Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Kwanza ubunge wenyewe aliupata kwa nguvu ya CHADEMA, hana hata uwezo wa kujenga hoja....huko ndiko anakokimbilia kwenye mwisho wake. CUF na Tarime wapi na wapi bwana....bye bye Mwera!
 
Msaliti! yafaa jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake na atoswe baharini.

Chonde wakulu .......KISA TU AMETOKA CHADEMA NDO AFUNGIWE JIWE NA ATOSWE BAHARINI....?JE AKIWAKWAZA MOJAWAPO YA WADOGO HAWA AFANYWEJE?
 
chonde wakulu .......KISA TU AMETOKA CHADEMA NDO AFUNGIWE JIWE NA ATOSWE BAHARINI....?JE AKIWAKWAZA MOJAWAPO YA WADOGO HAWA AFANYWEJE?

Mkuu inafahamika wewe na kada mkubwa wa chama cha mafisadi.
Unashauri nini kifanyike ili uondokane na uliyoweka kwenye signature yako?
 
Cha msingi ameenda CUF na sio kwa wazee wa chukua Chako Mapema
 
Baadhi ya watu humu wana chekesha. Mtu Aki hama chama chake na kwenda Chadema kila mtu humsifia na kumuita mpiganaji na hutetewa kwa nguvu zote akisemwa vibaya. Mtu akikihama Chadema na kwenda chama kingine watu ghafla wanamponda au kuwa neutral. Wengi tumesema tokea mwanzo tatizo la watu kuhama hama chama haswa wakati wa kuelekea uchaguzi baada ya teuzi mbali mbali lakini inaelekea "umalaya" wa kisiasa ni tatizo pale tu mtu anapo hama chama fulani au kwenda chama fulani.
 
avatar16950_1.gif

Kama unamtoto nyumbani analilia bila mpango nadhan ukimwonesha hii avatar anyamaza mara moja kulia..duh !
 
13yidrl.jpg


tukiweka ushabiki wa vyama vyetu kando. Hivi wanasiasa wanalengo kweli la kuleta ukombozi tanzania au ni maslahi binafsi? Maana jimbo limesharudi kwa wenyewe.


Ndugu umechelewa wapinzani ni matapeli wenghi wanafwata ulaji ndio maana ukigusa hata baadhia ya ndugu ama jamaa wa wahusika uchelewi kutukanwaa ama kuonywa na mtu mkubwa tu wale wanajua wanachofanya.
 
Ata wewe ukionja utotaka kutoka kule anejua siri yake ni alieonja tu
 
mkuu inafahamika wewe na kada mkubwa wa chama cha mafisadi.
Unashauri nini kifanyike ili uondokane na uliyoweka kwenye signature yako?

Soma baibo vizuri katika zab

Dont touch my annointing angalia maneno yako yasikuaribie maisha kumbe umemgusa masihi wa mungu



ole
 
Ni nani asiyejua kuwa wapinzani wanatumia muda, rasilimali na jasho lao kwa kipindi kikubwa sana ili kuikomboa nchi yetu kutoka katika madudu ya wasioipendea mema nchi na wananchi wake bali waliotayari kujineemesha wao na familia zao?

Tuchukue mfano mrahisi, wakati mimi na wewe tukienda kazini kwa ajili ya familia zetu na maisha yetu binafsi, kuna wakina Freeman Mbowe, Wilbroad Slaa, Zitto Kabwe, na wengine weeeengi ambao wanatumia muda wao mwingi kuzunguka huku na huko kuwaamsha watanzania wengi waliolala waone jinsi gani wanadhulumiwa haki zao.

Cha kushangaza, hatuwaungi mkono watu hawa, inafika kipindi watu hawa wanaingia mifukoni kutoa chochote kwa ajili ya mpambano huu. Badala yake wengi wetu tunawakejeli na kuona ni haki yao na ni wajibu wao kufanya hivi!

Hii ni aibu kabisa! Itakuwaje wao nao wakaamua kutundika daluga na kuamua vision zao ziwe kwenye familia na maslahi yao binafsi? What if wakiamua upinzani sasa basi, kama ndo imekuwa hivi basi acha iwe kila mmoja afe na lake? Unafikiri katika miaka kumi kutakuwa na Tanzania tena?Mmeliona hili?
What if na wenyewe wangeamua: Sasa basi, acha na wao wakubali fulana za kijani na njano na wapokee hizo takrima za chini chini washabiki wa ccm wanazopewa kwa sasa?

Cha ajabu sana, watanzania wanasahau mapema kweli kweli. Juzi tu hapa, wapinzani hawa tunaowakejeli leo wamefanya kazi nzuri sana bungeni hatimaye tukaona kilichokuwapo EPA na RichMond, leo hii watanzania wanajidai wamesahau. TUCTA nao watu wa ajabu sana, juzi walikuwa na mwelekeo huu, leo out of blue wanamwelekeo wa kiaina fulani. Media na yenyewe, juzi juzi ilikuwa na uzalendo, leo hii naona wameanza kuwa na mwelekeo wa U-CCM.

Ninajiuliza, unafikiri tunawakomoa wapinzani? Unafikiri ni wajibu wa wapinzani kumwagika jasho ili nchii hii iwe ya neema hapo baadaye?

Wangapi leo hii mnashabikia tu sera ya kilimo kwanza na ongezeko la bajeti ya kilimo wakati ki-uhalisia ukichambua hicho kitu hakipo? (Dr Slaa aliwachambulia vizuri - mchango mwingine wa upinzani makini kwa hatima ya nchi hii)

Kama watanzania wanafikiri ni muda wa kuwakomoa wapinzani, basi wajiaandae na maumivu zaidi.
CCM ni wataalamu wa kuuma na kupuliza, leo wanapuliza, ngoja uchaguzi upite tuwaone!
Leo hii fedha ya Tanzania inashuka thamani kila kukicha, kwenye mzunguko wa fedha leo hii, Tsh. elfu kumi na Elfu tano (noti kubwa) zimekuwa za kawaida kuwepo kwenye mzunguko wa kawaida kabisa wa maisha hata yale ya kawaida sana. Ndio maana hadi kesho, watanzania mishahara haitatosha na gharama za maisha zitazidi kwenda juu kila kukicha.

Wizi wizi wa mali za umma, na ubadhirifu utazidi kuongezeka, tusitegemee mapya kutoka kwa CCM.
na sitashangaa sana, ifikapo mwaka kesho katikati, watu wataanza kulalamika tena kuwa serikali ni mbovu ilhali katika uchaguzi walikubali kurubuniwa.

Angalia wasanii majuukwaani wanavyoimba kinafiki? Mimi sina jingine zaidi ya kusikitika. Ni lini watu hawa wooote watafunguka macho na kuona magumu na mazito yanayoikabili nchi yetu chini ya CCM?Akili ipo kichwani mwako, fanya maamuzi sahihi mwananchi
 
Kweli CUF chama mbadala tena hivi karibuni tu kitaitw chama tawala
 
Mwayaona ya Mbeya tu mbona msemi kilichotokea TUNDURU wakati wa uchaguzi mdogo CHADEMA walipomsimamisha msaliti SHAIBU AKILOMBE kuipinga CUF!!
Jamani nashukuru tunalizungumzia swala hii na tunawataka Dr. Slaa na Seif Sharifu watupe majibu na kutuhakikishia kwamba upumbavu wa kupigana vita wenyewe kwa wenyewe haupo. Prf Lipumba mwalimu wangu alishapoteza muelekeo siku nyingi kwa tamaa ya urais. Pamoja na kwamba tunafahamu kuwa ama kwa mtazamo ama kwa sababu binafsi watu kama kina Jussa siwakuaminika katika mapambano haya kwa kuwa wamekua wakitumika na kuendelea kutumiwa na CCM kupitia kwa mafisadi. Kwa hiyo Jussa hawezi kusema lolote na hili liko wazi, ndio hapa pa kujiuliza je CUF ni kweli chama cha upinzani ama pandikizi la CCM. Mfano uliotolewa wa mbeya vijijiji kwenye uchaguzi mdogo ni wamaana pale ndipo nilipowadharua sana sana CUF huku wakijua kabisa hawana nguvu bara walidhoofisha chadema kwa faida ya CCM, unless kama wanatumabia hawana akili za kujua nguvu na udhaifu wa chama chao
 
Wijwijwij :becky:,bwa ha ha haa ha ,kha !! Sasa hivi CUF ni chama kikuu cha upinzani sio Tanzania tu bali hata east africa ,ni Chama ambacho kinajulikana hadi ndani ya UN au umoja wa Mataifa kutokana na tifu zake, ila ninyi wengi wenu ni wepesi wa kusahau kwani CHADEMA ni chama cha umimi ,sisi tu ,

Yaani CHADEMA ni watu wa majigambo na kwa jinsi wanavyojisahau hujiona akuna kama wao ,hivyo pale wanapohitajiwa kuwa wakae pembeni ,huwa hawaamini kuwa katika eneo hilo wao hawana wateja na hawana nguvu ,kumbukeni tu kule Tarime CHADEMA waliachiwa na zaidi hata nguvu za wanachama wa CUF zilitumika katika kuisaidia CHADEMA na kufanikisha kuiangusha CCM ,ila wanapotakiwa na wao wakae pembeni na kusaidia ubavu ndipo wanapozua mbinde na mijineno kibao ya kujilabu.

:mad2: Data za chaguzi zote zinaonyesha bado CUF ni tishio kwa CCM na wenyewe CCM wanalielewa suala hilo ,CCM wanaelewa kuwa kizingiti kikubwa ni CUF na hawa wengine si lolote si chochote ,palipo na CUF basi CCM yupo tayari kuuwa kutumia kila kitu vikiwemo vyombo vya dola vya aina zote ,hapo panatosha kukutanabahisha kuwa CUF sio Chama cha kulumbana kwenye viriri vya majukwaa. Kama tulivyoona CHADEMA na maguruneti yao ya ufisadi ,hivi hapa tulipo tujiulize CHADEMA wamifika wapi ??? Au wamefikia wapi ???

:A S 100: Ni rahisi mtu kusema sijui kuna kesi zinaendelea zote ni sababu ya CHADEMA na CUF wamefanya nini kubwa ? CUF ni chama chenye mawazo endelevu na uwono wa mbali kinajua fika wakati wa kurusha maguruneti na yakajeruhi ,wakati ambao haujafika,,,,, ukirusha sassa hivi yote yatafulia kama yalivyo fulia ya CHADEMA.[/QUOTE
Wafumbue macho. na kwa kuthibitisha hayo,hivi juzi tu tumesikia takriban viongozi wa Cuf 138,ikiwemo asilimia 74 ni viongozi wa kuchaguliwa na wananchi ktk serikali za mitaa na vitongoji,na walobaki wengi wanatarajiwa kugombea ktk uchaguzi ujao wamesekwa ndani na tena hata dhamana hawakupewa na hawana kesi yoyote. hebu niambieni kuna wa chadema aliesekwa ndani? nani tishio kwa ccm? je chadema ni ccm b?

kumbuka mlivyosababisha watu wakafa Pemba na seif akakimbia uarabuni, wapemba wakaenda ukimbizini na majambia yao, ni lini CUF itaacha kujipambanua kama chama cha udini?
 
Ni miezi michache imebaki kuelekea uchaguzi mkuu wa Tanzania.Vyama
vimejikita katika kampeni meneo mbalimbali na hali bado ni ya amani
huku kila chama kikinadi sera zake.Toka Tanzania imeingia katika mfumo
wa vyama vingi mwaka 1992,kuja uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi
(formal 1st multiparty election in Tanzania) ambapo Augustine Lyatonga
Mrema wakati huo akiwa NCCR Mageuzi hadi leo kuna ukweli ambao
wapinzani wameshindwa kutueleza kama watanzania.Kampeni nyingi
zimekuwa za lawama zaidi dhidi ya Chama tawala badala ya kutueleza
sisi kama Watanzania ni kitu gani wao kama wapinzani watafanya
kuendeleza nchi.Again,mwaka 2005 Freeman Mbowe wakati huo akigombea
uraisi aliainisha katika ilani yake kwamba angependa serikali ya
majimbo (ikumbukwe kwamba wakati huo huo Taifa lilikuwa na tatizo na
mpasuko huko Zanzibar).Historia inaweka wazi ni muda gani nchi inaweza
kuchukua kubadili katiba kuwa na federal governement.Huu ni
mkanganyiko wa pili ambao Freeman Mbowe alitaka aliletee taifa katika
wakati ambao tayari tulikuwa na mambo ya msingi kabisa kufanya.Again
upinzani umeshindwa kuwaambia watanzania ni kwa nini wameshindwa
kujiunga pamoja kupata angalau robo ya kura za CCM katika uchaguzi
wowote ule!And let me stress this,this is not about a party,am talking
about a nation with people who are lying at zero assurance of
accountability to people and to put things worse ndani wapo vijana
wadogo ambao wanaburutwa bila kuelewa ukweli wa mambo.Hivi kweli
unashabikia mtu anayekutaka uamini kwamba the increase in export and
overseas trade in USA and the west (which is one of the major causes
of the fall of our currency stability against the mentioned
currencies) kuwa ni uzembe wa serikali!!!!People,someone,somewhere
within the so called vyama vya upinzani is not telling the truth kwa
sababu anazozijua yeye.At times,all that a student needs is not a new
school uniform but taking a good care of what he/she has.

-Nimeweka majadiliano hayo katika mtandano wa wanajamii ili kutanua uwanja wa majadiliano,come up with critical views,otherwise just read-
 
Kama niliwahi kusema kuwa Chadema ni CCM ushahidi wa wazi ni huu hapa:-

...Kasinga alijitosa katika kinyang'anyiro hicho kwa lengo la kupambana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye anatetea ubunge kwa tiketi ya CCM.

Akizungumza na gazeti hili juzi, Kasinga alisema uamuzi wake wa kuchukua fomu katika jimbo hilo ulizua mvutano mkubwa ndani ya Chadema na hata aliyekuwa mbunge wa Mpanda Kati, Said Arfi (Chadema), kutangaza kujitoa katika uchaguzi iwapo chama chake kingesimamisha mgombea Katavi.

Hali hiyo pia ilisababisha Mwenyekiti na Muasisi wa Chadema wa Wilaya ya Mpanda, Juma Mnusi, kujivua uanachama na kuhamia NCCR-Mageuzi na chama hicho kumteua kugombea udiwani katika kata mpya ya Makanyagio.

Hata hivyo, chanzo cha uhakika cha habari kutoka ndani ya Chadema, kilieleza kuwa chama hicho ndicho kilichokuwa kikishinikiza Pinda apite bila kupingwa katika jimbo hilo, lakini baadhi ya viongozi wa CCM walikuwa wakitaka awepo mgombea ili wapate fedha za kampeni.

Hali hiyo pia inadaiwa kusababisha kutofautiana na Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Mohamed Nyawenga, aliyeonekana akifanya juhudi za kweli kuhakikisha Pinda anapita bila kupingwa.
 
Back
Top Bottom