- Thread starter
- #3,001
Msihangaoike sana, hilo tatizo dogo sana. Aende hospitali. Kifafa kinatibiwa au kuzuiliwa na kidonge kimoja tu kwa siku, tena kidogo sana na wala hakina side effects za kumstua mtu mzima.Mkuu Arsis, mimi ninaye Dada yangu anateswa na tatizo la kuanguka kifafa.
Tatizo hili limemuanza akiwa mkubwa. Kwa maelezo yake yeye, anadai kuna siku alikuwa anafua nguo zake huko ziwani akatokea ndege jamii ya mwewe akampiga na mbawa zake!
Akawa ameanguka na akapoteza fahamu!
Sasa tangu siku hiyo, tukio la kuanguka na kupoteza fahamu limekuwa likijirudia. Ni zaidi ya miaka kumi sasa Dada yangu anateswa na hii hali.
Tumezunguka sehemu nyingi kutafuta tiba ya ndugu yetu lakini hali hutulia kidogo lau kwa miezi miwili tu lakini wa tatu ataanguka tena...!
Hali hii inamnyima raha Mama yetu. Make hakubali mwanae aishi katika haya mateso. Bado hachoki kutafuta tiba...!
Sisi kama familia tulimshauri apumzike tu amwachie Mungu make uzee nao ushaanza kumsumbua, amebaki kutulaumu kwamba tumemtelekezea mwanae...!
Mkuu nimekuja kwako. Nakuomba utusaidie kumtibu dada yetu aondokane na haya maladhi na Mama yetu apate kutulia.
Kwa sasa yupo Mwanza ila kama inabidi kumsafirisha sisi tupo tayari.
Aanze kukutumia hivyo bila kuacha baada ya mwezi uje kutupa jibu hapa, hali inaendelea au vipi? Tutazama mengine ya kufanya.
Samahani nilikua sijaliona hili swali kabla ya leo.
Simba.