Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Turudi kwenye hoja, malipo ya nyumba ile yanaendana na soko? Taratibu zilifuatwa? Lakini kama lengo lenu ni kumsulubu Sitta, mnaweza kuendelea na wala hamtapata suluhisho maana kesho akiwa Spika Slaa au Hamad Rashid au Marmo nk, atalipiwa nyumba hivyo hivyo kama hatutamaliza tatizo la Nyumba kwa viongozi wa Kikatiba.QUOTE]

this is materially FACT!and indeed we need to go through this plan
 
Duh! sasa kama hujui tofauti kati ya Spika na Naibu Waziri.. tutakuwa na mjadala mrefu kweli.

Nilichokuwa najaribu kuzungumzia ni Nyumba ya Spika , na sio wadhifa wake.


NO it does not! He is not the King of the Parliament!

Hivi kweli unaijua nguvu ya Spika katika Bunge la Jamhuri ?
 
Nashukuru sana kwa majibu yako , ambayo kiasi fulani yamenihuzunisha sana ! Kwa hiyo kamati ya bunge iliona ni kuzalilishwa kwa Spika kupangiwa nyumba hapo Kijitonyama ! Hivi watu wakifika hapo Bungeni mbona wanajichukulia too serious, Spika ana tofauti gani na naibu waziri. Na bunge litadhalilishwa vipi kwa yeye kuishi kwenye hizo nyumba. Mimi naona tatizo ni low self esteem !




Tunamlaumu Spika kwa sababu when it comes to our parliament issues, THE BUCK STOPS WITH HIM. Mwanasiasa yoyote makini angependa kujua ni kiasi gani kimetumika katika kulipia gharama mbali mbali zinazomhusu yeye.

Usihuzunike kwani hapa tunajadiliana na mjadala hata siku moja usi assume kuwa kila mtu atakuwa anakubaliana na hoja zako. Huzunika na hoja ninazotoa na usihuzunike na mimi kama Zitto.

Spika ni mhimili wa Dola. Kuna mihimili mitatu. Spika anafanya maamuzi mazito sana Bungeni na wakati mwingine maamuzi yaliyo kinyume na mhimili mmoja, hasa ule wa Utendaji ambao unaundwa na Waziri Mkuu na Mawaziri na Manaibu wao.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hawezi kukaa na Manaibu Mawaziri. Spika wa Bunge anapaswa kukaa katika makazi rasmi yaa Spika. Nimesema, makazi hayo rasmi yaliuzwa na hivyo ikabidi apangiwe nyumba kwa muda mpaka hapo makazi mapya yatakapopatikana ambayo Spika yeyote atakayekuja atakaa (yasiuzwe tena).

Hayo makazi ndiyo kodi yake hiyo. Je kodi hiyo inaendana na bei za soko?

Hakuna mahusiano kati ya makazi ya Spika na Mikopo ya wanafunzi kwani kwa vyovyote vile ni lazima mikopo ilipwe na ni lazima Spika akae katika makazi rasmi kwa mujibu wa dhamana aliyonayo.
 
Nashukuru mheshmiwa Kabwe na MKJJ kwa kuwafunua watu kutoka ndani ya tunnel vision. Maana mjadala huu umekua mrefu hivi kwa watu kuangalia mtu badala ya mfumo.

Mara spika aache kupambana na ufisadi, mara msaliti,...kaazi kwelikweli.
 
sorry.. mapendekezo yako yote yanamfanya asifanane na Mtanzania wa kawaida. Mtu mwingine ataona ni kumtengenezea maisha ya anasa. Labda umodify ili yote utakayoyapendekeza yasimfanye aonekane ana maisha ya kifahari. Kutumia dola 10,000 kwa safari watu wachache sana wanaweza kutumia hizo.

Halafu dola 120 kwa mwezi ni chini ya kiwango anacholipwa Polisi, daktari, n.k sasa siyo tu umemfananisha na watu wa kawaida, bali umemshusha mno. Na kama ana watoto wadogo au walio shule atamudu kweli hata kama ana wito? Siyo kwamba tutamtengenezea mazingira ya kutafuta "fedha ya ziada pembeni"..

Unapoangalia "Mtanzania wa kawaida" usiangalie hao watumishi wa umma tu, anagalia na wakulima wa vijijini huko wengine wana GDP per capita ya $ 600, bei ya laptop kwa wenzetu.

Kimsingi wabunge na huyu spika ni watumishi wa umma, sasa sioni ajabu mishahara ya mabosi (wananchi) ikiwa mikubwa kuliko ya watumishi wao (wabunge). Au tunavyosema kila siku kwamba hawa ni public servants tunakuwa tunapiga lip servuice tu? Iweje wao wawe "servants" wetu halafu wawe na mishaharaminono na perks nyingine nyingi?

Hilo la kwenda nje na budget ya 10,000 you have to consider anaenda nchi ya watu na entourage ya watu watatu, tuiketi peke yake zitakata nusu ya hiyo, na hiyo ni kwa panga la wote watatu, kama safari zina tija zitajilipia zenyewe.

Breakdown revolutionary hiyo.Mi nakwambia ukiweka mambo hivi miaka 10 tu unaona GDP inapanda.

Na kuhusu ku justify ubadhirifu eti kwa sababu wakilipwa kidogo tutawapa vishawishi hii ni hogwash, mbona sasa wanalipwa perks zote hizi na bado tamaa iko pale pale? Tamaa ni hulka, kama mtu ana tamaa atakuwa na tamaa tu, mpaka mumbane, hata mkimzidishia mshahara kiasi gani anaweza kuendeleza tamaa tu, na mara nyingine kuzidisha anasa ndiko kunakozidisha tamaa, kapanda S 600 sasa atataka Maybach, kapanda Maybach sasa atataka Maybach tatu na ving'ora juu.

Piga palanja la uhakika hapa, peleka hela kwenye shughuli za maendeleo huko.Kila mtu ale rhumba kali, watajua kuleta maendeleo within 10 years.
 
Nashukuru mheshmiwa Kabwe na MKJJ kwa kuwafunua watu kutoka ndani ya telescopic vision. Maana mjadala huu umekua mrefu hivi kwa watu kuangalia mtu badala ya mfumo.

Mara spika aache kupambana na ufisadi, mara msaliti,...kaazi kwelikweli.


Hili ndio tatizo letu kubwa sana. Tunahukumu haraka sana! Haki (justice) inataka tuhukumu baada ya kuwa na taarifa zote muhimu. JF haipaswi kuonea wala kupendelea, bali kusimamia ukweli na ukweli mtupu!

Hata hivyo hukumu hizi zinatokana na hasira ambazo watu wanazo kuhusu hali ya nchi yetu na ufisadi uliokithiri. Ni mchakato muhimu kupitia (yaani kuwa na hasira). Ninaamini baadae tutakuwa tunahukumu kwa haki.
 
Usihuzunike kwani hapa tunajadiliana na mjadala hata siku moja usi assume kuwa kila mtu atakuwa anakubaliana na hoja zako. Huzunika na hoja ninazotoa na usihuzunike na mimi kama Zitto.

Spika ni mhimili wa Dola. Kuna mihimili mitatu. Spika anafanya maamuzi mazito sana Bungeni na wakati mwingine maamuzi yaliyo kinyume na mhimili mmoja, hasa ule wa Utendaji ambao unaundwa na Waziri Mkuu na Mawaziri na Manaibu wao.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hawezi kukaa na Manaibu Mawaziri. Spika wa Bunge anapaswa kukaa katika makazi rasmi yaa Spika. Nimesema, makazi hayo rasmi yaliuzwa na hivyo ikabidi apangiwe nyumba kwa muda mpaka hapo makazi mapya yatakapopatikana ambayo Spika yeyote atakayekuja atakaa (yasiuzwe tena).

Hayo makazi ndiyo kodi yake hiyo. Je kodi hiyo inaendana na bei za soko?

Hakuna mahusiano kati ya makazi ya Spika na Mikopo ya wanafunzi kwani kwa vyovyote vile ni lazima mikopo ilipwe na ni lazima Spika akae katika makazi rasmi kwa mujibu wa dhamana aliyonayo.

Zitto,

Tatizo kubwa hapa ni kwamba hiyo kodi inayolipwa haiendani na bei ya soko hata kidogo. Tanzania ni nchi masikini sana hivyo ingekuwa ni vyema na busara hili suala likaangaliwa upya. Hiyo mishahara ya wakuu uliowataja nayo pia ni katika kuumizana bila sababu ya msingi. Wanalipana mishahara kwa kuangalia mtu wa cheo chake wa nchi nyingine analipwaje, hapa haileti maana kwani uchumi, matatizo na malengo ya nchi hazifanani.
 
Hili ndio tatizo letu kubwa sana. Tunahukumu haraka sana! Haki (justice) inataka tuhukumu baada ya kuwa na taarifa zote muhimu. JF haipaswi kuonea wala kupendelea, bali kusimamia ukweli na ukweli mtupu!

Hata hivyo hukumu hizi zinatokana na hasira ambazo watu wanazo kuhusu hali ya nchi yetu na ufisadi uliokithiri. Ni mchakato muhimu kupitia (yaani kuwa na hasira). Ninaamini baadae tutakuwa tunahukumu kwa haki.

Nimeongelea juu ya udhaifu wa Spika katika level zote mbili, kama an institutional leader, na pia kama alivyoshindwa personally, ameshindwa kuwa na empathy ya kuanzisha movement against graft overspending wakati analo rungu la kuinfluence muelekeo huo.

Lakini pia nikapoint out hili kama a systemic issue, na kwamba Sitta ni poster boy, wengine wamo, kwa hiyo tunapomkemea Sitta, tunatumia mfano wake tu lakini tunaongelea kulaani mfumo mzima unaoruhusu Sitta kuwa na perks hizi za ajabu.

Kwa hiyo there is no excusing Sitta.

Kama mnasema Sitta si peke yake nitaelewa, na nitaomba majina mengine na details nyingine tuwachabange wote hapa.

Lakini kwa Spika wa Tanzania kuchukua $ 8000 kwa mwezi kwa nyumba tu ni ufisadi wa hali ya juu.

Ex president Bill Clinton wa USA anakaa Chappaqua, Westchester County NY (one of the wealthiest and most expensive places in the US), analipwa posho ya $ 10,000 kwa mwezi na serikali ya Marekani, Marekani!

Sisi tuna uchumi gani wa kusustain ulimbwende usio tija kama huu? Is this really proportional?
 
Usihuzunike kwani hapa tunajadiliana na mjadala hata siku moja usi assume kuwa kila mtu atakuwa anakubaliana na hoja zako. Huzunika na hoja ninazotoa na usihuzunike na mimi kama Zitto.

Sijasema ya kuwa nimehuzunika na wewe kama Zitto, bali nimehuzunika na hoja ulizozitoa zaidi nikizingatia ya kuwa wewe ni Mbunge wa jamhuri wa muungano. Umesema ya kuwa kununua fenicha za hizo gharama ni part ya commonwealth tradition , kwa hiyo inaonekana tunafanya vitu kwa sababu ni part ya tradition bila ya kujali uwezo wetu. Kwa hiyo inaonyesha hatuna maamuzi yetu wenyewe , ni kama mchezo wa monkey see monkey do.

Ni lazima nyie wabunge pamoja na Spika mtambue ya kuwa cheo mlichopewa ni dhamana , na Tanzania (Tanganyika, zanzibar) ilikuwepo kabla yenu na itakuwepo even after y'all have long gone! Nyerere, alitumikia taifa kwa miaka zaidi ya ishirini lakini alipostaafu serikali ilibidi imjengee nyumba . Nadhani kwa standard za bunge letu la leo hakuilinda hadhi yake vizuri ! The whole thing is ridiculous , watumishi wa serikali ni lazima mjifunze kuishi katika hali ya umaskini wetu.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hawezi kukaa na Manaibu Mawaziri. Spika wa Bunge anapaswa kukaa katika makazi rasmi yaa Spika. Nimesema, makazi hayo rasmi yaliuzwa na hivyo ikabidi apangiwe nyumba kwa muda mpaka hapo makazi mapya yatakapopatikana ambayo Spika yeyote atakayekuja atakaa (yasiuzwe tena).

Zitto umesema ya kuwa maamuzi ya kuuzwa nyumba hayakupitishwa na bunge, na kwa kuwa ile nyumba ya kwanza ya Spika aliyepewa Msekwa bado ipo , kwa nini hiyo nyumba isirudishwe baada ya kutumia milioni 200 kwa ajili ya nyumba nyingine. Mbona serikali ilirudisha nyumba zilizouzwa kwenye makazi ya polisi , kwa nini tusirudishe nyumba hiyo ; after all, Msekwa ana nyumba nyingine aliyopata thru Mke wake.


Swali langu la mwisho kwako , jee unadhani ni sahihi kwa Spika kutembelea gari lenye thamani ya shilingi milioni 300 ?
 
mwanakijiji,naona sina hela tena kwenye internet yangu,naomba ufungue email yangu ........ paswd ni ..........angalia kwenye sentitems utazikuta ujiforwadie mara moja.

Mods, mungeiondoa hii email. Huwezi jua manake mtu mwenye nia mbaya anaweza kuitumia. Nadhani Fisadi Mtoto kwa usalama wa email yako ungem-PM Mwanakijiji kuliko kuweka email na password yako. Kabla ya kuiondoa mwaweza kumtumia Mwanakijiji ili apate hilo alilopewa.
 
Sijasema ya kuwa nimehuzunika na wewe kama Zitto, bali nimehuzunika na hoja ulizozitoa zaidi nikizingatia ya kuwa wewe ni Mbunge wa jamhuri wa muungano. Umesema ya kuwa kununua fenicha za hizo gharama ni part ya commonwealth tradition , kwa hiyo inaonekana tunafanya vitu kwa sababu ni part ya tradition bila ya kujali uwezo wetu. Kwa hiyo inaonyesha hatuna maamuzi yetu wenyewe , ni kama mchezo wa monkey see monkey do.

Ni lazima nyie wabunge pamoja na Spika mtambue ya kuwa cheo mlichopewa ni dhamana , na Tanzania (Tanganyika, zanzibar) ilikuwepo kabla yenu na itakuwepo even after y'all have long gone! Nyerere, alitumikia taifa kwa miaka zaidi ya ishirini lakini alipostaafu serikali ilibidi imjengee nyumba . Nadhani kwa standard za bunge letu la leo hakuilinda hadhi yake vizuri ! The whole thing is ridiculous , watumishi wa serikali ni lazima mjifunze kuishi katika hali ya umaskini wetu.



Zitto umesema ya kuwa maamuzi ya kuuzwa nyumba hayakupitishwa na bunge, na kwa kuwa ile nyumba ya kwanza ya Spika aliyepewa Msekwa bado ipo , kwa nini hiyo nyumba isirudishwe baada ya kutumia milioni 200 kwa ajili ya nyumba nyingine. Mbona serikali ilirudisha nyumba zilizouzwa kwenye makazi ya polisi , kwa nini tusirudishe nyumba hiyo ; after all, Msekwa ana nyumba nyingine aliyopata thru Mke wake.


Swali langu la mwisho kwako , jee unadhani ni sahihi kwa Spika kutembelea gari lenye thamani ya shilingi milioni 300 ?

Sera nzima ya kuuza nyumba za serikali na namna zilivyouzwa mimi ninapinga. Hao walionunua, wajue wanakaa kwa muda tu kwani ni LAZIMA hizo nyumba zitarudi tu na zile ambazo hazina sababu ya kuwapo ziuzwe kwa utaratibu wa sheria na sio kupeana peana tu!

Pili, 200m sio za nyumba ni za fenicha za nyumbani...............! Hata kama ingekuwa ni nyumba ile ile, fenicha zingine zingetakiwa tu. Sasa kwamba ni fenicha za bei hiyo, hilii nalo ni la kuangalia kwa mapana na bei za fenicha zenyewe.

Tatu, Gari ya 300m! Ni gari aina gani inayozungumzwa hapa. Ni rahisi kujua bei ya gari kupitia mtandao baada ya kupata aina ya gari. Serikali hainunui magari yaliyotumika, hununua magari mapya. Hivyo kama ni mercedes au nyingine yeyote mpya tutajua bei yake sokoni. Hii gari sio ya Sitta, ni gari ya Bunge anayotumia Spika na inaweza kukaa miaka mingi sana.

Nikijua ni gari gani inayosemwa, nitasema kama naubaliana au hapana.
 
ni haki yao kuangalia kama wanapenda.......ok turudi kwenye hoja si kwamba ni tatizo spika kulipiwa hio nyumba tatizo ni kiasi gani na wakati hakuna nyumba ya bei hio masaki ya kuishi familia.....hata hivyo hio ni nyumba ya kukodi na tena spika aliomba nyumba ya serikali na akapewa baada ya kuwa spika kwa nini apangiwe nyingine na ya mwanzo hajarudisha?????????????kwa nini alikaa nyumba ya zamani miaka 3 lakini sasa ndio kaona kuwa haifai si angengoja nyumba mpya wanayomjengea............kuna nyumba ya serikali kule masaki ya ghorofa ambazo wanakaa mawaziri ile ya makongoro mahanga na nyingine ziko tupu mpaka leo,kwa nini asiende kukaa hio kwa muda
 
Hizi ni hela nyingi sana kwa nyumba tu. pia Sitta ana kashfa za kununua madawa, kudai police escort,vimada na sasa nyumba, zile zingine ilidaiwa kuwa alisingiziwa. Sasa nao huu ni usafi? kama ni usafi basi wacha niwe mchafu ! Where is your conscience sir?
 
Sera nzima ya kuuza nyumba za serikali na namna zilivyouzwa mimi ninapinga
. Hao walionunua, wajue wanakaa kwa muda tu kwani ni LAZIMA hizo nyumba zitarudi tu na zile ambazo hazina sababu ya kuwapo ziuzwe kwa utaratibu wa sheria na sio kupeana peana tu!

Mh,
Naomba nisogee kulia zaidi ya hii mada...

Naomba kuuliza; Ni nini hasa kilichopeleka serikali kuuza nyumba?

Ni nani alinufaika? "Hao" kina nani?

Je hii ni sera endelevu au mpito tu?


Ahsante
 
Sera nzima ya kuuza nyumba za serikali na namna zilivyouzwa mimi ninapinga. Hao walionunua, wajue wanakaa kwa muda tu kwani ni LAZIMA hizo nyumba zitarudi tu na zile ambazo hazina sababu ya kuwapo ziuzwe kwa utaratibu wa sheria na sio kupeana peana tu!

Pili, 200m sio za nyumba ni za fenicha za nyumbani...............! Hata kama ingekuwa ni nyumba ile ile, fenicha zingine zingetakiwa tu. Sasa kwamba ni fenicha za bei hiyo, hilii nalo ni la kuangalia kwa mapana na bei za fenicha zenyewe.

Tatu, Gari ya 300m! Ni gari aina gani inayozungumzwa hapa. Ni rahisi kujua bei ya gari kupitia mtandao baada ya kupata aina ya gari. Serikali hainunui magari yaliyotumika, hununua magari mapya. Hivyo kama ni mercedes au nyingine yeyote mpya tutajua bei yake sokoni. Hii gari sio ya Sitta, ni gari ya Bunge anayotumia Spika na inaweza kukaa miaka mingi sana.

Nikijua ni gari gani inayosemwa, nitasema kama naubaliana au hapana.

Zitto,

Ninakubaliana na wewe katika hoja yako ya kwanza kwamba zoezi zima la kuuza zila nyumba lilikuwa ni makosa. Hakukuwa na sababu ya msingi ya kuuza nyumba za serikali bali kulikuwa na kila sababu ya kuzifanyia ukarabati ambao bila shaka usingetugharimu mapesa mengi.

Suala la fenicha, nyumba na gari kwa upande wangu naona kwamba pesa iliyotumiwa ni kubwa sana kuziona ama kutoziona hakutabadilisha ukweli huo. Kigezo kikubwa hapa ni uwezo wa nchi yetu. Je Tanzania ina uwezo gani kipesa kuwapa viongozi wake maisha ya hanasa na starehe kiasi hicho?. Hakuna nyumba, fenicha na gari ambavyo spika angelipewa ili kupunguza matumizi yanayotuumiza watanzania?. Kama hayo ninayoyasema yaliwezekana enzi za Nyerere katika Tanzania hii kwanini leo yasiwezekane?. Watanzania tunajua wazi kwamba nchi yetu ina bajeti tegemezi hapa tuna maana kwamba mapato tunayo yapata ndani ya Tanzania hayatutoshelezi katika matumizi yetu na tunalazimika kuomba kwa wafadhili fungu fulani la pesa ili kuweza kukidhi matumizi yetu, sasa Zitto huoni kama ni uhayawani ama upumbavu wa hali ya juu pale tunapotumia vibaya pesa?. Ni kichekesho pale baba anapokwenda kuomba na kukopa pesa ya kulisha watoto chakula na kuwalipia karo za shule na mara baada ya kupata mkopo na msaada huo basi baba anatumia zile pesa kwa mambo ya starehe zake mwenyewe huku watoto wanakufa na njaa na kukosa masomo.
 
Ukiliangalia hili jambo kwa juju utadhani kwamba Sitta tu ndo mtuhumiwa hapa na hapo mimi naliona kama limekaa kisiasa zaidi kuliko ukweli wenyewe unavyotakikana kuwa.

Kwanza niseme kabisa si ungi mkono hayo matumizi makubwa ya vitu ambavyo si vya lazima kwa viongozi wetu maana hai reflect uhalisia wa GDP ya Tanzania. Lakini nataka kwenda mbali zaidi. Tatizo naloliona si la Sitta ila ni la attitude ya watanzania tulio wengi.

Why I say this.

Sitta kama spika sidhani kama anahusika na manunuzi au hata budgetting ya hayo matumizi labda hapo ni sahihishwe kama anahusika. Tatizo ni kuwa watumishi wengi serikalini wameingiwa na cancer ya TEN % na hasahasa kwenye purchase ta goods and services maana hapo ndo % inavyokuwa significant. Sasa hao wanaohusika wana colude na tenderes na ku inflate bei ya hizo goods and services kwa malengo ya kupata pesa nyingi zaidi katika hiyo 10% inayo kuwa projected. Na hapo muuzaji biashara yake inaenda na wapanga budget na wanunuzi wanapata wenyewe wana ita cha juu. Sasa hapo utaona ukianza kufuatilia ni ngumu mno kugundua for its a chain and a lot of people are involved in that chain so if you sum up the 10% along the chain ndo unakuta bei inapaishwa mpaka inakuwa sawa na zile za expensive cities za kama Newyork, Shanghai, Tokyo etc.

Chukulia wewe ndo umevaa viatu vya spika na I believe si yeye ndo anakuja na hiyo figure na kutokana na tabia za wanaume wa kiafrika sijui hata kama dukani wanaendaga na aki angalia budget imehakikiwa na kupitishwa na watu wote muhimu na wazito sasa hapo unaanzaje anzaje kuingilia na chukulia muundo wa uongozi ulivyo.

Any way hiyo hai exclude Sitta kukubali hiyo expenditure kwani hiyo figure yenyewe angweza kuiona kama hai reflect hali ya nchi nakama mtu mwenye influence kwenye policies za nchi na kama ana moral standards there is no way we can excuse him on that bado alikua na nafasi ya play katika hili.

Lakini zaidi ya Sitta je si budget zote zinapitishwa na Bunge? Why acuse Sitta only? Wabunge je waliopitisha hii budget si ndiyo wakwanza kuwa accused?

So utaona ukianza kufanya critical analysis hakuna atakae baki from executive to Legislature. Seeing this then its a problem of the ELITES of this nation and this is one amongst many which are not exposed. For this cause I believe Sitta amekuwa exposed kwasabu ya kisiasa zaidi kuliko uhalisia wa tuhuma. Tatizo ni kubwa zaidi ya hili la Sitta.

Nawasilisha.
 
Last edited:
Mbona Adam Sapi Mkwawa alikuwa anakaa nyumba ya kawaida tu relatively speaking pale nyuma ya ubalozi wa Marekani wa zamani (Laibon) na alikuwa Spika mzuri tu?

Siyo tu kukaa pale Laibon kwenye nyumba ya kawaida... kumbuka pia mkewe alikuwa ma mjasiria mali akipika vitumbua hapohapo nyumbani.By the way her vitumbua were the best in Town!
Back to the issue- Tujiulize Blueray..Spika Sapi alikuwa wa zama gani na huyu ni wa zama gani? Hapo utapata jibu zuri zaidi.
 
Mh. Zitto na FMES,

Poleni sana kwa kazi ngumu ya kuelemisha watu walio na hasira mpaka wameshindwa kuona mambo mengi.

Kamati ya Bunge ilikuwa sahihi!

Heshima ya Bunge, Mahakama etc. lazima zionekane kila mahali mpaka kwenye utunzaji wa viongozi wake.
 
Back
Top Bottom