Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

shida yako ni NENO TAWHEED au yanayofundishwa ndani ya tawheed?
Hio sio shida yangu Sheikh, hio shida yako kuzusha au kufata kitu kilichozushwa na unakifata kama kipofu au kiziwi.

Nimekuuliza maswali mengi sana, lakini naona hata moja hukulijibu, kwanini?

Mojawapo nimekuuliza, unajua elimu za kusoma zilizopo kwenye Qur'an?

Tena nikakwambia hauzimalizi kabla haujaanza kuzusha zako mpya.
Simba.
 
Tawheed maana yake nishakuelezea sasa kama watu kujifunza upekee wa ALLAH kuzijua sifa zake ili wajiepushe na shirki ni uzushi basi kila kitu kitakuwa uzushi kwenye dini.
Jifunze kwa nidhamu ndugu usije kukufuru elimu inataka utulivu mkubwa.
Vitu vingi sana kwenye dini uzushi, hilo nalijua, nimeanza kuchambua uzushi wa Adam kua ni mtu wa kwanza, kabla sijamaliza, umeleta "tawheed" halafu unasingizia mambo chungu nzima, maana yake ulioitoa ni potofu kama somo lenyewe.

Inaweza kua wewe unajifunza kwa nia njema kabisa, lakini sababu ni ipi? Kupoteza muda? Wakati Qur'an ipo wazi kabisa, inasema Sema, Allahu ni "Ahad" katika Surat Ikhlas. Sasa hio tawheed inahusu nini zaidi ya kupotosha watu tu?

Mtume Muhammad alisomesha somo linaloitwa "Tawheed"?
Simba.
 
Sina swali lolote siamini dini yoyote lakini naamini Mungu yupo
Safi sana, Huyo Mungu unaemuamini na sisi gtunaamini Mwenyezi Mungu ni mmoja tu, hajazaa wala kuzaliwa. Kama ni huyo unamuamini basi mimi na wewe hatuna tofauti.
Simba.
 
Ninakupata vyema Simba, ILA sasa je wakija kwa mlengo wa ulaghai, mfano kwenye kisa cha dokta mrembo alivyofanyiwa na mzee Ali. Hapo dokta anaamini kabisa hawa ni wema maana wanamtatlia tatizo lake kumbe ndo analiongeza.

Sasa point yangu ni hii, utamtambuaje huyu ni mwema( jiweke upande wa dokta), maana pia alikuwa anafanyiwa tiba inayoonekana ni jambo jema linalokwenda kutatua shida yake.
kwanza kabisa ukisoma utaona nimewekaweka points mara kwa mara, kua ukiona mganga anaanza kutaka kafara au chano. elewa hapo sipo. Kila tunavyoendelea kusoma utaelewa watu wanajichumia vipi, kisa hicho hicho cha Dokta, hakijaisha utaona watu wanatengeza vipi kwa ushirikina kama bado hujaona.
Simba.
 
hakuna dawa hio, utaibiwa. Kuna mashine, inafanya reverse osmosis, hio unainunua kwa kiasi cha lita unazotaka kusafisha kwa siku.

Ni nzuri sana tena sana ni teknolojia tu. Inakutolea maji safi unaoweza kunywa hata ya shimo la choo.
Simba.
Parameters zote zita meet standards...
 
Msihangaoike sana, hilo tatizo dogo sana. Aende hospitali. Kifafa kinatibiwa au kuzuiliwa na kidonge kimoja tu kwa siku, tena kidogo sana na wala hakina side effects za kumstua mtu mzima.

Aanze kukutumia hivyo bila kuacha baada ya mwezi uje kutupa jibu hapa, hali inaendelea au vipi? Tutazama mengine ya kufanya.

Samahani nilikua sijaliona hili swali kabla ya

Mlimsitishia dawa kwa ushauri wa daktari au mliamua wenyewe tu?

Kama mliamua wenyewe kosa, nawashauri mrudi kwa daktari muanze tena dozi, hilo la kukukonda mngelirudish kwa daktari kabla hamjachukua uamuzi.

Subiri nikufahamishe kitu; Ugonjwa wa kfiafa upo kwenye ubongo, ubongo unakua kama umepigwa shoti fulani ya umeme, tiba yake ni hio ya muda mrefu, ukiiacha unarudi. Wachache sana huwaondoka kabisa hio hali. Sasa ile shori kwa kua ni ua umeme wa chini sana, haiwi kama umeme wa tanesco, ikikupiga badala ya kuyaona haya tunayoyaona, ubongo unaleta majegajega kwa wengine, zinafumuka memory mbalimbali, hata huyo kunguru pengine hakuwepo ni ubongo tu unafanya majegajega.

WaathirikahHuwajia mambo tofauti tofauti, ambayo mimi nayaita majegajega, . Sayansi unalijua hilo tatizo, hakuna siri, mpelekeni hospitali. Siku hizi kuna vipimo wanajua mpaka kwenye athari ni wapi.
Simba.
yah dawa za kumeza kola soku maisha yako.ndio kama hizo tegretol mg 200. au phenytoin mg 100 mara 2 siku.
 
kwanza kabisa ukisoma utaona nimewekaweka points mara kwa mara, kua ukiona mganga anaanza kutaka kafara au chano. elewa hapo sipo. Kila tunavyoendelea kusoma utaelewa watu wanajichumia vipi, kisa hicho hicho cha Dokta, hakijaisha utaona watu wanatengeza vipi kwa ushirikina kama bado hujaona.
Simba.
Naendelea kufungua macho. Ulipo ongelea viashiria kama kafara na kutaka pesa nilikuelewa zaidi. Chano maana yake nini, hapo sijaelewa.
 
K
Huwa sikisii.

Hakuna torati kwenye biblia.

Kuhusu swali lako la biblia ina vitabu vingapi?

Inategemea na biblia ipi, ya wakatoliki vitabu 73 biblia ya maprotestanti vitabu 66. Bivlia ys janisa la Kimisri, Coptic Church, vitabu 81. Biblia ya kanisa la Wahabeshi, Ethiopic church vitabu 84.

Licha ya hayo, kuna matoleo (versions) kibao za biblia tofauti.

Sio tafsiri, matoleo. Kila mmoja akiamua anafyatua toleo lake tu.
Umbukumbu la TORATI
 
Vionjo vya Arsis 5-11 Majini ya Kibuki - Unguja.

nilivyokutanishwa na majini ya Kingazija (Comoros) na Kipemba Kojani.


Sikuchelewa sana nikampigia simu wife, tukaongea mawili matatu, nikampigia mzee na yeye sikua na story nae nikalala mapema tu, usingizi mzuri kabisa.

Alfajiri nikawahi kuamka kama kawaida yangu, nikajitayarisha nikasali pale poale chumbani. Nilipomaliza nikapiga kahawa pale sijakaa sana babu kapiga. Tukasalimiana pale.

