Inatokea post namba 98.
Haukupita muda nikaingia pangoni kulala. Cha ajabu ni kua, lile pango lilikua kubwa sana, lakini sikuhisi uoga hata kidpogo kulala mule.
Haikupita muda nikapitiwa na usingizi. Kstika kulala kwangu nikaota ndoto ya wazi kabisa. Nikawa kwenye ndoto naisikia ile sauti ya mwenye pete. Ikiniambia wazi ?mimi naitwa Arsis", kuniita si lazima upige kelele kama ulivyofanya leo. Unawe kuniita hata kwa kufikiria gtu, mimi nitafika, kuongea na mimi pia kukiwa na watu sio lazima useme kwa sauti, ukifikiria tu unachotaka kuongea na mimi, nitakujibu. Hii ndio nilikwambia mapema inaitwa "telepathy".
Sijui niite ndoto au mawasiliano ya upande mmoja yakaendelEA; Kuanzia sasa wewe nitakua nakupa ujuzi wa vitu mbali mbali, utavyoweza kufundisha wengine uwafundishe, vile ambavyo huvielewi niulize. Usifiundishe mtu kitu usichokielewa. Kitu kikubwa sana cha kuwafundisha atu ni namna ya kutatua matatizo yao na tiba zao. Kuna tiba utazielewa na kila utayoielewa upo huru na ni lazima ufundishe wengine. Si umeona afanyavyo babu yako? Babu ako hamnyimi mtu dawa na mengi hayafichi. Ukiona hujasikia kitu kutoka kwake elew kua hicho hana ujuzi nacho, huwa anasaidiwa na wengine bila nyinyi kuona au kuelewa. Sasa yote ya babu yako utayapata wewe na zaidi z)sana. Saidia sana binadam wenzako matizo yao. Usibagie tajiri na masikini, wogte ni kitu kimoja. Tatizo la tajiri na tagtizo la masikini halina tofauti. Hakuna utajiri mkubwa zaidi ya afya.
Basi hayo ndio niliweza kuyashika ckear kabisa kwa siku hiyo na sitasahau. Haujapita muda baada ya hio ndoto, nikaamshwa usingizini. Nikaamshwa na wanawake wawili, wakanimsha kwa upole kabisa. Wakajitambulisha majina, yao, huku mimi nikiwa nimekaa pale nilipolala, mmoja akasema sisi ni majini wazuri au wengine wanatuita maruhani. Hatupo hapa kudhuru mtu, tupo hapa kwa ajili wewe umechaguliwa kutatua matatzio ya watu, sisi wote tunafanya kazi chini ya mwenye hio pete ulioibvaa lakini hatuna mamlaka nayo, na sisi tumepoewa pete zetu utatuona sana tukiwa kama binadam, utatujua kwa kuziona pete zetu, pete zetu zinafanana na zina kito chekundu lakini kito chake hakijakooza kama chako na vito vya duara, tu. Zitazame. Wakanionesha vodole vyao. Nikawauliza "mboina siwaoni sura zenu". Mmoja kajibu sisi huwezi kutuona ssura zetu za asili, utatuona kwa sura za kibinadam tutakapoona mitaani huko. Tutakuja kwa sura tofauti z umri tofauti, usitegemee kutuona kwa sura au umbo utakalo lizowea, tunabadilika badilika, ndio kawaida yetu. Lakini pete hazibadiliki, hata tukija na mapambo mengine pete hizi tulizokuonesha zinakuepo na zinabaki hivi hivi kwenye vidole hivi hivi vya pete. Tumekuja kujitambulisha. njoo kidogo tukutenbeze kwenye pango.
Nikaamka nilipokaa, mmoja, aliekua haongei, akatangulia mbele, yule mwengine akawa ubavuni kwangu. Sikuwa na uoga kabisa wla sikuhisi hofu yoyote. Yule akaendelea kunambia. Huyu ni mama angu mzazi, yeye haongei sana. Nikamuuliza sijamsikia kuongea. Yule ambae haongei, akasema, mimi ni mtu mzima sana naitwa... Akanitajia jina lake, akanambia sisi kazi zetu atakueleza mwanangu, yeye ndie utamuona maa kwa mara, mimi nimekuja kujitambulisha tu, nikija utajua nimekuja, Huna haja ya kuniita. Isipokua napenda kukuelewesha kua kuanzia sasa tupo pamoja na wewe. Mweney hizi pete ndio mfalme wetu kwenye ulimwengu usioonekana na kwa ulimwengu wenu wa kibinadam wewe ndio mfalme wetu na enzi yako ni hio pete yako. Sisi hatuwezi kukita kwa jina tutakuita "bwana mkubwa" kuanzia sasa. Babu yako kaanza kukuita bwana mkubwa kunzia mchnga. Babu yako ni mtu anaeheshimika sana katika ulimwengu wetu, kwa ajili ya ukoo wake, ukoo wake usioonekana ni ukoo wa simba, ni wakali sana na wanaogopewa sana. Hakuna simba ambae hana damu ya kifalme kwenye dunia yetu.
Tukafka kwenye kama njia panda hivi ya pango, yule mama akanyamaza, akingia uoande wa kulia, akaanza kuongea mwanae. Huku sasa unakwenda njia ya kwenda kwetu, huku haruhusiwi mtu kuingia bila kukaribishwa. Wewe peke yako unaruhusiwa kuja, ukija na mgeni hawezi kufika huku, ataishia pae njia panda. Hatua chache mbele tiukakuta kama ukumbi mkubwa umepambwa vizuri sana, wakanmbia karibu, ukae, kuna kama makochi lakini ya mito mitupu, mizuri, yiule mtoto akakaa kwanza na mimi nikakaa tunatazamana, mama yake akaaga akasema yeye ndio anaondoka, ana mambo mengi ya kufanya. Nikamwabia "kwageri" akanijibi "kwaheri" akapihga hatu mbili tatu kueleke ndni akapotea sikumuona tena pangoni.
Yule aliebaki akanambia mimi hutohitaji kuniita, wewe utamuita mwenye pete tu akiamua yeye nije utajua uwepo wangu, ikibiudi na mama aje basi utajua uweoo wake. Nimekuleta upajue kwetu, hapa ni mbai sana na unapolala lakini mfalme kaifupoisha sana safari. Kwa leo usiulize chochote, tulikuja kujianbulisha tu kwako, kama una swali lolote utamuuliza mfalme. Nikamwabia "sawa, nimeelewa". Akanamia haya twende nikurudishe, karibu sana wakati wowote ukija hapa chukulia kua umeshakaribishwa, Ukihitaji kuja usisite, tutakuepo. Tukaondoka mpaka pale njia panda akanambia si unajua njia ya kurudia, mimi naishia hapa. Nikamwabia ndio naijua. Tukaagana akaondoka na mimi nikaondoka kurudi.
Ie barudi nasikia sauti kwa ne ya pangi watu wanaongea, na yule kijana wa babu ninae lala nae nikasikia anaongea nje, na sauti ya babu. NIkatoka nje.
Itaendelea.