Nimeibiwa kiboya kweli, hata sijielewi

Nimeibiwa kiboya kweli, hata sijielewi

Step by step

We lala tu! Mpaka wale tigo ndo utakaa kimagutu!
Fuga pets wakuzoee wakiona mtu tofauti tu wanaita kwa namna fulani hivi.
Juzi juzi aliibuka msela night kali paka wangu alilia nyau nyau mpaka nilipotoka
Nikakuta msela alishafunguwa geti, sijuwi alitaka atoke na gari au vipi!
 
Last edited by a moderator:
“Ασπασία, τι γκαντεμιά! Εγώ τη
ψυλλιάζομαι τη δουλειά, φιρί-
φιρί το πάνε να μας την πέσουν οι
Λακεδαιμόνιοι. Πρέπει να τους
σπάσουμε τον τσαμπουκά!”
 
Yelewiiiiii
Wiki 3 zilizopita nimeibiwa hivi aiseee
Katv laptop na remoti kushnehi

Kijichi hakukuwa na huu mchezo....sijui umeanzia wapi

Wamepiga jeki dirisha wakafanya yao
Halafu huwezi amini nilikuwa sebuleni mpaka saa nane...kuamka kumi na moja nikakuta washafanya yao...

Nadhani wanachukua tv kwa kuwa ni rahisi kuiba.....

Sasa hivi nafungaje nyumba sasa...na remoti naficha mbaliiiiiii



wamekupulizia dawa mi yashanikuta hayo kijichi kule nikahama kabisa kuondoa mkosi


Inauma sana na ni kurudishana nyuma aisee

Usisikie kabisa hio kitu haina baunsa. Niliwahi kutoa machoZi. Niliwaza mammbo mengi sana asubuhi ya siku hio. Niliamka wamechukua music system yaani ....
 
Umenikumbusha miaka ya themanini huu mchezo wa kukata waya kipindi kile walikuwa wanachomoa luva na kufungua dirisha tukawa tunaweka kopo dirishani akichomoa luva akitaka kufungua dirisha ataligusa kopo na kuanguka hata kama umelala utashituka , sasa watu wengi kopo likianguka tu akikulupuka usingizini ni kelele za mwizi tu ila ilikuja kusumbua kipindi cha kipupwe makopo yalikuwa yanadondoka ovyo sababu ya upepo watu wakaacha kuyaweka, ilikuwa kila dakika kelele za mwizi mkitoka na kuja kuchunguza dirishani hakuna dalili ya kuwepo mwizi .
 
huyu atakuwa ndogo wako wa mwisho anakutania, anasema braza kwa nini unapenda kukaa peke yako na mavyumba yote hayo? siku nyingine uwe unajenga nyumba ya chumba kimoja cha kwako sebule , jiko choo na bafu, unaacha tofari za matoleo, mkeo akijifungua mtoto akafikisha miaka mitano, unaongeza chumba, kama wote midume unaacha kujenga kama ukiongezea jike ongeza kingine awe ankaa na beki tatu. Usiweke chumba cha wageni, wageni wakija wakaa sebuleni wawe walinzi.

nimecheka sana mkuu umeifanya siku yangu kuwa good
 
Usisikie kabisa hio kitu haina baunsa. Niliwahi kutoa machoZi. Niliwaza mammbo mengi sana asubuhi ya siku hio. Niliamka wamechukua music system yaani ....

dah umeandika kwa hisia sana mwana pole lakini cha ajabu humu kuna watu wana comment kama vile wao ndo top wajanja haitawatokea
 
Mkuu Step by step huu wizi ni common sana wala usihuzunike.
Ilishawahi kutokea kwetu, siku hiyo tulilala ndani tena vyumba vyote zaidi ya watu7 na wamwisho alilala saa7 usiku lakini tulilizwa siku hiyo.
Alitugutusha dada yetu saa2 asbuhi baada ya kuamka na kukuta mabadiliko makubwa sebureni!
Siku hiyo walibeba screen,music system na fridge. Tulilala usingizi wa kifo asikwambie mtu.
Tulifunga milango yote na kuiacha funguo mezani. Jamaa walipiga tochi wakaiona funguo, wakachana nyavu,wakachukua mti na kuupaka superglue then kiulaiini wakainasa funguo na kwenda kufungua mlango. Mlango ulikuwa na komeo kwa ndani ikabidi wachane nyavu tena dirisha ambalo bahati mbaya sana lilikuwa karibu sana na mlango.. so ikawa rahisi sana kupitisha mkono na kufungua komeo!!
Walikusanya vyao wakajiondokea kiulaiiini!!

Ikabidi nianze msako chini kwa chini kwenye vijiwe vyote vya wahuni na wavuta ganja pale mtaani angalau nijue jamaa huwa wanafanikisha vipi oparetions zao.
Simlizi zao ni ndefu sana ila moja ya zana na nyenzo nyepesi kabisa ambayo wakiiapply lazima usinzie ni MOSHI WA CD ni sumu hatari sana hii ikipuliziwa kisha ukavuta moshi wake au hata hewa/harufu ikikufikia nyakati ambazo kuna upungufu wa circulation ya oxygen.
Kinga kuu ya zoezi hili ni kuacha wazi chombo kilichojazwa maji nyakati za usiku na mara zote hakikisha unalala na funguo zako kitandani mwako uzilinde zikulinde!!
Pia ufugaji wa mbwa nao ni ulinzi tosha ila lazima wawe fully trained japo nao kuna namna wanakamatika kilahisi sana.
 
Last edited by a moderator:
Nasikia wanapuliziaga dawa ya usingizi kuna ukweli wowote au ni porojo tu
 
Pole subiri wakongwe wa kuiba na kuibiwa waje waweke uzoefu wao

Hahahhahaaaa, umenifanya nionekane kilaji kimekolea hapa bar, eti Wakongwe, duh umetisha. Ila hii comment itamnyima mshikaji haki ya kujua maujuzi
 
Mkuu Pole sana kwa tukio hulo.Na mumshukuru saana mungu kwamba mpo wazima.

Hembu tuambie Weekend yako uliianza vipi na kuimalizia jana kwa style ipi?

Maana kuna Mshkaji wangu yeye alilala nyumba yoote milango wazi,cha ajabu gari aliiacha Bar na yeye akakodi Taxi.
Cha kushangaza kuamka asubuhi akaanza kuitafuta gari na kusema imeibiwa,akaenda vituo vyoote vya Polisi kusema kwamba Gari yake Imeibiwa na nyumba imefunguliwa kwa Master Key.

Sasa alitokea jamaa mmoja mwenzie akamuambia mkuu haujavunjiwa nyumba wala haijafunguliwa,utakuwa ulilala milango wazo,jamaa alimtukana balaa,na kumuambia oyaaa mie ninaakili zangi timamu,siwezi kulala mlango wazi.
Basi jamaa akawa mstaarabu,na kumuambia unajua kwamba gari yajo uliicha Bar?na uzuri Bar yenyewe kwa mlio Zanzibar ni Gymkhana Bar ambapo ulinzi upo mzuri sana.Ikabidi jamaa aliganda akavuta kumbukumbu kwa aibu akasepa wiki nzima mtaani hayupo.

Sasa nakuuliza kujua je weekend yako iliishaje mkuu na mlikuwa nanani siku hiyo
Hahahhahaaaa, duh huyu alikunywa sumu sio pombe, hapo atakuwa alikuwa nusu kuzimu nusu duniani
 
Ile mbinu ya walimu kuingiliwa kinwilib ndo iliyotumika kwako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom