Niulize chochote nikujibu

Niulize chochote nikujibu

Nini tofauti ya upendo na mapenzi
Upendo ni hisia ya dhati ya kuheshimu, kuthamini, na kujali mtu au kitu bila kulazimika kuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Lakin
Mapenzi ni sehem ya upendo inayohusisha hisia za kimahaba na mvuto wa kimwili kati ya watu wawili.mfano wewe na mpenzi wako
 
Mungu alitoa wapi maada/Material ya kuumba huu ulimwengu?
Pia naomba kujua alipata wapi akili alizonazo wakati hakukuwa na shule
Nitakujibu kutokana na Imani yangu;
Katika imani nyingi hususan za kikiristo, kiislamu, na kiyahudi, Mungu anaelezewa kama mwenyezi, mwenye uweza wote na mjuzi wa yote. Kwa mujibu wa biblia(Mwanzo 1:1) "Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi." Hii ina maana kuwa Mungu hakuhitaji material aliumba ulimwengu kwa neno lake tu (Mwanzo 1:3). Pia katika uslamu, Qur'an inasema:
"Hakika amri yake anapotaka jambo ni kulisema tu: 'Kuwa!' Likawa." (Qur'an 36:82)
 
Nitakujibu kutokana na Imani yangu;
Katika imani nyingi hususan za kikiristo, kiislamu, na kiyahudi, Mungu anaelezewa kama mwenyezi, mwenye uweza wote na mjuzi wa yote. Kwa mujibu wa biblia(Mwanzo 1:1) "Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi." Hii ina maana kuwa Mungu hakuhitaji material aliumba ulimwengu kwa neno lake tu (Mwanzo 1:3). Pia katika uslamu, Qur'an inasema:
"Hakika amri yake anapotaka jambo ni kulisema tu: 'Kuwa!' Likawa." (Qur'an 36:82)
Acha nikae kimya 😆
 
1.Ungepewa nafasi ya kuwa president walau kwa dakk 5, ni nini ungekibadilisha unaona hakipo sawa ?

2,,ufe masikini ama upate pesa za madawa uwe tajri wa kuishi kwa masharti ?
1. Mkuu ikiwa ningekuwa rais kwa dakika 5 ningetangaza msamaha wa madeni kwa vijana wanaojitahidi kujiajiri lakin wamekwama kwa sababu ya mikopo midogo. Pia, ningetangaza sera ya dharura ya kupunguza gharama za elimu na huduma za afya kwa watu wa kipato cha chini.

2. Bora nife maskini lakini nikiwa na amani moyoni mwang kuliko kupata utajiri kwa njia haramu na kuishi kwa hofu na masharti. Pesa si kila kitu ikiwa inakuja na mateso au kuhatarisha maisha ya wengine(kizazi changu).
 
Dhambi ilitoka wapi?
Kwa mujibu wa bibilia dhambi ilianza mbinguni wakati shetan alipoasi dhidi ya Mungu (Nukuu Isaya 14:12-15, Ezekieli 28:12-17). Pia mkuu duniani dhambi ilianza pale Adamu na Hawa walipomwasi Mungu kwa kula tunda lililokatazwa katika Bustani ya Edeni (Mwanzo 3).
 
Kwa mujibu wa bibilia dhambi ilianza mbinguni wakati shetan alipoasi dhidi ya Mungu (Nukuu Isaya 14:12-15, Ezekieli 28:12-17). Pia mkuu duniani dhambi ilianza pale Adamu na Hawa walipomwasi Mungu kwa kula tunda lililokatazwa katika Bustani ya Edeni (Mwanzo 3).
Kwahiyo Mungu aliiumba dhambi?
 
Back
Top Bottom