Nini hasa kimeondoa Corona Tanzania?

Nini hasa kimeondoa Corona Tanzania?

Corona ipo!

Ila ni vigumu kutuathiri sisi Watanzania kwa sababu sisi vyakula vingi tunavyokula ni fresh ukilinganidha na wazungu hivyo vina kinga kubwa yani vinatumika kama dawa. Ukitaka kuamini hii pointi chukua mfano kutoka South Africa na Egypt ni nchi ambazo ziko mbele sana kimaendeleo na hata Corona zimeathirika sana. Sisi Corona kuja ituathiri ni nadra sana tunatumia dawa Kama chakula
 
Hakuna kitu kama hicho. Corona inatandika Afrika kama kawaida, issue ni vile nchi nyingi za kiafrika hazipimi wala kutoa taarifa sahihi za kitakwimu.
Wengi wanapata maambukizi ya corona lakini si wote wanakua wagonjwa mahtuti. Wanaoingia na magonjwa sugu na wazee ndiyo walio kwenye hatari kubwa.

Jamii za Wahindi ziliathirika sana kwakua wengi wanaishi na magonjwa ya moyo na kisukari.

wazungu wengi wazee na waagonjwa wenye kifua cha mshipa ndiyo pia wanene wengi ndiyo walipata madhara.
 
...HAKUNA MWENGINE,yeye ndiye anatufanya hata sasa tunaishi kwa amani.kama hili suala lingekuwa siasa tusingeyaona yanayofanyika Tanzania kama sasa CCM kufanya vikao vyao kwenye kumbi sealed huku hakuna hata mmoja aliyevaa barakoa,refer kikao kikuu Dodoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tena na Rais mwenyewe anasalimia watu kwa kushikana mikono kabisa.
 
Wengi wanapata maambukizi ya corona lakini si wote wanakua wagonjwa mahtuti. Wanaoingia na magonjwa sugu na wazee ndiyo walio kwenye hatari kubwa.

Jamii za Wahindi ziliathirika sana kwakua wengi wanaishi na magonjwa ya moyo na kisukari.

wazungu wengi wazee na waagonjwa wenye kifua cha mshipa ndiyo pia wanene wengi ndiyo walipata madhara.

Sisi hatuna wazee? Wenye kisukari na magonjwa ambukizi? Mbona hatuna matatizo waliyonayo sehemu nyingine?
Nani aliyekuwa anafagilia kufungiwa ndani? Imemsaidia nani globally?
 
Hello JF,

Ningependa kujua out of curiosity, nini kimeiondoa corona Tanzania? Je, Nyungu ilisaidia? Watu kuhimizwa kula tangawizi na malimao?

Na watu wakachukulia serious kula tangawizi na malimao. Hivyo miili yao ikajijenga ku-fight virus? Ama watu walichukulia serious kuosha mikono na kuvaa barakoa hivyo rate ya maambukizi ikapungua? Nini hasa kilichoiondoa Corona Tanzania?

Its good to know, ili janga liingine likija, we use the same strategies.

Ni Taifa lililobarikiwa katika Nyanja nyingi na Baba Muumba Mwenyezi Mungu lakini hata Rais JPM wa Tanzania nae ana ' Baraka ' kubwa za Mola.
 
Ndugu yangu ukiamini kuwa corona imeondoka Tanzania utakuwa unaamini ndivyo sivyo kama ulimfuatilia Dr. Janabi wa Taasisi ya moyo ya Jakaya kikwete alizungumza vizuri sana kuhusu hili na alisema asilimia kubwa wataugua na watapona na asilimia chache watalazwa na kupona na asilimia chache pia watalazwa na kufariki sikumbuki exactly figure lakini alisema haya ukitafuta hii habari utaelewa kwani kinachokuaminisha imeisha sio kipimo sahihi cha kujua kama ugonjwa upo au laa( nakushauri endelea kuchukua tahadhari).

Ni kweli Mwenyezi Mungu anatusaidia sana kwenye mambo mengi na hatupaswi kuacha kumwomba kila uchwao lakini naomba tusijiinue kwenye hili suala kwani hata mataifa mengine wanaomba Mungu kama watanzania wanavyoomba hivyo basi tuendelee kumwomba kila siku sio kwa sabab ya korona tu ila kwa kila jambo ( endelea kuchukua tahadhari corona haijaisha).

Kuhusu ndugu na majirani kufa wengi wanasema hakuna hata jirani yao amekufa lakin mim nina ushahidi usio rasmi sis huwa tunapewa taarifa kupitia email ya ofisi mfanyakazi anapofiwa na mke/ mume/ mtoto / baba/mama na wakwe kiukweli pamoja na kwamba taasisi ina wafanyakazi zaidi ya 4000 kwa sasa taarifa ya vifo imeongezeka kwa siku unaweza kuona mpaka email 10 kuhusu misiba tofauti na zamani hii inamaanisha nin? ( endelea kuchukua tahadhari corona bado haijaisha)

Sina uhakika sana na wanaosema kuhusu nyungu, malimao, swaumu na vinginevyo kwani ninachojua kitaalam vitu vyote hivyo vina madhara mwilini endapo vitatumika ndivyo sivyo; Nyungu mtalaam Ndungulile alishaizungumzia, limao kwa sabab ya acid nyngi ni chanzo kizuri cha vidonda vya tumbo na sasa mtu yeyote mwenye ndugu ambaye ni dr. aongee nae kesi za vidonda vya tumbo zimekuwa nyingi ghafla mahospitalini. Kitunguu swaumu nacho kinafanya kazi sawa na ( warfarin ) hii ni dawa ya kuyeyusha dam waliowahi kuugua thrombosis watakuwa wananielewa vizuri hapa hivyo ukitumia hivi vitu kuwa makini sana.( endelea kuchukua tahadhari korona bado ipo)

Naungana na mkuu mmoja amessema korona haijaisha tumeondolewa hofu tuu, kwani ingekuwa akifa mtu anapimwa na watu wanapewa majibu kama wanavyofanya hapa Kenya naamini comments nyingi kwenye huu uzi zisingekuwepo , Namsihii mkuu mmoja aliesema wanakufa wazee achunge kauli zake kwani hata wao walikuwa vijana na kiasili kila binadam anapenda kuishi ( endelea kuchukua tahadhari korona haijaisha).

Mwisho naomba wote waliochangia kuwa imeisha wanisaidie wametumia kipimo gani kujua kuwa imeisha?
Watu wanaangalia jinsi hii mikusanyiko iliyopo tena bila tahadhari zozote ni wazi hali hii ingesababisha maambukizi mengi hivyo wengi wangekuwa wanaugua na hivyo hata kama wanapona ila ingewatia woga kujua corona bado ipo na ina athari hivyo wasingeendelea kujiweka kwenye mikusanyiko isiyo ya lazima tena bila tahadhari. Jambo hilo ndio linafanya watu kuona corona imeisha.
 
Corona ipo!

Ila ni vigumu kutuathiri sisi Watanzania kwa sababu sisi vyakula vingi tunavyokula ni fresh ukilinganidha na wazungu hivyo vina kinga kubwa yani vinatumika kama dawa. Ukitaka kuamini hii pointi chukua mfano kutoka South Africa na Egypt ni nchi ambazo ziko mbele sana kimaendeleo na hata Corona zimeathirika sana. Sisi Corona kuja ituathiri ni nadra sana tunatumia dawa Kama chakula
Kenya wanakula nini?
 
Hello JF,

Ningependa kujua out of curiosity, nini kimeiondoa corona Tanzania? Je, Nyungu ilisaidia? Watu kuhimizwa kula tangawizi na malimao?

Na watu wakachukulia serious kula tangawizi na malimao. Hivyo miili yao ikajijenga ku-fight virus? Ama watu walichukulia serious kuosha mikono na kuvaa barakoa hivyo rate ya maambukizi ikapungua? Nini hasa kilichoiondoa Corona Tanzania?

Its good to know, ili janga liingine likija, we use the same strategies.
Mungu ametuhurumia wajinga wake, sasa watu wanapeana mikono kama kawaida.
Jambo kubwa ni watu kutolewa hofu tu.
 
Ndugu yangu ukiamini kuwa corona imeondoka Tanzania utakuwa unaamini ndivyo sivyo kama ulimfuatilia Dr. Janabi wa Taasisi ya moyo ya Jakaya kikwete alizungumza vizuri sana kuhusu hili na alisema asilimia kubwa wataugua na watapona na asilimia chache watalazwa na kupona na asilimia chache pia watalazwa na kufariki sikumbuki exactly figure lakini alisema haya ukitafuta hii habari utaelewa kwani kinachokuaminisha imeisha sio kipimo sahihi cha kujua kama ugonjwa upo au laa( nakushauri endelea kuchukua tahadhari).

Ni kweli Mwenyezi Mungu anatusaidia sana kwenye mambo mengi na hatupaswi kuacha kumwomba kila uchwao lakini naomba tusijiinue kwenye hili suala kwani hata mataifa mengine wanaomba Mungu kama watanzania wanavyoomba hivyo basi tuendelee kumwomba kila siku sio kwa sabab ya korona tu ila kwa kila jambo ( endelea kuchukua tahadhari corona haijaisha).

Kuhusu ndugu na majirani kufa wengi wanasema hakuna hata jirani yao amekufa lakin mim nina ushahidi usio rasmi sis huwa tunapewa taarifa kupitia email ya ofisi mfanyakazi anapofiwa na mke/ mume/ mtoto / baba/mama na wakwe kiukweli pamoja na kwamba taasisi ina wafanyakazi zaidi ya 4000 kwa sasa taarifa ya vifo imeongezeka kwa siku unaweza kuona mpaka email 10 kuhusu misiba tofauti na zamani hii inamaanisha nin? ( endelea kuchukua tahadhari corona bado haijaisha)

Sina uhakika sana na wanaosema kuhusu nyungu, malimao, swaumu na vinginevyo kwani ninachojua kitaalam vitu vyote hivyo vina madhara mwilini endapo vitatumika ndivyo sivyo; Nyungu mtalaam Ndungulile alishaizungumzia, limao kwa sabab ya acid nyngi ni chanzo kizuri cha vidonda vya tumbo na sasa mtu yeyote mwenye ndugu ambaye ni dr. aongee nae kesi za vidonda vya tumbo zimekuwa nyingi ghafla mahospitalini. Kitunguu swaumu nacho kinafanya kazi sawa na ( warfarin ) hii ni dawa ya kuyeyusha dam waliowahi kuugua thrombosis watakuwa wananielewa vizuri hapa hivyo ukitumia hivi vitu kuwa makini sana.( endelea kuchukua tahadhari korona bado ipo)

Naungana na mkuu mmoja amessema korona haijaisha tumeondolewa hofu tuu, kwani ingekuwa akifa mtu anapimwa na watu wanapewa majibu kama wanavyofanya hapa Kenya naamini comments nyingi kwenye huu uzi zisingekuwepo , Namsihii mkuu mmoja aliesema wanakufa wazee achunge kauli zake kwani hata wao walikuwa vijana na kiasili kila binadam anapenda kuishi ( endelea kuchukua tahadhari korona haijaisha).

Mwisho naomba wote waliochangia kuwa imeisha wanisaidie wametumia kipimo gani kujua kuwa imeisha?
You're absolutely right Mkuu Tingitane!

Wananchi wa nchi za kimaskini hujenga kinga madhubuti katika miili yao baada ya kuathirika na magonjwa mengi katika maisha yao ambayo hayaisumbui tena katika nchi nyingi za kitajiri kama typhoid, dengue fever na malaria.

Dawa tunazozitumia miaka kadhaa sasa za kuponya haya magonjwa ndio dawa wanazojaribu kutumia wazungu kuwaponyesha wagonjwa wa corona19 sasa hivi au kujenga kinga dhidi yake. Kama umeshawahi kuumwa malaria au typhoid, unapoumwa corona19 itakusaidia kupona hasa kama una kula vizuri na mwenye afya.

Corona19 ipo Tanzania na duniani kote. Watu wanayo na wanaambukizana sana ila wengi wataumwa na kupona na wenye afya mbaya, watakufa. Pia wengine watakufa kwa kukosa ventilator waheme vizuri au kuwa mbali na hospitali. Wananchi watazoea na kuishi na huu ugonjwa kama wanavyoishi na ukimwi na malaria.

Tatizo letu kubwa ni kuweka siasa katika sayansi.
 
Corona bado ipo sema watu wanakufa kimyakimya kwa manufaa ya kisiasa
Manufaa ya kisiasa unadhani Magufuli hataki kuishi ale mema ya nchi awamu ijayo?Majaliwa hataki,kundi la mawaziri wa CCM wao hawataki baada ya miaka 5 waje tena kupokea kiinua mgongo 240Mill,ulimuona pale Mkapa,Mwinyi na uzee wake yupo above 90 tena na mkewe,Dk Shein,White mzee wa Msoga wote wanakula mema ya nchi unafikiri kungekuwa na hatari ya afya zao jinsi tunavyoaminishwa wangekubali kujifungia mule ukumbini washangilie kiasi kile na wajumbe zaidi ya 1500 wasiokuwa na barakoa hata mmoja hali ya kuwa tunaaminishwa Corona inaambukizwa hasa kwenye mrundikano wa watu.

Sense ya kawaida tu inakataa fikiri vizuri!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uko sahihi sana,ukiangalia idadi ya watu wanaovaa barakoa na kutumia sanitizer na kufuata masharti ya social distancing ni wachache mno,hii ni kuonyesha hao wengi ambao hawafuati masharti ni kuwa huko kwenye familia/jamii zao wanakotoka cases ni chache au hakuna kabisa,hakuna mtu ambaye angeona watu wanaendelea kufa/kupukutika halafu asifuate masharti,kwahiyo kwa jinsi hali ilivyo ni almost kama umeisha.

Vyuo vimefunguliwa na shule zote zimefunguliwa hatujasikia mpaka sasa hivi case yoyote kwa wanafunzi wetu,kwahiyo sidhani kama kuna mzazi yuko tayari kuachia mwanae aende shule wakati watoto wanakufa,hakuna mzazi wa hivyo wala hajazaliwa,mtoto anauma ndugu zangu sikieni tu ,cha muhimu ni kuendelea kumuomba Mungu wetu aendelee kutupigania...
Shuleni na vyuo hali ni shwari kabisa.
Hakuna barakoa wala vitakasa mikono.
 
Hello JF,

Ningependa kujua out of curiosity, nini kimeiondoa corona Tanzania? Je, Nyungu ilisaidia? Watu kuhimizwa kula tangawizi na malimao?

Na watu wakachukulia serious kula tangawizi na malimao. Hivyo miili yao ikajijenga ku-fight virus? Ama watu walichukulia serious kuosha mikono na kuvaa barakoa hivyo rate ya maambukizi ikapungua? Nini hasa kilichoiondoa Corona Tanzania?

Its good to know, ili janga liingine likija, we use the same strategies.
Dada ulishaiona wapi? Corona ni uongo uongo tu.
 
Back
Top Bottom