The Spirit of Tanzania
JF-Expert Member
- Mar 7, 2020
- 539
- 930
Hivi hiyo meter separator inafanyaje kazi mkuu? Yani naiconnect wapi na vipi ili iweze kunisomea units ninazotumia kwa mwezi?
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimeambiwa na mpangaji mwenzangu kuwa tunatakiwa kuchangia kila mmoja sh.30000/- kila mmoja yaani umeme wa sh.60,000/- ndiyo unatosha kumaliza mwezi eti kwa kuwa kila mmoja ana TV screen na kwamba kwa Siku TV moja inatumia units mbili,naomba anayeujua ukweli aijuze tafadhali!!!
Kuna jamaa yangu ni mwanasheria ana deal na kesi kama hizo. Njoo inbox nikupe namba umfungulie mashtaka. AnakuhujumuNimeambiwa na mpangaji mwenzangu kuwa tunatakiwa kuchangia kila mmoja sh.30000/- kila mmoja yaani umeme wa sh.60,000/- ndiyo unatosha kumaliza mwezi eti kwa kuwa kila mmoja ana TV screen na kwamba kwa Siku TV moja inatumia units mbili,naomba anayeujua ukweli aijuze tafadhali!!!
Simple. Mwambie msichange ila mnunue kwa zamu. Aanze yeye anunue wa elfu thelathini, ukiisha ndo wewe ununue. Case closed wisely
Asante kwa ushauri nitaufanyia kazi!Tatizo yeye ananilaumu eti TV yangu ndiyo inatumia umeme mwingi kitu ambacho sikumtegemea kuwa mjinga hivyo kwa sababu ni injinia kitaaluma
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa mfano ukilipa sh.10000/-unapewa units 28,sasa hiyo ni tarrif ipi?Muda mwingine tuache utani tumshauri mtu mambo ya msingi na sio kumpotosha, haya mambo ya umeme yanategemea na tarriff mtu aliyopo.
ᵃʳᵉᵉᵐ
Asante kwa ushauri nitaufanyia kazi!Jichange mkuu hata ujenge chumba chako kimoja uhame hapo.huo ni zaidi ya wizi
Mi naweka sh 5000 napatiwa units 41.2 kWH. Labda kuna tofauti jinsi umeme unavyotolewa
Yes. Nipo Mbeya. Ila nasikia tanesco wanacharge tofauti sehemu na sehemu. Lakini kiukweli mimi ninapokaa napewa hizo units 41.2 kwa 5000 tu
Aiseee bhasi Dar mambo ndo magumu mamaee khaaa...!! 500 sisi ni unit mojaaa mkuuHuwa napata Unit 8 kwa shilingi 1000/- tu , na shilingi 500 wananipa Unit 4
Hii ni sawa... Rafki wangu yuko kwenye tarrif ambayo anapata unit 75 kwa 9150..kwa mwezi.. Zikiisha kabla mwezi haujaisha akinunua wa 10.000 anapewa unit 28.
Jagi silitumii Mara kwa Mara huyo mpangaji mwenzangu ndiyo ana friji na jiko la umeme ajabu anadai kuwa havitumii!!
Asante kwa ushauri
Ili kuwa na uhakika kuwa havitumii mwambie aviweke chumbani kwako.Jagi silitumii Mara kwa Mara huyo mpangaji mwenzangu ndiyo ana friji na jiko la umeme ajabu anadai kuwa havitumii!!