Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Kitila,
FMES atakuambia ni ubepari. Nilikuwa Singapore a few years ago na wao pia wana nyumba kama tulizo nazo Oyster Bay. Nikamwuliza tax driver hizo ni nyumba za nani akasema ni za serikali zilijengwa na wakoloni lakini zinamilikiwa na serikali. Sasa hii ya ubepari na serikali kutomiliki nyumba ni kasumba iliyo myopic, kwa mtazamo wangu.
 
- Mkuu Jasusi, heshima mbele sana unajua sana mkuu kwamba ushauri wa kuuza nyumba za serikali haukuwa wetu, ni wa tabia za kibepari tunazofuata ikiwa ni pamoja na kuuza mashirika yetu kwa mara ya kwanza katika historia ya taifa letu toka tuwe huru sasa mashirika ya siagara na bia yanaingiza faida na kuliingizia taifa dola millioni nyingi sana through kodi, yaani baada ya kuuzwa,

- Now look at this, eti hizo nyumba zinamilikwa na nani unasema ni tatizo la wapangiwaji? Are you serious mkuu au?

Respect.

Kamanda FMEs!
FMES,
Nimeuliza nyumba inamilikiwa na nani kwa sababu nimekuwa cynical siku hizi kutokana na ufisadi uliokithiri Bongo. Isije ikawa ni deal iliyotengenezwa kuwawezesha wajanja wanyonye nchi. Kwa dola elfu kumi kwa mwezi hata Manhattan utapata pent house nzuri tu.
 
Tatizo siyo spika kukaa kwenye nyumba ya mabilioni.Tatizo ni mifumo na taratibu zilizomo kwenye mambo mengi ya kiutawala katika nchi yetu na zile maskini hasa barani Afrika.Tutaweza kukesha hapa tukiuliza maswali na majibu tusiwe nayo.

Kwa utaratibu au mfumo uliopo sasa hivi, wa kuweka marupurupu ya kutisha kwa watawala na viongozi katika nchi maskini kama yetu, hata ingekuwa wewe msomaji huenda ungefurahia hiyo hali na kuona ni stahili yako.Lets be honest!

Ni pale tu watakapoweza kubadili huo mfumo na kuwafanya viongozi kuwa na mtizamo tofauti kuhusu dhima ya uongozi - kwamba kiongozi anatakiwa kuwa mfano na mtumwa wa wale anaowaongoza ndipo tutaweza kuwa na mjadala productive.
Cha kufanya ni kuhakikisha tunawapata viongozi waadilifu, wasiokuwa wabinafsi, waliotosheka n.k. Je tutawapata wapi ilhali watu wengi wanaingia siasa kwa sababu za kibinafsi zaidi?Ni kwanini wastaafu wengi sasa hivi wanakimbilia ubunge?
 
Not as simple as you would want us to believe. Kwamba anapangiwa na ameukuta huo utaratibu sio hoja kwa sababu kama angetaka angebadili, uwezo huo anao. Aliweza kubadilisha kanuni za bunge atashindwa vipi kubadilisha utaratibu wa ovyo wa kukufuru matumizi ya walipa kodi maskini?

Hoja iliyopo hapa ni je ni sawa kwa kiongozi maskini kama Tanzania, ambayo zaidi ya 50% ya watu wake wanaishi chini ya sh. 1,300 kwa siku (chini ya sh. 39,000 kwa mwezi na chini ya sh. 500,000 kwa mwaka), kuishi katika nyumba ambayo pango lake ni zaidi ya sh.9,000,000 kwa mwezi (zaidi ya sh. 108,000,000 kwa mwaka) na kutembelea gari la zaidi ya sh 300,000,000 na kununua fanicha za zaidi ya sh 200,000,000? Inawezekanaje spika wa bunge la wananchi la nchi ambayo watoto wa shule wanakaa chini kwa kukosa madawati ya sh. 200,000 akae katika nyumba yenye fanicha za thamani ya sh 200,000,000 ambazo zinalipwa kwa hela ya walipa kodi maskini wasio na uwezo wa kula mara tatu kwa siku? Kwani angetembelea gari la sh. 50,000,000 angepungukiwa vipi na hiyo unayoita security? Hivi akilala kwenye nyumba yenye fanicha za sh 5,000,000 anapungukiwa vipi na hiyo security? Yeye kulala kwenye nyumba ya kodi ya sh. 1,500,000 kwa mwezi inamfanya vipi asiwe spika mahiri? Yaani yote haya wewe hayakusumbui isipokuwa huo uspika na hizo sheria zilizoweka huo utaratibu wa aibu?

Sasa kama kuuliza haya maswali ni 'ignorance' acha mimi niwe kwenye hilo kundi, na kama kuuliza haya maswali yatatufanya wananchi wasituchague, acha tuendelea kuwa chama cha upinzani!

- Mkulu mawazo mazito lakini siwezi kusumbuliwa na matokea ya sheria iliyopitishwa na viongozi wangu wa CCM kwa kushirikiana na Upinzani, kama vile ambavyo wabunge wetu wa Upinzani wasivyosumbuliwa na malipo ya ajabu wanayolipwa na kodi zetu wananchi, yetu katika taifa ni matatizo ya uongozi mbovu, as long as Spika anaishi within the budget ya ofisi yake sioni tatizo mkuu na wala sisumbuliwi,

- U-Spika huwa unagombewa na viongozi wa pande zote mbili ndani ya bunge sijawahi kusikia wabunge wa Upinzani wakilia kwamba malipo kuanzia yao yapunguzwe kwanza, sijasikia wakilia kwamba hela wanazopewa za ruzuku zipunguzwe, hela wananzopewa za uchaguzi zipunguzwe, mnatumia mpaka helikopta kwenye uchaguzi so much for good soldiers wa kubana matumizi ya serikali,

Respect.

Kamanda FMEs!
 
hata ingekuwa wewe msomaji huenda ungefurahia hiyo hali na kuona ni stahili yako.Lets be honest!

Hapana sio wote ambao tungefurahia na kuiona hali hiyo kuwa ni stahili. Baba wa taifa wasn't balling like these goons here...these goons are balling way out of control....

Mimi dhamiri yangu itanishitaki nikifanya hivyo huku najua kuna akina mama wajawazito wanalala chini kwenye sakafu. I just can't do it.
 
- Mkulu mawazo mazito lakini siwezi kusumbuliwa na matokea ya sheria iliyopitishwa na viongozi wangu wa CCM kwa kushirikiana na Upinzani, kama vile ambavyo wabunge wetu wa Upinzani wasivyosumbuliwa na malipo ya ajabu wanayolipwa na kodi zetu wananchi, yetu katika taifa ni matatizo ya uongozi mbovu, as long as Spika anaishi within the budget ya ofisi yake sioni tatizo mkuu na wala sisumbuliwi,

- U-Spika huwa unagombewa na viongozi wa pande zote mbili ndani ya bunge sijawahi kusikia wabunge wa Upinzani wakilia kwamba malipo kuanzia yao yapunguzwe kwanza, sijasikia wakilia kwamba hela wanazopewa za ruzuku zipunguzwe, hela wananzopewa za uchaguzi zipunguzwe, mnatumia mpaka helikopta kwenye uchaguzi so much for good soldiers wa kubana matumizi ya serikali,

Respect.

Kamanda FMEs!
FMES,
Slaa kishawaudhi wabunge wenzake wa CCM kwa kusema kuwa malipo yao yapunguzwe. Mara ya mwisho nilipoangalia Slaa alikuwa mpinzani.
 
FMES,
Slaa kishawaudhi wabunge wenzake wa CCM kwa kusema kuwa malipo yao yapunguzwe. Mara ya mwisho nilipoangalia Slaa alikuwa mpinzani.

Mkuu Rais wangu Dr. Slaa unasema aliacha kuchukua hizo hela zote siku hizi au? Hana lile ngingi tena?

Respect.

FMeS!
 
Hapana sio wote ambao tungefurahia na kuiona hali hiyo kuwa ni stahili. Baba wa taifa wasn't balling like these goons here...these goons are balling way out of control....

Mimi dhamiri yangu itanishitaki nikifanya hivyo huku najua kuna akina mama wajawazito wanalala chini kwenye sakafu. I just can't do it.

Huenda kuna wachache wangeona aibu. Lakini wengi wangefurahia... na hawa ndio wale wanaokimbilia siasa baada ya kutumikia taifa hadi kustaafu.Mwenzangu na mie kuku mgeni asiye na Godfather wa kuwavuta kamba na kuwashika mkono... ukijaribu tu...utatupiliwa mbali na hata kuchafuliwa jina lako hata kama una nia ya kweli kushiriki uongozi.Maadam tunawapa kura na kuwapa dhamana, tutaishia kushangaa kama tunavyoshangaa nyumba ya spika sasa hivi.
 
Ni lazima tutambue kitu kimoja , wakati nyumba za serikali zinauzwa Spika Sitta alikuwa ni mbunge. Kwa jinsi ninavyojua mimi , nyumba zille ziliuzwa baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kutoa idhini. Kwa hiyo walijua ya kuwa Nyumba ya Spika inauzwa, ingawa vyama vya upinzani vilipinga wao waliamua kuuza. The point I am trying to make is these people knew what they were doing as well as consequence . If they really care about hadhi ya spika, they should have thought about it then .

Ni lazima pia tutambue ya kuwa , sio kila kitu kisicho sawa lazima kiwe stipulated na katiba ! Mfano , jee bunge leo likiamua kununua Yatch 10 ambazo zitagharimu serikali $ 500 million, jee tutasema bunge lina haki ya kufanya hivyo kwa sababu sheria inaruhusu Bunge kushughulikia masuala ya approppiation. Mimi nadhani huu utakuwa ni mtazamo shallow sana. Pili tunapozungumzia masuala ya hadhi, mbona hatuzungumzii kulinda hadhi ya viongozi wetu kwenye barabara wanazotumia, airport wanazotumia ...Mimi nadhani kutokana na hadhi yao hawa viongozi wanahitaji barabara ambazo zinareflect hadhi zao na airport pia zenye sifa hizo. Kwa hiyo tuwajengee barabara, mahospitali na services nyingine zitakazolinda heshima zao.

Mimi nalipinga hili jambo kwani kwa kufanya hivi tunaset precedent moja mbaya sana, vipi kesho kama mtu mwingine atachukua nafasi na hiyo na kuamua kutumia sheria hiyo hiyo kukodisha nyumba yenye thamani mara kumi ya hiyo , je tutaema sheria inamlinda ? and where are we going to draw a line?
 
Hapa tunazungushana maneno tu. Tunajaribu kufanya ionekane kuwa hili la Spika ndilo limesababisha hali mbaya ya maisha ya wananchi wetu. Tunataka (kwa makosa) kubebesha mzigo wa lawama wa matatizo ya wananchi wetu kwenye mgongo wa nyumba ya Spika wa Jamhuri ya Muungano. Kwamba madawati hayatoshi sababu ni nyumba ya spika, n.k

Sasa mimi naomba wale ambao wanaona kuwa this is extravagant watupe angalau mchanganuo wao wa kile anachostahili Spika. Lets assume siyo mtu anaitwa Samuel Sitta.


a. Mshahara wa Spika uwe kiasi gani kwa mwezi?

b. Apewe gari/magari mangapi na ya aina gani?

c. Nyumba yake kama Spika iwe na thamani ya kiasi gani na iwe na ukubwa gani? na amenities gani?

d. Kama ni ya kukodi, iwe kati ya kiasi gani na maeneo gani?

e. Je apewe ulinzi wa nyumba na binafsi na wa idadi gani ya walinzi?


f. Je awe na bima ya afya inayogharimiwa na serikali au la na yenye kiasi gani?

g. Je akisafiri kwenda nje kikazi safari zake zisidi kiasi gani? Je aende na msaidizi yeyote?

La kuzingatia katika majibu yenu, naomba mhakikishe kuwa kitu chochote mnachompatia hakizidi hali ya maisha ya Mtanzania wa kawaida.
 
Mzuvendi,
Once again you are right. But according to FMES our spika deserves an expensive house because of security reasons while it is the same CCM government that sold our taxpayers houses which were already paid for and had adequate security arrangements to accomodate ministers and the house speaker. And by the way who are they renting the house from?

Jasusi:

What I know is in many countries top government officials live in government owned properties. For example, PM minister of Britain lives at 10 downing street. Next to him lives the Chancellor of the Exchequer at 11 Downing Street. As a matter of fact the speaker there live in his official residence.

For God sake, i don't know what kind of security our leaders need today. I remember in early 90 I saw Adam Sapi working without a single bodyguard.
 
Hapa tunazungushana maneno tu. Tunajaribu kufanya ionekane kuwa hili la Spika ndilo limesababisha hali mbaya ya maisha ya wananchi wetu. Tunataka (kwa makosa) kubebesha mzigo wa lawama wa matatizo ya wananchi wetu kwenye mgongo wa nyumba ya Spika wa Jamhuri ya Muungano. Kwamba madawati hayatoshi sababu ni nyumba ya spika, n.k


Hakuna mtu aliyesema ya kuwa Nyumba ya spika ndio imefanya watu wawe maskini, kusema ukweli huku ni kuwatukana wale wanaopinga matumizi machafu ya serikali. Tunachopinga hapa ni matumizi mabaya ambayo hayaendani na uchumi wa nchi yetu. Ni lazima mtambue ya kuwa hatuwezi kuafford kuspend nusu bilioni kwa mwaka kwa ajili kuhakikisha Spika anaishi aisha ya kifahari wakati huo huo 40% ya budget is being financed by donors. Tukiendelea na hii tabia ya watu wachache kujiona miungu watu tutaifilisi nchi. Mimi siku zote najuliza hizi hela zinatoka wapi? It seems like these crooks are just printing money; no wonder inflation inakua kwa kasi ya ajabu !
 
Hapa tunazungushana maneno tu. Tunajaribu kufanya ionekane kuwa hili la Spika ndilo limesababisha hali mbaya ya maisha ya wananchi wetu. Tunataka (kwa makosa) kubebesha mzigo wa lawama wa matatizo ya wananchi wetu kwenye mgongo wa nyumba ya Spika wa Jamhuri ya Muungano. Kwamba madawati hayatoshi sababu ni nyumba ya spika, n.k Sasa mimi naomba wale ambao wanaona kuwa this is extravagant watupe angalau mchanganuo wao wa kile anachostahili Spika. Lets assume siyo mtu anaitwa Samuel Sitta.


a. Mshahara wa Spika uwe kiasi gani kwa mwezi?

b. Apewe gari/magari mangapi na ya aina gani?

c. Nyumba yake kama Spika iwe na thamani ya kiasi gani na iwe na ukubwa gani? na amenities gani?

d. Kama ni ya kukodi, iwe kati ya kiasi gani na maeneo gani?

e. Je apewe ulinzi wa nyumba na binafsi na wa idadi gani ya walinzi?


f. Je awe na bima ya afya inayogharimiwa na serikali au la na yenye kiasi gani?

g. Je akisafiri kwenda nje kikazi safari zake zisidi kiasi gani? Je aende na msaidizi yeyote?

La kuzingatia katika majibu yenu, naomba mhakikishe kuwa kitu chochote mnachompatia hakizidi hali ya maisha ya Mtanzania wa kawaida.


Mkuu,

Naomba kuongeza, na kuuliza...Kwa mantiki uliyotumia mwanakijiji

Mawaziri je? A to G
 
- Mkuu ya serikali kumiliki nyumba yamepitwa na wakati sasa hayapo tena, hizi hela lazima ziwe injected kwenye uchumi wetu kupitia mikononi mwa wananchi na ndicho kinachofanyika kufuatia ushauri wa World Bank, ndio maana pamoja na mapungufu yake yote Mkapa bado uchumi ulikuwa ni one his of strength,


- Huko upande wa pili wa glass mnashindwa kuelewa kwamba gaharama za namna ya kuishi kwa viongozi wetu wa juu sio uamuzi wao, ni bunge letu ndilo linaloamua, sasa kumlaumu Spika ni kutomtendea haki kabisa! Sikatai huenda Spika ana madhambi yake mengine lakini hili la nyumba kwa maoni yangu hapana mkuu hakuna enough facts za kumhukumu.

Respect.

Kamanda FMEs!


Yes, I don't expect a messanger or a drive to live in a goverment owned property but top 100 officials I do.

You say it's not their decision, then whose this decision is?
 
Hakuna mtu aliyesema ya kuwa Nyumba ya spika ndio imefanya watu wawe maskini, kusema ukweli huku ni kuwatukana wale wanaopinga matumizi machafu ya serikali.

Matumizi machafu ya serikali kumgharimia Spika? Ni kiasi gani cha matumizi ya serikali kwa spika tunaweza kuyakubali kuwa ni masafi?

Tusema kuwa angekuwa anapanga nyumba kwa dola 5000 kwa mwezi na kuendesha corolla au nissan altima tutasema ni masafi? Vipi kama tungeamua kumjengea nyumba sehemu fulani katikati mjini kwenye mitaa yetu walalahoi, itamleta karibu zaidi na wananchi siyo?


Tunachopinga hapa ni matumizi mabaya ambayo hayaendani na uchumi wa nchi yetu.

Matumizi mabaya yapo lakini hadi hivi sasa sijaona hayo ya Spika kuingizwa katika ubaya huo. Matumizi mabaya ni yale ambayo hayajulikani kiasi chake, yanakwenda wapi, na yanatumiwa na nani. Matumizi mabaya ni ya mtu anayetumia fedha ya serikali kwa uamuzi wake mwenyewe kujinufaisha. Hadi hivi sasa sijaona mahali ambapo panasema Spika ndiye amejitengea fedha hiyo na kujilipa yeye mwenyewe.

Ubaya wa matumizi ya serikali kwa Spika ni upi hasa?
Ni lazima mtambue ya kuwa hatuwezi kuafford kuspend nusu bilioni kwa mwaka kwa ajili kuhakikisha Spika anaishi aisha ya kifahari

Vipi kuhusu Waziri Mkuu, Makamu wa Rais, Rais mwenyewe, Jaji Mkuu, Mkuu wa Majeshi, Mkuu wa POlisi n.k kwanini ni hili la Spika tu ndio linaleta matatizo? Kama kweli tunataka kupunguza matumizi na kuleta nidhamu kwanini tusililie kile tunacholilia sisi wengine nacho ni kusitisha misaada ya kigeni ili hawa viongozi wajifunze kutumia kidogo tulichonavyo kwa umakini?

wakati huo huo 40% ya budget is being financed by donors. Mimi siku zote najuliza hizi hela zinatoka wapi? No wonder inflation inakua kwa kasi ya ajabu !

Hivi unafikiri tatizo la Tanzania ni fedha? Yaani, unaamini kuwa umaskini wetu sisi unasababishwa na ukosefu wafedha. Mnachozungumzia kwenye Spika ni dalili tu ya tatizo lenyewe.
 
Mkuu,

Naomba kuongeza, na kuuliza...Kwa mantiki uliyotumia mwanakijiji

Mawaziri je? A to G

ndiyo hivyo.. mtu atusaidie tu.. kwa sababu hofu yangu ni kuwa hili la Spika lina zaidi ya suala la matumizi. Kuna zaidi ya malipo ya dola 10,000 kwa mwezi au magari. I really want to know what is this about.. maana haya mapambano ya fronts nyingi kweli.
 
Hapa tunazungushana maneno tu. Tunajaribu kufanya ionekane kuwa hili la Spika ndilo limesababisha hali mbaya ya maisha ya wananchi wetu. Tunataka (kwa makosa) kubebesha mzigo wa lawama wa matatizo ya wananchi wetu kwenye mgongo wa nyumba ya Spika wa Jamhuri ya Muungano. Kwamba madawati hayatoshi sababu ni nyumba ya spika, n.k

Mwanakijiji,

Kuna tofauti kubwa kati ya kusema

1. Matumizi ya Spika yamesababisha umasikini wetu,
2. Culture ya matumizi kama ya Spika yanatudumaza katika umaskini wetu,
3. Matumizi kama ya speaker yako insensitive kuhusu umasikini wetu

La kwanza haliwezi kuwa kweli kwa sababu, ingawa matumizi ni extravagant, ukiyaweka katika national perspective si makubwa kiasi cha ku affect uchumi wa nchi nzima.

Hili la pili na lile la tatu yana mantiki. Spika huyu hapa amekuwa kama "poster boy" wa hii graft overspending, ukiangalia karibu kila sehemu matumizi mabaya ya fedha zetu chache ni kama mashindano, na kila mtu anataka ku qualify kwenda kwenye Olympics.Kwa vile hizi resources ziko limited, the more we take away from our coffers to finance these lavishly regal lifestyles, the more we are taking away from teachers salaries, and underfunded rural dispensaries etc etc.Kwa hiyo Spika anavuma lakini wako wengine wengi, na tutaanza na yeyote ambaye data zake ziatapatikana na kuonekana kuwa ana matumizi yaliyo outrageous. Mimi binafsi sijali innuendos za Rostam vs Sitta wala nani vs nani, as far as I am concerned wote wachafu tu na vita vya panzi furaha ya kunguru, wakianikana na kuandamana ndivyo tutakavyojua maovu yao zaidi na zaidi.kwa hiyo tofauti na wewe, sichelei kumuumbua fisadi mmoja eti kwa sababu kumuumbua ni sehemu ya vita kati yake na fisadi mwingine, ningefurahi na kambi ya Sitta nayo imwage data tuwaumbue wote, kama wanavyosema watoto wa mjini "ukimwaga ugali namwaga mboga".

Kuna mwaka alikuja Waziri Mkuu wa Sri Lanka ziarani Tanzania, akashuka kwenye ndege ya commercial airlines, tena alipanda economy, watu wakashangaa Prime Minister kapanda economy, lakini yeye akaeleza nchi yangu masikini sana na mimi nasevu hela nyingi sana kwa mwaka zinazotumika kwenye maendeleo mengine simply kwa kupanda economy.Hapo hata kama unaenda kuomba msaada dodnor country wanakuelewa, sio unaingia na GulfStream za kuwashinda wao, wananza kujiuliza huyu masikini kweli? Au wakija kuongea na Spika kwake wanaona vile vi apartment vyao kama matusi kulinganisha na makasri yetu (mawaziri wa nchi za ki Scandinavia sishangai kusikia wanakaa kwenye vi apartment, na wao ndio donors!).Kwa hiyo Sitta is just an anecdote to punctuate this story.But we have to start somewhere.Na sijui the underlying innuendos zikoje, lakini the simple mathematics za GDP per capita ya mtanzania haziruhusu hii extravagant profligacy.

Kwa hiyo ndiyo maana nikasema huko juu kwamba Spika Sitta yuko responsible twice, kwanza kama kiongozi wa institution ya bunge yeye alitakiwa kuwa mfano wa kupiga vita extravagancy hii katika institutional level.

Lakini pia kama Samuel Sitta alitakiwa kuwa na dhamiri itakayomsuta, akiangalia wakulima wa Urambo na maisha yao na yeye anavyoishi kisultani, ilitakiwa imuume kiasi cha kukataa huu uungu mtu usio na mpaka.Ndiyo maana nikasema point ya tatu hapo juu, matumizi kama ya Speaker yako insensitive kwa umasikini wetu.Anakuwa kama hajali umasikini wetu anasema kila mtu kivyake.This is simply not a good quality of leadership for someone leading in a poor country, no empathy at all, no integrity, we do not need such greedy narcissist.

Kuhusu hizo breakdown za perks zao ingefaa wote wapigiwe hesabu za kufuatana na GDP per capita ya mtanzania, na kuwekewa viwango kwamba wakitaka perks zao zipande, wapandishe GDP Per capita (ambayo sasa hivi ipo about 1,300 by 2007 estimates from CIA Worldbook), labda ingeweza kuwapa incentive ya kufanya kweli.
 
Ni lazima tutambue kitu kimoja , wakati nyumba za serikali zinauzwa Spika Sitta alikuwa ni mbunge. Kwa jinsi ninavyojua mimi , nyumba zille ziliuzwa baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kutoa idhini.

Kuweka taarifa sawasawa, Sitta hakuwa Mbunge kati ya 1995 - 2005. Hivyo, wakati nyumba zinauzwa hakuwa Mbunge.

Pili, kuuzwa kwa nyumba hakukuidhinishwa na Bunge na ndio maana kuna azimio la Bunge la kutaka nyumba zirudishwe.
 
..
Kuhusu hizo breakdown za perks zao ingefaa wote wapigiwe hesabu za kufuatana na GDP per capita ya mtanzania, na kuwekewa viwango kwamba wakitaka perks zao zipande, wapandishe GDP Per capita (ambayo sasa hivi ipo about 1,300 by 2007 estimates from CIA Worldbook), labda ingeweza kuwapa incentive ya kufanya kweli.

sawa.. given

Unajua GDP ya Tanzania
Unajua hali mbaya ya maisha ya Watanzania
Unajua matatizo yetu ya kiuchumi n.k

Sasa tuseme unatoa pendekezo la kuonesha kuwa Spika hawi extravagant. Ni kipi kiwe anastahili kama spika na ni kipi kiwe ni pecks ambazo si za lazima, assuming kuwa hawajafanya lolote kuinua GDP?


a. Mshahara wa Spika uwe kiasi gani kwa mwezi?

b. Apewe gari/magari mangapi na ya aina gani?

c. Nyumba yake kama Spika iwe na thamani ya kiasi gani na iwe na ukubwa gani? na amenities gani?

d. Kama ni ya kukodi, iwe kati ya kiasi gani na maeneo gani?

e. Je apewe ulinzi wa nyumba na binafsi na wa idadi gani ya walinzi?


f. Je awe na bima ya afya inayogharimiwa na serikali au la na yenye kiasi gani?

g. Je akisafiri kwenda nje kikazi safari zake zisidi kiasi gani? Je aende na msaidizi yeyote?

La kuzingatia katika majibu yenu, naomba mhakikishe kuwa kitu chochote mnachompatia hakizidi hali ya maisha ya Mtanzania wa kawaida.
 
Back
Top Bottom