KakaJambazi
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 18,830
- 12,292
KakaJambazi Njoo huku useme mliibaje
Hana hela uyo, ulabu ndo ulimzidi.
Last edited by a moderator:
KakaJambazi Njoo huku useme mliibaje
hivi mnajua kuwa mkojo ni kiboko ya makufuri yaliyoimara???
ulipuliziwa dawa ya usingizi next time ukilala hakikisha umeweka ndoo ya maji ikiwa wazi ,ikipuliziwa inanyonywa na maji ya ndoo
Wakuu, naleta kwenu hili ili nipate uzoefu na namna ya kujikinga isitokee tena.
Ni hivi, nina nyumba yenye ukuta wa kozi saba kote na geti na ninaishi mimi na wife tu ndani kuna vyumba viwili havikaliwi na mtu. Sasa naamka nakuta flat sceen na remote yake haipo na mlango mkubwa uko wazi wakati kabla ya kulala niliufunga nakumbuka.
Jamaa karuka ukuta, kachana nyavu ya dirisha, kachukua funguo kafungua mlango kaingia sebleni kawasha taa kazunguka room zote manake nimekuta pamepekuliwa na mashuka yametanduliwa kama alikua anatafuta kitu isipokua chumba nilicholala mimi tu na taa kawasha cha ajabu kabeba hiyo tv na remote yake tu pamoja na raba zangu zilizokua mlangoni nje na kuacha vitu kibao vya thamani ambavyo vilikua wazi tu.
Baada ya hapo katoka na funguo kafungua geti then funguo kazitupa mlangoni. Naamka sioni tv, kuchek mlango umerudishiwa tu kuzunguka nje nakuta funguo zangu ziko nje zimetupwa ikanibidi nicheke tu na kushukuru Mungu.
Katika mazingira ya kawaida sio rahisi mimi na wife kulala hivi lazima kuna ujanja wamefanya hebu tupeane uzoefu na namna ya kujikinga na hizi mambo jamani manake ni hatari sana.
EXPERIMENT. napenda majaribio. polisi jamii wangekuwa wanaelimisha watu kupunguza wiz au hawajui kitu hii.Inatakiwa Unapolala HAKIKISHA unaweka maji yaliyo wazi aidha kwenye dish au kibeseni! itakusaidia coz dawa wanazotumia kukupiga nusu kaputi huwa zinavutwa kwenye maji mithili ya sumaku.... NOTE THAT!
Pole sana. Weka komeo pia funguo usitoe kwenye Kitasa pia ipinde isiwe 90 degree kwa kuwa itakuwa rahisi kuisukuma kwa kutumia funguo nyingine. Pia kazi ya kufunga milango usi delegate kwa Wife uifanye mwenyewe kujiridhisha. Mbwa ni mzuri ila siku hizi wezi wanajipaka mafuta ya Chatu na mbwa akisikia harufu hujikunyata kama kuku alielowana.
ulipuliziwa dawa ya usingizi next time ukilala hakikisha umeweka ndoo ya maji ikiwa wazi ,ikipuliziwa inanyonywa na maji ya ndoo
Kabla ya kulala hakikisha ndoo.moja ya.maji.inakuwa wazi , maana haya wezi kuna dawa huwa wanapulizia utalala ucngizi ambao hujawahi.kulala maji.yanavuta harufu yote ya hiyo.dawa inakosa nguvu so unakuwa salama kabsa pole an
Milango ya grill ni muhimu mkuu
Kabla ya kulala hakikisha ndoo.moja ya.maji.inakuwa wazi , maana haya wezi kuna dawa huwa wanapulizia utalala ucngizi ambao hujawahi.kulala maji.yanavuta harufu yote ya hiyo.dawa inakosa nguvu so unakuwa salama kabsa pole an
Mtafute mtu anaitwa Mamakibunju humu anauza CCTV Camera.
Unajua wezi wengi wanaangalia udhaifu wa Nyumba yako.Na huyo anaijua nyumba yako vizuri.
Jiji limekuwa silo siku hizi.Vibaka na wezi wa kawaida ukiweka Cameras au ukiwa na Mbwa wa Kisasa basi utasikia tu wenzio ndio wanalia kwa kuibiwa.
Diva Beyonce huyo KE (mbwa jike) why anacost sana kuliko ME?Na inashauriwa kulala na maji kwenye ndo wazi ili wakipuliza hyo dawa maji yana neutralize nguvu ya dawa na haiwi na madhara.
Pia huyu mleta mada afuge tu mbwa wanasaidia sana hasa kwa hawa wezi wadogo wadogo. Mbwa kwetu wamesaidia sana hata akibweka sana ni alert kuwa kuna jambo la hatari.
Mleta mada mpole huyo mwizi ni MTU anayewafahamu in and out na anajua kila kitu cha hyo nyumba. Cha kushukuru ni wote mumekua salama.