Nimeoa mke mlokole ila sikushauri uoe mlokole

Nimeoa mke mlokole ila sikushauri uoe mlokole

Wakuu habari , mi nimeoa mke mlokole Ila changamoto nazopitia no balaa tupu, mke anshinda church kuaanzia asubuhi Hadi jioni

*Anarudi hapiki anasema alikuwa na kazi kwa mchungaji

*Ukiomba game anasema amechoka

Yapo mengi kweli mpaka niamua nihame nyumba na kumuacha yeye aendelee na Mambo yake
Wanaume dhaifu wanazidi kuongezeka, mnapenda wanawake mteremko mwisho wake ndio huu, Mwanamke uliyemtongoza mwenyewe na kumuona mwenyewe bila shinikizo anawezaje hata kujaribu kunifanyia mambo anavyotaka? Anakuona wewe ni poyoyo
 
Kanisani kulikua na mfungo wa kukaa siku tatu bila kula kitu chochote, siku zote 3 mnashinda na kulala kanisani.

Nilikua darasa la 5 mama akanichukua tukaenda, mkiingia wote mlango unafungwa unafunguliwa jioni kwenda nje kujisaidia tu halafu mnarudi ndani.

Imefika jioni njaa inaniuma sana nikaanza kulia! Mama ananiambia nijikaze tumalize mfungo wote.
Walivyoniona nazidi kulia wakaniita mbele wakaanza kuniombea eti nina mapepo.

Njaa inauma nazidi kulia na wao wanazidi kuniombea mapepo yatoke, walivyoona mapepo hayatoki nikafunguliwa mlango mama akanipa hela niende kwa ndugu yangu yeye anabaki kwenye maombi.

Nilivyofika huko nilikula na kilio kiliisha.
Kanisa gani hilo mbona mlifika mbali sana
 
Mchungaji mwenye akili timamu hawezi kuhusu hiki. Inawezekana kuna agenda ya Siri kati ya mchungaji na mkeo. Kwa harakaharaka usihangaike. Mtafute huyo pasta au namba ya mke wa mchungaji ukishindwa kabisaa tafuta namba ya huyo pasteri unipe nimkanye mshenzi mkubwa huyo anaharibu ndoa yako na wewe unakuja huku badala ya kumface.
 
Mimi wangu ni mlokole na anaishi chini ya sheria niliyoiweka, hakuna biashara ya kutaja taja mchungaji....

Ila naanza kumuweka sawa' maana nahisi asije kuwa kichaa, hizi tabia zao za wao kujiona watakatifu na kuona wengine wanadhambi ndio zinaniumiza kichwa...

Kidogo tu' mara sijui nimeota vibaya hivyo hii ndoto inamaanisha sijui nini... Dah' Mungu baba alinde hichi kizazi maana hawa wachungaji baadhi badala ya kufundisha maandiko na kulinda maadili wao wanaharibu, mwisho wa siku unaona mkeo anaenda kumfulia mchungaji nguo za ndani....

Kwishaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom