Nini hasa kimeondoa Corona Tanzania?

Nini hasa kimeondoa Corona Tanzania?

Serikali huenda kuna kitu wanakijua kuhusu huo ugonjwa so wakaamua kucheza na saikolojia za watu, huku wakihimiza tahadhari ikiwa kama njia ya kufanya chochote kitu mixer maombi na nyungu.

Kusema kinga duh! Napata hofu kidogo maana hao wazungu hula vyema Sana mazoezi n.k kushinda huku ambapo wengi wao kula nini huchaguliwa na maisha na si kuchagua!.. mi nahisi kuna namna nyengine zaidi ya hizi tunazoziona kuhusu huu ugonjwa.
100% True..
 
Soma vizuri kichwa cha habari ya hii habari tunayo ijadili, kisha rudi tena uisome comment yako hii, utajiona uko nje ya mada kabisa.
Sister Corona ipo tofauti na mataifa mengine wanavyo ichukulia.

Mataifa mengi yanaathiriwa na hofu, sio Corona.
Kiuhalisia Corona haitishi sana kama wazungu walivyo taka tuamini.
Maambukizi ya Kenya hayajafikia Brazil, Brazil wanakufa 500 kwa siku.
Huu mtego nashukuru Rais wetu kautegua.
 
Jaribu siku moja mgeni aje kwako na uwe huna muda nae endelea na yako hutojua hata kaondoka muda gani,,
Ndio corona ilivyo fanyiwa Tz ikaamua kusepa
 
😁😁 Rebeca 83
Ujasiri wa Rais wetu na serikali yetu makini ndio kilichoondoa COVID Tanzania.
Serikali ilichagua mfumo sahihi wa kupambana na janga lile. COVID bado ipo lakini sio kama ilivyotangazwa kwa vitisho, ipo tuu kama ilivyo malaria, UTI na magonjwa mengine
Tungelock down tungepata stress na njaa na tungekufa sana halafu ingetangazwa tumekufa kwa COVID
 
Hello JF,

Ningependa kujua out of curiosity,nini kimeiondoa corona Tanzania? Je, Nyungu ilisaidia? Watu kuhimizwa kula tangawizi na malimao?

Na watu wakachukulia serious kula tangawizi na malimao. Hivyo miili yao ikajijenga ku fight virus? Ama watu walichukulia serious kuosha mikono na kuvaa barakoa hivyo rate ya maambukizi ikapungua? Nini hasa kilichoiondoa Corona Tanzania?

Its good to know, ili janga liingine likija, we use the same strategies.
Corona bado ipo sema watu wanakufa kimyakimya kwa manufaa ya kisiasa
 
hivi sasa ni kiangazi

na lile futa linalobeba makorona linajiyeyukia lenyewe,kama ilivyo Mafia

na jingine korona inaogopa maombi,sawa tu na Polisi na kibaka
 
Kuna mama mmoja alikuwa jirani yangu, kwake wageni hawaishi kumbe kisiri siri alikuwa akipika gongo na kuuza hapo hapo nyumbani kwake kwa miaka zaidi ya 30.

Katika maisha yangu yote sikuwahi kujua wala kuhisi huyo mama alikuwa akifanya hayo mpaka siku alipofariki ndio nikasikia watu fulani mitaa ya mbali sana wakipiga story za mama muuza gongo kafariki mtaani kwetu. Nilistuka kusikia jina lake likitajwa, nilipoamua kufanya udadisi sana nikajagundua hadi manjagu walikuwa wakifika kwake kunywa gongo!

Kinachoendelea kuhusu Corona hapa Tz ni kitu kama hicho.
Sasa mkuu ikiwa hiyo issue ya gongo ulishindwa kujua miaka yote hiyo,je katika hili la corona umewezaje kujua kuwa ipo ila inafichwa?
 
Nani kasema imeondoka??
Tatizo hutuwezi kutofautisha kuwepo kwake na kutokuwepo kwake,tokea kipindi kile mwanzoni wakati tunapima na kutoa takwimu na hospitali zilikuwa na wagonjwa wa corona kabisa,bado huku mitaani hakukuwa na wingi wa vifo. Na vifo vilivyokuwa vinatangazwa tulikuwa tunaambiwa hao marehemu walikuwa na maradhi mengine(hata Kenya ni hivyo hivyo) na tunajua hayo maradhi yalikuwa yanauwa kabla hata kuwepo corona.
 
Hello JF,

Ningependa kujua out of curiosity,nini kimeiondoa corona Tanzania? Je, Nyungu ilisaidia? Watu kuhimizwa kula tangawizi na malimao?

Na watu wakachukulia serious kula tangawizi na malimao. Hivyo miili yao ikajijenga ku fight virus? Ama watu walichukulia serious kuosha mikono na kuvaa barakoa hivyo rate ya maambukizi ikapungua? Nini hasa kilichoiondoa Corona Tanzania?

Its good to know, ili janga liingine likija, we use the same strategies.
Ndugu yangu ukiamini kuwa corona imeondoka Tanzania utakuwa unaamini ndivyo sivyo kama ulimfuatilia Dr. Janabi wa Taasisi ya moyo ya Jakaya kikwete alizungumza vizuri sana kuhusu hili na alisema asilimia kubwa wataugua na watapona na asilimia chache watalazwa na kupona na asilimia chache pia watalazwa na kufariki sikumbuki exactly figure lakini alisema haya ukitafuta hii habari utaelewa kwani kinachokuaminisha imeisha sio kipimo sahihi cha kujua kama ugonjwa upo au laa( nakushauri endelea kuchukua tahadhari).

Ni kweli Mwenyezi Mungu anatusaidia sana kwenye mambo mengi na hatupaswi kuacha kumwomba kila uchwao lakini naomba tusijiinue kwenye hili suala kwani hata mataifa mengine wanaomba Mungu kama watanzania wanavyoomba hivyo basi tuendelee kumwomba kila siku sio kwa sabab ya korona tu ila kwa kila jambo ( endelea kuchukua tahadhari corona haijaisha).

Kuhusu ndugu na majirani kufa wengi wanasema hakuna hata jirani yao amekufa lakin mim nina ushahidi usio rasmi sis huwa tunapewa taarifa kupitia email ya ofisi mfanyakazi anapofiwa na mke/ mume/ mtoto / baba/mama na wakwe kiukweli pamoja na kwamba taasisi ina wafanyakazi zaidi ya 4000 kwa sasa taarifa ya vifo imeongezeka kwa siku unaweza kuona mpaka email 10 kuhusu misiba tofauti na zamani hii inamaanisha nin? ( endelea kuchukua tahadhari corona bado haijaisha)

Sina uhakika sana na wanaosema kuhusu nyungu, malimao, swaumu na vinginevyo kwani ninachojua kitaalam vitu vyote hivyo vina madhara mwilini endapo vitatumika ndivyo sivyo; Nyungu mtalaam Ndungulile alishaizungumzia, limao kwa sabab ya acid nyngi ni chanzo kizuri cha vidonda vya tumbo na sasa mtu yeyote mwenye ndugu ambaye ni dr. aongee nae kesi za vidonda vya tumbo zimekuwa nyingi ghafla mahospitalini. Kitunguu swaumu nacho kinafanya kazi sawa na ( warfarin ) hii ni dawa ya kuyeyusha dam waliowahi kuugua thrombosis watakuwa wananielewa vizuri hapa hivyo ukitumia hivi vitu kuwa makini sana.( endelea kuchukua tahadhari korona bado ipo)

Naungana na mkuu mmoja amessema korona haijaisha tumeondolewa hofu tuu, kwani ingekuwa akifa mtu anapimwa na watu wanapewa majibu kama wanavyofanya hapa Kenya naamini comments nyingi kwenye huu uzi zisingekuwepo , Namsihii mkuu mmoja aliesema wanakufa wazee achunge kauli zake kwani hata wao walikuwa vijana na kiasili kila binadam anapenda kuishi ( endelea kuchukua tahadhari korona haijaisha).

Mwisho naomba wote waliochangia kuwa imeisha wanisaidie wametumia kipimo gani kujua kuwa imeisha?
 
Back
Top Bottom