Babu; Vipi Simba? habari za huko?
Mimi; Poa babu.
Babu; Alinipigia Meneja jana akanielez umefika salam na upo vizuri na Sheikh... kafurahi sana jana ulikua kwake muda mrefu, niliongea nae pia.
Mimi; babu, hivi haya mambo ya kishirikina kwanini unanoishirikisha na mimi?
Babu; Simba wewe na mimi sio washirikina, lakini nataka uyaone, ukisikia sijiui kibuki, ukisikia simba ukisikia sijui mizimu gani uelew mbinu zao. Tena wala usiwe na shka ya kua mimi naweza kukuingiza kwenye ushirikina, toka babu nimekukabishi hivyo viumbe umegfanay ushirikina uapi au vimekwambia ufanye ushirikina upi? Hivyo vyotevipo kwa kazi moja tu, ni walimu wako hao kwa niaba yangu,, hakuna zaidi. Babu utajinea watu wanavyohangaika wanataka msaada wanadhulumiwa, mtu atasema anakwenda kwa mganga kumbe anajiingiza kwenye shimo zaidi. Si umeona ya huyo Dokta kwa mZee Ali? Sasa yaone ya huko ndio jamaa zake na majini ya kikwao hayo, wala usiwe na shaka na babu. Ukiona kuna chochote kibaya, ondoka wala usinisikilize mimi. lakini hapo babu uytajionea mamboi amabyo ukihadithiwa tu huwezi kukubali, utaona uzushi tu.
Mimi; Sawa babu, naombea iwe ni eleimu tu.
Babu; kwani yale ya kwanza Unguja hujasoma kitu Simba? Hukuona watu wanavyofanya ushirikina wa kijinga kabisa? Uliambiwa ufanye shirki ipi? Labda mimi nipo mbali siyajui babu. Lakini usiwe na shaka, ukiona chochote hakiendani na Uislam wacha hapo hapo ondoka labisa, hata mimi stakua radhi.
Mimi; Nimekueleea babu.
Babu: haya bwana mkubwa, leo unakwenda kuliona hilo mama, kubwa la kibuki Unguja, ukisikia kuna watu wanapunga vibuki Umguja, woite ni wezi tu, hilo kubwa lao kiukoo, huyo Bi S ukisikia Ndama Mulaki ndi huyo yakimjia madudu yake. Utajiponea, sitaki nikuhadithie.
Mimi: babu we sema Jini2 kishanihadithia mengi.
Babu; hawezi kuyamaliza, kayaone mwenyewe, ya kuhadithiwa si ya kuyaona. Hilo tu, upo vizuri, hoteli nzuri> Upo sasalama?
Mimi; Niko poa kabisa, boinge la hoteli, sidhani kama kuna Watanzania wanachukua vyumba hapa, ngoja baadae nitauliza bei z vyumba.
Babu; Sawa, hata mimi nimeauliza hawakunambia.

Tukaagana pake na babu, mimi nikapiga restaurant, walipopokea nikauliza naweza kupata supu ipi nzito znito, wakanambia chumbani au breakfast room?
Mimi; Popote tu.
Chef: Brakfast r0om tayari unaweza kwenda kuna supu aina tatu, ukitaka nzito nyepesi na mambo mengi tu pengine upende zaidi Mr, Simba.

Nikashangaa jina langu kalijuaje lakini nikajua ni utaratibu wa Hoteli hizi kubwa kujua majina ya wateja wao, maana hata walipokuaja kunipokea waliniigta Mr. Simba. Nilipomaliza kuvaa vaa vizuri nikaelekea kwenye breakfast.

Kweli nikakuta mamboi mazuri kuliko kuagiza chumbani ujnajichagulia mwenye, aina za mikate kibao, supu yule kanambia aina tau, nikakuta kama aina ytano hivi, ujia aina kadhaa, yaani mambo yalikua mazuri, Nikasogea kwenye supu, binyti mmoja akanambi ipi Mr. Simba, tazamahiihii ni mbuzi, hii ni ng'ombe na mbiga mboga, hii nimbiga tupu, hii ni nyama ya kuchnganya na mboga nzzito sana, hii, tunaweza kuifanya uzito unaopenda ndani ya dakika moja.

Nikamwabia nipe ile nyepesi ya ng'mbe na mboga. Nikpiga breakfast heavy pale, nikarudi chumbani kwangu kidogo ishuke ile shibe, maana walijua huyu mswahili hajawahi kuona mambo haya, sikuwajali.

Nikapitiwa kama na kijiusingizi, kustuka saa nne. Nikakogakoga pale nikafikiria nimwite yule mshikaji au nichukue gari la hoteli, nikaona bira nimwite mwenyeji wangi wasione vibaya. Nikampigoa DSheikh, akanambi abasi hachelewi mwenzako namjulisha sasa hivi, tena alikuulizia. Nikamwabia haujapiga bado uppepo wa karavuu umekulaza. Akacheka.

Nikajimwagia maji nikavaa kashual tu nikatoka kwa nje nikasubiri kidogo akaja peke yake mshikaji, nikapanda, akawa anaielekeza hapa wapi hapa wapi, akanambia ngoja nikupitishe msitu wa jozani, kitu kama hivyo, tukanda pale nikaona sijui kima wale sijui tumvuroiri wanavidole vitatu tu, nikaambiwa hayo matinda wanayokula ni sumu, hakuna hata ndege au mnyama mwingine anaekula, hta binadamu ulila ni simu hio, watu wanachukua hayo matunda kutengenezea sumu sijui wanagfanyia uchawi, mwenyeji wangu akawa ananielekeza. Tukapita kama mikoko hibi imejngewa vinjaia, nikapenda sana, niasema kwetu kuna mikoko lakini hatunyi hivi, yaani mtu unatembea kama unatembea juu ya maji lakini ni vidaraja vimejengwa na ileile miti ya mikoko, haiozi kwenye maji ya chumvi, nikapenda sana ile dizaini.

Akaniuliza una safari yoyte? Nikamwabia nilikua nataka kwenda fuoni kwa Bi s? Akasema father wake kamwambia lakini yeye hajawahi kufika lakini gtukifika seje)hemu alionielkeza Mzee tutafdika tu, ni maarufu sana huyo mama, mimi namfahamu lakini kwake sipafahamu.

Tukaenda mpaka fuoni, kumuuliza mtu mmoja, akatuonesha, aksaema paleee, kuna duka yupo mumewe Bi Sofia, mkifika hapo ndio mmeshafika, Tukaenda dukani tukashuka, Tkamkuta jamaa mmoja wala sio mzee, ni mtu mzima, lakini anaonesha mtu wa ndum na mitungi sra yake. Nikajitambulisha akanambia mimi naitwa K, Kwa bi S ndio umefika hapa, mimi mumewe, karibuni kaeni mpige kahawa nimfahamishe kuna wageni wake. Tukatolewa viti viwili vya plastiki tukakaa, akaktukabis)dhi chupa ya kahawa,a akatoka nje dukani, naona simu hazishiki, ngoja nimfate. Ni pale, akaonesha nyumba kubwa hivi ina geti kubwa akanambia nyumn)bani pale , hapa napo nyumbani lakini hapa ni biashara gtu. Nakuja sasa hivi.

Akaenda huko akakaa kama nusu saa, akarudi akanam bia karibu mgeni, tukaamka mimi namwenzangu, K akasema nilidikiri mgeni huyu tu, wewe nikajua umemleta tu , nakujua wewe, si uko pale.... Akamwabia hata mimi nakujua lakini nilikua sijui kama ndio mumewe Bi S. Sasa umejua, haya twendeni.

Tukaoingia kwenye geti kubwa tukakuta bonge a ua, naona ule ua moubwa kuliko nyumba, na jumba lenyewe kubwa la kig)fahari ka standard zetu. Kuna viti pale kuna seheu kunalivuli akatwambia tukae tusubiri, na yeye akakaa na sisi mara akaitwa na mtoto akarudi akanambia wewe mhgeni twende, bwana wewe mwenyeji subiri kidogo, si unajua pengoine ana mambo yake ya siri huyu na Bi S. Nikaingia ndani, nikamkuta Bi S mwanamke mpana hivoi kwa mfuoa sio kwa unene, tukasalimiana anaongea Kkunguja kabisa, akamwabia K basi kakae na mhgeni mwingine acha niongee nae umenambia unaitwa nanivile, nikamwabia Simba. Akacheka, Simba huyu simba ninae mjua mimi? mboni wanitisha? Nikacheka.

