Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Nothing good will come out of politics...nashangaa watu wanavoumiza vichwa vyao kwene solution ambayo haijawahi kuwa proven popote. Pretty absurd indeed.
 
I have said this before and I will say it again, majina ya vyama vya wapinzani should only be on paper lengo lao liwe 1 permanently getting rid of CCM. Hii haitawezekana kama wapinzani watapondana na kurushiana maneno kila wakati.

Naam wewe umeeleweka vizuri Chadema inaihitaji Cuf na CUF inaihita Chadema na wanaposhindwa kukubaliana wakubliane hivyo sio kushutumiana hakuna mpinzani wa mwenzie wote lengo ni moja kuing'oa CCM
 
Kwa nini unatilia mashaka kuhusu wanaCUF ndugu?

Wakati Chadema wanaendeleza harakati za kuiondoa CCM madarakani, CUF kwa upande wao wanalilia na wao kuingia madarakani kwa kushirikiana na CCM kwa kinachoitwa serikali ya mseto. Hivyo kwa vyovyote vile lazima waendeshe upinzani dhidi ya Chadema ambao hata harufu ya CCM hawataki kuisikia. If you cant fight them, join them na maadam CUF wameamua kushirikiana nao, hayo madai ya kuing'oa CCM ni usanii tu, period. Ukishirikiana na mwizi ujue na wewe ni mwizi tu.
 
Jamani, hebu tuna nini vichwani mwetu, huu ugomvi wa CHADEMA NA CUF, mbona inafahamika siku nyingi? kuwa CUF wanaona kama wanapokwa na kukimbiwa na wapiga kula?
 
Mara kadhaa nimeona wapenzi/washabiki/wanachama wa CUF wakikishambulia CHADEMA kuliko vyama vingine ikiwemo hata CCM!

Mfano mzuri ni uchaguzi mdogo wa Mbeya Vijini ambapo CUF kiliweka pingamizi dhidi ya mgombea wa CHADEMA, Shitambala. Pamoja na mgombea huyo kujitoa bado CUF kiliendelea kukilaumu CHADEMA ambacho kilikuwa nje kuliko CCM ambayo walibaki nayo kuchuana. Humu JF tumeona thread zikidai kuwa CUF ina sifa kadhaa ukilinganisha na CHADEMA! Sijui kwa nini walinganishe na CHADEMA badala ya TLP, NCCR, etc?

Swali la kujiuliza: Hivi CUF ni chama cha upinzani kwa CHADEMA tu?
Mkuu nadhani hapa unapotosha kidogo..Mimi na wewe hatufahamu kilichotokea baada ya vyama hivi kufikia maafikiano kisha wakageukana..Ni baada ya kugeukana, sijui kama CCM ilihusika au laa ndipo vyama hivi zilianza mashambulizi baina yao wenyewe kwenye hizi chaguzi ndogo. Nakumbuka ni Chadema waliweka mgombea Mbeya vijijini dhidi ya CUF....Chadema pia waliweka mgombea somewhere huko usukumani dhidi ya TLP na Mrema akapiga kelele sana. CUF na TLP nao wakaweka wagombea wao huko Tarime na sehemu mbili nyingine za Chadema.
Kati yao nani aliyeanzisha uhasama huu hata sielewi....Lakini wote walidai sababu kubwa ni kuwepo kwa Mapandikizi ya CCM ndani ya chama cha mwingine.
Je, kuna ukweli hilo ndio somo jipya!
 
Jamani nashukuru tunalizungumzia swala hii na tunawataka Dr. Slaa na Seif Sharifu watupe majibu na kutuhakikishia kwamba upumbavu wa kupigana vita wenyewe kwa wenyewe haupo. Prf Lipumba mwalimu wangu alishapoteza muelekeo siku nyingi kwa tamaa ya urais. Pamoja na kwamba tunafahamu kuwa ama kwa mtazamo ama kwa sababu binafsi watu kama kina Jussa siwakuaminika katika mapambano haya kwa kuwa wamekua wakitumika na kuendelea kutumiwa na CCM kupitia kwa mafisadi. Kwa hiyo Jussa hawezi kusema lolote na hili liko wazi, ndio hapa pa kujiuliza je CUF ni kweli chama cha upinzani ama pandikizi la CCM. Mfano uliotolewa wa mbeya vijijiji kwenye uchaguzi mdogo ni wamaana pale ndipo nilipowadharua sana sana CUF huku wakijua kabisa hawana nguvu bara walidhoofisha chadema kwa faida ya CCM, unless kama wanatumabia hawana akili za kujua nguvu na udhaifu wa chama chao
 
ipo siku mtaujua ukweli,maana nyinyi wenyewe wana chadema mara mnaongea Zitto anatumiwa na ccm,mara mbowe,mara slaa,hizi ni kauli zenu wenyewe,nakumbuka hata wakati wa uchaguzi wa chadema Slaa alitamka wazi kuwa tuna viongozi wanatumiwa na ccm,sasa karibu litapasuka la kupasuka. wana Cuf huwasikii kusema Lipumba au maalim au duni wanatumiwa,bali Cuf wakiona tu kidudu mtu tayari wanamfatilizia na wakiona ukweli basi wanamshusha cheo kwa utaratibu hatima yake mwenyewe anajiondoa,tumeona kina hiza na tambwe na wengine... ukiangalia ugomvi wa chadema na cuf ulianza kwa chadema kuwageuka cuf na humu humu tulijadiliana baada ya Slaa kutamka hadharani kuwaambia Cuf.. SASA UPEPO UMEGEUKA. cuf ndio wakashtuka alaa! Tulidhani hawa wenzetu kumbe si wenzetu,hapo cuf nao wakaanza kujibu mapigo, na hata TLP wakawasusia chadema kwa kusema wanageuka wenzao.
 
CUF vs CHADEMA, ngoja tusubiri tena uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu!
 
Mi ninavyoamini haukuna ugomvi wala upinzani kati ya CUF na CHADEMA ni CCM tu hao wanaojaribu kuzusha zusha na kuleta uchonganishi kwa makusudi ya kudhoofisha vyama hivi ambavyo vinashirikiana vizuri katika kujenga siasa za ushindani, sijapata kuona hitilfu wa switafahamu za hivyo baina ya vyama hivi, tungewaomba nyinyi CCM mtazame ya kwenu zaidi kuliko ya wenzenu, yenu mengi tu hamuyaoni, mnaghushi, mnaiba, mnafanya kila ufisadi...hamuoni kuwa huu ni ugomvi kati yenu na wananchi mnaojidai wamekuchaguweni kwa kukubali ilani yenu...?
Shughulikeni na hayo kwnza ya CUF na CHADEMA hamuyawezi wakati ya CCJ hata hayajakaa vizuri yanawakosesha usingizi.
 
Mi ninavyoamini haukuna ugomvi wala upinzani kati ya CUF na CHADEMA ni CCM tu hao wanaojaribu kuzusha zusha na kuleta uchonganishi kwa makusudi ya kudhoofisha vyama hivi ambavyo vinashirikiana vizuri katika kujenga siasa za ushindani, sijapata kuona hitilfu wa switafahamu za hivyo baina ya vyama hivi, tungewaomba nyinyi CCM mtazame ya kwenu zaidi kuliko ya wenzenu, yenu mengi tu hamuyaoni, mnaghushi, mnaiba, mnafanya kila ufisadi...hamuoni kuwa huu ni ugomvi kati yenu na wananchi mnaojidai wamekuchaguweni kwa kukubali ilani yenu...?
Shughulikeni na hayo kwnza ya CUF na CHADEMA hamuyawezi wakati ya CCJ hata hayajakaa vizuri yanawakosesha usingizi.
Tusubiri vitendo, sio maneno tu ndugu yangu! CCM Zenj na CUF ndio wanalala ndani ya net moja sasa hivi! Madaraka matamu acha mchezo bwana!
 
Profesa Lipumba: Ah, Ushirikiano bado upo. Kwa mfano, ushirikiano wetu na TLP na NCCR Mageuzi bado mzuri sana. Lakini bado hatujajiweka vizuri pia katika Bunge.
Wabunge wetu bado wanaendelea kushirikiana, kambi ya upinzani bado inaendelea kuwapo kwa hiyo hatujayaweka mambo haya uzuri kwamba kanuni zetu ziwepo. Halafu pale tatizo jingine (CHADEMA) wameshafikia maamuzi kwamba hawawezi kushirikiana na vyama vingine.
Hilo ni wazi kwamba wao (CHADEMA) kushirikiana na NCCR-Mageuzi wanaona kwamba hilo ni jambo haliwezekani au kushirikiana na TLP ni jambo ambalo haliwezekani. Sasa katika hali hiyo ya kutoaminiana, sintofahamu hiyo inakuwa mbaya.
source
Haki Sawa kwa Wote

Kwa maana hiyo, upo uwezekano wa kushirikiana na CUF bila shaka!
 
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labor (TLP), Augustine Mrema, ameibuka katika Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma na kugeuka kivutio pale alipomsifia Rais Jakaya Kikwete kwa utendaji bora wa kazi, huku wakiwashutumu wana-CCM wanaomtuhumu na kupendekeza atoswe.


Mrema alijikuta akishangiliwa mara kwa mara na wajumbe wa mkutano huo, kisha kikundi cha uhamasishaji cha CCM (TOT) kikapiga wimbo wenye maneno yanayosema `wembe kupita ule ushindi, wembe kupita ule ushindi’ wakati kiongozi huyo wa TLP akizungumza.


Wimbo huo uliwafanya wajumbe wa mkutano huo kwenda mahali alipokuwa amesimama Mrema na ambaye kwa wakati huo alikuwa anacheza, wakampongeza kwa kumshika mikono na kumtuza fedha ambazo idadi yake haikujulisha mara moja.


Mrema alisema, Rais Kikwete, amefanikiwa katika mambo mbalimbali ya kijamii hususan vita dhidi ya ufisadi, rushwa na maovu mengine.
Wakati Mrema akisema hayo, Rais wa awamu ya pili na ambaye alimshinda Mrema katika Uchaguzi Mkuu wa 1995 na 2000, Mzee Ali Hassan Mwinyi, alikuwa akifurahi, kucheka na mara nyingine kupiga kofi mezani.


Mrema alisema ufisadi, rushwa na vitendo viovu vilikuwepo nchini tangu enzi za tawala zilizopita, zikiwemo za Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, lakini hakuna kiongozi ama mwanachama wa CCM aliyependekeza viongozi hao watoswe kama inavyofanyika kwa Kikwete.


"Inashangaza kuona hivi sasa linaibuka kundi la wana-CCM wanaojenga hoja ya kumtaka Rais Kikwete kuchukua uamuzi mgumu dhidi ya uovu, jambo hili lina mrengo wa kumuonea kiongozi huyo wa nchi" alisema.


Ingawa Mrema hakuwataja wana-CCM waliopendekeza Rais Kikwete kuchukua uamuzi mgumu, lakini Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, aliyehudhuria mkutano huo, aliwahi kukaririwa akitoa pendekezo hizo.


Huyu na Dokii wana tofauti gani?
 
Kama anakubali JK anafanya vizuri kila kitu, anafanya nini upinzani? Au hajui analosema??
 
Mkuu NN, kwa kweli upinzania Tanzania unasikitisha sana. Huyo Mrema na Cheyo wameshadhihirisha kwamba wao ni mamluki wa CCM na walijifanya ni wapinzani ili kuhakikisha wanavuruga juhudi zozote za upinzani kujiimarisha ili kuiondoa CCM madarakani. Kwa hali hii ya CCM kuwapandikiza mamluki miongoni mwa wapinzani, itawachukua wapinzani miaka mingi ijayo kuweza kujiimarisha na kuweza kupambana na CCM, nilikuwa naupinga sana ule usemi kwamba CCM itatawala Tanzania milele lakini sasa naona una ukweli kutokana na njama za CCM kufanya kila wawezalo ili kuudhoofisha upinzani.

Miaka ya nyuma nilikuwa namheshimu sana Mrema hasa kwa kusimamia kikamilifu kampeni ya kusafisha jiji la Dar na kuliweka safi na pia utendaji wake alipokuwa Waziri lakini sasa hivi nimemdharau mno kanitoka kabisa.
 
Kama anakubali JK anafanya vizuri kila kitu, anafanya nini upinzani? Au hajui analosema??

Aliwahi kusema mtu huyu huyu wakati huo yeye ni hot sana kuwa chama chochote nia yake ni kuingia ikulu ajabu leo anipigia debe CCM. Halafu akaona kuwa amepata jukwaa la kuombea kura za ubunge, jamaa kamjibu flat na sisi tuna weka mgombea mtu.
 
Mkuu NN, kwa kweli upinzania Tanzania unasikitisha sana. Huyo Mrema na Cheyo wameshadhihirisha kwamba wao ni mamluki wa CCM na walijifanya ni wapinzani ili kuhakikisha wanavuruga juhudi zozote za upinzani kujiimarisha ili kuiondoa CCM madarakani. Kwa hali hii ya CCM kuwapandikiza mamluki miongoni mwa wapinzani, itawachukua wapinzani miaka mingi ijayo kuweza kujiimarisha na kuweza kupambana na CCM, nilikuwa naupinga sana ule usemi kwamba CCM itatawala Tanzania milele lakini sasa naona una ukweli kutokana na njama za CCM kufanya kila wawezalo ili kuudhoofisha upinzani.QUOTE]

Halafu mnasema wapinzani waungane what is common amongst you ? CCM wamefurahi kila mtu leo mkutanoni anasema hata upinzani unamkubali inabidi waelewe kuwa Mrema sio mpinzani hata siku moja
 
There is nothing like chama cha upinzani cha kweli Tanzania. All what pretends to be opposing CCM are there to fulfill the international requirements for enhancing democracy in the country. Otherwise they are all fun of CCM.
 
Halafu mnasema wapinzani waungane what is common amongst you ? CCM wamefurahi kila mtu leo mkutanoni anasema hata upinzani unamkubali inabidi waelewe kuwa Mrema sio mpinzani hata siku moja
Mkuu kwani CCM wakifanya jambo jema huwezi kuwasifia?
 
Mkuu kwani CCM wakifanya jambo jema huwezi kuwasifia?


Kuwasifia kama wamefanya kitu cha maana lazima, hiyo sikatai asilani, lakini Paster hebu nitajie vitu tisa vya kusifia. Usiseme chuo kikuu Dodoma maana lile ni time bomb hela ya wafanyakazi imetumbukizwa kwenye ule mradi sio hela ya serikali ile. Ukishanipa hivyo tisa naomba uelewe kuwa ambacho mrema anasifia CCM ni "Kupambana " na ufisadi sidhani kama Agustino alikuwa serious.

Kati ya malalamiko kadhaa ya ufisadi ni kesi chache tu zimeokotwa na kupelekwa mahakamani, na kati ya hizo ni moja tu imekwisha na na mshtakiwa amefungwa ( kama tutayaita hayo ni mafanikio) kuna ngazi mbili za rufaa vipi huyo aliyefungwa akiachiliwa katika moja kati ya ngazi hizo? Bado tutasema kuna mafanikio?

Mafanikio ya kupambana na ufisadi si wingi wa kesi bali ni kuwafanya wananchi ( hasa viongozi) waogope vitendo vya kifisadi, yaani kutibu kabisa hii kansa ya Rushwa ambayo inaangamiza jamii hapo na mimi ningesifia kwa nderemo na vifijo lakini sio kwa wingi wa kesi au ukweli kuwa waziri kafikishswa mahakamani hicho sio kipimo kabisa.
 
Back
Top Bottom