Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Usiidharau, majini na malaika wanakuja ndotoni.

Kuna siku Arsis alielezea kidogo humu kuhusu ndoto ni nini, kaniacha hoi.
Simba.
Ndoto ni halisia bro
Inawezekana hapa ndio tupo ndotoni.
Sijui lakini
 
Kisa hicho cha nwisho cha Simba huko Unguja kimeniliza machozi. Kwa kuwa naifahamu hiyo familia ya Kiunguja, iliowa "toto" la kariakoo, kutoka ukoo maarufu sana.

Dunia ni hatari sana jamani, baba mtu anamtowa mwanawe kwa tamaa za kidunia.
. Arsis karibu sana na kisa cha Adam.

Allah atustiri.
 
"theology"
Vionjo vya Arsis 4 Kumwokoa Msukule Unguja 8.
Inatokea post namba 2358.

Sheha; wachawi wenzenu wengine wa hapa mtaani ni kina nani?

Afisa; Hio ni siri ambayo hatuwezi kuisema hadi kifo. Mmeshatushika sisi na wote waliohusika na hii kazi, ambao hawajahusika hata kanuni za kikawaida zinakatzaa kuhusishwa.
Bakora: Mimi namuunga mkono kwa hilo. Tuendelee na mengine.

Sheha; Tueleze waliohusika.
Afisa; Wameshikwa wote na sikjii kama wapo hai mpaka sasa, maana hukumu ya hili ni kifo tu, haina mjadala kichawi. Hata chama chetu tukikamata waliongilia himaya yetu bila kukubaliana kabla tukiwakamata ni kifo tu. Labda tusiwakamate.
Bakora; Huyu analeta mambi ya kichawi ili apoteze muda. Mimi nashauri kwa kua ewotw wamekiri wahukumiwe.
Sheha, wapelekwe mahakamani?
Bakora; ndio, hilo moja na sisi tutapitisha hukumu yeytu kwanza na nyinyi, hususan wewe, upo hapa Kiserikali huo utakua uamuzi wako. Sisi hukumu yetu, hatuwezi kuisema hapa mbele za watu, tunajua tuwajulisha vipi, hatutaki kesi.
Sheha; Nimeelewa. Mimi wacha nipige simu polisi, mkubwa wa kitiuo cha hapa jirani namfahamu.
Bakora: hautompata huyo leo, wala kesho. Labda umpigie msaidizi wake.
Sheha, aah kasafiri?
Bakora; Ndio.
Sheha, wewe ngeni Sheikh, unajuaje?
Sheha: Mimi tunafahamiana nae, najua kua kasafiri alfajiri ya leo. Uliza hata ofisini kwao waytakueleza.
Sheha; Sasa tunafanyaje?
Bakora; Wazo la kuwashitaki hawa ni zuri, ushahoidi woite upo na wao lazima watakiri hawatoisumbua mahakama, kwa kua binti yupo hai, sijui hukumu yao itakuaje kiserikali.
Sheha: Wacha nipige simu hapo nje,. jamani akam kuna hawa leteni ytunywe. Haya si mabo madogo, maana naanza vbipi kuwael;eza polisi?
Bakora: Waeleze ukweli kama ulivyouona na kuusikia kuanzia alfajiri. Watuhumiwa si hawa hapa mnao?
DSheha; Sawa wacxha niende nje nikapige simu.
Kijana: Na mimi wacha niende nje, kweli kama kuna kahawa uje jamani.

Kuna wanawake wakainuka, waksema kule ipo nyingi wacha tukalete na vikombe.

Mimi, Kijana, Balora tukatoka nje. na wengine wote wakatufata kasoro watuhumiwa tu. EWakabaki wamekaa, kama wamepigiliwa misumari.

Kutoka nje mimi na kija n na Bakora yukaenda kukaa pembeni, tukawacha pale Waunguja na Sheha wao.

Bakra: sasa hapa kaszi imeisha, hawa sisi tutatimiza hukumu kama ya wale, hawatiweza kufanya kazi kabisa, lak9ini cha kwanza inatakiwa mali za yule bwana lazima huyu binti na mamake walipwe kwa machungu waliopitia. Na huyu mumewe, ndio hana chake tena. Mtito yule asafiroshwe kabisa asibaki Unguja, maana hii hadithi tayari ipo mitaani saa hizi inazagaa kama moto wa makumbi.


Kahaw aikaja tukanywa pale.

Sheha; Polisi wanakuja kikosi cha maana.
Bakora twendeni ndani tukamalize sisi tuna safari jamani, hapalkaliki.

Tukaingia ndani wote, mimi nikaitwa ndani na kina mama huko, nikakuta kumbe mipango yao ya kumsafirish binti kwenda bara ytayari lakini hakuna alieambiwa, na ataondoka na mama yeke mdogo, kimyakimya. Nikaone heri. Ikaja sauti ya Arsis kichwani ikinambia, usiwe na wasiwasi, yupo chini ya ulinzi wetytu, wewe uytawaona Datr hao. Nyyie mnawsza kusafiri wakija polisi anagalia msisema lenu mkafanywa mashahidi, itakua ngumu kwenu nenda rudi. Nikamuelewa.

Ile tunatusi ndani hatujjakaa polisi wamegonga nje, akatoka Sheha akaanza kuomngea nao, nje, na sisi tukaaga,m hakauna aliesema chochote. Tukatoka mimi, Bakora na kijana, mama ndani huko washasuka kuondoka na binti na mamake mdohgo. Tukaondoka.

WWale mbwa wawili wakachukuliwa wakapelkwa polisi, wakaelezea kama walivyoelezea, wkawekawa ndani bila dhamana, mahakamni siku ilipofika kwa kua wanakiri makosa, wakahukumiwa jela. Walipokua jela ndio hukumu ya majini walioifanya hio kazi ikapitishwa.

Tutaendelea na kionjo kingine tutaporusi, hiki cha Unguja tukimalizie hapa.
Simba.



Itaendelea
S
Simba umeanza woga,
Hii story imeisha ghafla sana
 
Kweli, ashushe vitu.
Nina hamu ya kusoma story ya Adam na tupate uthibitisho kuwa hakua binadamu wa kwanza.

Tatizo hii thread ikishawekwa mambo ya dini (haswa hizi mbili Islam&Christian mzozo unakua mkali kweli)
 
Kisa hicho cha nwisho cha Simba huko Unguja kimeniliza machozi. Kwa kuwa naifahamu hiyo familia ya Kiunguja, iliowa "toto" la kariakoo, kutoka ukoo maarufu sana.

Dunia ni hatari sana jamani, baba mtu anamtowa mwanawe kwa tamaa za kidunia.
. Arsis karibu sana na kisa cha Adam.

Allah atustiri.
Acha tucheke na kutaniana tu humu,
Ila Dunia yakisenge sana
 
Kama unasema Adamu wapo wengi maana yake Waliumbwa Adam wengi, Huoni kuwa hiyo haibadilishi kauli ya kuwa mtu wa kwanza kuumbwa ni Adamu?
maana kama kuna adamu wengi basi yeyete katika hao adamu walioumbwa awe atakavyokuwa ila itabaki mtu wa kwanza kuumbwa ni adamu nafikiri logically nipo sahihi.
Ningetegemea useme kuwa adamu sio mtu wa kwanza kuubwa kisha utuambie kwa mujibu wa quran mtu wa kwanza kuumbwa ni.......... kisha utupe ushahidi, Lakini hoja ya kusema kuna Adamu wengi sio hoja kuwa adamu sio wa kwanza.
Mimi nasubiri useme kwa mujibu wa quran Nani ni binadamu wa kwanza ? na yeye adamu aliyetajwa katika baqarah ni wangapi ? huyo wa kwanza anaitwa nani? na katajwa wapi katika quran?
Tikienda kwa njia hii tutaelimishana vizur kuliko maneno mengi yasiyo na majibu.
Mimi navyomuelewa hapa Arsis neno Adam limetumika kama cheo/hadhi. Kwahiyo hicho cheo cha uadam, kilimirikishwa/hodhiwa na watu tofautitofauti kwa mihura kadha wa kadha...!
 
  • Kisa cha Adam; Utangulizi 1

    Salaamoun Alaikoum.

    Ni nini mbu?

    Leo tuna mada ambayo Kwa kweli nilisita sana kabla ya kuamua kuiwasilisha kwenu. Hii ni topic ambayo itakutingesheni sana uelewa wenu na mawazo yenu. Nawaomba sana, kila ataeisoma hii mada, ni ndefu sana, ajichukulie yeye kua ni mgunduzi wa elimu ambae itaifanya mawazo yake yajiulize kwanini sikulijua hili mapema? Utajiuliza ni kwanini hakuna mtu alieona hili kabla?

    Hii ni elimu, ni rejea kwa kila mtu bila kujali dini au imani yake. chanzo kikuu ni Qur'an kwa aslimia 100. Kuielezea tutatumia Qur'an kama asasi na mara moja moja tuweka hadithi zinazoendana na tunachokielezea. Tunaweza kutumia lugha zote ili kuufikisha ujumbe, kwa sababu, moja ya muujiza wa Qur'an, ilitumia Kiarabu. Kiarabu kina llisan nyingi sana mpaka kimekua lisan a sehemu na nyingine zina utofauti kama lugha tofati lakini ni ileile. ilitumia lisan ya pale kinapoelezewa kisa kwa kiasi fulani. Ingawa hakuna asiejua kua imeshushwa kwa Kiarabu cha Mtume Muhammad.

    Mfano ikiongelea watu wa Ibrahim itatumia lisan ya watu wa Ibrahim. Lisan ni ulimi kwa Kiswahili au lugha iliotumika pale, kwa maana ya (lexicon) au (locution) ya pale.

    Kisa hiki cha Adam tutaanza na aya ya 26 na 27 ya suratul baqara (Q2:26). Tutazichambua kuzifahamisha kadiri ya tulivyojaaliwa. Ingawa wengi huanza kumuona Adam kutokea aya ya 30 (Q2:30) sisi tuanzie hapo kufanya tafsil.

    Namaanisha neno "tafsil" sio tafsiri. Maana ya “tafsil” kwa ufupi ni kuchambua. Mfanpo uchukue kitunguu maji uanze kuchamvua ganda moja kuanza la nje mpaka ufike kwenye kiini cha kitunguu.

  • Tunaipata ukisoma ukisoma surat Fussilat".

    Kwanini tunafanya tafsili? Kwa sababu Qur'an inajieleza yenyewe, ina muujiza wa mfumo ambao tunaweza kuuita wa kiota (nestle). Kiota kina miti, vijiti, majani na mengine lakini yote yameshikana na hakuna katika vilivyojengea kiota kisicho na maana. Qur'an ni hivyo hivyo, inashikana na kuungana yote na hakuna neno au herufi isiyo na maana. Kama ulimsoma mtafsiri akaliacha neno au herufi kua hii imezidi au hii haina maana kwa sasa, elewa kua huyo hakuielewa maana ya hilo neno au herufi kwa ilivyokusudiwa. Kwa kufanya tafsil tunapitia hayi miti, majani matawi kwa kina ili kuipata maana halisi ya neno lilipotumika kwengie ili tupate maana ya neno au aya tunayotaka kuifahamu.

    Kwa kufanya tafsili tunahama sura hadi sura, aya hadi aya, neno hadi neno, herufi hadi herufi. Mpaka tunapojikinaisha tumepata uelewa wa maana halisi ya neno hilo au aya hiyo. Tunachokitafuta zaidi kwenye tkufanya tafsil ni uelewa wa maana halisi au iliokaribiana sana na hilo neno au aya tunaypoitafutia maana.
    Licha ya mbinu (method) ya tafsil, Qur'an ina mbinu nyingi, zake yenyewe za kulielewa. Na mojawapo nimeitaja juu hapo, ya "lisan" au ndimi (locution) iliotumika. Ndani ya Quur’an kwa kiwango kikubwa imetumika lisan ya Ibrahim (Abrahmic locution) na wakati tunaendelea,tutafahamu kwanini, na ikiwa kuna mtu atataka kuelewa mapema basi asisite kuuliza kwanini sana imetumika lisan ya Ibrahim.

    Mbinu zingine kadhaa, tutaziona kila tunavyoendelea na tutazielezea kadiri ya uwezo wetu kila itapohitajika.

    Q;2;26
    إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَسْتَحْىِۦٓ أَن يَضْرِبَ مَثَلًۭا مَّا بَعُوضَةًۭ فَمَا فَوْقَهَا ۚ فَأَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ فَيَعْلَمُونَ أَنَّهُ ٱلْحَقُّ مِن رَّبِّهِمْ ۖ وَأَمَّا ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟
    فَيَقُولُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَـٰذَا مَثَلًۭا ۘ يُضِلُّ بِهِۦ كَثِيرًۭا وَيَهْدِى بِهِۦ كَثِيرًۭا ۚ وَمَا يُضِلُّ بِهِۦٓ إِلَّا ٱلْفَـٰسِقِينَ ٢٦

    26. Hakika Mwenyezi Mungu haoni haya kutoa mfano hata wa mbu na ulio wa zaidi yake. Ama wale walio amini hujua ya kwambahiyo ni haki iliyo toka kwa Mola wao Mlezi, lakini wale walio kufuru husema:Ni nini analo kusudia Mwenyezi Mungu kwa mfano huu? Kwa mfano huu huwapotezawengi na huwaongoa wengi; lakini hawapotezi ila wale wapotovu,26


    Tarjama iliotumika ni ya Sheikh Ali Muhsin Barwani kwa jitihada zake binafsi, Qur'an yenyewe ni hio ya Kiarabu. Naweka angalizo hili kwa sababu katika kutumia mbinu ya tafsil, tunaweza kuweka tarjama nyingine kwa jitihada zetu. Lakini hatutothubutu kuongezea neno au maneno yetu au kupunguza neno au maneno ya Qur'an. Ukiona neno katika tarjama lipo kwenye mabano elewa tarjama au ytacsiri zilizo[po sasa, elewa kuwa hilo sio la Qur'an ni la aliyeandika tarjama, Qur'an haina mabano.

    Siifahamu maana ya neno "tarjama" kwa Kiswahili, anaeifahamu aielezee. Kwa Kiarabu kuna tofauti ya maneno "Tafsir, Tarjama na Tafsil.

    tafsiri linamaanisha kuielezea hiyo aya kwa njia nyepesi kwa lugha nyingine au hata kwa lugha ile ile.

    Tarjama linamaanisha kubadili neno / maneno kutoka lugha moja kwenda nyingine, ambalo kwa Kiswahili hutumika neno tafsiri.

    Tafsil, maana yake ni kuchambua, kama unavyochambua kitunguu, ganda kwa ganda mpaka upate kiini cha maana.

    Kwanini itumike tafsili? Sababu ni nyepesi sana; katika lugha ya Kiarabu neno hilo hilo moja linaweza kubadilika maana kutokana na sentensi lilipotumika. Pia neno moja la Kiarabu linaweza kua na maneno mengi ambayo yanatumika kutokana na linapotumika na kwa lugha nyingine likawa na neno moja ya kulielezea, mfano neno jicho au macho, inaweza ikawa Ain kwa Kiarabu, lakini neno hilo hilo, Ain, linaweza likawa linamaanisha kiini au likawa linamaanisha chemechem.

    Kwa hio katika kuielewa Qur'an ni muhimu sana kuelewa lisan au ulimi wa sehemu lilipotumika hilo neno. Qur'an ina muujiza huo bila kujielezea, kwa maandiko yake utaelewa.

    Pia mifano hai mizuri sana ipo kwenye Qur'an yenyewe, kila tunapoendelea tutaiona.
    2...
    Arsis.
 
Mimi navyomuelewa hapa Arsis neno Adam limetumika kama cheo/hadhi. Kwahiyo hicho cheo cha uadam, kilimirikishwa/hodhiwa na watu tofautitofauti kwa mihura kadha wa kadha...!
Hata mimi ndivyo nilivyomuelewa hivyo huko nyuma, lakini naona kwa sasa kaanza kukielezea hapa yeye mwenyewe, ingawa mimi ndio ninae chapa (gtype) lakini ni 100% kwa maagizo na kusimamiwa na Arsis hata wapi niweke koma na wapi niweke full stop.
Simba.
 
Nina hamu ya kusoma story ya Adam na tupate uthibitisho kuwa hakua binadamu wa kwanza.

Tatizo hii thread ikishawekwa mambo ya dini (haswa hizi mbili Islam&Christian mzozo unakua mkali kweli)
Arsis kaanza kuelezea kisa cha Adam kwa muono wake, mwenyewe anasema kama kilivyo kwenye Qur'an bila kuongezea lake. Kaanza post namba 2407.
Simba.
 
Simba umeanza woga,
Hii story imeisha ghafla sana
Sio uoga, niogope nini zaidi Mwenyezi Mungu?

Arsis alikua ananihimiza anataka aanze kisa cha Adam.

Nakaribisha maswali kuhusu kisa cha Unguja na kingine chochote nilichokileta humu mpaka sasa. Visa vingi vinakuja.
Simba.
 
Sio uoga, niogope nini zaidi Mwenyezi Mungu?

Arsis alikua ananihimiza anataka aanze kisa cha Adam.

Nakaribisha maswali kuhusu kisa cha Unguja na kingine chochote nilichokileta humu mpaka sasa. Visa vingi vinakuja.
Simba.
Kimsingi sina swali zaidi nilitaka nione mtoto baada ya kurudishwa nini kiliendelea,
Kuanzia kwa ofisa, .baba na mtoto mwenyewe. Hata na kundi la wachawi waliohusika. Maana wachawi walifungwa na majini ila huku kwao hujatuambia km waliyeyuka ulimwenguni au vp.
Ila nimejifunza kitu, binadamu ni mnafiki sana, na ni mbishi kuliko majini.
Wachawi wote wa kibinadamu walibisha hawana hatia pamoja na kukamatwa ktk tukio.
Ila wachawi wa kijini walikubali na kuhukumiwa Fasta tu.
Hii inanikumbusha hata mahakamani ukiwa mtuhumiwa unaposomewa kesi ni lazima uanze kwa kukataa kosa, hata km umehusika kweli.

Sasa sijui hili, je ni upungufu wa binadamu au ndio ukamilifu wa binadamu?
 
Arsis kaanza kuelezea isa cha Adam kwa, muono wake, mwenyeq anasema kama kilivyo kwenye Qur'an bila kuongezea lake. Kaanza post namba 1407.
Simba.
Kwanini hii elimu imeegamia upande mmoja wa dini?
 
Kwanini hii elimu imeegamia upande mmoja wa dini?
Haikuegemea upande wowote, Arsis kila dini utayomuuliza anasema yeye ndio hiyohiyo.

Isipokua anaamini kitabu cha mwishpo cha Mwenyezi Mungu ni Qur'an na hapa baada ya mabishano na Waislam aliwaambia nyie mnaijua na kuiongelea Biblia kuliko Qur'an, ndio akawauliza mmelitoa wapi na Adam kua ni mti wa kwanza kuumbwa duniani?

Ndipo lilipoanzia hapo. Kaamua kutoa elimu, ili WQaislam waajielewe na wasio Waislam wajielewe.

Kwani mama pretty kusoma kuna dini au dini ipo moyoni kwako?

Unaweza kujiita muislam ukawa mchawi, mwanga, mshirikina, kuna dini hapo> Halikadhakika unaweza kujiita mkristo ukaewa mwanaga, mchawsi, mshirikina, kuna dini hapo?

Tusiibague elimu kwa misingi amabyo haipo hata kwenye iani zetu. Mimi sijaona biblia ikikataza mtu kuisoma Qur'an wala sijaona Qur'an ikikataza mtu kuisoma biblia.

Tumia fusa hii kumsoma Arsis. Mbona anamsifu sana Che mittoga na kila siku anaukandamiza na kuuponda Uislam na Waislam? Hapo ndipo Arsis anaponiacha hoi. Na Waislam humu hujawasoma wanamshambulia Arsis badala ya kushambilia hoja zake? washamuita kila jina la kiajabu ajabu na la kukera, lakini yeye anaendelea kumwaga elimu kwa wote.
Simba.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom