Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Tafuta ufisadi wake ulio mpya endapo anao, hii tunangoja taarifa ya Mkaguzi wa serikali
 
Mkuu Kevo,heshima mbele mkuu.

Hii ngoma ya siku nyingi kweli ishajadiliwa kwa kirefu na ni moja ya mambo yaliyopandikizwa ili kumbomoa SITA mbele ya bunge na uma kwa ujumla.

Nilivyoona SITA nikajua kashfa mpya nikapata hamu ya kupitia hoja zako.
 
Huyu mheshimiwa angemuandikia shairi Khadija Kopa akaliimba ungekuwa ni mpasho bora kabisa, huenda na mimi ningejaribu kumuandikia shairi Nasma ili ajibu mpasho huo. Hii sio habari mpya. Tunatakiwa kuweka mkazo kwenye Mapapa ya ufisadi yale ndio yanayosumbua.
 
I did not know that, thanks for informing
 
Hii imekaa kama Mipasho fulani hivi, Mkuu Kevo haya yote ambayo unasema ni tone yalishapita humu labda kama unatukumbushia tuu.
Huwa hamkosekani.....utaomba ushahidi sasa hivi.....
 
Moderators inabidi kuondoa hizi habari zilizopitwa na wakati. Zinatupotezea muda wetu bure.

Au ningeshauri uongozi wa JF moderators waongezwe ili thread kama hizi ziwe merged timely na zilizopita zinazohusiana nazo.
 
The National Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi), the first opposition party to be registered at the introduction of multi-party politics in Tanzania through its earlier National Committee for Constitutional Reforms is calling for the immediate unconditional resignation of Samwel Sitta as speaker of the National Assembly.

``Speaker Samwel Sitta directly contravened the Witchcraft Ordinance through ordering scientific investigations on powdered dust found at Parliament Hall last month linking it with superstitious beliefs,`` declared James Mbatia, NNCR-Mageuzi National Chairman to the press yesterday.

The Ordinance forbids witchcraft beliefs.
Speaking in a telephone interview yesterday, Sitta said: ``I am not resigning.

If you read the Hansard you will realize nowhere had I said anything about witchcraft.

The debate was closed yesterday (Friday) by the Deputy Speaker and if one wants to continue with it, it is none of my business.``

Speaker Sitta had last month admitted that Bunge security cameras had captured two figures putting `unidentified substances` on legislators` seats inside the hall at a time when they were not supposed to be there and later told the House that scientific investigations on ` believed modern poisons` would be undertaken by the police, the national security and the government chemist.

Reacting to Deputy Speaker Anne Makinda that parliamentary debate on the issue was over, the party chairman remarked: ``Parliament is not above the people.

The people`s power will decide on this issue, and we are going to instigate a national debate because our country has suddenly and terribly lost its reputation abroad.

``In Holland (the Netherlands) where I am studying, and in Sweden, we Tanzanians are dubbed \'jujumen`.

We are already stained through Sitta`s position in this regard and in order to cleanse ourselves he has to step down instantly from the high office he is vested with by Tanzanians before any further actions are considered against him.``

Flanked by NCCR-Mageuzi Secretary General Polisya Mwaiseje and Dr. Sengodo Mvungi, head of the legal affairs wing, Mbatia fumed: ``The people must make all those involved in the saga accountable.

Our (Union) Constitution is the voice of the people on how we are to be governed, and because of that we are saying `a big NO` to stopping the debate prematurely unless Sitta, the man we are highly convinced is the cause of all this smear, and who perhaps believes in witchcraft, must let it go.``

The party, which said the witchcraft saga was above party politics and ideologies, has also proposed that the chief government chemist must be warned strongly for submitting to Speaker Sitta`s order of investigating the chemical properties of samples of the \'witchcraft\' substances.

``We know the chemist had acted on orders which should have been ignored in the first place so long as the substances would never reveal any `witchcraft or superstitious` contents after all,`` charged Mbatia, stressing that a private motion against Sitta was opportune by any legislator who had a responsibility to Tanzania first, the constituency second, the party third and inner conscience fourth.

Efforts to get the government chemist failed yesterday as he was attending a meeting.

SOURCE: Sunday Observer
 
Kama kamera za Bunge ziliona yeye anasemaje? Na kama hazikuona ilikuwaje akatoa taarifa za uongo? Na kwa hili anatakiwa kujibu ati.
 
Bogus bogus!!!! Mbatia umeishiwa pamoja na hao mafisadi waliokutuma!!! Kwani Spika Sita alisema uchunguzi ufanyike kwa sababu wamenyunyizia uchawi bungeni???? Fact ni kuwa uchunguzi ulifanyika kwa kuwa haikujulikana nia ya mtu anyesemekana alikuwa anamwaga unga na ni nini hasa alimwaga.... N.B. Mbatia umeshaacha ule mchezo wako???
 
Hivi ni kweli alikuwa anapiga mapanga bili za matibabu?

nimepata info kuwa hatalile CARPET la BUNGENI ambalo lilinunuliwa toka SPAIN alikuwa 10% yake na mbaya zaidi CARPET lilikuwa na bendera ya NCHI ambalo kila siku anaikanyaka

sasay alot about the man right?


sasa kama mytu ambaye yuko heartbeat from Urais ni hivi je kweli twaweza muamini na nchi?


KNasikia hata wakati wa ujenzi wa Bunge alikuwa aningilia mpaka kazi za ma ARCHITECTS kisa hakpata 10%

sasa how do we deal na mtu kama huyu ? maana ukwli ni kuwa hawezi kushitakiwa lakini tunayo freedom ya kuongea au mnasemaje?
 
Hivi ni kweli alikuwa anapiga mapanga bili za matibabu?

nimepata info kuwa hatalile CARPET la BUNGENI ambalo lilinunuliwa toka SPAIN alikuwa 10% yake na mbaya zaidi CARPET lilikuwa na bendera ya NCHI ambalo kila siku anaikanyaka

sasay alot about the man right?


sasa kama mytu ambaye yuko heartbeat from Urais ni hivi je kweli twaweza muamini na nchi?


KNasikia hata wakati wa ujenzi wa Bunge alikuwa aningilia mpaka kazi za ma ARCHITECTS kisa hakpata 10%

sasa how do we deal na mtu kama huyu ? maana ukwli ni kuwa hawezi kushitakiwa lakini tunayo freedom ya kuongea au mnasemaje?

Binafsi nahisi hizo allegations kwa spika ni false. Hasa kwa jinsi unvyo sound..'nasikia'....unasikia toka wapi? Kwa unakitu chenye mshiko mwaga bila konakona, tutaweza elewa.
 
Hivi ni kweli alikuwa anapiga mapanga bili za matibabu?

nimepata info kuwa hatalile CARPET la BUNGENI ambalo lilinunuliwa toka SPAIN alikuwa 10% yake na mbaya zaidi CARPET lilikuwa na bendera ya NCHI ambalo kila siku anaikanyaka

sasay alot about the man right?


sasa kama mytu ambaye yuko heartbeat from Urais ni hivi je kweli twaweza muamini na nchi?


KNasikia hata wakati wa ujenzi wa Bunge alikuwa aningilia mpaka kazi za ma ARCHITECTS kisa hakpata 10%

sasa how do we deal na mtu kama huyu ? maana ukwli ni kuwa hawezi kushitakiwa lakini tunayo freedom ya kuongea au mnasemaje?


