Nini hasa kimeondoa Corona Tanzania?

Nini hasa kimeondoa Corona Tanzania?

Amelaaniwa amtumainiaye mwanadamu. Sisi kama sisi hatungekuwepo hapa muda huu, ila tupo kwa kuwa tumemtumainia Mungu! Na kwa hali hii hatujikwezi kwamba sisi ni bora kulikuko wengine ila tunampa Mungu utukufu kwa kuwa ametuona udhaifu wetu na ametupigania. Hata hao waliokufa kwa corona sio kwamba wao sio bora kuliko sisi, tupo kwa neema ya Mungu tu. Tutumie nafasi hii kumshukuru na si kujiinua.
 
Serikali huenda kuna kitu wanakijua kuhusu huo ugonjwa so wakaamua kucheza na saikolojia za watu, huku wakihimiza tahadhari ikiwa kama njia ya kufanya chochote kitu mixer maombi na nyungu.

Kusema kinga duh! Napata hofu kidogo maana hao wazungu hula vyema Sana mazoezi n.k kushinda huku ambapo wengi wao kula nini huchaguliwa na maisha na si kuchagua!.. mi nahisi kuna namna nyengine zaidi ya hizi tunazoziona kuhusu huu ugonjwa.
Wakihimiza tahadhari ?? Ipi? Nenda kariakoo halafu niambie ni tahadhari ipi iliyohimizwa pale
 
Kitendo tu Cha kuficha takwimu kikupe tu jibu kuwa corona ipo sana hapa na inatafuna watu.Corona haikuwa mkondo wa upepo kwamba inapita tu na ikishapita haigeuki nyuma.Acha tuendelee kujitoa ufahamu Ila siku ikiguza penyewe tutaanza kuipa heshima yake
Mtaani kwenu mume zika msiba mingapi inayo husiana na Corona?
Ukweli Corona haitishi kama wazungu walivyo taka kutuaminisha.

Hofu ya Corona ipo juu tofauti na ugonjwa wenyewe.
Ahsante Rais wangu, kwa kushtukia janja hii.
 
Kuna mtaalamu WHO alisema Afrika kinachotusaidia ni
1. Vyakula tunavyokula, vinatoka shamba moja kwa moja havisindikwi...
Kwani Kenya ipo bara gani?
Nawe sister some time Unazinguaga tu.
 
Hofu ilikuwa ina Kula watu zaidi ya corona yenyewe niliwahi kusema Mwafrika sio mtu wa kufa na mafua, Kenya wamemchoka haswa Kenyata wana wish ata JPM angekuwa kiongozi wa EA nzima ili ujinga kama wa Curfew na baba yake Lockdown utupiliwe mbali
 
Kitendo tu Cha kuficha takwimu kikupe tu jibu kuwa corona ipo sana hapa na inatafuna watu.Corona haikuwa mkondo wa upepo kwamba inapita tu na ikishapita haigeuki nyuma.Acha tuendelee kujitoa ufahamu Ila siku ikiguza penyewe tutaanza kuipa heshima yake
Inawezekana inatutafuna sawa. Swali fikirishi, kwa nini mtanzania atafunwe kimiujiza na labda tufe sana na huku tunatembea tofauti na marekani, Brazil, India, uingereza, Spain, Italy nk nk,?
 
Kwanza kabisa ilikuwa ni muhimu kuondoa hofu miongoni mwa watanzania, kitu ambacho kimefanikiwa sana. Corona bado ipo, kuwa mwangalifu.
 
Kuna mtaalamu WHO alisema Afrika kinachotusaidia ni
1. Vyakula tunavyokula, vinatoka shamba moja kwa moja havisindikwi...
Hakuna kitu kama hicho. Corona inatandika Afrika kama kawaida, issue ni vile nchi nyingi za kiafrika hazipimi wala kutoa taarifa sahihi za kitakwimu.
 
Corona ipo kwa sana tu sema watu hakuna panic, watu wengi wakipata wanapona bila hata kujua, wanaoishia kufa kimya kimya ni wale wenye magonjwa yanayoathiri sanasana immunity.

Tanzania ni moja ya nchi yenye watoto na vijana wengi duniani kuliko wazee, na hilo ndo kundi ambalo likipata corona ni kama kijimafua tu kinapita.

Usishangae kuona watu hawana hata dalili. Wazee wanakufa daily ila hakuna anayehisi corona sababu hofu hiyo haipo tena, wanahisi ni magonjwa mengine tu
 
Back
Top Bottom