Yaani mkuu, majinn si ni viumbe kama sisi? Kwani wao hufanya juhudi na ibada ili kuonana na binadamu?
Wao wametuzidi nini sisi, si inasemekana sisi ni daraja la juu kuliko wao?
Iweje ukitaka kuonana na hao wa angani ni hadi ufanye ibada sana? Na wao wakitaka kuonana na wewe inabidi wafanye ibada sana??
(Kwa uelewa wangu mdogo ipo hivi!!)
Ulimwengu zimegawanyika kwenye makundi 2
1.A'alamul nasuut (ndo huu ulimwengu wetu, na ndio ulimwengu dhalili na dhahifu kuliko zote
2.A'alamul ghaib .... hapa ndo Kuna kila kitu (huu n ulimwengu usioonekana)
Note: ulimwengu usioonekana n 98% sasa huu ulimwengu umegawanyika kwenye makundi 3
Hapa ndo Kuna ghaibu ambayo ukifanya kitihada unaiona (ndo majinn wapo hapo)
Kuna ghaibu ambayo haionekani mpk siku ya kiama n.k
Sasa ipo hivi binaadam kuziona hizo ulimwengu zingine akiwa kwenye umbo lake la asili anaweza.... ila shart ni moja tu, mpk awe mchamungu sana na asiwe mtu wa maasw!!
Hapa sheria n kama ngazi... ukiwa ngazi ya juu unaona vyote vya chini ila ukiwa chini vya juu kwako n Giza, kwahyo viumbe waliopo ulimwengu zisizoonekana na daraja zake wao wanatuona sisi sababu sisi ulimwengu wetu n dhalili na ndio wa chini zaidi
Ila majinn na wao hawawaoni malaaika sabb wapo kwenye ulimwengu tofauti, na malaika pia wao hawamuoni Mungu sababu wapo ulimwengu tofauti
Ila Mungu anaona ulimwengu zoote sababu yeye ndo yupo level ya juu kabisa...
Kwahyo kuhusu binaadam kupata ukhalifa wake ni mpaka awe na vigezo... ukiwa mchamungu haswaa wewe utakuwa master wa majinn na malaika pia!!!
Lakini huko hatufiki sababu ya kutokuwa karibu na Mungu