Inna Lillah wa inna lilaah lajuun! X-P Mungu awe nawe na familia yako kwa ujumla hasa katika kipindi hiki kigumu cha majonzi ya kumpoteza mpendwa wetu! na Mungu akawatie nguvu na uvumilivu! Amen
X paster, poleni sana wewe na familia yako, mungu awajaze kheri ya kukabiliana na msiba mkubwa uliowafika, ni vigumu kukabaliana na hali hii lakini kwa rehema za mwenyezi mungu tunaamini mtaweza.
Pole sana mkuu dunia hii ni mapito na kila nafsi lazima itaonja mauti binadamu ni mavumbi na mavumbini tutarudi mungu ailaze roho ya marehemu baba yetu mahala pema peponi. Amen
X-PASTER,
pole sana mkuu Mwenyezi Mungu aiweke roho yake Peponi,
tuombe kheri sisi tuliobaki maana sote tu watu wa njia moja,
Yeye Muumba huamua atakalo, nasi yabidi kumshukuru
ingawa ni ngumu kwa jinsia ya mioyo yetu ya kibinadamu R.I.P MZEE WETU
Pole sana kwa msiba huo mzito sana maishani mwako. Mwenyezi Mungu awapeni nguvu na hekima nyingi katika kipindi hiki kigumu sana. Nipo pamoja nawe katika msiba huu kwa maombi na sala.
Kwa Mungu kila goti litapigwa na kila nafsi itauonja umauti.......! Mwenyezi Mungu ailazi roho ya mzee wetu mahali pema peponi ...Amen!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.