Bi S. Umetokea wapi?
Mimi; Dar.
Biu S; Dar kubwa, sehemu gani Dar?
Mimi; Ilala.

Boi. S. Ooh asili yenu watu wa Tanga?
Mimi; ndio.
Bi S; Wewe sio mtoto wa ... naoina damu ndio zilezile.
Mimi: Ndio hasa, mamangu huyo.
Bi S, hebu nisubiri kidogo, nakuja dakaika tani tu.

Nikaujua labda kaenda kujisidi, nikakaa nasubiri pale mara kaja mtoto akaniita, anko unaitwa ndani na bibi, njoo hukiu, nikanyanyuka nikaingoia ndani zaidi na yule mtoto kama chumba cha tatu hivi akaginga kidogo mlangoi akaugfungua, aknambi pita. Nikaingia, kuingia chumba kina mazulia mazuri ya thamani kananukia udi nikaona Bi S kakaa lakini sio yule nilieonana nae kule, alikua kavaa guo jeupe kama la cotton hivi kavaa na kilemba. Akanitazama huku anatabasamu.

B S. karubu, karubu kaa, umenisahau na hiki kilemba? Salaam.
Mimi; Salaam.

Bi S; Karibu kaa, mimi siwezi kukaa kama hwewe hujakaa kwanza, nipo chini yako sana. Nisamah sana kukita huku, ilikua wewe ndio uniite mimi Simba, naomba msamaha sana.

Mimi nikakaa.
Bi S; Unaniruhusu nikae?

Mimi; Kaa tu Bi S.

Bi S; Akacheka, mimi ngoja nijitambulishe kwana, akasimama, mimi naitwa Ndama Mulaki hayupo Bi Safia sasa hivi, mimi nimekuja kwa heshima yako, naoma hio pete yako ifiche inaniumiza macho sana.

Mimi nikaiugeuze)a nyumba mbele.
Bi S. Ahsabte sana Simba.

Akakaa chini, naama nitume Simba nipo kwenhye kukuhudumia, hii gfursa kubwa sana kuja kwako, miaka na miaka sasa. Mimi nikawa nashangaa shangaa, ikanijia sauti ya Arsis, huyo anamuona mfalme wa Simba sasa hivi usiwe na shka, anaona picha tu tumemuwekea, Hafahamu. Kusiki ahivyom nikapata ahueni kidogo, nikamtazama Bi S.
Mimi; Habari zenu?
Bi S; Nzuri Mkuu.
Mimi; Sitaki kukuchelewesha mimi mgani wa Bi S leo. Nimekuja kuonhgea nae, ananisikia?
Bi S; Ansikia na anaelewa kila kitu, niondoke uongee nae?
Mimi; Subiri kwanza.
Bi S; naam, mkuu.
Mimi: Nimesikia kuna sherehge hapa kesho usiku, kweli?
Bi S; Ndio kweli lakini sio kubwa sana mkuu, ukitaka tuifamnye kuu tutaifanya mkuu.
Mimi; Hapana, msibadilishe fanyeni kama mlivyopanga. Mimi nitakuwepo kwenye sherehe.
Bi S; tena tutashukuru sana ujio wako, tutafurahi sana tena, ni heshima kubwa sna Mkuu.
Mimi: basi wewe nenda tu, wacha noingee na Bi s.

Bi S; haya kwaheri Simba, nasamehe sana kukuita huku.
Mimi; hakuna neno, mimi mwenyewe nilikuja bila taarifa.

kwaheri mkuu, kwaheri mkuu, kwaheri mkuu.

Nikaona Bi s Kama kajinyoosha kidogo akatingisha kichwa.

Bi S; Salaam alaikum, makubw haya. Niseme nini sasa?
Mimi; Kwanini B S.
Bi S; Kwanza Simba b)nisameh sana, sikujua kama Simba mwenyewe amelkkuja, nilijua DSimba jina tu. Lajkini sasa nimeelea kila kitu, mwenyewe umetanda hapa, mimi nimepewa amri niwe chini yako kwa chochoiyte ukiytakacho na utakachiambia, utakachiniambia ni amri kwangu, awepo Simba asiwepo.
Mimi; Simba Mkubwa kishaondoka, nipo mimi simba jina.
Bi S. Nimestuka maana hilo onoyo nililopewa sio la kitoto la kukita huku ndani, naambiwa ilikua wewe uniite mimi nje kule.
Mimi: hapana , hapa nyumbani kwako siwezi kuthubutu kufanya hivyo hata siku moja.
Bi S; Kuanzia leo hapa ni kwako na fanya lolote upendalo nimarishe utakavyo iwe pekeetu iwe mbele zawatu uwe wewe au mwengine yeypoyte, mradi ni wewe upo basi amri ni yako, mimi sina kauli ytena kwako.
Mimi; Basi nimekuelewa, haya tuomngee kilichonileta kwako.
Bi S; Naam simba nakusikiliza.
Mimi; Nimekuja hapa kwanaza kukuona nilikua sikujui, nikaambiwa nikuten),mbelee maana wewe ndio mkuu wa huku wa vibuki vyote? Kweli?
Bi S; Kweli Simba.
Mimi; halafu nimesikia sasa hivi, kua kunasherehe hapa kesho, kweli?
Bi S; Ndio Simba kweli.
Mimi: Kesho, kabla sijasema BbI S akanikatiza.
Bi S; Simba kesho nakualika uwe mgeni wangu rasmi tafadhali usikatalie, sherehe ndogo lakini sasa hivi nitaifanya iwe kubwa ya hadhi yako, wanakuja watu 20 tu, wacha nifanya wawe 100, hata kwa gharama zangu.
Mimi; Hapoana usifanye hivyo kabisa. Wacha kama mlivyojkusudia, mradi isikose ada zote, msiache ada hata moja.
Bi S; basi Simba naomba wangezeke watu watani wa ngoima, ili ada zikamilike, maada sisi tuliona sherehe ndogio hatryukuwaita watu wa ngoma, watakua watano tu,, wawili wanaume watattu wanawake. Ili sherehe iwe na ada zote, Nakuahidi Simba itakua na ada zote mpaka mwenyeqe utafirahi, wengine tiutawaambia wafanye party huko huko mahoteli, lakini hapa tutabaki kamma tulivyopanga nitahahakisha kama ulivyonambia asizidi mtu.
Mimi: Asizidi wala wasioungue wala asibadilike mliopanga, sawa?
Bi S; Sawa Mkuu.
Mimi: Sitaki kukuchelewesha mambo yako, tafadhali njoo pale nje umsalimie kijana alienileta, umruhusu na mumeo akaendelee na kazi, na mimi niytaondokea palepale, usijali.
Bi S; Haya mkuu naomba dakaika tatu nibadili hizi nguo za ndama.


Nikamsubiri pale tulkatoka nae nje, Mumewe alikua kishaondoka.

Bi S; We nanihii mwite bau yako hapo nje haraka, kwanini kaondoka na kuna mgani ndani?
Mimi ; Huyu mwenyeji wangu, na huyu Bi S.
Kijana: Mimi nagfahjamu Bi S maarifu yeye labda ndio hanifahamu mimi.
Bi S; Hakuna neno sasa tumefahamiana, unaitwa nani? Wakatambuloishana pale, aahhh babako Sheikh... namjua sana na yeye ananijua mimi.

Matra mumee akaingia.
Bi S,bwana wewe imekuaje ukanichia wageni ukakimbia.
K; Niliitwa dukani kulikua kuna kitu muhimu, sema?

Bi S; Huyu bwaba Simba kesho mgeni wako naomba badilishaneni namba za simu na mimi Simba namba yako ntaichukua kwa K tutawasiliana zaidi kama kuna chochote.
Mimi; Hakuna tatizo, haya nisiwaharibie kazi zenu, kwaherini.
Simba.
..5.12
Vionjo vya Arsis 5-12 Majini ya Kibuki - Unguja.

nilivyokutanishwa na majini ya Kingazija (Comoros) na Kipemba Kojani.


Tukaagana pale, tukatoka mimi na kijana wa Sheikh alienoleta na K mumewe Bi S tukatoka nae.
K. Siku nyingine Simba ukija na gari tutakufungulia uiweke ndani, si unaona ndani nafasi kubwa sana, hata gari ishirini zinaingia na nafasi inabaki.
Mimi: Nimeona, ahsante.
K; Bi S, inaonesha mnaelewana sana, mimi sijawahi kukuona hapa.
Mimi; Anaelewana nawazazi wangu.
K; Mtu wa wapi wewe Dar?
Mimi; Ndio.

K haya jamaa karibuni sana, hiuyo mwenzako maaruf sana, tunajuana miaka mingi, tokea mjoini huko mambo ya kibaharia.

Tukaondoka.

Kijana; Huyu mzee kamal alikua bahjaria miaka mingi, yule Bi S mumewe alikua jamaa mmoja, sasa hivi mtu mzima, mtu wa UWT, alikua bpodigadi wa mzee karume, sema baadae yeye akapewa awe nao huyu Amani na Ali, ndio alikua akifatana nao sana zamani.
Mimi" Wewe umejuaje?
Kijana: Hizo story mimi kwa umri wangu nimehadithiwa lakini Unguja hii hakuna asiejua ya hawa watu maarufu, Ungujs Simba sote twajuana. Hata nikipika nini leo mji utapata habari. Si unaona mfano wewe mgeni wa Sheikh na tupo pamoja na mimi, wagtu washajua mpaka gtunapoenda. Ndio Unguja hii Simba, watu hawana kazi za kufanya, kazi maneno maneno tu. Huyo Mzee maarufu sana,ukitaka hata leo tunakwenda kumuona, siku hizi ana ofisi pale Hoteli ya Bwawani. Sasa Simba mtu amabe haupo matawi unafikiri utapata kupewa ofdisi opale?
Mimi; Kweli, nimekuelewa. kwa hio Kamal, mume wa pili?
Kijana; Ndio, tena siku nyingi ana watoto nae, sijiui wangapi. Na huyu mama Mwenyewe hizi shughuli zingine anazuga tu, huyu lazima ni hjaohao watu wa siri wa serikalini. Hakuna asiemjua huyu Bi S. Unguja hii, hata huko bara anajulikana, vibuki wapo mpaka huko, huwa wale matajiri wenye vibuki wanamleta huko. Unaambiwa hakuna jini mwenye gharama zaidi yake na walionao wakiwapa ada zao na wao wanazidi kutajirika. Vipi, Simba na wewe unae nini?
Mimi; Hapana, babako anataka nitembee niijue dunia labda anataka nijuane na watu maarufu hawa.
Kijana; Baba ndio zake hizo, ngoja wewe, akikupenda atakujullisha wazee wote wa baraza la mapinduzi toka la mwanzo lile, waliopo hai, mpaka wa sasa wanamjua, wazee wa zamani hawa.
Mimi; Safi sana.

Tukafika kwao, tukapiga [oigs story tukaend akusali Ijumaa, tulipomaliza, tukarudi kula kwao na wageni wageni wengine. Pamechangamka, tukajulishan pale, mimi nikapiga simu niletewe gari ya hoteli, nisimuangaishe kijana wa babu.

Nikwamuaga Sheokh pale, akasema unaenda wapi, kaa utaenda jiponi. Nikamwambia hii biriani ulionilisha leo, inanitia usingizi, wacha nika[u,mzike, tutaonana kesho, leo nitatembea mitaa ya kule kule jirani na hoteli.

Sheikh; Sawa, ukitaka kwenda mahali huna haja ya rukhsa yangu, kijana mwenzako mshazoeana sasa, mwambie tu wakati wowote.

Mimi; sawa, wala asihangaike leo, nimeshaagiza gari ya hoteli, mwache na yeye apumzike, biriani heavy hili.
Sheikh; Kwanini unajitia hasara bwana, gari zao ghali sana ukizitumia.
Mimi; Usijali, ni ofa hii, silipii.
Sheikh; Sawa bwana. Sisi tupo kwa ajili yako.

Nikatoka, kijana akanitoa nje, trukakuta gari ya hoteli imeshafika, wanajuana na dereva wakaongea pale tukaondoka.
Dereva: Bro bahati sana mimi nilikua bandarini nilipopigiwa, hakuna abiria, nikaona niwahi kuja kukuchukua.
Mimi: Ahsante.

Tulipofika hotelini nikaenda zangu chumbani moja kwa moja, kwanza nikapumzika, usingizi mzito ukanipitia kustuka 12 na jioni. Nikaamka nikakoga koga pale, nikaona kahawa wacha nikanywe nje huko, kwenda kunywa kahawa mara Meneja na yeye kaja. Tukakaa nae tunakunywa kahwa wote.
Meneja; Vijana washakujua hoteli, wananambia ndugu yako yuko huku anakunywa kahawa, ndio nimekuja.
Mimi; Ahasangte, nisikuharibie kazi zako, mimi nipo OK kabisa.
Meneja; Hapana, mimi nilikua natembea tembea, kuna wageni kutokea Dar kina mama wawili tunawategemea.
Mimi; Wagtanzania au wageni wa nje?
Meneja: Watanzania, jamaa zangu kwa mbali hao, unajua mimi mngazija. Na wangazija sote ndugu kwa namna moja au nyengine. Kuna Watanzania wanafikia sana hapa, sio wageni wa nje tu, bei zao kidogp zinatofautiana na wa nje na Watanzania wanalipa kwa shillingi wageni wa nje mara nyingi wanakuja package yao wameshalipi hukohuko kwa ma agent wao, hapa wakitumia vitu extra tu amabavyo havipo kwenye package. Mfani wana ziara ya kwenda na kurudi mjini huko mara mbili kila siku, moja day time moja night time, hii ya usiku inakwenda forodhani, hii inatusaidia sana sisi kupunguzaa gharama.
Mimi; Kwanini? kwa sababu sisi hapa tunakua tayari gharama mpaka za kula asubi, usiku na mchana, sasa wakienda stone town wanakula huko wengi wao hawali tena hapa, inakua tumeshusha gharama sana.
Mimi; Oooh, nimeelewa.
Meneja: hapa mimi kazi yangu kubwa ni kuhakikisha nashusha gharama za matumizi ya hoteli bila kiushusha ubora, ndipo faida kubwa itaonekana.

