...
Chakula kilikua kimewekwa jikoni na kuna wahudumu wawili wanatupakulia kabisa kila mtu, kinyumbani ile sio kihoteli. Tukawa kila mtu anachukua sahani yake anakaa sehemu ya kulia, ilikua meza kubwa gtu ya watu 10.
Bi H1; Leo Meneja naona kinyumbani kabisa, mambo ya T ni haya?
Sh; sasa hapa kwani hoteli jamani, hapa nyumbani kwake, yeye kaweka ordrer tiu hoteli kama mteja yeyote mwingine.
Tukawa tunaongea hapa na pale, kila mmoja na leke...
Mimi: Manager, mimi tukisha kula na safari ya kwenda mjini sijawaona wenyeji wangu mjini naona roho hainipi.
Dokta; mjini sehemu gani?
Mimi; hata sijiu dio Kikwajuni pale wenhgine wanasema Mwebeladu.
Sh; Yote moja hio, hapoo kwa hjapo tu.
Dokta; Kama mnaenda na gari mnishushe Mombasa mana muda umekwenda, maana hawa mabibi washasema wao hawaondoki leo.
Meneja; Sawa naona Simba, njia ndio hio hio. Nisalimie sana huko sowezi kwacha wageni peke yao, tungekwenda wote, leo nimejipa off.
Simba; Poa.
Tulipomaiza kula.
Dokta; Nyie mabibie kuna vitu vyangu chumbani kwenu twendeni mkanipe.
H 1; Twende mpenzi umepata ji Simba leo nisikucheleweshe, anawez kuwahi cha kuahgana.
Meneja: Simba hupigi kahawa kabla hujaenda?
Mimi; Haina haja, huko ni kahawa mwanzo mwisho, Ahsante sana Meneja, nitakujulisha nitaporudi.
Sh; Tena tunakungoja huku, usichelewe.
Mimi; haya kwaherini jamani, tukatoka na wote wakatusingiza hatua mbili tatu nje wengoine wakarudi, tukaenda na Dokta na Bi H wote. Njiani tukaachana, chumba chao kiko upande wa baharini kabisa, wakaenda kushoto, mimi nikaenda moja kwamoja, chumba changu kilikua hakipo beach kabisa lakini sio mbali. nikaingia chumbani kuatazaama simu yangu miss calls kibao.
Nikaanza ya babu. Tkasalimiana pale.
Babu; Vipi Unguja, njema?
Mimi: njema tu babu.
Babu; mbina hupatikani kwenye simu, umeshaoa nini huko?
Babu; Niliiwacha simu ina chaji, mimi nilienda kwa maneja alinilika chakula, ndio kwanza narudi.
Babu: Sheikh... ana wasiwasi anakupoigia hupatikani kuanzia asubuhi, kidogo amtume mwanae akufate hoteklini, mimi ndio nimemzuwia. Nimemwambia sio kawaida yako labda simu tu au ntwork msijitie gharama ya kumtuma mtu. Wapigoie basi.
Mimi: Okay, poa babu, hivi nilikua nakwenda kwao, usiwapigie nim surprise Sheikh.
Babu; Mpigie halafu msurprise, gfanaya yote mawili.
Mimi; Okay, sawa babu, tugtaongea nikirudi.
Nikampigia Sheikh nikamweleza kama nilivyomweleza babu, sikumwambia nakewwenda kwake.Nikamuuliza swahiba yangu yupo. Aksema usingepiga alikua anakuja huko akutafute. Nikacheka. Nikamwabia tutaongea zaidi baadae. Tukaagana.
Nikatoka resepshen nikakuta tayari mabibie wapo resepsjen, Dokta alafata handbag yake tu chumbani kwao, nikawaambia reception gari. Wakanambi ipo hapo nje ukitoka tu akikuona anakufata hapo hapo mlangoni sisi tunampigia. Tukatoka wote wanne nje, mabibie wakaagana na dokta ytukapanda gari tukaondoka.
Dokta; Huwa unakuja mara kwa mata Unguja?
Mimi; hapana hii mara yangu ya pili.
Dokta: umeuja kwa kazi?
Haana: kutembea siku mbili tatu tu, ilikua leo niondoke lakini wenyeji wangu wamenizuia.
Dokta" Au umeshapata totoz ya Kiunguja?
Mimi; Hapana Dokta, mke wangu mmoja kwa sasa ananitosha.
Dokta: tena Waunguja ukiwaambia una mke ndio wanafanya makusudi, kama wanaume zao, ukiwaambia mke wa mtu ndio wanajishaua wanajifanya wao wanaume sana.
Mimi: Dokta unaongea kama sio Muunguja?
Dokta mi e nishakua mbara, hata mambo hya Kiunguja nimeyasahau.
Mimi; jasiri haachi asili.
Dokta; Asili haiondoki, ipo tu. Unafikiri nakutania, si unaona wale wawili wamebaki kwa ajili yako na Meneja. Na hawa wa mbea wa Dr mpaka waujue mwisho. Nikaona nibadilishe topic, hua sipendi kuongelea watu amabao hawapo na sisi.
Mimi; Dokta umemkubusha dereva?
Dokta; Nitampigia nikiondoka tu na boti. Tena kaniagiza halwa, nikienda bandarini nitapita kumchukulia Darajani pale.
Mimi; Ooh, umenikumbusha, na mimi nitanunua, zawadi nzuri hio.
Ikawa karibia tunafika kwao, akasema hapo mbele ingia kulia, kuna shortcut, dereva akaingia, mbele kidogo akamwabia nyumba ile inayokutazama. Si ungenambia kwa Tall pale. Hakuna asiemjua, mtu mrefu Ungija nzima. nani wako?
Dokta: mdogo wangu.
Ikawa tumeshafika tukaagana na Dokta.
Dokta: Muhimu sana tuonane Dar ukija nijulishe tafadhali.
Mimi; sawa. safari njema.
Nikaondoka moka kwa Sheikh. baada ya kusalimiana pale, kama alijua nilipoisikia halwa njiani ikanijia hamu.
Sheikh, hebu leteni halwa ile bado haijapoa, bahati kuna mtu alipita akaikuta ndio imetoka kuopolewa akaituletea, imekua na wewe rizki yako Simba.
Tukawa tunapiga kahawa na halwa. Mimi nimekuja kukuaga Sheikh, kesho naondoka asubuhi. Ilikua niende leo nikaona si vizuri bila kukuaga.
Sheikh: Nimeabiwa na jamaa zake yule binti, jana kamaliza ada yao ya Kingazija vizuri kabisa, Wamasema anaonesha yupoo vizuri kabisa. Tumuobee dua awe salama. Maana amebeba mizigo mizito, lakini hawa vibuki ma afriti siwaamini kabisa.
Mimi; Kwanini sheikh?
Simba: Kile kimekua kama chama, haoa Unguja kuna wacheza kibuki wengi tu, lakini cha Bi DS ndio kubwa lao, hawa wenye vibuki wadogo wote pale ndio makao makuu. Hapo ni ma biga biss wote wenye noti zao, pale kila mwanamke au ana kazi nzuri na cheo serikalini, au mke wa mkubwa fulani au mke wa mfanya boiashara, wengina mabishara yao. Mpaka mashoga wapoo wana vibuki, lakini sio mashoga njaa, hawaruhusiwi hata kusogea. Mishoga ile yenye fedha zao.
Mimi; Wote wangazija?
Sheikh: Wengi wangazija lakini wapo kila kabila waarabu,m wahindi, watu wa kila aina, lakini ukiwaona kwa bibi yule ujue ni watu wenye hali nzuri za Kimaisha. pale Sheikh mwanamke ailikwa tu ni lazima aende na lazima alipe millioni moja. Mbali mambo yao mengoine ya mapombe na mbali moichango chango ya mingine. Hapao kama hana millioni hajaenda. Na hawakosi wakilikwa.
Mimi; Siku hana?
Sheikh: hawajui hana wale, hilo tunajua sisis Simba. Wale watu wana majina yao. Sijasikia wakisem "sina" labda ni aibu kwao. Ni watu wa kujifaharisha sana, ninao jirani zangu wawili hapa, wanakuja sana hapa kwangu kulketaleta sadaka zao aza madfrasa na kufanya dua. wamezoeana sana na mke wangu. Hao ni mabopar kweli kweli wanawake wa Kiarabu hao, hawana hata chembe ya Ungazija lakini wana vibuki.
Mimi; Nimemuona yle Dokta leo hoteli na wenzake wanne, akanijulkisha anao wawili wa Dar, lakini sijuani nao. Na wawili wa hapa, walikuja kula hoteli kule.
Sjeikh; Si unaona Simba, hoteli la kitalii lile, ndio mambo yao hayo, hawaendi vihoteli vya hovyo hoivyo wale, pesa hizo Sheikh. baso wote hao wanachama wa kibuki cha Bi S, tena hizo za ibuki afadhali. Akiwa na harusi mmoja wao. Mchango wa chini kabisa ni million 10 kila mtu. Harusi zao za Kingazija zinajulikana Sheikh, siku saba mfululizo, sasa fikiroia pesa ngapi, na sherehe zao ni kama mashindan, Huyu akichapiisha kadi za harusi Dubai, yule akifanya yake zitatoka Ufaransa, mambo yao ndio hayo Simba.
Mimi basi kuzuri kuoa huko, kama wana pesa namna hio?
Sheikh: huko wale wangazija ukioa kwanza lazima ukafanye harusi ya ada kwao huko, unaijua hio Sheikh?
Mimi; Hapana.
Sjeikh: hio bwana ukioa kama hujaifanya huna hadhi huko, ukiifanya ndio unapoata hadhi kweli kweli, na kilemba unapewa, wana vilemba spesho vinafumwa kwa mkono vya aiana ya peke yake, Ijumaa au siku za sherehe lazima ukipige hicho basi ulipiga hicho hata kama sehemu ya kuingoa kwa kadi wewe huulizwi, kwa kilemba tu ushajialika.
Hiyo kama huna fedha huifanyi bwana. Kwanza harusi ya ada hukoi lazima wadondoshe ng'ombe mmoja wawili kila siku, kwa siku zote za harusi, kama una uwezo hata watatu, sio ng'omb hawa wa kawaida. Ng'ombe wale wanatoka sijiui batra ipi kwenu huo, wanapemne kun)bwa akuliko ng'ombe wote. Wana bei hao. Na mwiko kupata nbei wakiuzwa wale, wanauzwa kwa mnada, halafu harusi za ada ili washindane vizuri zote zinakua mwezi wa saba na wanane, basi zinaongozana Sheikh, mpaka wanaogopa kufanya siku moja inabodi waambizane ili zisikutane, maana zikikutana mmoja anaweza akakosa watu wakaenda kwa mwingoine, hio aibu kubwa kwao.
Nikapigwa story nyingi nyingi tu, mwisho nikaaga. Swahiba yangu akaniwahi usiagoze gatoi hya hoteli, mimi nakupeleka leo. Nikamwabia itakua vizuri nikakupe mke wa Kingazija huko. Huku tunaondoka zegu kwenye gari. Ile kuingia tu ndio akajibu...
Swahiba; Nitawaweza wapi maskini mimi?
Mimi; Wana pesa zao hao si mchezo.
Swahiba: Wapo rafiki zangu ameolewa huko, kweli wanaoa huko, lakini kule ni kuolewa. na wale wanawake wa kibuki mradi awe na mume jibna yu, ni sifa kwao na njia yao ya kupatia pesa.
Mimi; Kivipi?
Swahiba: Wale washagundua siri ya wanaume wenye pesa. Mwanamme mwenye pesa sheikh yupo tayari kutoa mamilioni amle mke wa mtu, sijui wana siri gani na wake za watu. hao vibuki Simba, wanajuloikana Unguja nzima hii mambo yao. hakuna mwanamke wa kibuki mwenye mume mmoja, anakua na memu mmpoja jina tu awe na pesa asiwe na pesa, wlaiobaki micheppuko, ile fedha zao, miwili mitatu, wananyang'nyiana wenyewe kwa wenyewe.
Mimi; Na wanaume hawayajui hao waliowaoa kama mji mzima wanayajua?
Swahiba: Kuna mawili Simba; wengi wao wanajua lakini ndio wanzidiwa nguvu na majini a kibuki, wanaku hawana kauli. Ma wale amao hawana hela ndio wafanye nini? Wazikose raha na starehe za pombe na bangi kila siku. Kula vizuri kulalavizuri, wanaona wacha akaliwe, mtradi yuangu yananiendea. Yaani Simba ni ushetani mtupu.
