MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,564
- 847
Upinzani haushindi kwa sababu Tanzania hamna upinzani wa kweli. Watanzania wengi wana jiuliza kwa nini mpaka leo hii miaka karibia ishirini tokea uingie mfumo wa vyama vingi bado vyama vya upinzani havifui dafu kwa CCM. Ni kwa sababu ya mazingira ambao yaliambatana na kuanzishwa kwa vyama hivi. Ni vigumu kwa vyama hivi kuondokana na mzigo wa historia ya uanzishwaji wao. Nita fafanua mtazamo wangu.
1. CCM ndiyo kilikua chama pekee Tanzania kwa muda mrefu. Kwa maana hiyo CCM ilikua na muda zaidi wa kujijenga kiuongozi, kirasilimali na kiumaarufu. Watanzania wengi hawana vyanzo vya kuaminika na vya haraka vya kupata habari kama wengi wetu humu JF. Kwa hiyo bado kuna Watanzania wengi (amini usiamini) wanaishi "jana".
2. Kabla ya kuruhusu vyama vya upinzania, CCM, chama kilicho kuwa madarakani kilikua na muda wa kujiandaa. Katiba ya kuruhusu vyama vya upinzani iliandikwa na wao na muda wa kujiandaa na mabadiliko wa mazingira ya kisiasa walikuwa nao.
3. "Personalities" nyingi zilizo unda vyama vya upinzani ni wana CCM wa zamani. Ukimuangalia Mrema Sharif Hamad, Mtei wote ni watu waliokua ndani ya mfumo wa CCM. Hata Ibrahim Lipumba ambae sina uhakika kama alikua CCM au la alikua mshauri wa Mwinyi kipindi fulani. Je hii ina wezaje kuwa tatizo kwa vyama vya upinzani?
a) Baadhi ya viongozi waliongia upinzani ina wezekana walikua mamluki ambao walikua hawana mpango wowote wa upinzani wa kweli.
B) Baadhi ya viongozi walioingia upinzani ni watu ambao walikua hawana future CCM kwa hiyo walihama kwa ajili ya kujaribu bahati yao. Hiyo ni kusema upinzani ilipokea watu ambao hawakua nyota wa kisiasa bali "has beens" wa CCM.
c) Baadhi yao ni watu waliyo ondoka CCM kwa maana hiyo mfumo wa fikira ulikua huo huo. Hauwezi kumshinda mwalimu kwa kumpa mtihani wake mwenyewe.
4. Wengi wa viongozi waliounda vyama vya upinzani kwa sababu moja au nyingine ita kuwa wali fikiria kwamba CCM ita shindika kiurahisi. SI ajabu baadhi yao wakadhani kwamba 1995 wange kiondoa CCM madarakani. Kwa maana hiyo basi vyama hivi vya upinzani vilivyo anzishwa vilikua havina mipango ya muda wa kati au mrefu kwa maumaini kwamba uchaguzi una kuja na wao wata shindda. Mpaka leo hii sioni mipango ya kueleweka ya muda mrefu wa chama chochote cha upinzani.
Kwa hiyo basi kama vyama vya upinzani kweli vina taka kushinda basi ni lazima kuwepo na mabadiliko. Lazima waletwe vijana ambao watakua katika mfumo wa vyama vyao. Lazima walete watu ambao hawaku wahi kuhusika na CCM ili kuleta mawazo na fikira tofauti. Ni lazima waji tazame na wajiunde upya. Kusema ukweli sioni chama cha upinzani kati ya hivi vilivyopo sasa kufanya mabadiliko yoyote ya kisiasa labda vyama vipya vita kapo anzishwa au viongozi wa sasa waliotoka kwenye mfumo ule ule, mawazo yale yale na mafunzo yale yale wakija kuondoka.
Ndugu wana JF tuna muda mrefu bado mpaka upinzani wa kweli Tanzania uibuke. Leo hii hatuna wapinzani bali wasindikizaji. Kwa maana kila kabla ya uchaguzi tayari imesha julikana chama gani kita shinda uraisi na chama gani kita kuwa na wabunge wengi Bungeni. Huo si upinzani.
1. CCM ndiyo kilikua chama pekee Tanzania kwa muda mrefu. Kwa maana hiyo CCM ilikua na muda zaidi wa kujijenga kiuongozi, kirasilimali na kiumaarufu. Watanzania wengi hawana vyanzo vya kuaminika na vya haraka vya kupata habari kama wengi wetu humu JF. Kwa hiyo bado kuna Watanzania wengi (amini usiamini) wanaishi "jana".
2. Kabla ya kuruhusu vyama vya upinzania, CCM, chama kilicho kuwa madarakani kilikua na muda wa kujiandaa. Katiba ya kuruhusu vyama vya upinzani iliandikwa na wao na muda wa kujiandaa na mabadiliko wa mazingira ya kisiasa walikuwa nao.
3. "Personalities" nyingi zilizo unda vyama vya upinzani ni wana CCM wa zamani. Ukimuangalia Mrema Sharif Hamad, Mtei wote ni watu waliokua ndani ya mfumo wa CCM. Hata Ibrahim Lipumba ambae sina uhakika kama alikua CCM au la alikua mshauri wa Mwinyi kipindi fulani. Je hii ina wezaje kuwa tatizo kwa vyama vya upinzani?
a) Baadhi ya viongozi waliongia upinzani ina wezekana walikua mamluki ambao walikua hawana mpango wowote wa upinzani wa kweli.
B) Baadhi ya viongozi walioingia upinzani ni watu ambao walikua hawana future CCM kwa hiyo walihama kwa ajili ya kujaribu bahati yao. Hiyo ni kusema upinzani ilipokea watu ambao hawakua nyota wa kisiasa bali "has beens" wa CCM.
c) Baadhi yao ni watu waliyo ondoka CCM kwa maana hiyo mfumo wa fikira ulikua huo huo. Hauwezi kumshinda mwalimu kwa kumpa mtihani wake mwenyewe.
4. Wengi wa viongozi waliounda vyama vya upinzani kwa sababu moja au nyingine ita kuwa wali fikiria kwamba CCM ita shindika kiurahisi. SI ajabu baadhi yao wakadhani kwamba 1995 wange kiondoa CCM madarakani. Kwa maana hiyo basi vyama hivi vya upinzani vilivyo anzishwa vilikua havina mipango ya muda wa kati au mrefu kwa maumaini kwamba uchaguzi una kuja na wao wata shindda. Mpaka leo hii sioni mipango ya kueleweka ya muda mrefu wa chama chochote cha upinzani.
Kwa hiyo basi kama vyama vya upinzani kweli vina taka kushinda basi ni lazima kuwepo na mabadiliko. Lazima waletwe vijana ambao watakua katika mfumo wa vyama vyao. Lazima walete watu ambao hawaku wahi kuhusika na CCM ili kuleta mawazo na fikira tofauti. Ni lazima waji tazame na wajiunde upya. Kusema ukweli sioni chama cha upinzani kati ya hivi vilivyopo sasa kufanya mabadiliko yoyote ya kisiasa labda vyama vipya vita kapo anzishwa au viongozi wa sasa waliotoka kwenye mfumo ule ule, mawazo yale yale na mafunzo yale yale wakija kuondoka.
Ndugu wana JF tuna muda mrefu bado mpaka upinzani wa kweli Tanzania uibuke. Leo hii hatuna wapinzani bali wasindikizaji. Kwa maana kila kabla ya uchaguzi tayari imesha julikana chama gani kita shinda uraisi na chama gani kita kuwa na wabunge wengi Bungeni. Huo si upinzani.