Vionjo vya Arsis - Majini ya Kojani- Pemba 10.
Baada ya kukoga kogas na kujitoa jasho la matembezi ya sokoni. Nikajinyoosha kitandani, nikawa nawaza mkasa mzima huu wa kojani, nikasema nitawauliza maswali mengi sana, sina majibu nayo. Nikaanza kupitiwa kama na kiusingizi cha uvivu nikasikia mlango unagongwa. Nikajua Jini 1, nikamwambia pita, akafungua mwenyewe m;lango, mimi nikawa nimekaa kitandani yeye akaenda kukaa kwenye kiti, baada ya kusaimiana.
Jini 1; Pole sa Simba naona mambo ya Kojani yamekuchosha, unaonesha umechoka.
Mimi' Sio kimwili, kimawazo. Nina maswali mengi sana, lakini sina majibu.
Jini 1: kama maswali ya kujua tu mambo, subiri tumalize zoezi la leo halafu utaulliza maswali yako, nitaloweza kuyajibu nitayajibu, nikishindwa yupo mama, yupo Aris watakupa majibu.
Mimi; Poa, naona sia mawali ya dharura isipokua ya kuelewa tu.
Jini 1; Basi usiwe na hofu subiri. Sasa sikiliza kilichonileta sasa hivi.; Leo kuna mpoango wa sinema ya mwisho, mpoango mdogo tu, umepangwa na Kamanda, ili muweke na kulinda hehima yenu na yao kwa kazi walioifanya.
Mimi; Mpango geni tena, niliyoyaona na kuyasikia ya Dokta yamenitosha jamani.
Jini 1; Ya Dokta ukurasa wake wa Kojani umeshafungwa, wala hautousikia tena. Mmefanya kazi nzuri sana. Dokta sasa yupo fiti kabisa hana tatizo lolote la vijini na wala hatokua na tatizo labda kwa uwezo wa Muumetu. ba w, vivuli na vijini na vijini vya tarasimu vyote vya kijingajinga vya Mzee Ali vimesambaratishwa, vingine vimeuliwa, vingine vimefungiwa kufanya kazi, vinatiwa adabu na wenyewe wakubwa zao, pale pangini, kwa makubaliano na Kamanda.
Mimi; Vimeuliwa? Mbina hili jipya kwangu.
Jini 1; Si unakumbuka Mzee Ali antengez vijini vingine vya rtarasimu? Hivyo alivyomsukumia Dokta vimeuliwa, yule mzee ni mjinga sana, badala ya kutumia ujuzi aliopewa kwa faida, yeye alikuwa anutumia kufanya mambo yakijinga kabisa. Tena ashukuru Mungu sana, bakora kamuombea sana kwa Kamanda na kwa mmku bwa wao, wamuachie lakini akiri kua atafanya toba ya kweli na ataacha mambo ya utapeli na kuumiza eateja wake wanaomfata.
Si unajua majini hawa wakubwa wanaheshimiana sana, Wakaheshimu ombi la Bakora, wakaweka mkataba na Mzee Ali na wakubwa zake, akiponyoka tu ndio anamalizwa kila kitu, sasa hivi atakua mtu wa sadaka sana. Alikua kishakata tamaa, Bakora akamuhurumia, lakini hajamwambia kama ni yeye Bakora aliyemuombea, Ilikua Mzee Ali ahame kabia Dar. Karuhusiwa arudi lakini kwa heshima na adabu. kma kuambiwa ataambiwa na majini yake huko...
..Kwaa hio vijini vya tarasimu vimeuliwa, vivuli, hivi hajavituma kwa Dokta, alikua anaviweka awapchike watu wanaokwenda kwake, navyo vimeuliwa vyote, na kaapishwa kua hatorudia kutumia uchawi wa kijinga ule. Yeye ataruhusiwa kuwatoa kwa wateja wake na kuwaua au wakubwa zake watavyompa maagizo, basi. Umeelewa Simba?
Mimi; Nimeelewa kuhusu mzee Ali, lakini...
Jini 1; Subiri Simba, sikuja kwa haya lakini mradi tumeyaanza wacha nimalizie kwa ufupi.
Jini 1; hapa ndio patamu; Unajua Dokta alitupiwa vivuli na mama mkwe wake wa mumewe wa kwanza ili asithaminike kwa mumewe, yaani amuone kama kero tu, sasa hata alivyoachika hivyo vivuli vilikuwepo. Hivyo havikuwa shida sana itmpata aliyevitengeza alikuwa hai, Mzee mmoja wa Kigunya, wa Kenya huko, kishakua mzee sana, sasa anafanya toba anaagua tu, sema alikua na kasoro moja...
Alishaingia mikataba zamani na majini wa kumletea vivuli, ikawa kila mwaka anachinja kafara ya wale wakubwa zao, na wale wakiwepo ama hawajatolewa kwa mgtu aliepachikwa nao, ikitolewa kafara kwa wakubwa zao wanawaambia andeleeni na kazi mliopewa, vikawa mara kwa mara vinamzonga hata kazini anaonekana kama nuksi na mkporofi kaingia. Ndio ikawa mchezo huo huo miaka na miaka. katika hivyo hivyo ndio vilimfanaya asimalizie shahada yake ya juu kabisa. lakini sasa kwisha hivyo.
Jini 1; Vilivyowapa tabu kina mama na Bakora mpaka ikabidi waongee na Kamanda na kamanda ikabidi alete majini wa kuchunguza, sio hivyo. Hivyo vingine vya kutengenezwa, alisukumiwa kutokea Tanga, na mke mwenzie kwa mumewe wa pili, na huyu mumewe wa pikli ni Dokta vile vile, lakini sio mkubwa kama yule wa kwanza.
Hivi kama nilivyokwambia, vilikua vijini vya kutengeza, na yule alievitengeneza kafa muda tu, na alivificha vitu vyake akavimwagia uchawi visionekane, vilikua bya vya watu wengi tu, sio Dokta peke yake, maana alipoanza kuummwa yule akajua haponi yale maradho yake. Sasa waliomrithi hawajui kavificha wapi vitu vingine, kumbe alivichimbia makaburini, akamwaga na dawa zake juu, hilo kaburi la zamani sana, hata wenye marehemu aliezikwa pale wakienda kumuombea dua marehemu wao, kaburi hawalioni...
Hivyo ndio vilivyoleta kasheshe kiasi, lakini vikapatikana, hilo lilifanyika Dokta aliporudi tu kutoka Unguja, wala hajaambiwa hayo ya mkwewe wala ya huyo mke mwenzie yataleta chuki, yalifanywa kimya kimya tu.
Na wewe usimweleze lolote Dokta kuhusu hayo, Ndio ujue kutunza siri za watu. kwa ufupi na vyenyewe vimeuliwa. Ukitaka kujua zaidi mambo hayo muulize Arsis.
Jini 1; Sasa kilichonileta; Leo unatakiwa uende Kojani ukiwa umejificha kwa pete yako, kuanzia juu huko kabla hujavuka, utanikuta mimi nitavuka na wewe. Bakora hatokuwepo kivukoni. Tutaenda moja kwa moja, utaenda kukaa alipokaa Bakora lakini usifichue kabisa, mpaka Bakora atapokwambia, hata Bakora utamuona wewe tu, hakuna jini waa bunadam mwengine atakaemuona. baada ya hapo utafata maelekeso ya Arsis. Hauna kazi yoyote leo, kazi yako ni kujificha tu, utaelewa kwanini zoezi lisha. Umeelewa?
Mimi; Nimeelewa.
Jini 1; haya kwaheri, uwahi huko hakifanyiki kitu bika ya wewe kuwepo.
Mimi; Kwaheri.
Nikaona nikilala hapa nitachelewa, nikaona nitoke tu, niliona maji ya miwa barabarani kule nitatembea tembea ninywe maji ya miwa nikisha sali ndio nitaenda Kojani, kama kuchelewa wacha wachelewe, niliuona msikiti pale barabarani. Nikatoka zangu.
...
Vionjo vya Arsis - Majini ya Kojani- Pemba 11.
