Hivi hii nimekua nikiangalia na kusoma kwa shauku historia fupi ya kikwete toka alivyokuwa kijana mpaka sasa hivi , malengo yake haswa ya kuingia ccm yalikuwa ni nini , kwanini alikataliwa kugombea uraisi mwaka 1995 na mambo mengine kem kem
Pamoja na kusoma haya maandishi yote nimekuja kugundua Nyerere hakuna na uhusiano mzuri na kikwete pamoja ya yeye mwenyewe kikwete anavyojitapa anapotembelea maeneo mbali mbali nje za nchi na jinsi anavyojifnaya kumwabudu nyerere .
Mwaka 1995 wakati wa kuchagua watu watakaogombea uraisi kwa tiketi ya CCM , majina mengi yalipelekwa lakini wa mwisho alikuwa ni Kikwete na jamaa wengine hakuna aliyekuwa anajua kama mkapa kweli atachaguliwa au la , nah ii ni kutokana na mkapa mwenyewe msimamo wako tokea akiwa mwanafunzi wa makerere , mwandishi wa habari mpaka alivyokuwa waziri historia yake ilimweleza ni mtu wa aina gani
Watu wengi haswa huko CCM walikuwa wanataka DAMU changa ambayo wanafikiri ingeendana na Mwinyi au tofauti kidogo ambayo ingeleta mapinduzi katika Nchi husika lakini hapo hapo nchi iendelee kuliwa kidogo kidogo .
Ndio hapa Nyerere aliingilia kati na kuamuru MKAPA agombee na kumwacha Kikwete solemba , Baba wa taifa alikiri mwenyewe hayuko tayari kumwona Kikwete akiongoza nchi wakati yeye akiwa Hai kwa sababu alishajua kile kikwete na jamaa zake wengine wanachotaka hichi ambayo wanakifanya sasa hivi .
Hapo tukampata mkapa , kwa kweli mkapa alifanya kazi na kubadilisha mambo mengi katika nchi hii , mpaka pale Nyerere alipoaga dunia , CCM ikawa haina mbabe , kigogo aliyebaki ambaye hakuonyesha kiburi wakati nyerere akiwa hai ni mkapa , hapo ndio mkapa akaanza kuwa mjasiriamali
Ndio historia ya Mkapa kufanya biashara wakati akiwa Bado kiongozi wa nchi inapoanzia ingawa alikuwa akifanya lakini kwa siri haswa na maswahiba wake wa Uganda na vigogo wengine aliosoma nao chuo kikuu cha makerere .
Kama nilivyosema hapo juu Mkapa ni mtu Mkimya lakini Jeuri sana , wakati nyerere akiwa hai alionyesha Ukimya wake na pengine nyerere asingefariki mkapa asingefanya hizo biashara na hujuma zingine ambazo amezifanya kwa nchi hii kwa sababu kungekuwa na mtu wa kumuuliza na kuhoji .
Mwaka 2005 ukafika mambo ya kuchaguana yakafanyika tena , wakati huu watu waliongezeka kidogo lakini ambao walivuta hisia ni Kikwete yule yule na Salim , kama unavyojua waandishi wetu wa kitanzania ni vipofu hawakuweza kuhoji wala kudadisi ni nini haswa kilimkosesha Uongozi kikwete 1995 ?
Bado waandishi wetu wa habari hawataki kutuambia ukweli waliendelea kumlamba kikwete miguu yake , kumsifia na kumpamba na mambo kibao ambayo hayana msingi wowote , kikwete aliweza kuwanunua mpaka wachungaji wa makanisa ambao tunawaheshimu wamsaidie kumpigia kura makanisani na misikitini .
Mbaya zaidi alifanikiwa mpaka kutengeneza ubaguzi wa rangi pale alipomtuhumu salim yeye ni mwarabu ,na mmoja wa ndugu zake ni offisa wa jeshi huko Arabuni , lakini la kutisha zaidi inasemekana kikwete alihusika na mauaji ya mmoja wa walinzi wa Salim huko Addis Ababa , sina uhakika kuhusu hili na waandishi wa habari wamejaribu kuficha sana kadhia hii .
Lakini faulo zake zilianza pale alipoanza kwenda Mwanza ndege imejaa babu zake wa bagamoyo , washirikina na wanga ambao walikuwa wanaenda nae safari nyingi kuhakikisha wanafanya mazingira mpaka apate ushindi hapo ndipo kasheshe zilipoanza .
Ni ukweli usio fichika kwamba Nyerere alishajua kabisa kwamba Kikwete sio chaguo la wananchi wala la mungu wala la mtu wowote alishatoa utabiri wake sema watanzania wengi sio wadadisi na sio wazalendo wangehoji tangia mwanzo
Huu ni mwaka mmoja na nusu , tangia kikwete raisi hajafungua barabara yoyote , hajafungua mradi wowote ule mkubwa na wala hajaafanya lolote la maana ambalo litamfanya akumbukwe hata akitutoka sasa hivi sijui ana malengo gani na nchi hii ?
Uwanja wa taifa ulitakiwa ufunguliwe toka aprili mpaka leo haujafunguliwa kwa sababu ambazo raisi anazijua mwenyewe , BOT makao makuu ilitakuwa ifunguliwe nayo mpaka sasa hivi hatujui nini kinachoendelea zaidi ya kashfa na bilali wake ambaye ni kiongozi pale BOT .
Ni kweli Nyerere alijua haya ?