Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

wakati mwingine Arsis anazingua yeye akiulizwa shida zinazohitaji tiba amekariri jibu moja tu "fanya ibada,sali sana acha maasi" ndo imeisha hivo inaweza jambo hana ufahamu nalo basi amwite Arsis au bakora amshirikishe hao watajua tu kwa njia zao kisha yeye simba ndo atoe majibu hapa atakayopewa na hao watu wa kazi sio kukimbilia fanya ibada,acha maasi kwani ni nani ambae hana dhambi maana wafanya ibada na sala ni wengi sana ila wachamungu ni wachache.!
Hilo ndilo la kwanza, unaweza kutafuta mchawi kumbe mchawi ni wewe mwenyewe. Husali una mlolongo wa maasi, utakosa wapi kua na matizo ya kiroho?

Kuna Hasad, ni tatizo kubwa kuliko uchawi, lakini mara nyingi hasad tunaikaribisha wenyewe bila kujijua. Hasad ni husuda.

Tiba za kiroho ni tofauti na tiba za kiganga na kitabibu.
Simba.
 
Naam, Nitajaribu kuweka katika mpangilio ambao unaweza lete mtiririko mzuri nitaanza na Jinni

JINNI - Ni kiumbe wa Allah aliyeumbwa kwa lengo la kumuabudu Allah, Wameumbwa kwa moto na wanauwezo wa kuchagua kufanya mema au maovu, sawa na wanadamu.
Wanaulimwengu wao ambao wanadamu hatuwezi kuwaona labda mpaka ufunguliwe macho kama bwana Simba. Wapo wema na wabaya lakini wana maisha simple compared na mwanadamu yaani wengi katika majini ni waasi wanafanya mabalaa sana habari zao kwa undani zipo katika Quran Surat jinn lakini pia Quran 51:56, 6:128.

INSAN - Huyu ni mwadamu ameumbwa kwa madhumuni maalum ya kumuabudu Allah na kuwa khalifa duniani, Kama walivyo majini basi na wadamu wana uhiari wa kufanya mema au maovu. Habari za mwanadamu zimejaa katika quran.
Kuhusu uumbwaji wake 23:12 -14 Inaeleza malengo ya kuumbwa kwake 51:56 Inaeleza.
Mpaka hapa utaona viumbe ambavyo vimeumbwa kwa lengo la kumuabudu Allah na wana uhiari ni majini na wanadamu ndio maana hukmu siku ya malipo ni kwa ajili ya majini na wanadamu tu.

IBLIS - Huyu ni katika majini, Ndiye aliyekataa kumsujudia Adam, na akafukuzwa katika rehma za Allah, Jambo ambalo watu wengi hawajui ni kuwa Iblis anawadanganya sio wanadamu tu bali hata majini wenzake.
Majini kwakuwa wanaweza kuwa wema au wabaya basi iblis huwa anawadanganya majini wenzake wamuasi Allah kisha anawatuma waje kuwadangaja wanadamu pia, Hivyo kuna majini wengi tu hawaijui haki kwasababu Iblis anawachezea kwa kuwalaghai.
Imeelezwa katika hadithi kuwa iblis ana kundi kubwa la wafuasi na anawatuma kila siku kuwafarakanisha wanadamu

عَنْ جَابِرٍ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ: «إِنَّ إِبْلِيسَ يَضَعُ عَرْشَهُ عَلَى الْمَاءِ ثُمَّ يَبْعَثُ سَرَايَاهُ فَأَدْنَاهُمْ مِنْهُ مَنْزِلَةً أَعْظَمُهُمْ فِتْنَةً. يَجِيءُ أَحَدُهُمْ فَيَقُولُ فَعَلْتُ كَذَا وَكَذَا فَيَقُولُ: مَا صَنَعْتَ شَيْئًا. ثُمَّ يَجِيءُ أَحَدُهُمْ فَيَقُولُ: مَا تَرَكْتُهُ حَتَّى فَرَّقْتُ بَيْنَهُ وَبَيْنَ امْرَأَتِهِ، فَيُدْنِيهِ مِنْهُ وَيَقُولُ: نِعْمَ أَنتَ»

Tafsir : Kutoka kwa Jabir, alisema: Mtume Muhammad ﷺ alisema: "Hakika Iblisi huweka kiti chake juu ya maji kisha anatuma vibaraka wake. Yule ambaye anaonekana kuwa karibu naye zaidi ni yule ambaye anafanya maasi zaidi. Mmoja wao huja na kusema: ‘Nimefanya hivi na hivi,’ naye (Iblisi) husema: ‘Hujafanya chochote.’ Kisha mwingine huja na kusema: ‘Sikumuacha mpaka nilipomtenganisha yeye na mkewe,’ naye (Iblisi) humkaribisha karibu naye na kusema: ‘Wewe ni mbora''
Hapo utaona jinsi Iblis anavyowatuma majini kufanya mabaya lakini pia Wanadamu wapo wanaomuabudu huyu Iblis.

SHETANI - Hii ni sifa ya kiumbe muovu katika majini na wanadamu hivyo jinni au mwanadamu akiwa muovu anakuwa shetani ingawaje katika quran kuna aya nyingi zinataja shetani zikimaanisha Iblis hii ni kwa sababu Iblis aliaswi na akahukumiwa moto na lengo lake nikutafuta kundi kubwa katika majini na watu wa kwenda nae motoni hivyo Iblis ni shetani moja kwa moja, Jinni na mwanadamu wanaweza kuwa mashetani kwa vitendo vyao vya kufru. Nawaweza wasiwe mashetani kwa wema wao na uchamungu.
Ndio maana kabla ya kuanza kuosoma Quran tunataka hifadhi kwa Allah kutokana na shatani kwa maana wabaya wote katika watu na majini na Iblis mwenyewe Allah atukinge kwao.

Nitaendelea Inshaalah.
Kuna mtu aliuliza juu ya maana ya haya maneno ninayoelezea kwa mujibu wa quran nadhani ni FaizaFoxy naendelea nilipo ishia.

AFRIT au IFRIT - ni aina ya majini.
Katika maelezo ya Qur'ani na Hadithi, 'Ifrit ni majini wenye nguvu Wanajulikana kwa uwezo wao mkubwa na mara nyingi wanahusishwa na uovu na uasi. wametajwa katika quran surat Naml aya ya 39
قَالَ عِفْرِيتٌۭ مِّنَ ٱلْجِنِّ أَنَا۠ ءَاتِيكَ بِهِۦ قَبْلَ أَن تَقُومَ مِن مَّقَامِكَ ۖ وَإِنِّى عَلَيْهِ لَقَوِىٌّ أَمِينٌۭ
Tafsir : Akasema Ifrit Mimi nitakuletea kiti chake kabla hujainuka kutoka mahali pako, na mimi nina nguvu juu yake na ni muaminifu.’"
Katika aya hii, Nabii suleyman (a.s) aliwauliza baraza lake na tunajua nabii sulyman alipewa utawala kwa wanadamu na majini na wanyama hivyo aliuliza nani anaweza kwenda kuniletea kiti cha malkia wa sheba aliyeitwa balqis ndiyo huyu ifrit akamjibu mimi naweza kuleta kabla hujanyuka kutoka kwenye kiti chako.

Pia katika kisa maarufu cha Isra na miraj Bwana mtume Muhammad (S.a.w) wakati wapo na jibril mtume aliona kiumbe kuna wafuata mtume akamuuliza jibril ni kiumbe gani hicho ndipo jibril akamwambie mtume huyo ni Ifrit minal jinn nikufundishe maneno ambayo ukiyasema ataacha kutufatilia, Jibril a.s akamwambia sema.
بِسْمِ اللَّهِ الَّذِي لَا يَضُرُّ مَعَ اسْمِهِ شَيْءٌ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
Bismillahi alladhi la yadurru ma'asmihi shay'un fil ardhi wa la fis-sama'i,Wahuwas-sami'ul-alim":
Tafsir:
Kwa jina la Allah, ambaye hakuna kinachodhuru, iwe kwenye ardhi au angani, naye ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua."
Baada ya mtume kusema maneno haya jinn huyu akaacha kuwafatilia hii ni dua ya muhimu na inasisitizwa waislamu kuisoma katika adhkari za asubuh na jioni.

Kwa ujumla, Ifrit ni Majini wenye nguvu na waovu, lakini siyo wote wanakuwa na tabia mbaya. Kama majini wengine, wanaweza kuwa na tabia mbalimbali na uwezo wa kuchagua matendo yao.

MALAIKA - Kwa mujibu wa Qur'ani, malaika ni viumbe wa kiroho walioumbwa na Allah kwa nuru kwa ajili ya kutekeleza amri zake na kusimamia masuala mbalimbali ya ulimwengu. Malaika wana sifa maalum ambazo zinawafanya kuwa viumbe wa kiroho tofauti na wanadamu na majini.

Sifa za malaika​

  1. Viumbe wa Kiroho : Malaika ni viumbe wa kiroho
  2. Wanawajibika kwa Amri za Allah : Malaika hutekeleza amri za Allah na wanapokea maagizo kutoka kwake. Hawana uhuru wa kuchagua kama wanadamu; wao huishi na kutekeleza amri ya Allah kwa utii kamili.Sura ya 16 aya 49-50.
  3. Wanaweza Kujidhihirisha : Malaika wanaweza kujidhihirisha kwa watu kwa umbo maalum au kwa njia ya kiroho.
Wapo wengi sana ila kubwa zaidi kwao hawamuasi Allah wanatekeleza wanaloamrishwa tu wametajwa sana katika quran na hadithi kuna Jibril, Mikael, Israfil, Munkar, Nakir n.k na wanamajukumu tofauti tofauti na wapo wengine wao wanafanya ibada tu na kumtukuza Allah.
 
Swali lako zuri sana tena sana.

Alieandika Qur'an aliukuta moto upo tayari.

Alitia kidole ukamuunguza. Wewe kwani ulijuaje kama moto unaunguza?
Simba?
Mwenzio kaandika ulikuwa Moto wa tofauti ina maana sio huu unao uongelea hapa.
Sasa nataka kujua huo Moto wa tofauti ukoje ?
Aweke sifa zake hapa Kama unachoma ukitoa chumvi au lah.
 
Somo la Adamu ungeendelea nalo inaonekana limebeba mambo mengi.
kuhusu hili la sasa la majini kuumbwa kwa moto umesema quran imetumia tashbiha katika hili tupe ufafanuzi, Inaposema majini wameumbwa kwa moto ina maana gani?
Mara nyingi kazi yao kuharibu.

Tutafafanua kwa kina siku za usoni, kupitia Qur'an.
Simba.
 
tusubiri jibu la Arsis maana shida kama hizi hatoagi majibu ya maana yeye amekariri jibu lake la "fanya ibada,sali sana acha maasi" ndo kamaliza hivo hakupi suluhisho ya kipi ufanye ujitibu shida yako..ngoja aje
Unajua, cha kwanza kabisa kabla hujamtibu mtu mambo ya uzazi unatakiwa uelewe, ameolewa au anataka kuzaa kwa uzinzi tu?

Ukijua ni uzinzi kwanza umpe ushauri mpaka aolewe na huyo anaetaka kumpa ujauzito ndio umtibu.
Simba.
 
Kuna kitu kinachoweza kufahamika kama 'kufungika/kufungiwa ya kunasibika kuyajua kwa wakati'; kwa kiingereza ni mambo ya 'compartmentalization'...

Katika majukwaa kama haya, 'mada' ni jambo lenye asili ya kujiwekea mpaka wa kuyasikia na kuyajua kwa wakati; lakini vipi ikiwa 'asili ya mipaka katika kutaka/kupenda kuyafahamu kuyajua mambo' husigana na nasibu ya Ujumuifu wa 'Maarifa na Maarifu'(?)

Kwa mfano, huu uzi unajina: "niliyoyashuhudia-nilipofunguliwa macho"

Je, unatambua jambo la 'Kufunguliwa macho' lina asili ya 'Nuru ya Ufahamu, Maajabu na Mastaajabu' yake?

Ipi inaweza kuwa 'mada' katika 'Nuru ya Ufahamu, Maajabu na Mastaajabu yake' khasa?

Kiufundi, sisi sote ikiwa ni watu wa 'akili' na basi nasibu ya 'dini', adui mkubwa wa kupambana naye ni 'Kasumba' ya 'Mafungu Elimu'...

Labda iwe sisi watu hatuna mpango na 'Maarifa na Maarifu' ila 'kujifurahisha na hili ama lile kwa wakati'; haya ni mambo ya kujichagulia...

ALRIGHT, Simba, 'Ninachangamsha Jamvi'--Ukiona nazidisha sana kupilitiliza mipaka, sema!
Isome mada utapima wewe nini ninachokijua na nini nisichokijua. Ndio kwanza tupo chapter 1.

Wanasema. kisichopimika hakipo.
Simba.
 
Hapa point kubwa ni kubadili lifestyle, kuwa na staili ya maisha iliyobora, kutaimarisha afya ya akili, mwili na kiroho.
Kwahiyo kama ni mtu wa maasi acha au punguza. Kama hufanyi mazoezi basi hujachelewa na kama ni mtu wa kula vitu vya hovyo mradi tumbo lijae, acha. Badili mfumo wa maisha.
Usipunguze, acha kabisa.
Simba.
 
Usipunguze, acha kabisa.
Simba.
Ni suala la mchakato, kuacha pigo za “cold turkey” ni mwanzo wa kufeli. Kwahiyo una taper down mdogo mdogo mpaka unaacha kabisa.
 
isome mada utajua nini ninachokijua na nini nichokijua. Ndio kwanza tupo chapter 1.
Simba.
Simba, ninakusoma na ninakusoma tena...

Mambo ya 'Chapter/Chapters'....

Huu ukumbi ni wako; sema kila unachoandika 'kinapimika' ama/na 'kutathminika'--kwa kheri lakini.

Siyo kwamba hauna unayoyakosea ama vipi--ila unayo liberti ya kushiriki kusudi lako; ni vema hili kusudi lifanywe safi, safi tena safi iwezekanavyo...

Wakati mmoja, yote ambayo umewasilisha humu lakini 'hayajafanyika bora' yanaweza kuja kuboreshwa na wewe mwenyewe kwa 'msaada utakaopata isivyo moja kwa moja'...

'Moyo Mkunjufu' ni silaha ya ulinzi katika 'Rehema na Fadhili'...

Hmmm
 
Hujawahi kusikia Jini anaitwa Subiani? au Jini Habashi? Au Jini makata? Au Jini Kibuki?
Kariakoo, kwa kina FF yupo Jini maarufu sana anaitwa Binti Mkunguni. Umewahi kumuona?

Dar ni jiji la kutisha sana, misukule wa kujiuza wanakwenda kufanya ngono na wateja wao makaburini. Wengi wapo makaburi ya Kinondoni yale ya zamani, yapo toka enzi za Mjerumani.
Unayajua?
Simba.
I bet huyo Biti Mkunguni ni Muislam na hata hao uliowataja hapo juu usikute ni Waislam pia. Nakumbuka mwaka jana niliwahi kukutana na jini FaizaFixy pale Mtaa wa Tandamti, Kariakoo, alikuja kwangu kwa tabasamu na kunipa halwa akaniambia katumwa kwangu eti nijiue kwa kuvaa mabomu mwilini kisha nijilipue ili nikifa nikapewe mabikra 72 kule motoni. Nikakataa, kugeuka nyuma sikumuona tena ila nashangaa eti yupo hapa Jamii Forum.
 
Ndiyo kuna mambo 'yanasubiri'...

Hakuna namna,

Wanajamii inabidi wafanye bidii kutafuta kujua ilivyobora--hakuna 'njia ya mkato' kwa 'maarifa'.

Maarifa yana 'Mbegu ya U-JUA-JI' -- hili linataka nidhamu ya aina yake na siyo mambo ya 'Tumbuizo Asilia' kwa stori stori za maisha...

Na ndiyo, In Shaa Allah, uwezekano wa kufika kwenye 'Shams al Maarif' kwenye huu uzi upo...

Ngoja wadau wakidhi uwezo wa kukomaa na mambo ya kiufundi wa kawaida kwanza...

Hmmm
Bro maandish yako mtu akisoma kidogo inabidi aende Instagram kwanza akapumzishe macho ndo arudi .. au we ndio robot wa CCM nini
 

Attachments

  • Screenshot_20240910_191839_Chrome.jpg
    Screenshot_20240910_191839_Chrome.jpg
    108.4 KB · Views: 27
I bet huyo Biti Mkunguni ni Muislam na hata hao uliowataja hapo juu usikute ni Waislam pia. Nakumbuka mwaka jana niliwahi kukutana na jini FaizaFixy pale Mtaa wa Tandamti, Kariakoo, alikuja kwangu kwa tabasamu na kunipa halwa akaniambia katumwa kwangu eti nijiue kwa kuvaa mabomu mwilini kisha nijilipue ili nikifa nikapewe mabikra 72 kule motoni. Nikakataa, kugeuka nyuma sikumuona tena ila nashangaa eti yupo hapa Jamii Forum.
FaizaFoxy ni jini...?!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom