Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

huo mzozo sasa,full kupeana ulaji!!hii ndio tanzania ya wenye nacho!!!hatari sana km ni hivi!!
 
Mmmm!!!!! huu mzaa sasa ina maana huyu mama sita bado mama yake yuko hai?
 
Mmmm!!!!! huu mzaa sasa ina maana huyu mama sita bado mama yake yuko hai?

..hivi kwani hujui jina lingine la Mhe. Sitta? muulize MWK atakuelewesha zaidi ila anajulikana kwa jina la mzee wa vimada,so inategemea huo ukwe ni wa kimtindo gani
 
wajameni ufisadi siyo huo tuu.hata bank nazo wanatumaliza.
uwezi kuamini wakati mkuuu huyu wa crdb anaingiza hiki kimrija cha kuwamaliza watanzania alikuwa anatudanganya ni kusaidia walipa kodi kutembea na pesa kwa usalama wao,lakini watanzania wengi walijaribu kupiga kelele za kuuzwa kwa utu wao.lakini serikali ikiongozwa na chombo kikubwa kabisa cha nchiTRA wakashikia bango kwamba ni sawa usalama wao wa pesa ni kulipia na kadi na si banker chq kama ilivyo kwa nchi zote duniani,na kama ni kadi basi tutumie kadi za bank yoyote ili kama ni kuchunga hizo pesa watu watumie account walizonazo kwenye bank zingine ,lakini kwa kuwa ilikuwa ni juhudi ya kuchunga maslai ya watu fulani,Tra wakasema hapana kadi ni ya crdb pekee.

watanzania kwa vile wamezoea kupiga kelele na kufwata walikubali kuongeza gharama kwa kununua Tembo kadi kwa jumla ya shs 10,000.na kuweka hizo pesa huko ni shs mia tano.

Tumeendelea na suluba hiyo kwa zaidi ya mwaka na ushe sasa.
sasa kwa kuwa hii ilikuwa ni mipango ya wakurugenzi wa bank ya crdb na vigogo wa Tra wameshajua sasa mambo kwao ni shwari kabisa.
badala ya yale mategemeo ya walala hoi wa Kitanzania kupunguza gharama sasa wametoka kutoka shs 500 mpaka shs 1500.kwa kuweka pesa kwenye kadi ya Tembo kwa ajili ya kulipa kodi ya TRA.

Sasa nauliza swali la ufahamu kama walijua hii si manufaa kwa mtanzania kwa nini wanajaribu kuwanyonya watanzania kwa kujiweka kwenye kivuli cha msaada ???/??

USHAURI WANGU NI HUU
NI VIZURI KAMA KADI IMEPANDA HIVYO NI BORA TUKACHUKUA KADI ZETU ZA BANK ZETU NA KULIPIA TRA KAMA ILIVYOKUWA MWANZO.
SIYO WIZI UNAOFANYIKA BANK YA CRDB KWA MANUFAA YA WATU WACHACHE NA WENGINE WAKIRISKI NA PESA ZAO KUTOKA BANK HII KWENDA BANK YA CDDB KWA AJILI YA KUWALIPIA HAO MAFISADI COMM ZAO ILI WAENDELEE KUSHIBA./.
NAOMBA KUWAKILISHA.
 
Jamani Huyu Mzee Kafanya Mafungo Ya Rc, Wapi Ukwale Haumwachi Mzee Ni Mdhaifu Hapo Kwa Zip ,pia Mama Mvumilivu Sana, Kwa Mzee Wetu Ngoja Tumchimbe Zaidi Na Tuweke Haoa Sebuleni,huyu Jamaa Yupo Kama Sisi Wazaramu.
 
Eeh huyu bwana nilisikia akitukana kwamba watu wana siasa za maji taka!!!!. Lakini kuna ukweli kiasi fulani kwamba huyu Bwana ana ugonjwa wa uzinzi. Mimi siwezi kukataa. Ninamfahamu dada mmoja ambaye nilifahamiana naye miaka mingi (ya 90 na kitu huko)pale Dodoma sasa ni marehemu na mwenyeji wa Kagera ambaye alizaa naye pia. Wakati huo Sita akiwa pale kama Bosi wa ustawishaji wa makao makuu. Inaelekea kuzaa nje kwake ni kitu cha kawaida na ana watoto rundo basi kama ni hivyo. Lakini vipi kuhusu ngono salama anashiriki? kama anaweza kuzaa na kila demu anayependana naye? Aangalie asije muweka mama Mage kwenye mtego wa HIV. Hata hivyo kesha zeeka vipi tena udenda kwa kila binti hata anayelingana na bintiye?
 
nahisi umefika wakati Tanzania inahitaji madikteta wenye uchungu na maendeleo ya nchi, vijana wapenda maendeleo kwa wote. Mambo ya urafiki na undugu katika uongozi ndio umechochea watu wenye dhamana ya uongozi kufanya ufisadi wakijua hakuna atakaye wawajibisha (mathalan, kwa vile baba yangu ni waziri mkuu hata nikifanya ufisadi atanilinda)

mama ninakuunga mkono na ni njia hii peke yake inayoweza kiliokoa taifa hili lililokufa au taifa la wafu na kwa kuanza mngeendelea na na huu mtindo wa kuwazomea na kuwatoa nishai hadharani mpaka wachanganyikiwe na mfanye hivi kwa yeyote anasemekana kwenda kinyume na maadili kama huyu mpya mwenye sura ya kufa s.ta najisikia vibaya sana when i remember about my nice country
 
Mbona mnajifichajificha humu...Wenye majina kama junior member wamezidi! 😱 Huu ni Ufisadi pia!

Haya yaliyobandikwa yamejaa. Huyu jamaa ni bepari anayejulikana, leo kusema ni Fisadi ni woga usioongopeka. Ni uwongo wa kogopeka, Ni Uwongo!😀

Checks and Balance!

Haya maovo yako kwenye sekta zote. Sio Barani mwetu peke yake, nasikia hata marekani na ulaya mtindo ndio huo huo, sasa hao wakuu wafanyeje kama wanaofanya checks and balances ni wadogo na wanahitaji uhuru wa uchumi?

Haya kweli ni mabweka tu! wuwu wuwuwu !!!! give me a Breki!!!
 
Basil Msongo
Daily News; Sunday,June 01, 2008 @00:01


Spika wa Bunge, Samuel Sitta amesema yeye si fisadi na hana hata senti moja nje ya nchi. Mbali na hilo, Sitta amesema ni vema sasa suala la mgombea binafsi likaamuriwa.

Pia alizungumzia serikali kuwasilisha mapendekezo ya Richmond pamoja na ya uchunguzi wa kashfa ya Akaunti ya Madeni ya Nje katika Benki Kuu (BoT) bungeni katika kikao kitakachoanza wiki moja ijayo.

Sitta aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipozungumza na watendaji wakuu wa vyombo vya habari, wahariri, waandishi waandamizi, na waandishi wa habari za Bunge ikiwa ni mwanzo wa utaratibu wake wa kuzungumza na wananchi kupitia vyombo vya habari kila mwezi.

Kiongozi huyo wa Bunge amesema Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali atatoa taarifa kuhusu tuhuma zinazomhusu yakiwamo matumizi mabaya ya fedha za umma. Alisema wabaya wake wamekosa hoja hivyo wameamua ‘kumgonga’ kwa kutoa tuhuma za kipuuzi za kijamii ikiwa ni pamoja na kuihusisha familia yake.

“Hainipi shida sana” alisema Sitta na kueleza kuwa mambo hayo ni sehemu ya maisha yake. Alisema kasi ya wabaya kumtuhumu imepungua baada ya kugundua kuwa yeye si fisadi na kwamba tuhuma kuwa anatumia Sh milioni mbili kwa ajili ya tiba yake kila mwezi ni upuuzi usio na kifani.

Sitta alisema anaamini yupo katika mstari mzuri katika kuliongoza Bunge na kwamba wabunge na wananchi katika jimbo lake la uchaguzi wanamuunga mkono. “Mimi sibadiliki hata kidogo…..kama tunavyoelewa katika siasa ukiwa unapika kwa kuni usiogope moshi,” alisema na kuongeza kuwa katika umri wake, amepita katika changamoto nyingi.

“Naamini hata wabunge wananiunga mkono,” alisema Spika wa Bunge na akatoa msimamo wake pia kuhusu masuala yanayogusa maslahi ya taifa ukiwamo uamuzi kuhusu kuwapo au kutokuwapo kwa mgombea binafsi, uchunguzi kuhusu wizi wa fedha za EPA na utekelezaji wa mapendekeo ya Bunge katika mkataba wa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond.

Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, alisema kuna haja ya kufikiwa kwa uamuzi wa mwisho kuhusu suala la mgombea binafsi kwa kuwa limeshajadiliwa kwa muda mrefu. ‘Tufike mwisho, tukubaliane au tusema haiwezekani,” alisema katika mkutano huo wa kwanza na vyombo vya habari ulioonyeshwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha serikali, TBC 1.

“Kama jambo limeamuriwa na majaji watatu, na bado hujaridhika, unaweza kukata rufaa likaamuriwa na majaji saba,” alisema Sitta akizungumzia suala hilo ambalo serikali imekata rufani Mahakama ya Rufaa kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu kuruhusu mgombea binafsi katika uchaguzi.

Kuhusu Richmond, alisema atashangaa kama serikali haitawasilisha taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya Bunge kuhusu mkataba huo uliozua utata na kusababisha kujiuzulu kwa mawaziri mawili pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, Februari mwaka huu.

Alisema pia anatarajia kuwa katika Mkutano wa 12 wa Bunge utakaoanza Juni 8, mwaka huu, serikali itawasilisha taarifa kuhusu maendeleo ya uchunguzi wa wizi wa fedha za umma kupitia EPA.

Spika Sitta alisema katika mkutano huo wa bajeti, atatoa uamuzi kuhusu kauli ya Mbunge Nazir Karamagi, kuwa uamuzi wa kuongeza mkataba wa Kitengo cha Makontena katika Bandari ya Dar es Salaam (TICTS) ulifanywa na Baraza la Mawaziri.

Alisema Karamagi amewasilisha ushahidi kwake, lakini isingekuwa busara kutoa maelezo ya suala hilo nje ya Bunge kwa kuwa suala hilo lilizungumzwa bungeni. Sitta alisema katika mkutano huo unaotarajiwa kumalizika Agosti 25, mwaka huu, Ofisi ya Bunge itaanza kuwadhibiti wabunge watoro wakiwamo wanaoingia kusaini asubuhi na kuondoka kisha wanarudi baadaye kuchukua posho.

Kwa mujibu wa Spika, miongoni mwa mipango yake hivi sasa ni kubadilisha jina la Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma kwa kuwa kwa sasa inahusika na mashirika yenye hisa zaidi ya asilimia 50 za serikali, lakini kuna mashirika mengine serikali ina hisa chini ya hizo.

Alisema atakapofanya mabadiliko hayo, kamati hiyo itaitwa Kamati ya Bunge ya Mitaji ya Umma. Spika pia alitetea azma ya wabunge kuongezewa mishahara akisema kuwa kiwango wanacholipwa kinajumuisha mahitaji yao yote zikiwamo gharama za usafiri na mishahara ya madereva.
 
Hata kama huna sent nje ya nchi lakini kama kiongozi ukipotoka kimaadili HUO ni UFISADI MKUBWA
 
Major
Huyu mshikaji hajatueleza kuhusu malipo yaliyofanywa kwa bi mdogo wake ya siku 50 kama night allowance wakati ule wa session ya bunge pale makao makuu ya nchi.
Hajatueleza kuhusu roli la maji linalopeleka maji daily pale upanga kwa bi mdogo wake mwingine kwa gharama za ofisi ya bunge.
Hizi ni hela nyingi,hizo milioni mbili za matibabu nia cha mtoto.
We are not judgemental, lakini katika hili la nyumba ndogo ,he can have as many as he wants, provided anazimaintain kwa pesa yake, lakini sio pesa yangu na yako major.
Kwa hilo tunaomba muongozo wake ......
 
Hata kama huna sent nje ya nchi lakini kama kiongozi ukipotoka kimaadili HUO ni UFISADI MKUBWA


Naona waandishi walitakiwa kumuuliza huyo mheshimiwa kama anajua maana ya UFISADI. Maana watu wengine wachekeshaji sana tu
 
Hata kama huna sent nje ya nchi lakini kama kiongozi ukipotoka kimaadili HUO ni UFISADI MKUBWA


Naona waandishi walitakiwa kumuuliza huyo mheshimiwa kama anajua maana ya UFISADI. Maana watu wengine wachekeshaji sana tu

unawajua waandishi wa bongo?? maswali mpaka watungiwe. wapo wachache wabunifu wa mijadala na viongozi....
 
Hivi katika viongozi na wastaafu wote waliotuhumiwa ufisadi kuna hata mmoja aliyejitokeza na kukiri "jamani ee mimi kweli fisadi"?
 
Bravo Mkodoleaji,
Huenda Sitta anadhani tafsiri ya ufisadi ni kuwa na mapesa mengi nje ya nchi tu..lakini kwa matendo yake anastahili kabisa kuitwa FISADI KIWEMBE...Na hao waandishi ubavu wa kumbana na maswali hawana??? au mambo ya vibahasha???? Teh!! teh!! Tehhhhhh!!!

Mkuu nasikia water bouser lilikuwa kimeo kama mesenja na barua ya bosi vile.Ni Kweli???...Asaalalee hawa wazee na vituko sana...
 
Wangejua tafsiri halisi ya ufisadi sijui kama kuna kigogo atasimama kutetea kuwa yeye si fisadi
 
Unajua tatizo la viongozi wa awamu ya nne wanafanya mambo kama vile wameingia kwenye uongozi awamu hii hii. Kumbe wengine tumeanza kuwakodolea siku nyingi sana wengine toka awamu ya Mwalimu ambapo mwalimu wa shule ya msingi aliweza kuwa mbunge mpaka sasa wameibuka kuwa mamilionea wa kutupwa. Akina Sitta walitumia kampeni chafu vile vile ili kumwondoa Msekwa na amekuwa akiona bunge kama nyumba yake. Si kwamba kwa kumsema Sitta nawatetea maadui zake lakini hawezi kuja kudai yeye ni msafi hapa wakati wenzie tumemkodolea toka miaka ya 80 alipoondoa shilingi kwenye wizara ya fedha kutokana na BoT kujiwekea hela nyingi kwa majengo yake. Wakati ule alikuwa my hero lakini alipungua ushawishi kwangu baada ya kumwona na yeye ni kama Msekwa tu kwenye kuliendesha bunge.
 
Hakuna jipya hapo. Hii imeshawahi kujadiliwa hapa JF huko nyuma.
 
Back
Top Bottom