibu bin maryam na wengine.

Inavyoonekana sasa hili amani iwepo na viongozi waendelee kunyonya basi kila mkoa ni lazima upate nafasi ya uwaziri na baraza la mawaziri liwe na watu wa dini mbalimbali.

Sidhani kama hili ni la msingi sana,ingawa ndo approach inayotumika sana.tunahitaji watu wenye uwezo.pia amani ya tz inaletwa na MUNGU na watz wenyewe,na si vinginevyo.

Rais na Waziri mkuu atoke kwenye makabila madogo yaliochoka. Na makamu wa rais atoke Pemba.

Hiii ndo sitaki kuisikia kabisaaaaaaaaa.Tunataka vichwa na wazalendo.

Nchi ni lazima ikubali kuwa vurugu zitatokea lakini vyombo vya serikali ni lazima viwepo kutuliza vurugu hizo. Na kama vurugu zina ukweli wake basi zifanyiwe kazi hili jamii iweze kwenda hatua moja ya kimaendeleo.

Yah hapo umenena bin maryam,lakini ni jambo la msingi sana,kutafakari kwa kina kiini cha fujo zetu na maandano yasiyo na maana,kwa jamii masikini kama yetu,watz tunatakiwa kupiga kazi na si kupiga longolongo.

Ngoja niingie market kuuza nazi zangu hapa,tutaonana midaoooo.
 
August:

Mbeya ilijengwa na Warusi, Dar Tech Mwingereza na Arusha Tech. Mjerumani. Hupati maendeleo kwa kutumia migongo ya watu.

Bin Maryam, kwanza nashukuru kwa mchango wako, pili hatuwezi kupata maendeleo kwa Mgongo wa Mtu, lakini kwa siasa na uchumi wa dunia ya leo au hata kesho ni lazima tuamini kwenye Open System, nafikiri unaelewa Management na Mambo yanao endana na Hiyo Concept ya Open System, nafikiri unaweza ku-google ukapata maelezo yake na pia kwa faida yako ukasoma Closed System.
Tukirudi nyuma kwenye maada yenyewe,utaona hata China walianza kwa ku-copy from other kwenye kutengeneza bidha zao au kwenye kukuza teke-linalokujia, so kama alijenga Mrusi etc ni katika mikakati hiyo hiyo ya maendeleo, sema baada ya kupewa hiyo misaada ni juu yetu kuitumia vizuri, na ku na concept ya kujitegemea kwa kuimarisha hiyo elimu yetu.
Leo hii, wengi wetu tunasoma iwe sheria, biashara, udaktari wa binadamu, uhasibu, etc , lakini concept tunachukua toka kwa wenzetu walio tutangulia.
Eg Siku moja uni kute natembea kwa mguu toka ubungo kwenda kibaha, ukinipa lift si utakuwa umenifikisha mapema kibaha hivyo kuniwezesha kukamilisha shughuli zangu kwa haraka, hivyo nitakuwa a step ahead ya jinsi nilivyo tarajia, sema siku nyingine nisitegeme lift yako maana ya weza kuja au isije. Lakini ili siku ulivyo nisaidia umewezesha tija yangu kuongezeka, hivyo hiyo tija inaweza kuniongezea kipato cha kuweza kununua means of transport, nisitegeme lift yako.
Nategemea tumeelewa.
 
Bin Maryam, kwanza nashukuru kwa mchango wako, pili hatuwezi kupata maendeleo kwa Mgongo wa Mtu, lakini kwa siasa na uchumi wa dunia ya leo au hata kesho ni lazima tuamini kwenye Open System, nafikiri unaelewa Management na Mambo yanao endana na Hiyo Concept ya Open System, nafikiri unaweza ku-google ukapata maelezo yake na pia kwa faida yako ukasoma Closed System.
Tukirudi nyuma kwenye maada yenyewe,utaona hata China walianza kwa ku-copy from other kwenye kutengeneza bidha zao au kwenye kukuza teke-linalokujia, so kama alijenga Mrusi etc ni katika mikakati hiyo hiyo ya maendeleo, sema baada ya kupewa hiyo misaada ni juu yetu kuitumia vizuri, na ku na concept ya kujitegemea kwa kuimarisha hiyo elimu yetu.
Leo hii, wengi wetu tunasoma iwe sheria, biashara, udaktari wa binadamu, uhasibu, etc , lakini concept tunachukua toka kwa wenzetu walio tutangulia.
Eg Siku moja uni kute natembea kwa mguu toka ubungo kwenda kibaha, ukinipa lift si utakuwa umenifikisha mapema kibaha hivyo kuniwezesha kukamilisha shughuli zangu kwa haraka, hivyo nitakuwa a step ahead ya jinsi nilivyo tarajia, sema siku nyingine nisitegeme lift yako maana ya weza kuja au isije. Lakini ili siku ulivyo nisaidia umewezesha tija yangu kuongezeka, hivyo hiyo tija inaweza kuniongezea kipato cha kuweza kununua means of transport, nisitegeme lift yako.
Nategemea tumeelewa.

Anza kwa kujikuna pale unapoweza na mambo mengine yatakuja yenyewe.

Kila taifa au jamii wamekopi kutoka kwa wenzao. Ni wachina walioanza kutumia noti kama pesa na ni waarabu walioanza kutumia hundi. Lakini pamoja na hayo mataifa ya magharibi yalikopi.

Hivyo kukopi ni kitu cha kawaida. Lakini kusaidiwa sio kitu cha kawaida. Hakuna nchi iliyoendelea kwa kupewa hata kama misaada yenyewe ni ya vyuo vya ufundi.
 
Bin Maryam,
Yeye ni mfano na Mwalimu ambaye akitaka mtoto aende shule basi atampa mtoto hotuba ya masaa matatu ya umuhimu wa kwenda. Ingawaje hotuba yenyewe ina mambo muhimu, upeo wa mwanafunzi ni mdogo kuunganisha umuhimu wa yeye kwenda shule na matokeo yake ya baadaye

Shukran sana inaonyesha sasa hivi tupo ktk highway moja tukielekea upande unaofahamika...Sasa unaposema UPEO wa wanafunzi wake ulikuwa mdogo, hii mkuu haikukaa sawa kwanza, kisha tunarudi pale pale kuwa sisi ndio wenye matatizo. Pamoja na kwamba sikubaliani na hilo neno UPEO wetu ulikuwa mdogo ina maana moja kuwa sisi tuna low IQ..Badala yake nasema sisi tulikuwa na tatizo la UTUMWA wa akili na mwili..(Wapuuzi na wazembe).
Sii kwamba tulishindwa kuelewa umuhimu wa hotuba zake kutokana na Upeo mdogo, hata kidogo isipokuwa tulipuuza kwenda shule (Ujamaa) kutokana na uzembe wa mioyo yetu kuwa vinara wa maendeleo yetu wenyewe. Moses alitumia pia hotuba na wa Israel wasokuwa wapuuzi na wazembe waliweza yafanya mazito pamoja na kupotea jangwani kwa miaka 40 ktk kujikomboa kwao. Leo hii nadhani tunategemea sana misaada kuliko wakati wowote ule kwani hatuna uwezo, mwongozo, kiongozi wala dira. Hapa tulipo sasa hivi mkuu itakuwa ngumu!

Nyerere sio tu aliweza kuhutubia aliweza kujenga vyanzo kibao vya maendeleo ya Mtanzania hazikuwa hadithi na kwa muda mfupi aliweza kuwa na wataalam tosha ktk nyanja muhimu hasa Kilimo ambacho kilikuwa uti wa mgongo wa Uchumi wetu (demand and supply) na hadi leo hii bado naamini kabisa kuwa Kilimo ni uti wa mgongo wa Uchumi wetu. Wapo wataalam wanaopinga maendeleo ya kutokea chini na hawa ndio wanaopinga kuwa Kilimo hakiwezi kuwa uti wa mgongo wa Uchumi wetu kwani dunia ya leo imebadilika ktk mahitaji yake. Hawa binafsi siwezi kuwaita kuwa wana Upeo mdogo kwani hata wao wanaweza sema hivyo hivyo kutokana na mtazamo wao. Lakini issue yangu kubwa hapa sio upeo wa mtazamo wangu ama wao ktk maendeleo ya Tanzania, tatizo langu ni UTEKELEZAJI wa itikadi hiyo Kiuchumi ambayo leo hii badala ya kutupeleka mbele tunarudi nyuma. Matokeo haya yanatokana na KUPUUZA, UZEMBE uliojaa ktk mfumo mzima wa uzalishaji nchini.
Tukirudi ktk swala la wakati wa Nyerere, kuchukua mfano wa Tanzania na nchi za magharibi nadhani mkuu tutakuwa tunarudi nyuma tena kwani hakuna asiyefahamu kuwa Ujamaa uliwawezesha serikali Ku control uchumi wetu tofauti na nchi hizo ambazo tayari zilikuwa na matajiri wanaoweza kuendesha uchumi wa nchi zao. Hapa Tanzania nani alikuwa na Credit tosha ya kuweza pata mkopo kujenga kiwanda peke yake... Ujamaa lengo lake ilikuwa kukusanya nguvu zetu kifedha kwa kutumia credit ya nchi kubeba mzigo wa deni kubwa la mikopo ya vyanzo hivyo kisha, tukumbuke pia kuwa Ujamaa kumuinua Mtanzania maskini asiyekuwa na uwezo wa kifedha pamoja na nchi ARDHI ambayo ilikuwa haina miundombinu kulinganisha na nchi kama Kenya. Tanzania wakati wa mwalimu 99.9% ya wananchi wake walikuwa maskini na nchi yetu ilikuwa kati ya nchi maskini kuliko zote duniani.. Where do you start?..
Mnapofikiria Ubepari nani angeweza kuwa bepari kama sii mgeni toka nje?... kulikuwa na posibility gani za Ubepari kuweza kuwainua wananchi asilimia 99 toka umaskini tofauti na nchi nyinginezo!...
Hivyo tulipoanza na Ujamaa ilibidi kutumia system hiyo kuweza kumwinua hata Mkandara ambaye hakuwa na nafasi yoyote ile. Yes ilikuwa vigumu kumwinua maskini toka chini lakini mwalimu aliweza kufanikiwa kwa kiwango kikubwa sana kwa kupitia matatizo mengi ambayo leo hii wengi wanashindwa kuyaona pamoja na kwamba wengi wetu tumesoma bure hadi vyuo vikuu na leo hii ndio tunashika madaraka. Nyerere mwenyewe alikuwa anakumbuka fadhila za wale walioweza kumsomesha na as a leader of the nation alihakikisha haki hiyo inakuwa ya kitaifa badala ya kutegemea matajiri wachache (aslimia chini ya moja) ambao wangeweza kusomesha watoto wao chini ya mfumo wa Kibepari.

Unajua mkuu wengi mnashindwa kuelewa kwamba Maendeleo ya Tanzania yataletwa tu na Mtanzania mwenyewe. Swala la mwalimu kukopa fedha nje lisionekane kama ni ujenzi wa nchi kwa kutumia migongo ya watu.. Laa hasha mkuu hapo sikubaliani. Nyerere alikopa fedha hizo na kuwapa contractor nchi za nje kujenga mashule na vyuo kwa sababu yetu sisi, jambo ambalo lisingewezekana kabisa chini ya mfumo wa mkoloni..
Sii kweli kabisa kwamba wakati wa Nyerere tulitegemea misaada kwa tafsiri unayojaribu kuiweka hapa.
Nadhani kama unakumbuka vizuri, Mwalimu alichukiwa kwa kuwa mkorofi ktk misaada (AIDS) hiyo kwani alisema huwezi kunipa msaada na kutupangia kitu cha kufanya. Tutachukua misaada (AIDS) na mikopo (GRANTS) kkulingana na umuhimu wa mahitaji yetu na sio yao wao. Na kutokana na kiburi hicho Nyerere alipewa misaada/mikopo kwa masharti magumu zaidi ktk usimamizi na pengine hakupewa kabisa.

Tatizo kubwa la misaada ya IMF leo hii ni kwamba wao ndio wapangaji wa mahitaji yako. Ndio maana tunaita kuwa huu ni Ukoloni mambo leo kwani wanatumia elimu zao kuutafsiri Umaskini na jinsi ya kuuondoa kutokana na vitabu vya elimu, hali mazingira ya Umaskini yanatofautiana nchi hadi nchi kutokana na WATU, ARDHI, SIASA na UONGOZI.
 
Bin Maryam,


Shukran sana inaonyesha sasa hivi tupo ktk highway moja tukielekea upande unaofahamika...Sasa unaposema UPEO wa wanafunzi wake ulikuwa mdogo, hii mkuu haikukaa sawa kwanza, kisha tunarudi pale pale kuwa sisi ndio wenye matatizo. Pamoja na kwamba sikubaliani na hilo neno UPEO wetu ulikuwa mdogo ina maana moja kuwa sisi tuna low IQ..Badala yake nasema sisi tulikuwa na tatizo la UTUMWA wa akili na mwili..(Wapuuzi na wazembe).
Sii kwamba tulishindwa kuelewa umuhimu wa hotuba zake kutokana na Upeo mdogo, hata kidogo isipokuwa tulipuuza kwenda shule (Ujamaa) kutokana na uzembe wa mioyo yetu kuwa vinara wa maendeleo yetu wenyewe. Moses alitumia pia hotuba na wa Israel wasokuwa wapuuzi na wazembe waliweza yafanya mazito pamoja na kupotea jangwani kwa miaka 40 ktk kujikomboa kwao. Leo hii nadhani tunategemea sana misaada kuliko wakati wowote ule kwani hatuna uwezo, mwongozo, kiongozi wala dira. Hapa tulipo sasa hivi mkuu itakuwa ngumu!

Nyerere sio tu aliweza kuhutubia aliweza kujenga vyanzo kibao vya maendeleo ya Mtanzania hazikuwa hadithi na kwa muda mfupi aliweza kuwa na wataalam tosha ktk nyanja muhimu hasa Kilimo ambacho kilikuwa uti wa mgongo wa Uchumi wetu (demand and supply) na hadi leo hii bado naamini kabisa kuwa Kilimo ni uti wa mgongo wa Uchumi wetu. Wapo wataalam wanaopinga maendeleo ya kutokea chini na hawa ndio wanaopinga kuwa Kilimo hakiwezi kuwa uti wa mgongo wa Uchumi wetu kwani dunia ya leo imebadilika ktk mahitaji yake. Hawa binafsi siwezi kuwaita kuwa wana Upeo mdogo kwani hata wao wanaweza sema hivyo hivyo kutokana na mtazamo wao. Lakini issue yangu kubwa hapa sio upeo wa mtazamo wangu ama wao ktk maendeleo ya Tanzania, tatizo langu ni UTEKELEZAJI wa itikadi hiyo Kiuchumi ambayo leo hii badala ya kutupeleka mbele tunarudi nyuma. Matokeo haya yanatokana na KUPUUZA, UZEMBE uliojaa ktk mfumo mzima wa uzalishaji nchini.
Tukirudi ktk swala la wakati wa Nyerere, kuchukua mfano wa Tanzania na nchi za magharibi nadhani mkuu tutakuwa tunarudi nyuma tena kwani hakuna asiyefahamu kuwa Ujamaa uliwawezesha serikali Ku control uchumi wetu tofauti na nchi hizo ambazo tayari zilikuwa na matajiri wanaoweza kuendesha uchumi wa nchi zao. Hapa Tanzania nani alikuwa na Credit tosha ya kuweza pata mkopo kujenga kiwanda peke yake... Ujamaa lengo lake ilikuwa kukusanya nguvu zetu kifedha kwa kutumia credit ya nchi kubeba mzigo wa deni kubwa la mikopo ya vyanzo hivyo kisha, tukumbuke pia kuwa Ujamaa kumuinua Mtanzania maskini asiyekuwa na uwezo wa kifedha pamoja na nchi ARDHI ambayo ilikuwa haina miundombinu kulinganisha na nchi kama Kenya. Tanzania wakati wa mwalimu 99.9% ya wananchi wake walikuwa maskini na nchi yetu ilikuwa kati ya nchi maskini kuliko zote duniani.. Where do you start?..
Mnapofikiria Ubepari nani angeweza kuwa bepari kama sii mgeni toka nje?... kulikuwa na posibility gani za Ubepari kuweza kuwainua wananchi asilimia 99 toka umaskini tofauti na nchi nyinginezo!...
Hivyo tulipoanza na Ujamaa ilibidi kutumia system hiyo kuweza kumwinua hata Mkandara ambaye hakuwa na nafasi yoyote ile. Yes ilikuwa vigumu kumwinua maskini toka chini lakini mwalimu aliweza kufanikiwa kwa kiwango kikubwa sana kwa kupitia matatizo mengi ambayo leo hii wengi wanashindwa kuyaona pamoja na kwamba wengi wetu tumesoma bure hadi vyuo vikuu na leo hii ndio tunashika madaraka. Nyerere mwenyewe alikuwa anakumbuka fadhila za wale walioweza kumsomesha na as a leader of the nation alihakikisha haki hiyo inakuwa ya kitaifa badala ya kutegemea matajiri wachache (aslimia chini ya moja) ambao wangeweza kusomesha watoto wao chini ya mfumo wa Kibepari.

Unajua mkuu wengi mnashindwa kuelewa kwamba Maendeleo ya Tanzania yataletwa tu na Mtanzania mwenyewe. Swala la mwalimu kukopa fedha nje lisionekane kama ni ujenzi wa nchi kwa kutumia migongo ya watu.. Laa hasha mkuu hapo sikubaliani. Nyerere alikopa fedha hizo na kuwapa contractor nchi za nje kujenga mashule na vyuo kwa sababu yetu sisi, jambo ambalo lisingewezekana kabisa chini ya mfumo wa mkoloni..
Sii kweli kabisa kwamba wakati wa Nyerere tulitegemea misaada kwa tafsiri unayojaribu kuiweka hapa.
Nadhani kama unakumbuka vizuri, Mwalimu alichukiwa kwa kuwa mkorofi ktk misaada (AIDS) hiyo kwani alisema huwezi kunipa msaada na kutupangia kitu cha kufanya. Tutachukua misaada (AIDS) na mikopo (GRANTS) kkulingana na umuhimu wa mahitaji yetu na sio yao wao. Na kutokana na kiburi hicho Nyerere alipewa misaada/mikopo kwa masharti magumu zaidi ktk usimamizi na pengine hakupewa kabisa.

Tatizo kubwa la misaada ya IMF leo hii ni kwamba wao ndio wapangaji wa mahitaji yako. Ndio maana tunaita kuwa huu ni Ukoloni mambo leo kwani wanatumia elimu zao kuutafsiri Umaskini na jinsi ya kuuondoa kutokana na vitabu vya elimu, hali mazingira ya Umaskini yanatofautiana nchi hadi nchi kutokana na WATU, ARDHI, SIASA na UONGOZI.

Mkandara:

Watu hawakuwa wapuuzi na wazembe. Tanzania haikutawaliwa na mwingereza. Hivyo wakati wa kuwepo kwao wazawa walikuwa na nafasi nyingi za kiuchumi ukilinganisha na nchi zingine zilizokuwa katika ukoloni kamili.

Hatukuwa na wasomi lakini hata yule masikini wa mwisho alikuwa ana kipande cha ardhi chenye kumwezesha kulima na kujipatia mahitaji yake. Hivyo napinga kwa nguvu zote usemi wako wa kuwa walikuwa wavivu na wazembe.

Sehemu nayotoka watu walimiliki mashamba ya mikorosho, miembe, misufi na mazao mengine yalioleta mzunguko mkubwa wa pesa. Kilichotakiwa ni kuongoza shule kidogo tu.

Uanzishaji wa mamlaka za mazao, vijiji vya ujamaa na operesheni maduka umevuruga kila kitu. Na hii sio IMF ni Man Made Disaster. Mtu anabolewa nyumba, kuacha mashamba na anachopewa ni chini ya shilling 200 kwenda kuanza maisha mapya.

Wanasema ukimfundisha mtu na kumwachia uhuru afanye anachotaka anafanya miujiza mikubwa kuliko ukimfundisha na kumlazimisha afanye unachotaka.

Ndio Nyerere aliweza kuanzisha mfumo wa elimu na kutoa wasomi wake lakini mfumo mzima wa maisha haukuwapa uhuru wa kufikiri.
 
Bin Marium,
Watu hawakuwa wapuuzi na wazembe. Tanzania haikutawaliwa na mwingereza. Hivyo wakati wa kuwepo kwao wazawa walikuwa na nafasi nyingi za kiuchumi ukilinganisha na nchi zingine zilizokuwa katika ukoloni kamili.
Nakuiomba fafanua usemi huu kwanza!
Kisha swala hapa sio uwezo wa KULA toka kwenye sahani kwenda mdomoni kupata shibe, tunazungumzia Umaskini in a sense ya Maendeleo..
Kuhusu mashamba, hili nalisikia leo kwani waliokuwa wakihamishiwa vijiji vya Ujamaa ni wale wasiokuwa na mashamba ama ardhi ya kumiliki kwa wakati ule walionekana kama wazururaji.
Binafsi naelewa kuwa wazee wetu wameendelea kuwa na mashamba yao hadi miaka hii ya juzi ambapo viongozi wengi wamevamia mashamba hayo, serikali imewachuuza wananchi kuchukua ardhi zao kuwapa wageni iwe ktk madini ama ujenzi wa viwanda ambavyo havijajengwa hadi leo. Binafsi tumenyang'anywa shamba letu huko Ukererwe hivi majuzi na tulikuwa nalo toka mababu zetu..Hii hadithi inatoka wapi mkuu umehadithiwa kuhusu vijiji vya Ujamaa ama?..
Nambie nani aliyenyang'anywa shamba lake na kuhamishiwa vijijini. lazima historia kama hii ina mifano hai. nani kati yetu ni matunda ya kuhamishwa huko yaani tumejikuta tumezaliwa ktk vijiji, kutakaacha miji na mashamba yetu ya asili.
 
Bin Marium,

Nakuiomba fafanua usemi huu kwanza!
Kisha swala hapa sio uwezo wa KULA toka kwenye sahani kwenda mdomoni kupata shibe, tunazungumzia Umaskini in a sense ya Maendeleo..
Kuhusu mashamba, hili nalisikia leo kwani waliokuwa wakihamishiwa vijiji vya Ujamaa ni wale wasiokuwa na mashamba ama ardhi ya kumiliki kwa wakati ule walionekana kama wazururaji.
Binafsi naelewa kuwa wazee wetu wameendelea kuwa na mashamba yao hadi miaka hii ya juzi ambapo viongozi wengi wamevamia mashamba hayo, serikali imewachuuza wananchi kuchukua ardhi zao kuwapa wageni iwe ktk madini ama ujenzi wa viwanda ambavyo havijajengwa hadi leo. Binafsi tumenyang'anywa shamba letu huko Ukererwe hivi majuzi na tulikuwa nalo toka mababu zetu..Hii hadithi inatoka wapi mkuu umehadithiwa kuhusu vijiji vya Ujamaa ama?..
Nambie nani aliyenyang'anywa shamba lake na kuhamishiwa vijijini. lazima historia kama hii ina mifano hai. nani kati yetu ni matunda ya kuhamishwa huko yaani tumejikuta tumezaliwa ktk vijiji, kutakaacha miji na mashamba yetu ya asili.

Mkandara:

Naona mzee huko mbali na reality. Sera za vijiji vya ujamaa hazikuwa na mpango wa kutoa mashamba kwa sababu kila mtu alikuwa nayo.

Sera zilikuwa na mpango wa kuanzisha centers zitakazokuwa na shule za msingi, sekondari, vituo vya maji na afya karibu na wananchi.

Na sera hizi zilikuwa blessed na World Bank na mapesa yalitolewa. Lakini wananchi hawakuzipenda na kusababisha mtafaruku mkubwa katika uzalishaji wa chakula na mazao mengine.

Na kwa mtaji niliosema juu naona unamshabikia Nyerere kama unashabikia timu yako ya mpira na una mapungufu katika uchambuzi wa sera zake.
 
Bin Maryam.
Duh, mkuu ama kweli mwenzangu mjuzi sana wa ku spin.. imekuwa hayo tena?..
Mwenyewe umeandika hivi:-
Watu hawakuwa wapuuzi na wazembe. Tanzania haikutawaliwa na mwingereza. Hivyo wakati wa kuwepo kwao wazawa walikuwa na nafasi nyingi za kiuchumi ukilinganisha na nchi zingine zilizokuwa katika ukoloni kamili.
Nimekuomba ufafanue usemi huo, umelitolea nje!.
Ukaongezea haya haya:-
Hatukuwa na wasomi lakini hata yule masikini wa mwisho alikuwa ana kipande cha ardhi chenye kumwezesha kulima na kujipatia mahitaji yake. Hivyo napinga kwa nguvu zote usemi wako wa kuwa walikuwa wavivu na wazembe
.
Nikakujibu hoja ya mada hii sio umaskini wa tonge toka ktk sahani kwenda mdomoni ila tunazungumzia Maendeleo.

Mwisho ukamalizia na maneno haya ambayo yanapingana na usemi wako huu mpya. Soma uone unavyojipinga mwenyewe..
1.
Uanzishaji wa mamlaka za mazao, vijiji vya ujamaa na operesheni maduka umevuruga kila kitu. Na hii sio IMF ni Man Made Disaster. Mtu anabolewa nyumba, kuacha mashamba na anachopewa ni chini ya shilling 200 kwenda kuanza maisha mapya.

2.
Naona mzee huko mbali na reality. Sera za vijiji vya ujamaa hazikuwa na mpango wa kutoa mashamba kwa sababu kila mtu alikuwa nayo.
Sera zilikuwa na mpango wa kuanzisha centers zitakazokuwa na shule za msingi, sekondari, vituo vya maji na afya karibu na wananchi.
Na sera hizi zilikuwa blessed na World Bank na mapesa yalitolewa. Lakini wananchi hawakuzipenda na kusababisha mtafaruku mkubwa katika uzalishaji wa chakula na mazao mengine.

Kweli hapa utanilaumu mimi hali sifahamu unachosimamia mkuu!... kibaya ni kwamba mimi mshabiki wa Nyerere ninayo timu lakini mwenzangu yaonyesha huna timu na kisha huufahamu mchezo huu wa Football, unazungumzia Soccer mkuu ... haaa haaa haaa!
 
Katika pirika pirika zangu nimekutana na hiki kitabu kinachomuelezea nyerere kama thinker on developmental issues

9780415337908.jpg


Ifuatayo ni summary yake.

The essential guide to the world's most influential
development thinkers, this authoritative text
presents a unique guide to the lives and ideas of
leading contributors to the contested terrain of
development studies.
Reflecting the diverse, interdisciplinary nature of
the area, the book includes entries on:
• modernisers like Hirshman, Kindleberger and
Rostow
• dependencistas such as Frank, Cardoso and
Amin
• progressives like Prebisch, Helleiner and Streeten
• political leaders enunciating radical alternative
visions of development, such as Mao, Nkrumah
and Nyerere

• progenitors of religiously or spiritually inspired
development, such as Gandhi and Ariyaratne
• development-environment thinkers like Blaikie,
Brookfield and Shiva.
This is a fascinating and readable introduction to
the major figures that have shaped the field, ideal
for anyone studying or working in the area.

FOR MORE DETAILS CLICK HERE.


 
When we look at the legacy of Mwalimu we are looking at a legacy of contradictions; To some people he was a hero, a nationalist, an African pioneer, a teacher and a philosopher-ruler. To these people Nyerere was and still is one of the greatest African intellectuals who ever ascended to power to lead a nation post independence Africa.

To others however, Nyerere was nothing else but a failure, a dictator camouflaged like a patriot, he was to them a leader in failure, a man of so many words but very few actions; he was a man of great ideas but very limited success in turning those ideas into reality. To these harsh critics of Nyerere there are those who hold him in contempt for the lack of nice cars, TVs, many schools, universities etc during his rule. To them, Nyerere was the single person who delayed the material development of Tanzania.

To the first group, Nyerere was a nation-builder, a leader committed to the welfare of his people and his nation; they remember his farewell words that "tell my Tanzanians that I love them" with fondness and emotions. To them Nyerere was and still is the greatest leader that came from Tanzania.

Was Nyerere a failure or a success? Where did he fail and where did he succeed?

Je kushindwa kwake kunaziba kabisa mafanikio yake to the point that his name should now be written with an asterik on the side? What were his failures and accomplishments? which one outweighed the other?

Focus:
 
Back
Top Bottom