FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,506
- 123,802
- Thread starter
- #141
Labda na mimi nikuulize swali kidogo,hivi hayo unayosema nyerere kasingiziwa ilistahili aambiwe nani unaedhani alistahili kupewa sifa hizo,
Hebu turudi kwenye post namba moja tuanza na point ya kwanza.
Hivi wewe unafikiri ni sifa nzuri ya kumpa mtu aliyeleta Uhuru kwa amani kumsingizia kuwa "alipigania Uhuru"? hauoni hapo unamshusha na unajishusha kuwa tulikuwa hatustahili kuwa huru mpaka "tumepigania"?
Sasa ikiwa unamsinguzia Nyerere "kapigania Uhuru" na hali ya nchi alivyoiacha miaka 27 baadae ikiwa hohehahe si kama unamwambia "ulipigania Uhuru" wakati umeshindwa kutawala? au wewe unaonaje?
Mimi nadhani tumpe sifa yake anayostahili ya kutuletea Uhuru usomi wake kwa amani bila kupigania wala kumwaga damu na tukaagana vizuri na Muingereza kukabidhiana madaraka kwa heshima bila damu kumwagika.
Kama kulikuwa na damu iliyomwagika basi ilikuwa ni ya yale makafara tu aliyokuwa akihudhuria Nyerere na kuchinjiwa mbuzi, ng'ombe, kuku. Au siyo?
Tukubaliane hili la kwanza halafu twende la pili. Au unasemaje?