Kaka
JF-Expert Member
- Nov 22, 2006
- 745
- 373
Last edited by a moderator:
pole jombaa hawa wezi ndo maana ukikuta wanachomwa moto unatakiwa kuongeza nguvu.
Mambo ya bongo watu wanmadawa ya kulevya ya spray wanakupulizia kupitia dirishani baada ya dk kumi hivi waingia kama kwao vile huwezi hata kushtuka unakuwa kama umezimia hivi
chakufanya
ukilala hakikisha una chombo kilicho na maji na kiwe wazi kama jagi hivi pana kiasi
maji huweza kusharabu sumu hiyo na kuipunguza kwa kiasi kikubwa sana kiasi kwamba wewe na waliomo ndani si rahisi kusinzirishwa kwa sumu hiyo,
swali zaidi kama unalo
Mambo ya bongo watu wanmadawa ya kulevya ya spray wanakupulizia kupitia dirishani baada ya dk kumi hivi waingia kama kwao vile huwezi hata kushtuka unakuwa kama umezimia hivi
chakufanya
ukilala hakikisha una chombo kilicho na maji na kiwe wazi kama jagi hivi pana kiasi
maji huweza kusharabu sumu hiyo na kuipunguza kwa kiasi kikubwa sana kiasi kwamba wewe na waliomo ndani si rahisi kusinzirishwa kwa sumu hiyo,
swali zaidi kama unalo
Kwa hiyo kuanzia leo tukitembelea kwako tukakuta tv ya chogo tuelewe flat iliibiwa au sio.
kweli mkuu Mbwa mwenye mafunzo ndio mpango mzima kwa vibaka kama hawa.
Wamasai siku hizi hawa maana kabisaa,wanajifanya watu wa kupiga dili vibaya.
Bora Paka kuliko kuweka Mmasai kama mlinzi
Hembu nipe cost ya Shepherd hapo na gharama za kila siku kuwahudumia
Mafuta ya chatu yanapatikana wapi mkuu?
Mkuu Pole sana kwa tukio hulo.Na mumshukuru saana mungu kwamba mpo wazima.
Hembu tuambie Weekend yako uliianza vipi na kuimalizia jana kwa style ipi?
Maana kuna Mshkaji wangu yeye alilala nyumba yoote milango wazi,cha ajabu gari aliiacha Bar na yeye akakodi Taxi.
Cha kushangaza kuamka asubuhi akaanza kuitafuta gari na kusema imeibiwa,akaenda vituo vyoote vya Polisi kusema kwamba Gari yake Imeibiwa na nyumba imefunguliwa kwa Master Key.
Sasa alitokea jamaa mmoja mwenzie akamuambia mkuu haujavunjiwa nyumba wala haijafunguliwa,utakuwa ulilala milango wazo,jamaa alimtukana balaa,na kumuambia oyaaa mie ninaakili zangi timamu,siwezi kulala mlango wazi.
Basi jamaa akawa mstaarabu,na kumuambia unajua kwamba gari yajo uliicha Bar?na uzuri Bar yenyewe kwa mlio Zanzibar ni Gymkhana Bar ambapo ulinzi upo mzuri sana.Ikabidi jamaa aliganda akavuta kumbukumbu kwa aibu akasepa wiki nzima mtaani hayupo.
Sasa nakuuliza kujua je weekend yako iliishaje mkuu na mlikuwa nanani siku hiyo
Mkuu pole sana...inshort inahitaji ujipange upya katika safu yako ya Security hapo Home kwako tayari weakness imeshaonekana..Kama utaweza jaribu kutumia ulinzi wa mbwa ni Salama na hauna rushwa wala hongo....Mimi nina German shepherd wawili tangu niwe nao sijawahi pata tatizo lolote iwe mchana hata usiku.
Ni walinzi wazuri sana..useme bei yao, mafunzo na msosi ndo inaweza kua shida kidogo ila ni afadhari kuliko kuweka masai.
View attachment 266122
Mtafute mtu anaitwa Mamakibunju humu anauza CCTV Camera.
Unajua wezi wengi wanaangalia udhaifu wa Nyumba yako.Na huyo anaijua nyumba yako vizuri.
Jiji limekuwa silo siku hizi.Vibaka na wezi wa kawaida ukiweka Cameras au ukiwa na Mbwa wa Kisasa basi utasikia tu wenzio ndio wanalia kwa kuibiwa.
kwenye kochi kulikua na ipad nazani hakuiona, kwenye meza ya tv kulikua na xternal hard disc imechomekwa kwenye tv kaichomoa na kuiacha, jikoni kuna ma brenda na vitu kibao tu na hizo room alizoingia kuna acccesories nyingi tu ila hajagusa na kote kaingia manake aliingia na viatu nimeona michanga ya miguu yake
TB ni kama chloroform sio dawa ya usingizi perse bali ni dawa ambayo inakufanya unapoteza fahamu kwa muda so haiwezi kutumika kwa watu wenye tatizo la usingizi maana sio kwamba wao wanataka kupoteza fahamu bali wanahitaji usingizi. Na zaidi ukizidisha ni byebye.Dawa hiyo ya usingizi inaitwaje?
inapatikana wapi?
mbona kuna watu hawapi usingizi na hawaambiwi lolote kuhusu hiyo dawa?
nani aliita ni dawa ya usingizi?
Shukuru tu hawajakukula min kabang with 4G internet connection.