Heshima mbele mkuu GT, Ila kinachonifurahisha kama si kunishangaza ukipotea kidogo na ukirudi hapa jamvini lazima uje na kitu cha kufurahisha baraza...... kwa hayo mimi bado sijakubaliana na wewe maana still bado unasikia, hukuona wala kuhakikisha so yawezekana kabisa kuyasikia kwako hayo mambo yakawa yanaendana na msemo huu SIASA NI MCHEZO MCHAFU
 
Hivi ni kweli alikuwa anapiga mapanga bili za matibabu?

si kweli. Limethibitishwa na uchunguzi huru na taarifa zikatolewa hadharani.

nimepata info kuwa hatalile CARPET la BUNGENI ambalo lilinunuliwa toka SPAIN alikuwa 10% yake na mbaya zaidi CARPET lilikuwa na bendera ya NCHI ambalo kila siku anaikanyaka

Mwenye kusimamia vinavyonunuliwa Bungeni si Spika, kuna utawala wa Bunge unaosimamia shughuli za siku kwa siku na mambo ya ujenzi. Kama kuna 10% ijengwe hoja ya kuonesha uwezekano huo ili watu waanze uchunguzi. Ni sawa na mtu kudai kuwa lile mojawapo ya majengo ya NSSF samani zake ziliingizwa toka Uarabuni ambapo Mkurugenzi alikuwa na 10% na mtu akadai kuwa "amesikia" hilo.


sasay alot about the man right?

there are a lot of things that say a lot about a lot of people, picking just one of them is in not too many words simply unreasonable.


sasa kama mytu ambaye yuko heartbeat from Urais ni hivi je kweli twaweza muamini na nchi?

Ni wazi huijui Katiba yenu, Spika hayuko a "heartbeat from Urais".
KNasikia hata wakati wa ujenzi wa Bunge alikuwa aningilia mpaka kazi za ma ARCHITECTS kisa hakpata 10%

this can be said about a lot of CEOs or upper management in the country. I'm thinking of one quick example...


sasa how do we deal na mtu kama huyu ? maana ukwli ni kuwa hawezi kushitakiwa lakini tunayo freedom ya kuongea au mnasemaje?

sijui umepata wapi wazo kuwa hawezi kushtakiwa? Uhuru wa kuongea upo ilimradi watu wasikimbilie kutishiana maisha tu na kupigana mikwara ya kitoto vile visivyopaswa kuongelewa vinapoanza kuongolewa. Otherwise, tuko pamoja mkuu.
 
Spika si ndio alidaiwa kuwa gharama zake za matibabu kwa mwezi Sh.2ml ??? Hawezi kuacha kuwa Fisadi na yeye si uzao ule ule wa Nambari 1??
 
Binafsi nahisi hizo allegations kwa spika ni false. Hasa kwa jinsi unvyo sound..'nasikia'....unasikia toka wapi? Kwa unakitu chenye mshiko mwaga bila konakona, tutaweza elewa.

Hata maandishi ni ya mpingompindo hivi,,, kama hajiamini vile. Kuwa wazi tukuelewe! lol
 
Spika si ndio alidaiwa kuwa gharama zake za matibabu kwa mwezi Sh.2ml ??? Hawezi kuacha kuwa Fisadi na yeye si uzao ule ule wa Nambari 1??

Naam! Na haya yalisemwa hadharani lakini je, ulifanyika uchunguzi wo wote kuzifuatilia ‘tuhuma' hizo au tuliambiwa kama alionywa? Pia hivyo 'vijisenti' alivyokula ni jasho la Walalahoi wanaofia Mwananyamala na MMC hospitals!

waga
"kwa hayo mimi bado sijakubaliana na wewe maana still bado unasikia, hukuona wala kuhakikisha so yawezekana kabisa kuyasikia kwako hayo mambo yakawa yanaendana na msemo huu SIASA NI MCHEZO MCHAFU"[/COLOR]

Inaelekea JF wakati mwingine tunajikanganya wenyewe. MJJ anasema "Uhuru wa kuongea upo ilimradi watu …." lakini papo hapo tunamlaumu GT kwa kutudokeza "aliyoyasikia". Hivi mimi nilidhani kuwa tukiisoma taarifa kama hizo nasi tufanye uchunguzi na baada ya siku moja au mbili ndio tumjibu hatukuthibisha cho chote au kumpa ukweli tunaoujua.
Jamani, kwani hamkumbuki kwamba SITTA aliyatafuna mamilioni ya CDA enzi zake mpaka ikabidi kumtoa huko Dodoma? Hayo Makao Makuu ya Bongo ni ‘Ramani tu' hadi sasa ‘hayajabalehe' – Mawaziri na Mabalozi wote na Ofisi zao bado zipo tu hapo Mzizima (Ubalozi wa Marekani utadhani ni Fort Knox ilivyojengwa na kulindwa na the most sophisticated surveiilance gadgets of modern times - kweli watahamia DOD hao hao??)

Je, kuna mwana-[B]JF anazo takwimu ni mabilioni kiasi gani yamemezwa hapo CHE-DE-A na bado Makao Makuu hayajakamilika? Hili likoje ??[/B] NAMI HAYO NILIYOYAANDIKA NIMEYASIKIA. JE, MTATAKA USHAHIDI NIUTOE WAPI NA NI SIRI ZA KIFISADI ????
 
Nimesoma nime elewa lakini sija elewa .Naenda pale bakhresa kutafuta kinywani nirudi cafe .Unasma haya ndiyo maisha ya Samwek Sitta ? Naomba uendelee kumwaga mambo hapa .
Hta mimi naona nitasoma vizuri nikiweka bingwa kichwani jioni
 
sitta1(2).jpg


Spika wa Bunge letu bwana SAMUEL JOHN TEGEZA SITTA anatuhuma za kutumia vibaya pesa za umma kwa njia mbali mbali kama vile:

Amekuwa akitumia msaidizi wake kuchota mapesa kwa kisingizio kuwa ni masurufu ya safari za ndani na nje ya nchi. Kila safari ya siku moja ndani ya nchi huchukua shilingi Milioni tano (5,000,000/=), na kila safari ya siku moja nje ya nchi huchukua shilingi Milioni Kumi na Tano (15,000,0000/=).

Alishindwa kufanya marejesho ya masurufu (imprest) hayo, licha ya kupeleka risiti kadhaa za kughushi/za uongo kwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Bunge. Mpaka sasa anadaiwa jumla ya shilingi Milioni sitini (60,000,000/=) za masurufu.


- SITTA aliwahi kupeleka risiti za uongo kwa Mhasibu Mkuu, zikionesha madai kutoka Oysterbay Pharmacy ya Shilingi Milioni Mbili ( 2,000,000/= ) aliyotumia kwa tiba kila wiki.


- Aliwahi kulazimisha hawara yake wa Hospitali ya Aga Khan naye alipwe posho kama wabunge anapokwenda naye Dodoma. Kwa mfano, hawara huyo alilipwa ‘per diem’ kuanzia tarehe 13/12/2007 hadi tarehe 31/01/2008 ( Siku 50). Huo ni Ufisadi mkubwa!


- Aliwahi kuwa na kimada wake mwingine anayekwenda kwa jina la ASIA ambaye aliiishi nyumba Na. 111 karibu na Mahakama ya Ardhi Upanga na amezaa naye. Huko mtaani kwao kimada huyo hujiita mama SITTA, na ni dada yake aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa iliyokuwa Tume ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC). Mwanamke huyo muda wote alikuwa akitumia gari la Ofisi ya Bunge STK 232 Toyota RAV 4.


- Pia anaye kimada mwingine ambaye anaishi kinondoni ( Livingstone), mtaa wa Honolulu katika nyumba ya kupanga inayomilikiwa na dada yake Kawawa. Nyumba hiyo inatazamana na Nyumba Na. KH.MK/No. 337 katika mtaa huo huo. Kimada huyo alikuwa anatumia gari ya kiofisi ya Spika mwenyewe STK 3002.


- Vimada wote hao walikuwa wanapata huduma za maji na umeme kwa gharama za Ofisi ya Bunge. Kuna kipindi mke halali wa Spika, aliwahi kulalamikia hali hiyo. Kuna siku maji yalikatika nyumbani, mke wa Spika akaomba apelekewe ‘ bowser’ la maji na Ofisi ya Bunge. Ohooo! Watekelezaji wakapeleka maji kimakosa kwa kimada. Mama Sitta akashtukia dili.


- Kuna taarifa kwamba mnamo Mwezi Oktoba 2007, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iligundua mapungufu makubwa katika matumizi ya fedha yaliyofanywa na Spika SITTA. nimedokezwa kuwa Spika aliwanyamazisha wajumbe wa kamati hiyo, ambapo aliwatishia kutowapatia posho na safari za nje kama wangeyafumua mapungufu yake hadharani! Hapo inaonesha kuwa wajumbe hao walipewa rushwa!!


- Kama JK anataka viongozi wa kisiasa na wa serikali watenganishe biashara na uongozi wa ku – ‘sacrifice’ kimojawapo, hilo litakuwa gumu kwa sababu Sitta alipokuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kituo cha cha Uwekezaji nchini (TIC) alitumia nafasi hiyo kuingia ubia na wafanyabiashara wengi wa Kigeni. Je, Wizara ya Maliasili na Utalii inatambua kuwa Spika ana hisa kwenye kampuni moja ya Kichina inayosafirisha magogo licha ya marufuku yaliyowekwa?!

Katika kutaka ukubwa basi amedemand apewe ulinzi sawa na SHEIN alipoambiwa hilo haliwezekani basi alidai apewe escort na magari,mapiki piki na vingora yote kwa ajili yake na kwa gharama za walalahoi

kwa kumalizia tuuu tusisahau kuwa huyu amekuwa kigingi kikubwa when it comes to transparency kwani kamati mabali mbali huyu SITTA amekuwa hataki ripoti zake ziwe kwenye public domain...hivyo hata suala zima la check and balances linakuwa na utata mkubwa sana.


michael-martin_1404212c.jpg

Huyu naye ni fisadi na resignation yake imetokana na presha kubwa baada ya ile listi ya matumizi ya wabunge kuwa LEAKED kwenye JF ya dunia yaani WIKILEAKS...mnaweza kuigoogal


Lakini in a nutshell huyu anatuhumiwa kwa yafuatayo:
High crimes & misdemeanours

October 23, 2000: Elected Speaker amid claims election was stitched up by close friend Gordon Brown

October 30, 2001: Forced to apologise after speaking out in favour of Home Secretary David Blunkett's abolition of voucher scheme for asylum seekers

May 9, 2006: Attacks Press for using the 'hurtful' nickname 'Gorbals Mick'

June 6, 2007: Private Eye says Martin spent £20,000 of public money hiring libel lawyer to challenge negative Press stories

February 17, 2008: Emerges that he used air miles accumulated on official business to fly his children and their families business class

February 23: His spokesman resigns after unwittingly giving 'misleading' details about Mrs Martin spending £4,200 of public money on taxis for shopping trips

March 25, 2008: Speaker's 'shameless' last-ditch legal bid, costing £120,000 of public funds, to cover up MPs' expenses

March 29: Report that refurbishment of Martin's official residence, Speaker's House, cost taxpayer £1.7m over seven years

April 1: Standards Commissioner John Lyon launches sleaze probe into Mrs Martin's taxi trips

November 27: Provokes fury by failing to stop police raiding office of Tory MP Damian Green

May 9, 2009: Report that he claimed £1,400 for chauffeur-driven car trips that included visits to Celtic FC

May 18: Makes disastrous statement apologising for role in expenses fiasco

May 19: Bows to pressure by announcing he will quit on June 21 - first time a Speaker forced out of office since 1695
Source:MPs' expenses: the demise of Speaker Michael Martin - Telegraph


Halafu what is it na hawa na MSPIKA na mijumba na ofisi za Kifahari? Maana SAMUEL SITTA ile ofisi yake na ofisi aliyoojenga BALALI zinafukuzana sema ya SITTA imejaa madubwana mengi kama ile ya MARDOFF wa upatu

of course yote kwa hisani ya Tax payers money



Lakini itakuwa si vibaya kujikumbusha huko tulikotoka....

Sitta achunguzwa

na Happiness Katabazi...TANZANIA DAIMA..28 March 2008


TUHUMA za ufisadi zilizosambazwa katika mtandao wa intaneti zikimlenga Spika wa Bunge, Samuel Sitta, zimesababisha Ofisi ya Bunge kuanzisha uchunguzi dhidi ya kiongozi huyo wa juu wa mamlaka hiyo ya dola.

Taarifa za kuanza kwa uchunguzi huo zilitangazwa na Katibu wa Bunge, Damian Foka wakati alipofanya mahojiano na gazeti hili, ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.

Kwa mujibu wa Foka, madai ambayo atayafanyia uchunguzi ni yale yanayomhusisha Spika na tuhuma za kuwasilisha katika ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Bunge risiti za kughushi za matumizi yake.

“Ofisi za Bunge hazina taarifa za Spika kughushi risiti, nipeni muda niwasiliane na wakuu wa vitengo husika, ili tutafute ukweli kuhusu tuhuma hizo, na iwapo tutabaini lolote tutatoa majibu. Ile ni ofisi ya umma na mali zake zinatakiwa zitumike kwa matumizi yanayopaswa na si vinginevyo,” alisema Foka.

Pamoja na hilo, Foka alikiri madai yaliyoandikwa katika mtandao wa intaneti yanayoeleza kuwa, Sitta aliwasilisha risiti ya shilingi milioni mbili aliyonunulia dawa kutoka katika duka moja la dawa lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Aidha, alisema baada ya kuwasilisha risiti hiyo, alimwelekeza alete pia cheti cha daktari kilichokuwa kikionyesha kuwa alitakiwa kutumia dawa zenye gharama hizo kutokana na matatizo yake ya kiafya katika kipindi cha wiki moja.

“Ni kweli kuwa mwezi uliopita, Spika Sitta alilipwa shilingi milioni mbili katika kipindi cha wiki moja kwa ajili ya kununulia dawa katika duka la dawa la Oysterbay,” alisema Foka.

Alisema malipo hayo ni halali kwa sababu Ofisi ya Bunge ina taarifa kuhusu matatizo ya kiafya ya Spika Sitta ambayo hata hivyo hakutaka kuyaweka bayana kwa madai kuwa maradhi ya mtu ni siri yake na daktari wake.

Hata hivyo taarifa ambazo gazeti hili linazo zinaeleza kuwa, Spika amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya miguu ambayo kimsingi ndiyo aliyokuwa akiyatibu kupitia dawa alizonunua katika duka hilo la dawa.

Kuhusu madai kwamba Spika amekuwa akijihusisha katika matumizi mabaya yasiyotambulika kisheria na kikanuni kwa madaraka yake, ya magari mawili ya Bunge aliyopewa kwa shughuli zake binafsi, Foka alisema hana taarifa hizo na kuongeza kuwa uwezekano wa kuwepo kwa jambo hilo ni mdogo.

Wakati Foka akitoa taarifa hizo, maofisa kadhaa wa Bunge waliozungumza na Tanzania Daima wanaeleza kuwa, siku chache zilizopita ofisi ya Katibu wa Bunge ilipata kumhoji Sitta kuhusu kuwapo kwa madai hayo yanayomhusisha na matumizi yasiyofaa ya magari ya umma.

Foka pia alikanusha madai kwamba Ofisi ya Bunge imekuwa ikilipa gharama za umeme na maji kwa baadhi ya watu walio na uhusiano wa karibu na Spika, ambao kimsingi hawastahili kupata malipo hayo.

Pia alikanusha madai kuwa, kamati moja ya kudumu ya Bunge iligundua kuwepo mapungufu katika matumuzi ya fedha yaliyofanywa na Spika, lakini wajumbe wake walinyamazishwa na Sitta mwenyewe baada ya kuwatisha kuwa, iwapo wangeweka hadharani upungufu huo, wangekabiliwa na adhabu ya kunyimwa posho pamoja na kutopangiwa safari za nje.

Akizungumza madai kwamba Sitta amekuwa akilipwa kiasi kikubwa kwa ajili ya safari anazofanya ndani na nje ya nchi, na pia kujilimbikizia deni kubwa linalotajwa kufikia sh milioni 60, Foka alisema anachofahamu, Spika anasafiri nje na huwa analipiwa huduma ya maradhi na nusu ya asilimia 20 ya posho kama fedha za matumuzi na si zaidi ya hapo.

Naye Mkurugenzi wa Elimu ya Umma na Uhusiano wa Kimataifa wa Bunge, Jose Mwakasyuka ambaye alikuwapo wakati Foka akihojiwa, alisema mali za Bunge zipo salama na kwamba tuhuma zinazoelekezwa sasa kwa Spika zina kila dalili ya kuwepo nia ya makusudi ya kumchafua.

“Hizi tuhuma ni za kupakana matope na kuchafuliana majina, kwani tuhuma zenyewe hazimtaji nani aliyezitoa. Nadhani kuna watu wanataka waandishi waache kuandika mambo ya msingi kwa ajili ya maendeleo ya nchi na badala yake wajielekeze kwenye tuhuma dhidi ya viongozi,” alisema Mwakasyuka.

Hivi karibuni, Spika Sitta alizungumza na gazeti hili kuhusu tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwake na kueleza kuwa, hawezi kuzizungumzia kwa sababu zinatolewa na wahuni wenye lengo la kumchafulia jina lake mbele ya jamii.

Mbali ya hilo, Sitta alilielekeza Tanzania Daima kuwasiliana na maofisa wa Bunge ili kupata ukweli wote kuhusu madai hayo yaliyoandikwa katika mtandao mmoja wa intaneti.

maelezo zaidi kwa hisani ya mzee wa busara



JAMII FORUMS..WHERE WE DARE TALK OPENLY!!
 
Last edited:
Of course hata ma cartoonist wa wenzetu kule hawakumkawiza MICHAEL MARTINS..

morland_557777a.jpg



Cartoon_559342a.jpg



LAKINI katika tradisheni ile ile ya kujikumbusha hebu tuendelee kusoma kuhusu SAMUEL SITTA...
Basil Msongo
Daily News; Sunday,June 01, 2008 @00:01


Spika wa Bunge, Samuel Sitta amesema yeye si fisadi na hana hata senti moja nje ya nchi. Mbali na hilo, Sitta amesema ni vema sasa suala la mgombea binafsi likaamuriwa.

Pia alizungumzia serikali kuwasilisha mapendekezo ya Richmond pamoja na ya uchunguzi wa kashfa ya Akaunti ya Madeni ya Nje katika Benki Kuu (BoT) bungeni katika kikao kitakachoanza wiki moja ijayo.

Sitta aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipozungumza na watendaji wakuu wa vyombo vya habari, wahariri, waandishi waandamizi, na waandishi wa habari za Bunge ikiwa ni mwanzo wa utaratibu wake wa kuzungumza na wananchi kupitia vyombo vya habari kila mwezi.

Kiongozi huyo wa Bunge amesema Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali atatoa taarifa kuhusu tuhuma zinazomhusu yakiwamo matumizi mabaya ya fedha za umma. Alisema wabaya wake wamekosa hoja hivyo wameamua ‘kumgonga’ kwa kutoa tuhuma za kipuuzi za kijamii ikiwa ni pamoja na kuihusisha familia yake.

Sitta alisema anaamini yupo katika mstari mzuri katika kuliongoza Bunge na kwamba wabunge na wananchi katika jimbo lake la uchaguzi wanamuunga mkono. “Mimi sibadiliki hata kidogo…..kama tunavyoelewa katika siasa ukiwa unapika kwa kuni usiogope moshi,” alisema na kuongeza kuwa katika umri wake, amepita katika changamoto nyingi.

“Naamini hata wabunge wananiunga mkono,” alisema Spika wa Bunge na akatoa msimamo wake pia kuhusu masuala yanayogusa maslahi ya taifa ukiwamo uamuzi kuhusu kuwapo au kutokuwapo kwa mgombea binafsi, uchunguzi kuhusu wizi wa fedha za EPA na utekelezaji wa mapendekeo ya Bunge katika mkataba wa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond.

Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, alisema kuna haja ya kufikiwa kwa uamuzi wa mwisho kuhusu suala la mgombea binafsi kwa kuwa limeshajadiliwa kwa muda mrefu. ‘Tufike mwisho, tukubaliane au tusema haiwezekani,” alisema katika mkutano huo wa kwanza na vyombo vya habari ulioonyeshwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha serikali, TBC 1.

“Kama jambo limeamuriwa na majaji watatu, na bado hujaridhika, unaweza kukata rufaa likaamuriwa na majaji saba,” alisema Sitta akizungumzia suala hilo ambalo serikali imekata rufani Mahakama ya Rufaa kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu kuruhusu mgombea binafsi katika uchaguzi.

Kuhusu Richmond, alisema atashangaa kama serikali haitawasilisha taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya Bunge kuhusu mkataba huo uliozua utata na kusababisha kujiuzulu kwa mawaziri mawili pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, Februari mwaka huu.

Alisema pia anatarajia kuwa katika Mkutano wa 12 wa Bunge utakaoanza Juni 8, mwaka huu, serikali itawasilisha taarifa kuhusu maendeleo ya uchunguzi wa wizi wa fedha za umma kupitia EPA.

Spika Sitta alisema katika mkutano huo wa bajeti, atatoa uamuzi kuhusu kauli ya Mbunge Nazir Karamagi, kuwa uamuzi wa kuongeza mkataba wa Kitengo cha Makontena katika Bandari ya Dar es Salaam (TICTS) ulifanywa na Baraza la Mawaziri.

Alisema Karamagi amewasilisha ushahidi kwake, lakini isingekuwa busara kutoa maelezo ya suala hilo nje ya Bunge kwa kuwa suala hilo lilizungumzwa bungeni.
Sitta alisema katika mkutano huo unaotarajiwa kumalizika Agosti 25, mwaka huu, Ofisi ya Bunge itaanza kuwadhibiti wabunge watoro wakiwamo wanaoingia kusaini asubuhi na kuondoka kisha wanarudi baadaye kuchukua posho.


Kwa mujibu wa Spika, miongoni mwa mipango yake hivi sasa ni kubadilisha jina la Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma kwa kuwa kwa sasa inahusika na mashirika yenye hisa zaidi ya asilimia 50 za serikali, lakini kuna mashirika mengine serikali ina hisa chini ya hizo.

Alisema atakapofanya mabadiliko hayo, kamati hiyo itaitwa Kamati ya Bunge ya Mitaji ya Umma. Spika pia alitetea azma ya wabunge kuongezewa mishahara akisema kuwa kiwango wanacholipwa kinajumuisha mahitaji yao yote zikiwamo gharama za usafiri na mishahara ya madereva.


Huyu Sitta aliwekwa pale na ROSTAM ambaye among other things anatuhumiwa kuwa ni FISADI na anapesa nje ya nchi sasa iweje huyu spika awe hana pesa za nje ya nchi?
 
Back
Top Bottom