Kulikoni: Mama Mwantumu Malale sio VC; yeye ni Chancellor. VC ni profesa fulani jina limenitoka.
Nafikiri hiki chuo sio secular angalau kwa vigezo vya udahiri wa wanafunzi na wafanyakazi. Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa katika udahiri wa kwanza chuo kilichukua wanafunzi wote wa kiislamu. Hata utawala, vigogo karibu wote (kama sio wote kabisa) ni waislamu! Naomba unisahihishe katika hili kama si kweli!
Mwanasiasa,
Yes, nlikosea mimi. Mwantumu Malale ni Chancellor, na ni mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya ukuu wa chuo nchini Tanzania.
Kwa nlivyoielewa maana ya secular aliyoitumia Mwl. Mushi, nlidhani kamaanisha courses zinazotolewa na curriculum kwa ujumla. Na kwa taarifa nlizonazo the chuo is secular in that sense.
I have another correction, the courses offered so far are B.A. Education, B.A. Mass Communication and B.A. Islamic Studies (nlikosea mwanzo nliposema ni law).
Kwa kweli sina takwimu rasmi za wanafunzi na wafanyakazi, ila nlimsikia muislamu mwenzangu aliekwenda chuoni hapo akilalamika eti kwa nini chuo cha waislamu kinakuwa na walimu na wanafunzi wa kikristo, na hata mavazi hakuna restrictions zozote... hata mama Malale havai hijabu per se, na hivyo basi, kwa mtazamo wake, sura ya kuwa ni chuo cha waislamu haipo. Tukabishana kiasi mimi nikisema kuwa hiyo ndio sawa kwa mazingira yetu ya Tz, hata kama chuo ni chetu hakuna haja ya kuwatenga wengine. Hii ndio 'source' yangu, kama mwenzangu una takwimu rasmi za udahili zitakuwa na nguvu zaidi kuliko 'source' hii.
'Vigogo' karibu wote kuwa waislamu sitashangaa sana, na nadhani sio kosa. Afterall ni chuo cha waislamu. Au kule Tumaini na kwengineko kuko vipi? Ila kwa kweli ntashangaa ikiwa kuna policy ya hata walimu nao kuwa ni waislamu watupu. Namna hiyo hatufiki.