Swahiba; Hujaona sikuil kwa ytule ibi anamuuliza mumewe mbele yetu kwa ukali kabisa, kwanini umeondoka? na jama yuko poa tu. Sasa unafikiri kiduka kile nidi kinejenga fahari ya jumba lile? Na unaambiwa ana majumba kila sehemu zuri ya Unguja bibi yule, ana nyumba hata 20 zinafika. Wao vibuki mimi nawapendea hapo, wao wanashindana kujenga tu, na mjumba yao majumba kweli kweli, hata wanaokodisha sana makampuni ya kigeni au wageni au serikali, mabenki.
Mimi; Wana akili basi.
Swahiba; Wana akili ya kujenga kuliko mchwa. Kw ahilo tu huwawezi. Simba huwezi kuamini, majumba yote wanayokodisha serikali, ya mawaziri, wakurugenzi, ya maafisa, yote ni ya wanawake wa vibuki. hilo soko lao wamelishika.
Tukafika hoteli, nikamwabia shuka tukanywe kahawa.
...
Tukashuka, swahiba mtoto wa Sheikh. Mtoto wa Sheikh aliikua ni kijana wa mjini kabisa Unguja, hakua amezubaa na mambo ya mjini anayafahamu kweli kweli kwa mtazamo wangu, ni kama kijana yeyote wa mjini Dar. Mfano kijana aliezaliwa na kukulia Ilala Dar huwezi mfananisha na kijana alie zaliwa na kukulia Kimara au Gongo la mbpoto Dar.Wana tofauti za muono na mpaka za maongezi.
Huyu alikua kijana wa katikati ya jiji la Unguja. Alikua amesoma vizuri kwa viwango vyetu, na alikua amesomea fani yangu ya umeme wa magari. Alienda chuo cha ufundi cha serikali Unguja kafaulu vizuri akaenda DIT Dar akafanikiwa kupata shahada yake ya mwanzo. Hivi alipo Unguja ana 'duka lake" mwenyewe, karakana yake ya umeme anaiita duka. Kwa kua licha ya kua fundi umeme wote kuanzia magari pikipiki mpaka majumbani, pia alikua anauza na kutengeza laptops na PCS aina zote. Alikua maarufu sana Unguja, hilo utalijua kwa simu zake ambazo, mara nyingi nimeona akiwa na mimi anaiweka simu silence na hapokei akiendesha.
Kufika to hoteli nikachukua kadi yangu ya mlango rresepshen nikamwabia karibu uvione vyumba vya hii hoteli, hujaviona wewe. Akanambia poa. Tukingia ndani. Akasema ni vizuri nimependa hii art ya Kizanzibari ya vigtanda na makochi humu ndani. Hata dirisha naona ni asrgt ya Kizanzibari iliowekwa kissa zaidi. Wamepatia sana.
Nikamwabia si hata Menejea umemuona ni Mzanzibari? Nimemuona, namjua yule Unguja, toka mimi bado mdogo sema ndio alipotea miaka kuibuka kaibukia huku
Mimi: ndio maisha.
Tukatoka nikamwabia twende pale beach saa hizi pazuri sana. Tukaenda kiukaa tunatazama beach, nikaagiza kahawa tukaletewa. Huku tunakunywa kahawa...
Swahiba: Simba hebu nielezze, juzi nimekupeleka kwa yule Bi S. lakini nimeona toka umekuja kwa Sheikh maongei yenu yamelenda sana vibuki, saa zingine mpaka mnaenda kuongea siri. Mna siri gani na vibuki wewe naSheikh? Au swahiba umepata jiko la pili huko?
Mimi; hapana, labda Sheikh anataka kukupatia wewe mke huko? Tukacheka wote.
Swahiba: Unajua leo ndio mlikua wazi kuonhgea mbele yangu mkaongelea Dokta, unajua mimi namjua huyo Dokta mnaemuongelea, yule kwao ni karoibu kabisa na pale kwetu sema siku hizi wamehamia Mombasa lakini mjomba yao bado yuko pale, ni maarifu sana na mkewe ni maarufu sana kupita kiasi.
Mimi; Huyo Dokta ndie alifanya nije kuwatemmbelea Unguja. Babu yangu ni swahiba sana na Sheikh, nadhani nia yao yule binti nimuoe, wameona njia ya kumsaidia ni kuolewa yule, kwani ana mambi ya kwao huko ya vibuki.
Swahiba: Yule usimwache wala usikatae, yule mtaani hapa wote wanamjua wanamsigfu ile mnbaya, yule unaa,biwa toka shule ya msingi mpaka anaenda chuo hajawahi kuchukua namba mbili. Yule mpaka serikali inamtambua uwezo wake. Yule kishapewa ofa na serikali hapa mara kibao lakini sijui chuo kikuu gani huko cha Marekani ndio kimemzuia, kimefungulia ofisi Dar na hapa anakuja sana yule kiazi, akija lazima aende kwa mjombake pale jirani yetu, kwao sasa yule ndio mwembe ladu orijino. Yote ni Kikwjuni lakini kwao pale ndio mwembe ladu.
Mimi; Sasa mwamaba umenitisha na watu wa kibuki hawa, mimi siyawezi, kua mume mwenza na wanaume wenzangu mwamba?
Swahiba; Yule msomi hayuko hivo labda wamemrpga ndio anakwend kutafutaytiba, maana kasomewa dua na Sheikh nyumbani, kila akija Unguja anakiuja japo siku mpoja kusomewa rokia.
Mimi: Mwamba kwanini humuoi wewe, ukimwambiaSheikh ni kama kusukuma mlevi.
Swahiba; Mimi mkubwa sana kwangu yule usimuone vile, simpati hata kwa dawa, yule kaolewa mimi niko primary.
Mimi: Kwani umei ni nini bwana Mbina mtume mke wa kwanza alikua mkubwa sana kwake?
Swahiba; Yule nipo tayari kumuoa hata sasa hivi, mwabie Sheikh na wewe nakupoa kazi mnipelekee posa kwao. Usiondoke kesho mnipelekee posa.
Mimi; Ongea na Sheikh hata kwa simu akikubali tupeleke posa mimi navunja safari.
Swahiba: Ongea na wewe Sheikh, mimi nikimwambia yule mzee atanitolea njiani, wenyewe washaniwekea kinbinti hicho hivi wanangoja kimalize chuo tu, wanisukumie.
Mimi; Wakusukumie tena?
Swahiba: Si unajuamke wa kupewa hujaongea nae hata siku moja, wazee wanasema tu, si ndio kusukumiwa huko?
Mimi; Ngoija swahiba, naona wewe una hamu wya kuoa, lakini huyo mtoto anakuchelewesha mpaka amalize chuo.
Nikachukua simu yangu nikapoga namba ya hoteli nikwaambi mimi fulani nataka kuongea na Meneja. wakaniunganisha nae.
Meneja: Nimerudi nipo hapa na swahiba yangu tunapiga kahawa beach hapa.
Menje; Njooni, njooni haraka, watanibaka huku.
Alivoonge mapaka mimi nkacheka.
Mimi; Mwaba twende nikakupe mke sasa hivi, huyo hurushi kabisa, umei wako, msomi. toto, toto kweli, sema ndio hao vibuki, usiseme sijakwambia, Huku tunaenda kwa meneja.
Swahiba; Tukatie macho Nuru, hawa vibuki bila kuwajua wana mambo makubwa, hao Sheikh sijui?
ulipogika kwa Meneja walikua kwa ndani, lakini Meneja naona katuona kwa dirishani tunavofika, akafungua mlango wa nje.
Meneja; Karibuni karobuni, mwamba hujaonekana tena? Hujaipenda hoteli yetu?
Swahiba: Nimeipenda sana sema mashughuli mengi na Simba hataki kuniita nije kumchukua.
Meneja: Jamani, mijimama ilikua inacheza nyimbo za mduara, maana kuna mziki mnene kwa Meneja, sio kawaida. H2 na T walikua wamejifunga kanga kinoni walipotiuona, wakazifungua.
H1; Simba, na usingetrudi leo, kesho usingeaondoka Unguja hii, umeleta ji handsome lingine?
Sh; Usijidai biutre mwache mtoto wa Sheikh... huyu fundi wangu huyu wa laptop yangu.
Meneja; Bwana wewe fundi wa computers?
Swahiba: ndio kazangu, si unamsikia bi Sh hapo, mimi electrical na electronidcs zpte kasoro mambo hya simu tu siyapendi, maana simu raha yake uwe na duka la simu, sio kutengeza tu.
Meneja: Unajua kuzitengeza?
Swahiba; Naijua lakini sijabobea huko kwa hio sina uazoefu nazo lakini ni simple, basics ni zile zile, hazina ugumu wowote kutengeza kwa kwake.
Meneja: Tukimaliza hapa tutaongea kazi.
Nikaona swahiba kamkodlea macho kila dakika anamytazama T. Meneja yiko sharp sana.
Meneja: Huyu boi Sh mnajiana, huyu hapa boi H na huyu Bi H, hawa wametokea Dar. Na huyu hapa Malkia T. huyu wa hapa haa Unguja mjini.
Swahiba; Mimi nafahamu sana mpka kwao, labda yeye hanifahamu.
T; Sura zako sio ngeni kabisa. Kwama wa Unguja nitakukumbuka tu si unajua saa hizi kukumbiuka shida huku anaonesha chupa za vinywaji.
Swahiba: Ukipenda nitakukumbusha.
Meneja; Twendeni nje, hapa mziki huu una kelele umenizbua masikio, halafu Simba anapenda kahawa yake bila kelele. Tukatoka nje, mimi meneja na mwamba, Meneja akarudoi ndani kidogo, kumbe kulikua kuna mhudumu wamemleta mdio anahudumia. Meneja akaja kukaa na sisi.
Mhudumu: Niwaletee nini wageni?
Meneja: mgeni mimi gtu hapoa, hawa wote wenyeji.
Mimi; Niletee juisi ypohyote ile fresh, hyakiwepo machiungwa nitafurahi sana.
Swahiba; Na mimi kama Simba hapo.
Meneja: Waletee na kahawa, hawa watu kahawa.
Ile tunaletewa vinywaji na mhudumu na miijimama ikatoka yote, wote wamebeba vnywaji vyuao wakkaa juu ya meza.
H1: Simba tueleze kuhusu mwenzio, usiwasikilize hawa Waunguja kama wao wanamjua sisi hatumjui.
Sh; Mkomenii kijana wa watu, hii mali yetu Unguja, hamumuoni alivyo spicey?
H1: hebu koma wewe, wacha dada zako tukiongea wewe sikiliza tunataka kusema nini. Sikiliza kijana, mimi ulivyotaja wewe fundi computers ndio nimekua interested, mimi nazileta sana laptop used kutoka Marekani na Uingereza, ndio biashara yangu kubwa Dar. Kuna soko hapa Unguja?
Sewahiba: Soko la hapa gumu sana la la[ptops, hutowez bei za hapa, watu wa bara wankuja kuchukua hapa tena kwa bei ya rehareha ya hapa wanakuja kuziuza Dar. Kuna kijana mmoja yupo Mgomeni, nampelekea sana laptos, yeye ana mtu wake hapa anamuuzi, mimi zinaletwa kwangu niweke software zile za awali na nihakikishe zinafanya kazi vizuri ndio namtumia, bei gani ananunua kwa huyo mtu sijui, mimi nazifanyia mamboi technical tu.
H1: Ndio wapo wengi wanaleta laptops kutoka huku, lakini hilo lisikutie wasiwasi, kma kunasoko huku, naweza kuzishusha mpoja kwa moja huku bila kuzilegta Dar. Kule napeleka mzigoi wao na hapa nashusha mzigo wa hapa. Umeongea la maana sana, fundi ni muhimu kua nae maanake karibu zote zinakuja hazina siftware kabisa, lazima ziwekewe na zifanyiwe marekebisho madogo madogo, mimi ndio hapo ninapoumizwa faida.
Swahiba; Kwanini?
H 1; Nawauzia watu wa jumla tu kwa sababu sina mtu reliable wakuzitia software na kuzifanyia marekebisho, watu wa jumla wanachukua hivyo wanazifanyia wenyewe halafu wanaziua.
Swahiba: Wewe ndio uko pale Kariakoo lile jengo chini wanauza matairi?
H1 ; Haswaa ndio mimi.
Swahiba: Vijana wa chuo nilichosoma dar ndio wanunuzi wako wakubwa wa jumla, hata mimi nishanunu amara mbilki kwako.
H1; Wewe umesoma DIT? Swahiba akajibu ndio.
H1; Bila nyinyi naifunga biashara. Na ukare wenu nimewawekea totpo linalowauzia lina tako hilo hata T kasingiziwa, hampindui wala hampatani.
Wote tukacheka. Njoo dar ufungue biashara ya rejareja ya laptops tufungue na duka la simu tuwe partners, inalipa sana.
Swahiba: Mie jiji lile haswa siliwezi, nimepata ofa nyingi.
Sh; Bora ubaki Mwamba, sasa wote mkihamia Dar, sisi nani atatungeneza kompyuta zetu zikiharibika?
H 1: Si mtazileta Dar?
Sh; Wewe ongea na T pale anatafuta biashra za kufanya, fungua nae duka la simu. pesa zimelala hapo hazina kazi za kufanya.
Meneja; na mimi nitawekeza.
Sh. Unaona mambo hayo? halafu wanataka kutuchukulia talents zetu zote wazihamishie bara.
Mimi: Tena mwamba ndio mke huyo, mashaallah, mabo yote yanjipa hapa hapa.
Sh: hawa Masheikh hawatutaki sisi, naogopa kusema yasiwe mengine hapa.
H 2: Mradi T ,wenyewe na Mwamba hapa wakikubaliana sisi tutasherehekea tu. Simba si tutakuja harusini?
Mimi; Tena mimi ndio bestman wake.
Sh; Unaona Meneja toto linakutoka hivi hivi unaliona.
H 1: Meneja kasema ana mchumbake na kila kitu tayari, mwache ajae huyo mzungu awe groupo letu. hatuna mzungu hivyo?
H2; Kweli hatuna labda aje kama mgeni tu, walishawahi kuja wageni wananihii hukumbiuki, wale wazungu wawili walikua wizara gani sijiu akawaleta kuwaonas(ehsa shughuli yetu kama utamaduni wa Kizanzibari.
SH; Wale wangekua wanakaa hapa wangekua members walipenda sana, maana lilikua ttamasha lile sio sherehe, watu kugtoa Dunia nzima ilikua July mwisho mwisho ile.
T; Si namimi ndio niikua siku ya kwanzaa yangu?
H1; Hswaaaa nimekumbuka sasa.
Meneja; Tuoingee ya maana sasa kabla sijasahau. Mwamba wewe ukipata nafasi njoo tuongee unafanya elecyrical works na electtronics zote? Swahiba akajibu, ndio.
Meneja; Njoo tuongee tuna kazi nyingi, sasa hivi tuna mkataba na kampuni ya Kenya ndio inafanya maintanace zote za umeme wa AC na DC, ia kitu. Wnapiga pesa nyingi sana. Bira hizo pesa zibaki kwetu hapa.
H1; Hii ndio faida ya vijana wetu kusoma. Usiiachie chance hio, Nyota ya jaa shida kuonekana, leo umeiona mapemaaaa. Umesoma dua gani ulipotoka kwenu, nifundishe na mimi peke yangu, hawa wengine shauri lao.
H2; kwanini na sisi tusiijue?
H2; Si unaona hapa, kila mmoja anagtaka kua partners na wewe na T pale kakaa kimya kama inaletwa posa tayari, ujuba wote umemuondoka, anatamani useme utamuoa. Meneja kisha mtolea nje live, bika chenga.
Meneja; Jamani sijakataa, nani atakikataa kiumbe kizuri namna hii, sema nimeshajicommigt na nimecommit mtoto watu anasoma Uislam sasa hivi. Kishaan kuujua kuliko mimi.
H1 anausome wapi huo Uislam?
Meneja; Hukohuko kwao Ulaya.
H1: Wazungu wanatushinda wite kwa Uislam siku hizi.
Sh; Unguja watalii kibao wa kizungu huwajui kumbe ni Waislam, utajuwa time za kusali, wanaingia misikitini. Na ukimuona mwanamke wa kizungu katitanda Kiunguja hata awe mtalii ujue huyo Muislam.
Meneja; Jamani kie nimefurahi mlivokuja Simba, naomba kaeni na wageni, mie napiuga raundi za kazi kidogo kama lisaa limoja nitakua nimeshatudi. Mnisamahe sana wageni.
Mimi; Poa, lakini wageni tumalizane nao habari ya ndoa ya T na mwamba hapa.
Meneja akaenda zake tukabaki na mijimama ya kibuki.
...