Nimefiwa na BABA Yangu Mzazi

Pole sana X-Paster mwenyezi mungu awatie nguvu na ujasili katika kipindi hiki kigumu,,
Tulitoka mavumbini na mavumbini tutarudi -Amen
 
Pole sana X Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu, may he Rest in Peace!
 
Pole sana mkuu, Mwenyezi Mungu awatangulie katika kipindi hiki kigumu.
 
Pole sana mkuu, tuko pamoja katika sala kipindi hichi cha majonzi
 
Poleni sana wafiwa, Mungu awatie nguvu...
Tunaiombea Roho ya Marehemi ilale mahali pema peponi
 
Pole sana X-Paster pamoja na familia yote. Mungu wape nguvu katika kipindi hiki kigumu. Amina.
 
Ni vigumu kupata maneno ya kukuliwaza hasa kipindi hiki kigumu. Amini kuwa hata sisi tulio mbali na Dar tuko pamoja nawe.
Mungu awapenguvu ya kuvumilia Msiba huu mzito. Pole sana ndugu yangu.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana Lihimidiwe. Amen
 
Pole sana Mkuu. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya mpendwa wetu mahali pema peponi.
 
Taarifa ya Msiba.

Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLlaah wa Barakaatuh,

Ndugu wapenzi, marafiki na member wa JF, kwa majonzi makubwa sana nawataarifu msiba wa Baba yangu mzazi ulio tokea tarehe 31 Aug 2010, uko Dar ES salaam kitongoji cha Sinza viwanja vya Sigara. Insha'Allah Mazishi yatafanyika Tarehe 1 Sept 2010. Saa saba mchana, kwenye makaburi ya Kisutu. Kwa wale wakazi wa Dar ES salaam kama wataweza kufika msibani basi watawawakilisha Member wengine.

“Sisi ni wa Mwenyezi Mungu nasi kwake tutarejea, Ewe Mwenyezi Mungu nilipe kwa msiba wangu na unipe badili yake bora kuliko huo”

إِنّا للهِ وَإِنَا إِلَـيْهِ رَاجِِعُـونَ ، اللهُـمِّ اْجُـرْني فِي مُصِـيبَتي، وَاخْلُـفْ لِي خَيْـراً مِنْـها.

Pole sana rafiki! Jikaze ndo ukubwa huo hasa kipindi hiki cha majonzi! Tupo Pamoja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom