Niliwahi kumwambia Hayati Dkt. Magufuli, nakwambia na wewe Rais Samia; Watanzania ni masikini sana!

Habari Watanzania wenzangu,

Kuna jambo ambalo naamini viongozi wetu huwa wanalipuuza wakifika kwenye viti hivyo.

Japo Tanzania ina utajiri mwingi sana, lakini Watanzania asilimia kubwa ni fukara sana.

Hii ni kuanzia kwa Mawaziri, Makatibu wakuu, viongozi wa Taasisi mbalimbali, Majaji, Bunge na Wabunge, Wawakilishi, Waziri Mkuu, Makamu na Rais; wote hawahisi kabisa magumu wanayopitia wananchi wengi waliopo ktk umaskini wa kutupwa.

Ukitaka kuthibitisha hili, angalia sera mbalimbali zinazotungwa na serikali. Haziakisi kabisa hali ya maisha ya Watanzania wengi!

SWALI: Shida ni nini?

Tuna sera za kijinga sana, tuna maamuzi mengi ya kipumbavu kweli kweli. Nchi imejaa mikorogano tu.
Ukiulizwa hii sera alitungiwa Mtanzania, hadi unahisi uchungu hadi moyo unataka kuchomoka.

Hawa akina Mwigulu, na Rais wetu Mh. Samia wana shida gani hasa?! Au shida ni vile ving'ora, au saluti wanazopigiwa, au misafara mikubwa mikubwa ile, Mbona hawaelewi kabisa uhalisia wa maisha ya WaTz wengi!

Niliwahi kusafiri hadi Bukombe, Geita huko. Nilimkuta Mwananchi mmoja, ameugua kweli, lakini kwa sababu alikuwa na Sh. 2000 tu. Hiyo hiyo anaitegemea kula, kuhudumia watoto, na kila kitu. Yule ndugu alichukua uamuzi wa kwenda kununua paracetamol (dawa za maumivu) za sh. 400/- ili ameze japo atulize maumivu ya mwili.

Watanzania wa aina hii wapo chungu mzima nchi hii. Mtu anaumwa, hana hela ya kumuona daktari, hana fedha ya vipimo, na wala uwezo wa kununua dawa. Anaamua kununua tu dawa za maumivu.
Si kwamba hapendi kutibiwa, la hasha, kipato kinakataa.

Nikuulize Mh. Rais Samia, huyu Mtanzania akitumiwa na ndugu yake sh 25,000/- aende hospital, mtumaji anakatwa tozo, na yeye akienda kutoa ana tozo. Rais wangu na wewe Dr. Mwigulu mnatengeneza Uchumi wa watu gani? Huu sio wa WaTz, labda mna watu wenu wengine mnaowawaza na kuwahudumia.

Ni wakati sasa Mh. Rais Samia ukate matumizi yote yasiyo ya lazima ndani ya serikali yako.

Haiwezekani Waziri, Naibu Waziri, Katibu mkuu, Wakuu wa Taasisi, Mamlaka mbalimbali, mkuu wa mkoa, n.k, atembelee gari ya thamani ya Tsh. 400 million, huku kuna Kijiji kizima hakina Zahanati, Kuna shule haina choo, kuna shule hawana madawati. Halafu unaweka Tozo kwenye sh. Elfu 10, unajiita Mzalendo, na tai ya rangi ya Tanzania unavaa. UNAFIKI!

KATA MATUMIZI YOTE YASIYO YA LAZIMA, KABLA HATUJAKWAMA KAMA TAIFA.

Watanzania ni fukara sana. Isipokuingia akilini hii, 2025 watakulazimisha upishe mwingine.
Huo ufukara wa waTz uliouzungumza wameuprogram wao na wataendelea kuuprogram ili kuendelea kutawala. Wanatumia kanuni hii "Ukitaka kumtawala mtu utakavyo mnyime elimu bora ili awe mjinga pia muue kiuchumi". Usitarajie huruma hapo ndugu.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Umezungumza kwa hisia. Kuhusu hoja ya umasikini vijijini; tunakubaliana kimsingi ni tatizo kubwa. Rural poverty ni tatizo kubwa si tu Tanzania bali ktk devoloping countries, hasa za Afrika zilizopo Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Chanzo kikubwa; ni kutokufanya mapinduzi ya kilimo. Kwa sababu rural economy ktk hizo nchi inategemea kilimo, lakini poor teknoloji, black market na ukosefu wa mitaji na utaalamu umefanya kilimo cha kujikimu, hivyo mnyororo wa umasikini tena wa kurithi (generational poverty) kuzidi kukua. Umasikini wa kurithi yaani masikini anazaa masikini hadi vijukuu. Kwa msingi huo, issue siyo tozo bali kufanya mapinduzi makubwa ya kilimo. NDICHO ANACHOKIFANYA MHE. RAIS SAMIA. Nampongeza sana Mhe. Rais.

Rais anafanya mapinduzi ya kilimo. Tusaidie mawazo kufanikisha mapinduzi ya kilimo maana ni mfumo endelevu wa uchumi na wa kukata mnyororo wa umasikini vijijini, kuhakikisha food security, kujenga taifa la watoto wenye lishe bora hivyo kuondoa udumavu wa akili na mwili. Tumsaidie Mhe. Rais SSH.🙏🙏🙏
Ati "issue sio tozo" na "tusaidie kufanikisha mapinduzi ya kilimo"! Eti unampongeza Rais...nk. Naona ungejisemea tunajipongeza ss viongozi kama ulivotuomba "tuwasaidie" kufanikisha.
Sjui una umri gani lkn haya mambo ya kilmo sio mapya! Toka enzi za Mwl Nyerere mnatuimbia lkn hamna formula yyt ya maana ya kutekeleza. Ingerahisisha zaidi mngejipungzia mishahara, maposho na hizo anasa zenu ili kupunguza hiyo 90% ya bajeti ya Kawaida ingalawa ifike 60% na ya maendeleo 40%-yaani badala ya 7tri/- za maendeleo ingawa zifike hata 70tri/-.
Ni maendeleo gani utaleta kw hako ka bajeti kanakolingana na ka manunuzi ya magari mnayopapanga kujinunulia!? Umeomba tukusaidie mawazo nami napendekeza hayo- yaani rudisheni bungeni hiyo bajeti inayolipiwa na tozo za wanyonge ili mlipie nyie toka kwenye maanasa yenu mliojipangia badala inayowaumiza mnaowaita wanyonge, au huoni mnazidi kuwanyong'oneza? Wasilie?
 
Mh. Samia apaswa kujua eti, mwanangu na hilo nendeni mkalitizame, sio kauli ya kiuongozi.
Hii kauli huwa inaniboa kinoma yaani imekaa kubembelezana sana, yeye kama mkuu wa nchi lazima atambue mamlaka aliyonayo na atoe maelekezo/amri ya nn kifanyike na kwa muda gani. Siyo kutoa kauli zenye loopholes au general general kama hiyo
 
naunga mkono hoja ya mtoa mada, Watanzania ni masikini sana naongezea na hili "MASIKINI NA PRIMITIVE"

Tuna kazi kuubwa sana hapo, kuondoa uprimitive na umasikini na bahati mbaya wenye mamlaka wameziba masikini.
 
Serikali imepunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kufidia tozo tuache kulalamika tozo zimesaidia kuimarisha sekta muhimu ya afya na elimu
Utakuwa unakalia kichwa sio makalio. Huwezi kuandika upuuzi huu hapa au na wee ni mlaji.

Mtoa mada katoa mfano ulo wazi :watanzania hawana mapato ya kujikimu hata kwenya matumiz ya lazima kama maradhi.

Wee unakuja kusema serikali imesitisha matumizi yasiyo ya lazima. (( labda utuambie ni yapi hayo) .

Kama mkuu wa nchi anakwenda kumzika mtu ambaye hajaifanyia lolote la msingi nchi hii. Kulikuwa na ulazima wakwenda msibani kwa malikia? ((Au hayo ni matumizi ya lazima?)) .

Unapo kuja humu andika vitu vyenye kueleweka . Usidhani sisi tunao katwa hatutaki maendeleo.
 
Masikini ni mtu mlemavu asiye jiweza kwa lolote.
Usitutie umasikini wako mkuu maana sisi tunajielewa na tunajiondoa katika hali hiyo kifikra na kimatendo.
Nashaka na elimu yako. Alafu FAKIRI utamuita nani. Kama masikini ni mlemavu basi wee ni wakwanza coz una ulemavu wa akili, maana hujui kutofautisha kati ya FUKARA NA MASIKINI
 
Serikali imepunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kufidia tozo tuache kulalamika tozo zimesaidia kuimarisha sekta muhimu ya afya na elimu
Kabla ya Tozo mambo yalikuwaje?

Unapoweka tozo, ni wananchi wamekuwa na uchumi mzurii au serikali Imefirisika inataka ichangiwe na iendelee na matanuzi yake ama?

Au ni wananchi wanaihudumia serikali..!

Mbona sasa ugumu wa maisha ndio imekuwa balaaa, na umasikini Kwa watu umeongezeka zaidi..
 
Masikini ni mtu mlemavu asiye jiweza kwa lolote.
Usitutie umasikini wako mkuu maana sisi tunajielewa na tunajiondoa katika hali hiyo kifikra na kimatendo.
Una matatizo kichwani

Ikiwa masikini ni mlemavu!

Unapoiita nchi yetu kuwa ni masikini, huwa mnamaanisha nchi yetu ni lemavu?

Pumbavu kabisa!
 
Kuna kiongozi mmoja alipiga picha na bibi mmoja ameweka umeme wa Tanesco kwenye nyumba ya udongo. Hawa viongozi hawana muda wa kumkwamua mtu wa chini ili awe na maish mazuri bali kumdidimiza ili awe masikini. Kuna Clip mmoja ya yule mzungu. Nilimuelewa sana. Yule bibi kazi aliyobakiza sasa hivi ni kusafiri tu mara yupo Kenya, yupo Uingereza kwa kodi na tozo za watanzania.
Sasa hivi bei ya bidhaa na huduma zipo bei juu mara 2 ya zamani. Ukitaka kuona hii serikali ya kinyonyaji kaangalie vifurushi vya TTCL halafu wanajiita wazalendo. Leo matumizi ya internet yapo juu kwa hela gani walizonazo watanzania?
Na bado wanasema ttcl imepata hasara.. aseeee
 
Una matatizo kichwani

Ikiwa masikini ni mlemavu!

Unapoiita nchi yetu kuwa ni masikini, huwa mnamaanisha nchi yetu ni lemavu?

Pumbavu kabisa!
Wewe ndio una matatizo makubwa zaidi.
Maana umeukubali umasikini kama mlemavu, nawe ni mlemavu zaidi wa akili.
 
Nashaka na elimu yako. Alafu FAKIRI utamuita nani. Kama masikini ni mlemavu basi wee ni wakwanza coz una ulemavu wa akili, maana hujui kutofautisha kati ya FUKARA NA MASIKINI
Semantics hazikusaidi kma bado wewe ni masikini.
Ondoa umasikini kwa level yako ya mtu mmoja mmoja na familia yako.
Baadaye Taifa litafaidika kama wengi wanaushughulikia umasikini na kuuondoa.
 
Hii kauli huwa inaniboa kinoma yaani imekaa kubembelezana sana, yeye kama mkuu wa nchi lazima atambue mamlaka aliyonayo na atoe maelekezo/amri ya nn kifanyike na kwa muda gani. Siyo kutoa kauli zenye loopholes au general general kama hiyo
Napata wasiwasi kwamba si yeye anayeongoza!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom