Tukubalinae pia,wezi wengi wa style hii ni vijana wa mtaani,yaani mitaa ambayo tukio linafanyika.
Mie Ushauri wangu ni ule ule.Kwamba wadokozi hawa wanaangalia nyumba dhaifu kwenye ulinzi.
Kuna Jamaa Mabibo,yeye alikuwa na rafiki yake anafanya kazi kwa wachina,basi kulikuwa na ma CCTV Camera mabovu kabisaa.
Basi aliyategesha kiuongo,basi huwezi amini Vibaka woote walihama njia.Yaani ni waoga balaa.Maana wanajua kabisaa kwamba Mshkaji atatujua tuu.Maana anajua ukipata picha yake kwenye Camera basi unatafuta muhuni mmja tu wa kitaa basi lazima atakutajia Kibaka wako alipo.
Au Pandisha ukuta,weka Mbwa.
Maana Vibaka nao huangalia zoezi la muda mfupi,kama kazi ni ndefu na wao ni waoga,wanaroho jamani.
Ukiona amekamatwa ndio utajua kwamba kutoka roho ni hali tata sana,kama unamoyo mwepesi utamuachia,ila yeye akikunasa kwenye purukushani lazima akuuwe ili ajinusuru.
-Tatizo jingine ni Ubishi wa watu wa Mtaani,unaweza kukuta kuna watu wanataka kuweka Polisi shirikishi kwa kulipia kila familia kwa mwezi kuna watu wabishi balaa.
Huku Zanzibar yale maeneo yoote tata ulinzi huu upo basi adabu mtu,maana hata mtu akipita na gari muda wa usiku mwingi lazima wakusimamishe.Hadi Raha yaani.
-Jingine ni kuangalia watu ndani ya nyumba mnaishije,wizi huu mwingine ni wa kukomoana kwa wapangaji wao kwao.
Yapo Mazingira ya kuwekewa dawa lakini lazima tukubali kwamba yapo mazingira ya watu kuuzana wao kwa wao kwa sababu binafsi.Au pia kuwa na wapangaji ambao kazi zao maalum hazifahamiki au za kuungaunga.
Unaweza kukuta akajifanya yeye ndio kaibiwa vitu vyoote,ili msistuke,kumbe alipanga kwamba yeye wachukue vitu vingi zaidi ili kwenu apige vile vya thamani,anakuwa kama amehamisha tu.
Hizi nyumba nazo tuziangalie saana kwa kina kabla ya kupanga.