Nikpigiga juisi ya maji ya miwa, nikaenda kuali nilipotoka, pale pale Masjid nje nikapata Kibajaji kikanipeleka kituo cha Kojani, nikamlipa kabisa mwenye Kibajaji nikiwa ndani ya Bajaji kabla hatujafika. Lengo likiwa nikishuka tu nijifiche, nisionekane.
Kufika tu nikaiminya pete kabla sijashuka, nikawa najisemea mwenye Kibajaji akigeuka kuatazama akiona hakuna mtu kazi kwake.
Niliposhuka nikamuona Jini 1 kwenye kona karibu na kiduka cha pale kivukoni, akaja, akanambia haya Sima tuwahi, umefanya vyema kabisa, mimi ningekua sina pete zetu hizi tusingeonana.
Tukavuka bila mimi kuonekana, Jini 1 pale hakijificha, alikua anaonekana yeye tu, maana yeye ndio alilipa alilipa pesa zaidi akamwambia Mwenye ngarawa, hizo zako, weka tu. Alikua hajui analipwa na nauli yuangu.
Tyulipofika viwanja vya chano, watu wanacheza, kama kawaida wakubwa wapo ndani, watu wamejaa vumbi, nikashangaa, nikaona leo walijipaka rangi nyeupe usoni, wengine zina mistari mekundu, wengine zina mistari meusi, wengine nyeupe tupu. Kufika meza kuu nikaona Bakora yupo pale na pembeni yake kuna nafasi ya kukaa, akanisharia nikakae pale. Nikamuona yule Mzee alioaibishwa na Bakora kwa kunyamazishwa na kukalishwa chini kiajabu yupo pale lakini alikuwa kawaida tu hana ile muonekano wa kugtamba tena, kanywea.
Watu wakaanza keleke tunachelewa tunachelewa. Mzee Ali akasimama akayamaZisha kila kitu, ngoma ile ya pale ndani ikasimama, nje uwanjani huko kulikua na ngpma zaidi ya moja, kama vikundi vikundi hivi hivi.
Mzee Ali; Endeleeni kushereheka, tunangoja wakuu waturiuhusu tuanze kumalizia ngwe ya mwisho ya shughuli yetu, anaeona anachelewa aondoke.
Bakora akaninong'oneza jifichue tu, na yeye akajifichua. Mzee Ali inageuka tu kuongea kutazama akae, akatuona, akashikwa na butaa, akatuuliza, tuendelee na shughuli wakuu au kuna maagizo yoyote. Nikaona hata meza kuu wote wameshangaa kutuona tumekaa pale.
Bakora: Endelea tu.
Mzee Ali; Akasimamisha tena ngoma kwa ishara tu, watu wakawa kimya; Shughuli yetu inaanza kama kawaida vyano vitapita nje hapo kama ada, na wakishapita watu wa chano wote ndipo sisi tutawafata nyuma. haya twendeni nje tukawapokee.
Mzee; Ali; Wakuu naomba twendeni, hapo mez kuu yote wameanza kushuka kuwahi nje.
Bakora: Nendeni, lakini msikipeleke chano mpaka sisi tufike, tangulieni, sisi tutakuja mwisho. Akshuka Mzee Ali akatoka nje ukumbi ukawa mytupi.
Bakora: Sikiliza, Simba, sisi tunakwenda kabla yao wakati wao wanapokea wenye kuleta Chano hapo nje, tutaingia kwenye maji ya tumbo, trunajificha kuanzai sasa wasituone, wakifika huko, tutajifichua kwenye maji watatuona sisi tunatokea baharini. Tukajificha tukaondoka.
Nje pale ndio nikaona kumbe zile rangi na walizojipaka na bendera zake na mwari wao aliebeba chano na kundi lao la ngoma. Ndio nikajoionea wapo watu wa kila aina hapo, taani waarabu, wazungum wahindi, na wakojani ndio wengi. Kila mmoja na kundi lake, wemye kucheza, wenye kulia, wenye kutingisha vichwa, yaani zaidi ya nusu waliokuepo pale nje wamepandisha mashetani.
Tukaingia kwenye maji kama Bakora alivinambia, hivyo hivyo na nguo zetu.
Nikaona wanakuja, Mzee Ali akaongea kitu na mbeba chano kikubwa. Lilikua sinia kubwa kweli, nikaona wamesimama ufukweni, yule binyti kasimama na chano Arsis akanambiajifichue tutoke. Nikasikia watu wanguna, haiwahi kuwatokea watu kutokea ghafla bahatini. Mzee Akawa anakodoa tu macho na wenzake wa meza kuu. Tukatoka tukasimasima pembeni kidogo, wakati tunatoka Bakora akamwambia endeleea na shughuli yenu. Maee Ali akaanza kupaza sauti...
Mzee Ali; Maini na mizimu ya pemba, na majini wote kutoka nchi na sehemu mbali mbali mliohudhuria, sasa kama ada ya hapa, kitatangulia chano kikubwa kupelekwa wengine wote mtabaki na vyano vyenu mpaka atoke mjumbe wa kupeleka chano. Aliebeba chano Kikubwa akaanza kuingia kwenye maji taratibu, huku Chano kipo kichwani.
Alipokua anaingia, wenye kushangulia wana shangilia, wenye kulia wanaliza, eengine wanapiga kelele za kufuru " mzimu mkuu wa kojani, gtutalie shida setu" mwengine nitatuiea shida zangu, yaani kila namna ya maombi anaombwa shetani. Mie nikawa naomba toba tu kimoyomoyo. Na hapo ndio nikajua kua yule mwari alikua akfungwa kanga tu kiustadi zilikuasio nguo zile, maana khanaga zilipoanza kuingia maji zikawa zinapanda, akaingia akatembea baharini mpaka maji takamfunika kabisa ikawa kanyua mikono kulibeba lile sinia, akaendelea kidogo mpaka likabaki sinia tu juu ya maji, naona akaliahcia lkakini ikawa kama analisuma kwa chini kuelkea baharini, yeye haonekani linaonekana sinia tu linakwenda, kufika sehemu, nikaona aja kutokea maji amabayo imetokeza shingo, na sinia lianenda zakw lenyewe.
Mie nikawa na shangaa na sinia linazidi kwenda tu lenyewe.
Bakora mchezo wa kuigiza tu huo, mazingaombwe tu hayo atakufahamisha Jini 1 baaadae.
Yule mnbeba chano aktoka moka nje Khanga zimerowa zimemnganda mwilini, ni binti kashibew wa haja kweli kweli, alipotoka tu.
Mzee Sli haya mpeni khanga zake mpya hizi hazirudiwi tena.
Kuna kina mama wakamletea kumfunga kanga mpoya wakafanya kama pazia hivi na khanga, walipotoa pazia ikawa yupo fresha na khanga zake kavu zimefungwa kiustadi kabisa.
Mzee Ali; Chanoi kikubwa kishapokelewa, haya sasa nyie pelekeni kwa mstari. Asiwafate asie na chano, kabisa tena, madhara yake makubwa.
Mabinti wakaanza kuelekea kama alivyofanya yule lakini hawa ikawa kila wakifika maji ya kiuno mooja anaenda kushoto mmoja kulia, yaana wanapanua wigo mpaka walipokaa mstari kwa baharini, wakaanza kuingia kama mpoka maji ya kunyatu mikono, kama alivonya yuule wa mwanzo mcheo ukawa huo wakaanza kutoka, sasa kila anaetoka kikundi chake akishatoika nje ndio kinafanya pazia anavikwa khanga mpya. Dah, hawa wabeba nikajua wanachaguliwa kweli kweli, yaani ni ushetani. Hakuna mwanamme rijali ataevumilia kuwamezea mate. Vile wanavyotoka zile khanga zingine zimepanda juu na zilivyogana mwilini show zote nje, si nyuma si mbele. Naona wanavotabasamu ni kama wamefundishwa kwa kina, waumize mioyo ya marijali.
Walipokwisha toka wote;
Mzee Ali; haya jamani, chano chote kimepokelewa, sasa kama kawaida yake mwenye lake aseme, mwenye chochote cha kupeleka baharini apeleka, na nawashauri sote tyujiyie kwenye maji japo mwili mzima upate maji, kila mtu kwa raha zake. Tukitoka hapa, karamu yetu kama kawaida kiwanjani, wale wapishi na wandalizi wawahi kutoka majini.
Bakotra; Haya simba wakati wanaingia bahatrini, jifiche tuondoke zetu.
Mzee Ali ndio alikua kaoingoiza msafara akaanzq yeye ne meza kubwa yote kuingia baharini, wakaftatia watu wote, wkubwa, wadogo, wazee, vijana, wanaume kwa wanawake. Mimi na bakora tukatazama kidogo oirika zao, wenye kwenda maji ya kina huko wenye kuongelea, waliobaki maji ya mwanzo mwanzo wanajizamisha haya.
Tukaondoka na Bakora akanambia, shughuli yao ndio imeisha, sasa wanapoakuliwa pilau, tukapita pale, hakuna watu uwanjani ndio nikaona masufuria makiubwa zaidi ya 20.
Bakora: Utangoja kula Simba?
Mimi; nani ale nyamafu hizo zilizochinjwa kwa ajili ya kafara za majini, twende etu bwana. Nimeshajionea shughuli zote za kishirikina za Kojani, inatosha. Bakora, haya twende, mengine atakuja Jini 1 kukueleza ukihitaji.
Bakora; Tulivofika karibu ya nbandari ya ngarawa akanambia jifichue tu. Tukapanda ngarawa na Bakora, upande wa pili tukakuta vibajaji kibao, tukaagana na bakora, nikapanda kimoja nikamuelekeza tukaondoka zetu.
Hoiteli, nikauliza resepshen kama Dokta amaesharudi, nikaambiwa bado. Nikapanda kwangfu nikakoga vizuei, nikasali. Nikakaa kuwasubiria, Niakapiga simu nyumbani kwa mama, baada ya kusalimian...
Mama; habari zote nazipata hapa, mkeo na mapoicha ananitumia. wanaonesha wamepapenda mkoani vijini huko.
Tukaagana nikapiga simu kwa wife. baada ya kusalimiana.
Wife; Nimekupigia sana simu inaita tu, umeshaoa Pemba mume wangu, hatiuambizani?
Mimi; Niliizima sauti msikitini nikasahau kuiongeza z)sauti. Vipi huko?
Wife; Ndio nilitaka kukuuliza muda mrefu, hapa madaktari wa Kipemba mashiga zake Dokta wa metuzuwia mpaka tule chakula cha usiku, sasa mume wangu, tutachelewa kurudi, si unajua vyakula na maongezi, tukichelewa usiwe na wasiwasi kama kuna choxxhote tutakujiulihsa. Hiwa wasi youer dayt?
Mimi; Siku nzuri nimetembea tembea nimeend mabli kidogo, nimerusi si muda mrefu. Vipi Dokta? Wife yupo, nimemwacha anaingea na wenzake, mimi nimetoka kidogo kuongea na wewe na simu. Njoo basi D. nikamwabia aah poa nyie endeleeni, sitaki kuwekwa mtu kati na wanawake watupu huko.
Wife; Unajifanya umesahau, ungesema hayo siku zile?
Mimi; Mke wangu tuombe tba tu, wala tusiyakubuke ya ushetani wa zamani, tulikua kizani.
Wife; Amiin, mimi naomba usku na mchana mume wangu kila nikisali, naomba sana Mwenyezi Mungu atutoie kabisa kizani.
Wife alikua kama mimi, haongei kabisa na simu zake mbele za watu, au kukaa, kua bize na meseji wakati anaongea na watu. Naona hio tabia, wote nyumbani tunayo.
Mzee anasema simu na wakati wake, nyinyi mushukuru sasa hivi tunapiga na lupokea simu wakati wowote. Zamani sisi ilkua hakuna hayo. Kupiga simu mpaka mtu aende posta ndio akapige. Nyinyi jopangieni, wakati wa simu n zisiwapotezee muda wenu, sana sana zinazidisha umbea tu. Tukawa tunamuelewa sana.
Nikawa sina budi, ni kuwasubiri tu.
...