Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Anaposema Yesu na Adam wana baba ana maanisha baba halisi wa kimwili au baba wa kiroho?

Pia muulize je, anaamini katika kitabu cha biblia?
Kama umesoma Biblia.. Adam ameumbwa na Mungu na Yesu amepatikana kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.. Nina kushauri kama bado hujasoma anza kusoma Mwanzo 1,2,3 ndio ina mzungumzia Adam.. Na Injili ya Mathayo, na Luka utapata habari za kuzaliwa kwake Yesu
 
Muulize Arsis kuhusu ismullah liadwam
Amelijibu hilo juu huko, anasema lipo. Lkini anataka watu walifanyie kazi walipate wenyewe. Sio jukumu lake kutaja jina ambalo sio lake. Isipokua ameanzaq kuonesha fomula ya kulipata.

Arsis ni mtata, anasema elimu haiji bila kuifanyia bidii. Yeye anatoa njia tu, mwenye kutupa elimu ni muumba wetu.
Simba.
 
Sababu hasa ya uwepo wa binadamu duniani ni nini?
Pia sababu ya kuwepo viumbe wengine wasio onekana km majini na Arsis duniani ni nini?
Kwanini viumbe wasioonekana hawawezi kuwa dhahiri kwa binadamu wanaogopa nini?
Tupo kwa ajili alietuumba kataka iwe hivyo. Tufate anachokiamrisha na tuache anachotukataza.
Simba.
 
Anaposema Yesu na Adam wana baba ana maanisha baba halisi wa kimwili au baba wa kiroho?

Pia muulize je, anaamini katika kitabu cha biblia?
Hilo nimeahi kumuuliza zamani akanijibu hivi;

Biblia ameisoma lakini haina majibu ya kutosha. Yeye anajua Torati ameisoma kabla haijapotea (kuhifadhiwa), anaijua Zaburi, anazijua kurasa za Ibrahim, anajua kitabu cha Yahya. Anaijua na elimu aliopewa mariam, mama wa Yesu. Arsis anamuita "meritaton".

Lakini vyote hivyo vimehifadhiwa isipokua Qur'an pekee ndio iliopo sasa yenye "summary" ya vyote hivyo na vinginevyo. Ukisoma simba utasoma na hivyo vingine. Siri ni kusoma na kuomba Allah akufungulie. Allah hamnyimi mja wake akitakacho labda kiwe ni shari kwake.
Simba.
 
Sio makaburini. Hicho ni kituo chamgu cha kukutana na Srsis kulikua kuna majengo mapya yanajengwa na ya zamani yanabomolewa, lakini hio sehemu ya hio miti hawajaigusa kabisa katika ujenzi wao. Kwanini d-sifahamu.
Huyo sio Jini bakora lakini ni jini ambae Arsis alisema :ni jemedari wa vita unayoenda kupigana Unguja".

Kisa cha Unguja kitakua kifupi lakini kitamu.
Simba.
Nilihisi ni ocean road ila kilichonichanganya ni uwepo wa hilo vumbi/udongo
 
Arsis; Hata wewe unahitaji mwili. Wewe sio huo mwili wako.
Simba
Kuna kisa kimoja Cha kweli kabisa naomba Arsis anipe ufafanuzi na Tiba:
Baba yangu ni mgonjwa (maradhi ya akili) wa muda mrefu sana. Maradhi haya yalimpata 1996 nikiwa na umri miaka ..... Kwa kipindi hicho alikua mjasiliamali mdogo huko kijijini na alikua anamalengo ya kuamia mjini Kwa wakati huokwa ajili ya kujitanua kibiashara.

Ugonjwa ulimpata akiwa polini anapasulisha mbao Kwa ajili ya ujenzi wa nyumba mjini, ghafla akapatwa na hayo maradhi akiwa uko poloni!

Sasa huu ugonjwa una mkangnyiko kutoka na ulivyotokea tunaamini amefanyiwa ushirikina. Kwa kipindi hicho chote watitembea sehem mbalimbali walishindwa baadae wakampeleka hospital akawa anatumia Sindano Kila baadae ya miezi 3. Kuanzia 1998 Hadi 2012 hivi ikawa zile dawa hazisaidii akawa tena Yuko serious sana.

Mwaka 2020 nikazunguka nae Mimi bila mafanikio nikampeleka milembe akapatiwa dawa ambapo hizi dawa alizopewa sasa ni mtihani sana Kwa sababu anatakiwa ameze Kila siku asubihi 3na jioni 1, Hadi Maisha yake yatakapofika mwisho. Kikubwa zaidi zinaua nguvu za kiume.
Kikubwa zaidi sana ni yeye kutotumia dawa hizo na hili hata alipokua anatumia Sindano hilokua ni changamoto kubwa sana. Hii inatokana na kutojitambua kama yeye ana maradhi ya akili.

Sasa hali hapo zamani ilipokua inataka kumtokea alikua anafaham kua siku zijazo atapatwa na hilo tatizo hivyo kama anapesa alikua anampatia mama anamwambia hii ni Ada ya Chama hata kama nikikuomba vipi usinipatie na anaweza akampatia na Pesa nyingine. Sasa Ile hali ikimjia tu anakua na huruma na ukarimu mkubwa sana mtu akija dukani kununua kitu anampatia vingine zaidi au kama Kuna mtu anapita nje anmwita anampatia ama Pesa au Mali kutoka dukani ni hivyo. Ile Pesa aliyokupatia akirudi kwenye hali yake yakawaida anakumbuka vizuri ikipungua hata 100 atakuambia.

Kwa ufupi ugomvi unatokea na hasira zaidi pale anapodai zile Pesa anakua na vitisho vikali na hata kutia kukupiga au kukupiga kabisa. Nilisoma Kwa namna hyo Hadi nikamaliza.

Kwa ufupi Hadi Leo baba yupo ni mgonjwa naomba Arsisi aniambie huu ugonjwa nini chanzo chake na unatibika na kama unatibika anifahamishe wapi atapata tiba.

Nina mengi ya kuongea athari tunazozipata au tuzazopitia kutokana na huu ugonjwa wa baba kama famiia na ukoo Kwa ujumla.
 
Kua makini unaelekea kukufuru, kama hujui uliza wajuaji kamwe usitumie 'binafsi naamini' kwenye mambo ya ghaib.. btw uko interested na unknown figure naona watu wametekwa na simple social experiment! hakuna dhambi kubwa kuliko shirki kwa muislam! Duh mmefikia hatua mnamuambia jamaa awaulizie kwa hlo dubuwana lake SMH

Iko wazi ata Quran inasema yesu hana baba, this dude promotes blasphemy yall.. kama mtume uswatul hasan hajawah kua na jini au ku promote kutafuta majibu kwa kiumbe chochote mnatekwaje kindezi hvo na huyu janjajanja?

Tufanye toba, Allahu A'aalam
Kwakweli kwa hili hata mimi nimewashangaa ndgu zangu katika imani..
Kuna mmoja huko juu anauliza kupata usahihi wa aya anazoamini toka kwa huyo Arsis.

Nilitegemea watu kuelimishana ila nachoona kuna wenye elimu ndogo wanatekwa na wanampa umungu mtu Arsis.

Mleta uzi waelimishe watu watafute maarifa kuthibitisha kama afanyavyo mata chache Faiza, la sivyo kuna viumbe mnatoa kwenye reli kabisa badala ya kuelimika.
 
Amelijibu hilo juu huko, anasema lipo. Lkini anataka watu walifanyie kazi walipate wenyewe. Sio jukumu lake kutaja jina ambalo sio lake. Isipokua ameanzaq kuonesha fomula ya kulipata.

Arsis ni mtata, anasema elimu haiji bila kuifanyia bidii. Yeye anatoa njia tu, mwenye kutupa elimu ni muumba wetu.
Simba.
Nakumbuka alisema ni mtajie idadi ya sura zinazoanza na Alif Laam Miim nimejibu ni sura 8 akasema tutaenda taratibu sasa ndio nauliza nini kingine alisema atatoa code, Code ya kwanza tayari Code inayofuata ni ipi?
 
Kama umesoma Biblia.. Adam ameumbwa na Mungu na Yesu amepatikana kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.. Nina kushauri kama bado hujasoma anza kusoma Mwanzo 1,2,3 ndio ina mzungumzia Adam.. Na Injili ya Mathayo, na Luka utapata habari za kuzaliwa kwake Yesu
Nimevisoma mkuu na kuvielewa vyema, ninachotaka kufahamu hapa ni kuhusu mtazamo wa arsis kama aniamini biblia au lah! Maana bado hajajipambanua yeye ni nani ila kupitia majibu yake nitaweza kuchakata na kumpambanua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom