Tunapoichukulia poa Ebola hata kuiita majina yasiyojulikana ni hatari

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,879
35,888
Tumekumbwa gonjwa hatari lenye kuuwa hadi 90% ya wahanga.

Sisi kwa tunachoita kuondoa taharuki tumependelea kuliita Marburg badala ya jina lake linalofahamika uswahilini, yaani Ebola.

Screenshot_20230323-045348~2.jpg


"Kwamba tumependa kutoliita koleo kwa jina lake."

Maajabu ya Mussa.

Tangu lini uswahilini neno Marburg likafahamika? Kwani gonjwa hili lilipokuwa Congo, Uganda, Guinea, Gabon, Sierra Leone au Liberia tuliwahi liita Marburg?

Katika kinachoitwa kuepuka taharuki gonjwa halipewi umuhimu wala coverage yoyote ya maana kwenye media zetu. Kwetu Simba au Yanga kwenda robo fainali ni habari kubwa, Lakini si gonjwa hili.

Maisha yanaendelea kama vile kila kitu ni sawa.

Ya nini kutoambiana ukweli wote tukajipanga kukabiliana nalo ana kwa ana kama nchi?

Kwenye tahadhali zilizotolewa na wizara katika namna za kujikinga, kutogusana nayo imo. Inawezekana namna gani kwenye maisha yetu ya kawaida watu kutokugusana masokoni, magulioni, mashuleni, makanisani, misikitini, kwenye mabasi au kwenye madala dala?

Ebola si ya maji tiririka, barakoa, michaichai, matango pori wala upigaji nyungu.

Walioyasikia ya kwetu wameshtuka kuliko sisi wakati sisi tukichukulia poa. Dhidi ya gonjwa hili dunia tayari inatunyanyapaa.

Angalia Rwanda, The New Times - Rwanda on Marburg alert after Tanzania outbreak

Angalia mabeberu, BBC News - Ebola-like Marburg virus kills five people in Tanzania

Coverage zao ni makini na kamilifu (extensive and focussed). Kwetu wenge la awamu ile na njama za mabeberu bado lingalipo.

Kwanini watu wasiambiwe ukweli wote kukiwa kungali mapema? Ya nini kujidanganya?

Magonjwa haya si vita (vya kiuchumi). Ebola si corona ambayo kuuwa kwake kulikuwa hadi 2%. Hiyo hata ikihusianisha uzee na uwepo wa magonjwa mengine pia.

Kwa hakika kwenye ugonjwa huu tusipoamka mapema, usanii wetu uliozoeleka utatuumbua.
 
Ishasemwa ni Ebola-like vp sasa useme ni Ebola? Tahadhari ni muhimu lakini kukoleza chumvi haipendezi.

Hakipo kinachokolezwa hapo. Zingatia mada ni mahsusi kwa watanzania. Neno uswahilini linawakilisha.

Zingatia ugonjwa huu haukuwahi kuitwa Marburg hapa nchini siku yoyote kabla.

Nini kimebadilika?
 
Kutokana na source yako ya kwanza,imeeleza kuwa ni Marburg...ni nini kilichokuaminisha kuwa sio?
Ebola na marburg vinafanana sana japo ebola ni hatar zaidi.View attachment 2562195

Ebola na Marburg kisayansi (yaani in scientific details) ni magonjwa mawili tofauti. Malaria na Plasmodium kisayansi ni vitu viwili tofauti. Uswahilini plasmodium haina maana yoyote ila malaria.

"Marburg and Ebola viruses are filamentous filoviruses that are distinct from each other but that cause clinically similar diseases characterized by hemorrhagic fevers and capillary leakage. Ebola virus infection is slightly more virulent than Marburg virus infection."

Ninakazia uswahilini neno Marburg halina maana yoyote ila ebola linalofahamika kuhusiana na huu ugonjwa.

Ya nini kujikinga mvua chini ya mwembe wakati nyumba za bati zipo?

Zingatia ugonjwa huu umekuwapo katika mataifa kadhaa kabla. Ni kwa mara hii tu Tanzania imeuita Marburg kwa watanzania. Kulikoni?

Mwongozo wako tafadhali.
 
Afu juzi BBC Swahili wanatangaza li Antony diallo la star tv likakatiza matangazo ili wa Tanzania wassisikie.

mitanzania inaweza kuwa mijinga ila siyo wote, wengine tunajitambua nini tunafanya

EBOLA IPOOO!!!!

Kina Ruble wanasema kuuita ugonjwa Kwa jina lake (ebola) ni kuukoleza.

Ebola inauwa. Hata sasa ni mjinga peke yake ndiye anayeweza kuamini kuwa walioathirika ni hao tu tuliokwisha kuambiwa.

Ni kweli kuwa tuna wajinga wengi nchini ambao ni mtaji muhimu zaidi wa serikali za CCM. Ila ni vyema wakajua SI wote.

Walisema fumbo mfumbie mjinga.
 
Kina Ruble wanaita kuuita ugonjwa Kwa jina lake (ebola) ni kuukoleza.

Ebola inauwa. Hata sasa ni mjinga peke yake ndiye anayeweza kuamini kuwa walioathirika ni hao tu tuliokwisha kuambiwa.

Ni kweli kuwa tuna wajinga wengi nchini ambao ni mtaji muhimu zaidi wa serikali za CCM. Ila ni vyema wakajua SI wote.

Walisema fumbo mfumbie mjinga.
Tanzania Wajinga Ni Wengi
By Godwin Mollel
Naibu Waziri Wa Afya Tanzania 🇹🇿
 
Back
Top Bottom