Meneja; hawa kina mama wa Kingazija wana mila na ada zao, ukiwaona wanakuja ujue kuna sherehe yao. sherwhe yao mara nyingi hua Jumamosi, na hawa watakuepo siku tagtu hapa, leo, keshoi na keshokutwa lazima wana sherfehe yao.
Mimi: Wewe umeshaona sherehe zao?
Meneja: Utotoni tu, ukianza kukua kua huruhusiwi kabisa mwanamme, hta ufanye nini. mambo yao ya mashetani shetani.
Mimi; Kwanini wanagfanya siri?
Meneja: hata sielewi wala sitaki kuelewa, hayo y mashetani ni hatari sana, samahani Simba, mimi hata kuyataja naogopa, bituko walivyokua wanagtufanyia hapa Hoteli? Mimi isingeaku Babu yako nilishasema na kwenda kujaribu mara ya mwisho, mambo hyakiendendelea nawacha kazi hapa natafu mengine ya kufanya.
Mimi; Ilikua serious sana?
Meneja; Ngoja nikshawapokea wageni wakitulizana niakupa stoiry, yetena itakua voizuri maana mengine hata babu yako nilikua sijamuelezea. Kwa hio wewe sikufichi kitu, niahidi utamfikishia babu yako.
Mimi; Si yamekwisha?
Meneja; Nashukuru yamekwisha lakini ngoja nitulizane nitakuja kukuhadithia au unatoka?
Mimi; Niende wapi usiku huu?
Maeneja: Aaah kuna disko hapa hotelim na kuke nbeke kidogo kuna disko, sema hili la hapa liko kule uoande wa pili, hili letu limechangamka sana, mimi nilifanya mpango na wenyeji wawe wanakuja, lakini soi wote wale wenye poesa zao tu, ili isiwe fujo. Tembelea huko usiku pazuri sana, utapenda, utapata kuiona Unguja by Night, utakuta wagtoto wa Kiunguja wale nyumba za kitajiri wanakuja kujirusha, wale awa kufugwa kama majini.
Mimi; Unanitamanaisha.+Meneja,; Huko kuanzia saa sita usiku moaka saa kumi alfajiri ndio kumekucha, kabla ya hapo wageni wageni tu wazungu, kwa kua linaanza saa tatu usiku. Mimi huwa natembelea huko kutazama tazama kama wageni zangu wapo salama na huduma zinapatikana bvvizuri.
Mimi: Nitatizama, kama sijachoka nitaenda nikajionee badala ya kuhadithiwa.


Tukaagana pale meneja akaenda zake, nikapiga kahawa yangu tena nikarudi chumbaini kwangu. Nikawaza, nikajua meneja hajaeewa kua na mimi nipo kwa ajili ya huyo kibuki.

Nikampigia babu, baada ya kusalimiana.
Mimi: babu leo nimemuona bi S wa kibuki. Nikamwelezea babu yote niliokumbana nayo
Babu: hayo muulize Arsis atakueleza, mimi naamini hakuwepo Simba hapo, hao hawawezi hata kuja, kwani tunamikata nao tayari lakini muulize Arsis.
Mimi; Sawa, nikamuelea nilichoongea na Meneja. Babu akacheke sana.
Babu: Mimi siku na haja ya kumsikiliza mengi, wewe msikilize kijana mwenzio huyo. Mimi nilijua likimalizwa tatizo moja yote yatakwisha, aliemaliza tatizo huko Bakora, kwa majani na mitishamba yake tu. Na mimi Alhamdulillah nilisoma sana Qur'an, imekua kubuli.
Mimi; Okay, najua nani atanipa mkasa wote.

Babu; Vipi lakini unaonaje tripu yako?
Mimi; Mpa sasa poa.
Babu; Utai[enda tu Unguja, anagalia usibaki huko, akacheka.
Mimi: Mbina unanitisha babu?
Babu; Sikutishi wenyewe wana msemo wao wanasema, Unguja ni njema atakae na aje.
Mimi: babu kwaheri.

Tukaagana pale.
Simba.
...13
 
kwanza kabisa ukisoma utaona nimewekaweka points mara kwa mara, kua ukiona mganga anaanza kutaka kafara au chano. elewa hapo sipo. Kila tunavyoendelea kusoma utaelewa watu wanajichumia vipi, kisa hicho hicho cha Dokta, hakijaisha utaona watu wanatengeza vipi kwa ushirikina kama bado hujaona.
Simba.
ni kweli tunayaona hayo kwa waganga wengi kucthanja chale mara leta jogoo mwekundu alafu anakatwa kichwa anakinga damu au ana achiwa anapapatika hadi anatulia mwenyewe akishatulia kisha mganga anasoma code pale tunajua damu ina nguvu ikiwa mgonjwa ana madudu machafu ukamwaga damu si ndio unayaamsha zaidi na kuyapa nguvu maradufu kuna kupona kweli hapo.! naomba elimu mganga anamkata kichwa kuku iwe kwa kisu au meno alafu anamuachia ahangaike hadi akate roho maana yake nini?
 
Naendelea kufungua macho. Ulipo ongelea viashiria kama kafara na kutaka pesa nilikuelewa zaidi. Chano maana yake nini, hapo sijaelewa.
Chano. Vyano vipo vya aina nyingi, inategemea na mganga, hii hua ni sinia au ungo unajazwa vitu wanavyosema ndio ada yaa huyo jini, kwenye chani inawez kuwemo, matunda, na vituvitu vingine, vyano vingine mpaka pesa zinawekwa. lakini kwa ufupi ni chakula, wanachosema cha huyo jini ili kumfurahisha.

Chano cha Kibuki lazima whisky iwepo. Hawataki utani na kinywaji chao. Simba wao Brandy.
Simba.
 
ni kweli tunayaona hayo kwa waganga wengi kucthanja chale mara leta jogoo mwekundu alafu anakatwa kichwa anakinga damu au ana achiwa anapapatika hadi anatulia mwenyewe akishatulia kisha mganga anasoma code pale tunajua damu ina nguvu ikiwa mgonjwa ana madudu machafu ukamwaga damu si ndio unayaamsha zaidi na kuyapa nguvu maradufu kuna kupona kweli hapo.! naomba elimu mganga anamkata kichwa kuku iwe kwa kisu au meno alafu anamuachia ahangaike hadi akate roho maana yake nini?
Nakazia hii.....bwana Arsis tupe elim hapa tunapigea sana aisee hehehee
 
Nakazia hii.....bwana Arsis tupe elim hapa tunapigea sana aisee hehehee
Tutapata tu elimu, mimi natoa nivijuavyo kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu, kuna wajuzi humu zaidi yangu.

Yupo kaka yake Etugrul Bey na Nourhan na wao wana elimu yao, ambayo sio yangu.
Simba.

Wapigaji ni wengi sana kupita kiasi katika haya mambo. Hawana dini wala kabila. Wapo wapigaji wakubwa na wadogo.
Simba.
 
Vionjo vya Arsis 5-12 Majini ya Kibuki - Unguja.

nilivyokutanishwa na majini ya Kingazija (Comoros) na Kipemba Kojani.


Tukaagana pale, tukatoka mimi na kijana wa Sheikh alienoleta na K mumewe Bi S tukatoka nae.
K. Siku nyingine Simba ukija na gari tutakufungulia uiweke ndani, si unaona ndani nafasi kubwa sana, hata gari ishirini zinaingia na nafasi inabaki.
Mimi: Nimeona, ahsante.
K; Bi S, inaonesha mnaelewana sana, mimi sijawahi kukuona hapa.
Mimi; Anaelewana nawazazi wangu.
K; Mtu wa wapi wewe Dar?
Mimi; Ndio.

K haya jamaa karibuni sana, hiuyo mwenzako maaruf sana, tunajuana miaka mingi, tokea mjoini huko mambo ya kibaharia.

Tukaondoka.

Kijana; Huyu mzee kamal alikua bahjaria miaka mingi, yule Bi S mumewe alikua jamaa mmoja, sasa hivi mtu mzima, mtu wa UWT, alikua bpodigadi wa mzee karume, sema baadae yeye akapewa awe nao huyu Amani na Ali, ndio alikua akifatana nao sana zamani.
Mimi" Wewe umejuaje?
Kijana: Hizo story mimi kwa umri wangu nimehadithiwa lakini Unguja hii hakuna asiejua ya hawa watu maarufu, Ungujs Simba sote twajuana. Hata nikipika nini leo mji utapata habari. Si unaona mfano wewe mgeni wa Sheikh na tupo pamoja na mimi, wagtu washajua mpaka gtunapoenda. Ndio Unguja hii Simba, watu hawana kazi za kufanya, kazi maneno maneno tu. Huyo Mzee maarufu sana,ukitaka hata leo tunakwenda kumuona, siku hizi ana ofisi pale Hoteli ya Bwawani. Sasa Simba mtu amabe haupo matawi unafikiri utapata kupewa ofdisi opale?
Mimi; Kweli, nimekuelewa. kwa hio Kamal, mume wa pili?
Kijana; Ndio, tena siku nyingi ana watoto nae, sijiui wangapi. Na huyu mama Mwenyewe hizi shughuli zingine anazuga tu, huyu lazima ni hjaohao watu wa siri wa serikalini. Hakuna asiemjua huyu Bi S. Unguja hii, hata huko bara anajulikana, vibuki wapo mpaka huko, huwa wale matajiri wenye vibuki wanamleta huko. Unaambiwa hakuna jini mwenye gharama zaidi yake na walionao wakiwapa ada zao na wao wanazidi kutajirika. Vipi, Simba na wewe unae nini?
Mimi; Hapana, babako anataka nitembee niijue dunia labda anataka nijuane na watu maarufu hawa.
Kijana; Baba ndio zake hizo, ngoja wewe, akikupenda atakujullisha wazee wote wa baraza la mapinduzi toka la mwanzo lile, waliopo hai, mpaka wa sasa wanamjua, wazee wa zamani hawa.
Mimi; Safi sana.

Tukafika kwao, tukapiga [oigs story tukaend akusali Ijumaa, tulipomaliza, tukarudi kula kwao na wageni wageni wengine. Pamechangamka, tukajulishan pale, mimi nikapiga simu niletewe gari ya hoteli, nisimuangaishe kijana wa babu.

Nikwamuaga Sheokh pale, akasema unaenda wapi, kaa utaenda jiponi. Nikamwambia hii biriani ulionilisha leo, inanitia usingizi, wacha nika[u,mzike, tutaonana kesho, leo nitatembea mitaa ya kule kule jirani na hoteli.

Sheikh; Sawa, ukitaka kwenda mahali huna haja ya rukhsa yangu, kijana mwenzako mshazoeana sasa, mwambie tu wakati wowote.

Mimi; sawa, wala asihangaike leo, nimeshaagiza gari ya hoteli, mwache na yeye apumzike, biriani heavy hili.
Sheikh; Kwanini unajitia hasara bwana, gari zao ghali sana ukizitumia.
Mimi; Usijali, ni ofa hii, silipii.
Sheikh; Sawa bwana. Sisi tupo kwa ajili yako.

Nikatoka, kijana akanitoa nje, trukakuta gari ya hoteli imeshafika, wanajuana na dereva wakaongea pale tukaondoka.
Dereva: Bro bahati sana mimi nilikua bandarini nilipopigiwa, hakuna abiria, nikaona niwahi kuja kukuchukua.
Mimi: Ahsante.

Tulipofika hotelini nikaenda zangu chumbani moja kwa moja, kwanza nikapumzika, usingizi mzito ukanipitia kustuka 12 na jioni. Nikaamka nikakoga koga pale, nikaona kahawa wacha nikanywe nje huko, kwenda kunywa kahawa mara Meneja na yeye kaja. Tukakaa nae tunakunywa kahwa wote.
Meneja; Vijana washakujua hoteli, wananambia ndugu yako yuko huku anakunywa kahawa, ndio nimekuja.
Mimi; Ahasangte, nisikuharibie kazi zako, mimi nipo OK kabisa.
Meneja; Hapana, mimi nilikua natembea tembea, kuna wageni kutokea Dar kina mama wawili tunawategemea.
Mimi; Wagtanzania au wageni wa nje?
Meneja: Watanzania, jamaa zangu kwa mbali hao, unajua mimi mngazija. Na wangazija sote ndugu kwa namna moja au nyengine. Kuna Watanzania wanafikia sana hapa, sio wageni wa nje tu, bei zao kidogp zinatofautiana na wa nje na Watanzania wanalipa kwa shillingi wageni wa nje mara nyingi wanakuja package yao wameshalipi hukohuko kwa ma agent wao, hapa wakitumia vitu extra tu amabavyo havipo kwenye package. Mfani wana ziara ya kwenda na kurudi mjini huko mara mbili kila siku, moja day time moja night time, hii ya usiku inakwenda forodhani, hii inatusaidia sana sisi kupunguzaa gharama.
Mimi; Kwanini? kwa sababu sisi hapa tunakua tayari gharama mpaka za kula asubi, usiku na mchana, sasa wakienda stone town wanakula huko wengi wao hawali tena hapa, inakua tumeshusha gharama sana.
Mimi; Oooh, nimeelewa.
Meneja: hapa mimi kazi yangu kubwa ni kuhakikisha nashusha gharama za matumizi ya hoteli bila kiushusha ubora, ndipo faida kubwa itaonekana.

Meneja; hawa kina mama wa Kingazija wana mila na ada zao, ukiwaona wanakuja ujue kuna sherehe yao. sherwhe yao mara nyingi hua Jumamosi, na hawa watakuepo siku tagtu hapa, leo, keshoi na keshokutwa lazima wana sherfehe yao.
Mimi: Wewe umeshaona sherehe zao?
Meneja: Utotoni tu, ukianza kukua kua huruhusiwi kabisa mwanamme, hta ufanye nini. mambo yao ya mashetani shetani.
Mimi; Kwanini wanagfanya siri?
Meneja: hata sielewi wala sitaki kuelewa, hayo y mashetani ni hatari sana, samahani Simba, mimi hata kuyataja naogopa, bituko walivyokua wanagtufanyia hapa Hoteli? Mimi isingeaku Babu yako nilishasema na kwenda kujaribu mara ya mwisho, mambo hyakiendendelea nawacha kazi hapa natafu mengine ya kufanya.
Mimi; Ilikua serious sana?
Meneja; Ngoja nikshawapokea wageni wakitulizana niakupa stoiry, yetena itakua voizuri maana mengine hata babu yako nilikua sijamuelezea. Kwa hio wewe sikufichi kitu, niahidi utamfikishia babu yako.
Mimi; Si yamekwisha?
Meneja; Nashukuru yamekwisha lakini ngoja nitulizane nitakuja kukuhadithia au unatoka?
Mimi; Niende wapi usiku huu?
Maeneja: Aaah kuna disko hapa hotelim na kuke nbeke kidogo kuna disko, sema hili la hapa liko kule uoande wa pili, hili letu limechangamka sana, mimi nilifanya mpango na wenyeji wawe wanakuja, lakini soi wote wale wenye poesa zao tu, ili isiwe fujo. Tembelea huko usiku pazuri sana, utapenda, utapata kuiona Unguja by Night, utakuta wagtoto wa Kiunguja wale nyumba za kitajiri wanakuja kujirusha, wale awa kufugwa kama majini.
Mimi; Unanitamanaisha.+Meneja,; Huko kuanzia saa sita usiku moaka saa kumi alfajiri ndio kumekucha, kabla ya hapo wageni wageni tu wazungu, kwa kua linaanza saa tatu usiku. Mimi huwa natembelea huko kutazama tazama kama wageni zangu wapo salama na huduma zinapatikana bvvizuri.
Mimi: Nitatizama, kama sijachoka nitaenda nikajionee badala ya kuhadithiwa.


Tukaagana pale meneja akaenda zake, nikapiga kahawa yangu tena nikarudi chumbaini kwangu. Nikawaza, nikajua meneja hajaeewa kua na mimi nipo kwa ajili ya huyo kibuki.

Nikampigia babu, baada ya kusalimiana.
Mimi: babu leo nimemuona bi S wa kibuki. Nikamwelezea babu yote niliokumbana nayo
Babu: hayo muulize Arsis atakueleza, mimi naamini hakuwepo Simba hapo, hao hawawezi hata kuja, kwani tunamikata nao tayari lakini muulize Arsis.
Mimi; Sawa, nikamuelea nilichoongea na Meneja. Babu akacheke sana.
Babu: Mimi siku na haja ya kumsikiliza mengi, wewe msikilize kijana mwenzio huyo. Mimi nilijua likimalizwa tatizo moja yote yatakwisha, aliemaliza tatizo huko Bakora, kwa majani na mitishamba yake tu. Na mimi Alhamdulillah nilisoma sana Qur'an, imekua kubuli.
Mimi; Okay, najua nani atanipa mkasa wote.

Babu; Vipi lakini unaonaje tripu yako?
Mimi; Mpa sasa poa.
Babu; Utai[enda tu Unguja, anagalia usibaki huko, akacheka.
Mimi: Mbina unanitisha babu?
Babu; Sikutishi wenyewe wana msemo wao wanasema, Unguja ni njema atakae na aje.
Mimi: babu kwaheri.

Tukaagana pale.
Simba.
...13
Nikaingia chumbani kwangu nikakoga koga nikavaa kashual tu ile sijatoka Simu ikaita, kupokea Jini 1. Tukasalimiana pale.
Jini1; Simba leo umekua mtu mkubwa sana Unguja.
Mimi; Kivipi tena?
Jini 1; Utaogopewa Unguja nzima, wewe utanambia. Ngoja kesho kutwa, utanambia.
Mimi; Kwanini?
Jini 1; Wewe huoni jinsi mkubwa wa vibuki vya Ndama Mulaki alivyokunyenyekwea?
Mimi; Akiona kuna simba, nilikua nataka kumuuliza Arsis hilo.
Jini1; Wala haina haja ya kumuuliza Arsis, yeye anasikia maonhgezi yetu. Kwanza mimi sikukupigia kwa hilo. Lakini kwa kua tumeshalianza nakuja kwako, nije?
mimi; Njoo.

Hata sekunde haijachukua mlango ukagongwa, kufungua Jini 1 kafungua ananukia udi halafu kapendeza huyo kavaa na abaya.
Mimi; kwema?
Jini 1; Kwema, mambi ya Unguja haya, ukiwa Unguja lazima uwe Muunguja, kwani nimechukiza?
Mimi; umependeza lakini wewe sura yako hutaki niione mika yote, kwanini?
Jini1; Wewe nae huchoki kuniuliza hilo, achana na hilo, mie ukiniona utakua hunikaribushi kwako au utakua hutaki nindoke.
Mimi: haya nambie kilichokuleta.
Jini 1: Kwanza ngoja tumalize swala la leo kwa Bi S. Bi S, kulikua hakuna simba wala jinni la Simba. Bi S. kawekewa picha tu kwa teknolijia ya kisasa, ile niliwahi kukwambia sijui Arsis anitaje na kizungu chenu. Hio hata wewe Simba huipati hio, sisemi mengi.


Sasa ile picha ya Simba aliwekewa na wewe ulipokua unaongea alipopandisha yeye, na jini lake likaogopa sana, wanamjua Simba, tena huyo aliewekwa picha kwako ndio baba lao. Ndama akaogopa akawa na anamwalaumu sana Bi S, kafikia mpaka kumwambia siku nyingine ukimakribiusha mtu mkubwa namna hii lazima tujue iki tumkaribishe kwa hadhi yake. Usirudie tena, lazima apewe heshima zote Simba. Huyo ni mkubwa sana kwetu sote sisi. Kwanza kakaufanyia heshima kubwa sana kuja, huyo haji bure bure tu. Kwa hio jichunge sana na kauli zako na mambo yako kwake. Muhheshimu huo kuliko mimi.

Jini 1: hayo ndio aliambiwa Bi S. Sasa mimi hayakunileta hayo, yamenileta nikupe umbea. Wageni walikuja leo hapa Hoteli, wameshafika huko. Wanajuana na Dokta, si unajua Wangazija wote wanajuana, wao walikua hawajui kama kaja hapa, Bi S ndio aliwaambia wana shughuli ya mtu wa hukohuko kwao Dar, wakauliza nani alipowaelekeza, wakamwambia gtunamjua sana, mtoto wa fulani yule. Akawajulisha kua mwenzao ndio shughuli yake ya kwanza. Waksema hii sio ya kuikosa, huyo tuwe nae, maana hapa Dar hapatikani sana, lakini tukijuana nae huko huku sasa itkua wepesi kuwa nae karibu.

Jini 1; hayo ndio yalioongelewa, mengine umbea wa kike tu sina haja ya kukwambia.
Mimi; Sasa inanihusu nini?
Jini1: Na wewe si umbea tu, unakua unajua kinachoendelea.
Mimi; haya Ahsante kwaheri.
Jini 1; Unaona upuuzi nilichokwambia, utakuja kukifurahia siku moja. kwaheri, akafungua mlango akaondoka zake.

Sijakaa sana, simu ya hoiteli ikaita, nikaipokea.

Meneja: Njoo bwana, umeshakula?
Mimi; bado ndio nilikua nafikiri maana leo nilialikwa biriani la nguvu njimini huko.
Meneja; basi vizuri kama haujala, niliwaalika hawa kina mama waliokuja chakula cha usiku, nikaona na wewe uje mpate kujuana. Watyu wa Dar hawa, labda mnajuana. Njoo bwana ni watu muhimu sana kujuana nao, utawapenda, wachesi sana.
Mimi; basi nakuja.
Meneja; kama nusuu saa watakua washakuja, unaweza kuja mapema tukapiga stroty, watatukuta.
Mimi; Poa.

Nikaona wacha nipige simu kwa wanangu Dar maana inaweza kua usiku nikakosa kuongea nao, nikawapigia nikaongea na wofe nikaongea na wanangu. Nikampigia mother na Mzee. Nikafikiria nikampigia na mshikaji. Ile kupokea tu.
Mshikaji: Ilikua nikupigie leo hata saa kumi usiku? Nambie dokta uko poa huko?
mimi: Sijamuona lakini nategemea kumuona kesho.
Mahikji; nambie kweli, unakwenda Unguja kitu kama kile huna habari nacho?
Mimi; Sasa yule si umesema demu wako? Nikuvunjie heshgima Mshikaji wangu?
Mshikjai: Wewe mwana nakujua, huna mazzagazaga siku hizi. Ingekua enzi zako, kwani anagefika hata Unguja yule, wadamganye wengine. Ingekua sijamuona kupanda boti na wewe inhgekua sijaenda kukupeleka bandarini, ningejua saa hizi umemficha sehemu, ile hoteli yenu ya kisenge mliokwenda kukaa sabam halafu sisi washikaji wako hatukupewa kadi.
Mimi; Nimekupigia kukusalimia na kukuuliza gari yake vipi.
Msshikaji: Mwanangu, dingi wako mchaawi wa magari hakuna siju cha kkompyuta zako wala nini, tumnehangaika sisi tumesagfisha tanki la mafuta, tamki lilikua safi kama jipya, mafut asafi, filter zote mpya, tukiitest gari iko vile vile.

Mwanangu dingi wako akasema fungueni boneti, tukafungua, dah, yule mzee sijui ananusa ugonjwa ulipo? Akatazama pale akasema washa gari ile kuwashwa, akaipiga resi kwa mbele, akasema zima gari. Mwanagu yule mzee noma. Kuna kidude hichoi kina paipu ndogoi ndogo na miwaya waya, akakichomoa mwenyewe dakika sifuri tu, akkaikupiza upoanda mmoja kisha akakipyuliza upande mwingine, akasema hii mixer sensor sijui kaita jina gani pale, ndio tatizo, akanambia mimi nkamletee ile sporay haitoki juu ya meza yake,kuoleta, akakipachua akakaippulizia akasafisha vizuri, akakirudishia akaki[puliza tena, akakpachika kwenye gari, cha kupachika pahika tu, hakihitaji hata spana. Ingekua wewe pale ungeitish spana za gereji nzima. Akacheka. Basi mwanagu kupiga stati, steringi mimi hapo, gari kam mpya, unaihisi gonjwa limekwisha, Dingi akasema haya kapige raundi uje usseme kama imebadilika au bado.

Mshikaji; Mwanagu, yule dingi wacha mikampuni imeletee migari yao, wanajua yule mchawi wa magari, yule ukisafiri hulali porini.

Nkaona huyu hanyamazi leo.

Mimi; Hoyaa, kwa hio gari iko poa.
Mshikaji: tena kutoka hapo nimeifanyia mwenyewqe usafi mwanzo mpaka mwisho. Yule Dokta mwenyewe akiiona ataisahau. Halafu mwanagu si nilikwambia yule mtu wa ndumu? Kaacha vizibiti kibao kwenye eshtrei, nimekuta vipisi vitatu, vile bvua mwisho kabisa, halafu yule anaonesha anapiga kavu kavu bila miksi bila nini, vipisi vimejaa asali.

Mimi: Hoyaa, poa bas nyamaza, nilitaka kujua hilo tu. Mie kabla ya kuja nitakupigia unifate.

Mshikaji; Lini mwananhgu, unajiua Unguja vifaa vinauzwa rahisi, mwananhgu nichukulie mziki mmoja mnene, wale nyokjko pale nyumbani wananiringishiavimziki vyao, nataka wakiwasha nikiwasha wangu wote wanazima.

Mimi; Nakuahidi mioana na Dokta nakuletea mimi zawadi ya mziki, lakini wewe si Sheikh siku hizi mziki mnene wa nini?
Mshikaji: Ule niwazime wale tu kelele zao, tutasikiliza Qur'an mule saa zote.

Mimi; Kwa heri. Nikajiweekaaweka swa nikatoka kwenda kwenye msosi.

Nikamkuta meneja, yupo nje ya chumba cha msosi, boitra umeytokea wewe kwanza, hawajafika bado, lakini hawachelewei, ilikua waje dakika 15 nyuma, mara ananamibia hao.
Meneje; Karibuni, karoibuni utafikiri mmeambizana na Simba hapa. Huyu ndie niliwaambia na yeye katokea Dar. Anaitwa Simba, Simba huyiu Bi H na huyu Bi H, wote majina yao yanaanzia na H lakini ni majina tofauti, nitawaita Hw na H2.
H 1: Jina lako linatisha, Simba wapo ngorongoro huko.
Mimi: usiotishike ni jina la ukoo tu, jina langu noi...
H2: hilo Simba ndio zuri zaidi, nimelipenda.
Meneja; Mimi nilichagua tukae pale te)wendeni, najua myatapapenda, alichagua meza amabyo unakiona chumba kizima cha chala.

Tukaenda kukaa pale akaja mhudumu akaleta menu.
H1; Weewe ndio umetualika chakula sasa tuchague tena, wewe tuagizie, wewe ndio unavijua zaidi.

Meneja: Pengine mna miiko ya chakula.
H2: Mimi sina mwiko kwenye kula kasoro kiwe cha halali tu.
H1; hata mimi, labda mwenzetu DSimba hapa.
;Mimi; Meneja mimi sina mwiko kama hawa mabibie hapa. Watachukula nwao na mimi nakula.

Meneja, basi poa, tutaanza na light salad ya kaa, pamoja soup ya Kithailanda inaitwa TomTun Gong, hiyo wenyewe wa Thai wanasema Ni Mfalme wa supu zote duniniani. mtaiependa sana, halafu tutaleta chakula mchanganyiko kidogo kidogo, kila mtu aatakula apendacho na njaa yake. Akacheka.
H1; Njaa nilonayo si ndogo.
Mimi nikakumbuka code yangu na wife nikataka kucheka nikajizuia, lakini H1 alishaniona nikitabasamu.
H1; mbona umefurahi Simba na wewe una njaa?

Meneja huku ananyanyuka, msiwe nashaka kuleni muwezvyo kama hamjatosheka semeni tu kinakuaja, mimi dakika tatu narudi.

H1; Simba umesikia, kula tani yuako kama hujatosheka ongeza tu.
Nikajua huyu bibie kishaipata code.
H2; Mimi ninhgepayta na wine ingekua traha kweli, wine inazisidisaha njaa.
H1; Una yako tu wewe, akanyoosha mkono.
Mhudumu kuona mkono akaja mbio mbio.
H1; Mna red wine zzuri kwa chakula? Zipo aina nyingi lkakini mimi na recommned, akataja jina gani sijui, kwa sababu naoana hio ndio wageni wengi wanaipenda.
H1: Wanaipenda pengine kwa bei rahisi.
Mhudumu; Mama hapa wine zote bei moja tu, niz zuri.
H1p haya tuletee.

Ikaletwa wine kwanza )tukaoneshwa, ikafunguiwa mbele yetu, akatia kwenye glass moja kidogo tuonje, H1 akasema mpe DSimba atuonjee. Mimi nikawaambia pass.
H1: Mpe huyo cha pombe alietaka wine.

Akapewa H2 akaionja kimadaha, akasema iko fresh sana, nitilie akatiliwa, akawa anakunywa peke yake.
Mhudumu; Kama nyinyi mtapenda niwaletee sparkling water ni nzuri kwa chakula.
H1; Wewe unajua mambo, leta hio.

Mhudumu alivyoondoka kuleta.

H2: hajui, sema kweli, angekuletea mambo yako yale, saa hizi ungem hug.
H1; Bado muda wake, subiri nione mazingira hyamekaaje kwanza.

Meneja akarudi na muhudumu akaja kaleta maji mara ikaletwa bakuli kubwa la salad ndogo ndogo nikaona imechangwa na nyama ya kaa. Meneje akaanza kutaka kuwapakulia, kina mama. Wakasema wewe tia chako, sisi tutati wenyewe, ahsante mwanangu. We simba huyu mamake na mimi babu yetu mmoja. kwa hio mimi mwanangu huyu.
Simba.
...113
 
Hio sio shida yangu Sheikh, hio shida yako kuzusha au kufata kitu kilichozushwa na unakifata kama kipofu au kiziwi.

Nimekuuliza maswali mengi sana, lakini naona hata moja hukulijibu, kwanini?

Mojawapo nimekuuliza, unajua elimu za kusoma zilizopo kwenye Qur'an?

Tena nikakwambia hauzimalizi kabla haujaanza kuzusha zako mpya.
Simba.
Unajua maana ya uzushi? Tuanzie hapa kwanza
 
Unajua maana ya uzushi? Tuanzie hapa kwanza
Kwa Kiarabu ni; Bidaa
Kwa Kingereza ni; heresy.

Umeridhika au bado?

Sasa na wewe rudia post zangu unapokuta alama ya kuuliza jibu ukweli wako. Nbona unakwepa maswali yangu? Yamelenga kutoa elimu.
Simba.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom