Sura-ya-Kwanza
JF-Expert Member
- Nov 17, 2007
- 568
- 12
Hapa ndipo tutakapo zikumbuka nyumba za serikali, hiyo Government Agency ya serikali ilitakiwa kuanza mkakati wa kubomoa nyumba za zamani na kujenga Maflay ambayo yangeweza kuweka wafanyakazi wengi zaidi na kutengeneza mazingira ya maeneo hayo, na pale wafanyakazi wa serikali wakiamua kuka katika nyumba zao, basi hizoi nyumba zingepangishwa kwa mtu yoyote, mradi pesa ya muhusika, kuhusu viongozi wanao stahili nyumba za serikali kutokana na nafasi zao basi wangelazimishwa kuka katika nyumba stahili ambazo zinamilikiwa na serikali, kama Mkuu wa jeshi, polisi, Mkuu wa Chuo Kikuu, Spika, Raisi , makamu wa Raisi, Waziri Mkuu etc au wafanye study wa nchi zingine wanavyo wapatia nyumba viongozi husika, au hiyo housing allowance. Na kwa kweli kiongozi atakaye shinda uchaguzi mwaka 2010 itabidi afanye mkakati huo wa kuona njia iliyo bora ya serikali kuwa na nyumba stahili kwa baadhi ya watumishi wake au ndio system ya Chuo kikuu ya Housing allowance ya 1m ni ipi inafaa? kuwapa mtaji zaidi hao government agency au tupeane mkononi kila mtu akajenge nyumba yake kwa kutumia hiyo housing allowance.
August,
Ninakubaliana na Housing Allowance!
Iwe ina vigezo...
Hii itawapa uchaguzi wa maeneo wanayotaka, na nyumba wanazotaka;
Kuhusu Nyumba za Serikali...kama ni Uamuzi wangu basi Raisi na Baraza lake tu ndio watapewa nyumba:- kama subsidies. Watalipa!