Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Tatizo moja la spika wetu ndugu wananchi,kwanza nampenda ila kuna baadhi ya mambo anafanya bila busara;kwanza asikujue wewe unataka kumjeruhi wallahi atauza hata nyumba kuhakikisha umekwisha,,sasa swala kama hii linalohusu maslahi ya taifa sidhan kama kuna muda wa kuulizia kwa nini PAC ikudiscuss..

PILI😛amoja na kumsshukuru Bw mapesa kwa kuwa muwazi naweza kusema rasmi bunge la tanzania limejaa unafiki na uzandiki....wewe mapesa ukiwa kama mwenyekiti wa kikao utaachaje kushugulikia mambo ya maana yanaowahusu watanzania;hivi ulifikiri hizo pesa walizochota amepewa urambo????lazima haki itendeke Mwenyekiti unatakiwa uulizwe kwanza riport iko wapi na ukishaitoa lazima uelezee wazi wazi kwenye TV kwa nini uliikalia .....je kama hiki kipande kimenyofolewa jamani ndugu watanzania ni mangapi yanayokuwa discuss na kamati za bunge yanapigwa chini...kumbe wako bungeni kinafiki...wakisikia mtuu kalipuliwa wanajifanya kushadadia huku wakijizomea kindani ndani....mmmmmhhhh haya sitta;wa madhabahuni ale madhabuhuni hata tupige kelele najua 2010 itaisha...ila ikifika wakati na mawe yatanyanyuka kupiga kelele.....kila la kheri....kuwa msafi tuwe wasafi
 
Kwa ujumla, ofisi nyingi za serikali hukutwa na mapungufu makubwa tu ya hapa na pale. Lakini hili la Ofisi ya Bunge kuandikwa na Tanzania Daima ni mfululizo tu wa vitendo vya kifisadi vinavyofanywa na akina RA na EL kutaka kulipa kisasi kwa Spika baada ya suala la Richmond. Hawa mafisadi wamegundua udhaifu wa wahariri wa Tanzania Daima hivyo wanawatumia ipasavyo! Jaribuni kufuatilia makala na maoni yao kuhusu Spika Sitta. Zinachefua, kwani unaona kabisa hawa watu wanatumiwa. Shame on you guys!-

Tuache unafiki ukweli ni kuwa mambo mengi yalikuwa na bado yanakwwneda kwa lulindana lindana. Kuteremshwa kwa Lowasa kutoka juu lilikuwa ni jambo zuri sasa na yeye anataka awateremshe wengine wanaojuana madhambi yao.

Kuna metahli isemayao vita ya panzi furaja ya kunguru. sasa hii methali uki reverse ni vita ya kunguru furaha ya panzi. Maana yake ni kuwa vita ya wakuu ( mafisadi) ni furaja au neema kwa wanachi kujua ukweli kuwa waadilifu ni wachache sana.

Watch Out
Inawezekana hata mimi na wewe tunachukuziwa na ufisadi kwa maandishi na maneno tu lakini ukija behind the scena au background, tumeiva kuwa mafisadi tumebaki kutumika tu kwenye ufisadi
 
Gazeti la Tanzania daima limeandika leo kuwa Spika Samwel Sitta anaandamwa.Sababu ni kuwa eti amepanga nyumba kwa shilling million kumi kwa mwezi huko masaki wakati tayari ana nyumba aliopewa na serikali huko oysterbay(bahati nzuri naijua hio nyumba ni ile ambayo inaangaliana na nyumba ya zamani ya kina jack ntuyabaliwe,alipewa spika baada ya kuchaguliwa kuwa spika,kabla ya hapo alikuwa akikaa major fisch ambaye alifukuzwa ili kumpisha spika mpya na nyumba hio kwa sasa inatumika kama danguro na baa inayoitwa deeds club)Hio nyumba Spika kapewa yoteyote na sio kama alipewa kwa muda.
Aidha,kajinunulia benzi kwa shilling million mia tatu ili lifanane na hadhi ya spika huku akidai kuwa anayo ridhaa ya rais ya kununua na kuishi kwenye nyumba ya thamani hio ya uongo………kwa walioona nyumba hio ukweli ni kuwa kwa sasa hakuna nyumba ya kuishi familia masaki inayopangishwa kwa shilling million kumi kwa mwezi…….huu ni wizi na aibu kwa spika ambaye kila alipopelekwa kuangalia nyumba alikuwa akigoma na kudai haina hadhi yake mpaka alipopata nyumba yeye mwenyewe na kuagiza ilipiwe.
Natoa rai watu waangalie nyumba aliokuwa akiishi spika pius msekwa ilivyo simple nay a kawaida……..
 
Nilisema na nitaendelea kusema kuwa Samwel kijana wangu hajapata na wala hatokuwa msafi asilani kwa kuwa ndio miasha yake siku zote.
 
Spika Sitta aandamwa

  • Sasa ahusishwa kwa matumizi makubwa
na Mwandishi Wetu

Nyumba yenyewe ni hii:

i578_hekalu2.jpg


MWENENDO wa kimaisha na kimadaraka wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta, umekuwa ukifuatiliwa kwa karibu na watu mbalimbali ndani ya Bunge na nje; Tanzania Daima Jumatano imebaini.

Taarifa za uhakika ambazo Tanzania Daima Jumatano imezipata kutoka vyanzo vya kuaminika serikalini na bungeni zinaeleza kwamba, kufuatiliwa huko kwa Sitta, kunachangiwa kwa kiwango kikubwa na hatua yake ya kutangaza kujitoa mhanga, kupambana na vitendo vya ufisadi miongoni mwa viongozi wa dola.

Vyanzo vya kuaminika vilivyozungumza na gazeti hili, vimedokeza kwamba, hatua ya kuanza kufuatiliwa kwa karibu kwa Sitta inatokana na kuvujishwa kwa taarifa ambazo zinaihusisha ofisi ya kiongozi huyo wa juu bungeni na matumizi makubwa ya fedha za umma kwa mambo yanayotafsiriwa kuwa ni ya anasa na yasiyo na msingi.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo vya habari, sababu kubwa inayochochea kufuatiliwa kwa mwenendo wa matumizi ya ofisi ya Spika, kumechagizwa na kuwapo kwa taarifa za Bunge kukabiliwa na hali ya ukata mkubwa kifedha zilizothibitishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Huduma za Bunge, Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo (CCM).

Moja ya eneo lililoibua maswali mengi kuhusu matumizi ya fedha katika ofisi hiyo, ni ile inayohusishwa na hatua yake ya kuamua kumpangishia Spika Sitta nyumba binafsi kwa gharama za dola za Marekani 8,000 kwa mwezi (zaidi ya shilingi milioni 10).

Katika hili, kikubwa kilichoibua maswali ni hatua ya ofisi hiyo ya Bunge kuamua kumhamisha kutoka katika nyumba ya awali aliyopewa na serikali kwa maelezo kwamba, haikuwa na hadhi inayolingana na wadhifa wa u-Spika ambao miezi kadhaa iliyopita Sitta mwenyewe alipata kuufananisha kimamlaka na ule wa uwaziri mkuu serikalini.

Mbali ya kodi hiyo ya pango, kingine kilichoibua maswali na taarifa zake kupenyezwa nje ya ofisi hizo za Bunge, ni hatua ya kutumia zaidi ya shilingi milioni 200 kwa ajili ya kununulia samani katika nyumba hiyo mpya ya Spika ambayo tayari ameshahamia.

Kama hiyo haitoshi, taarifa zaidi ambazo Tanzania Daima Jumatano inazo ni zile zinazohoji kuhusu fununu za Ofisi ya Bunge kuagiza gari jipya aina ya Mercedes Benz ambalo litakuwa likitumiwa na Spika likikadiriwa kununuliwa kwa shilingi milioni 300, huku tayari kiasi cha shilingi milioni 270 zikiwa zimeshalipwa.

Hata hivyo, wakati taarifa hizo zikivujishwa kwa malengo ambayo Tanzania Daima Jumatano haliwezi kuyabainisha japo kwa sasa, Shellukindo amejitokeza na kumtetea Spika na ofisi yake kwa maamuzi yote yaliyofanywa na ofisi yake.

Akizungumza na gazeti hili kwa simu kutoka Dodoma jana, Shellukindo alisema maamuzi yote yaliyofikiwa na Ofisi ya Bunge kuhusu mafao anayostahili Spika yalifanyika baada ya kupata baraka zote za Rais Jakaya Kikwete.

Shellukindo ambaye pia ni Kamishna wa Tume ya Huduma za Bunge, alitoa kauli hiyo baada ya kutakiwa kutoa ufafanuzi kuhusu madai ya tume yake kuidhinisha malipo makubwa kwa ajili ya kodi ya pango ya nyumba anayoishi Spika.

Katika majibu yake, Shellukindo alisema maneno yanayosambazwa sasa kuwa Bunge linatumia fedha nyingi kwa ajili ya kulipa kodi ya pango ya nyumba ya Spika, hayana msingi kwa sababu malipo hayo yameidhinishwa na Rais Kikwete.

Alisema, ingawa kwa sasa Bunge lina hali mbaya kifedha, ukata huo hausababishwi kwa namna yoyote na ukubwa wa malipo bali ni ukweli kwamba sehemu zote sasa zinakabiliwa na tatizo hilo.

"Spika ana stahili zake kama Spika, hivyo kulipiwa kodi ya pango kwa dola
8,000 kwa mwezi na samani zake za ndani kugharimu zaidi ya sh mil 200 si jambo la ajabu. Ni kiongozi mwenye hadhi hiyo. Rais anajua, ndiye anayeidhinisha stahili zote za Spika. Hivyo hakuna jambo la ajabu hapo," alisema Shellukindo.

Akizungumza kuhusu Spika kuishi nyumba ya kupanga badala ya ile aliyopewa na serikali, alisema hilo lilitokana na ukweli kwamba nyumba iliyopewa awali haikuwa ya hadhi yake, hivyo ilibidi atafutiwe nyingine ya kupanga kutoka kwa mtu binafsi.

"Kila kitu anachopata Spika sasa, ndiyo walichokuwa wakipata waliomtangulia katika wadhifa huo. Bunge hatuna nyumba ya Spika, sasa ile ya serikali haikuwa na hadhi ya Spika kwa kweli. Ikabidi atafute ya kupanga kwa watu binafsi.

"Hili tumeliona kuwa ni tatizo na sasa Bunge lina mpango wa kujenga nyumba ya Spika. Nyumba hiyo haitakuwa ya Spika Sitta, bali maspika wetu watakaokuwa wakichaguliwa ndio watakuwa wakikaa humo," alisema.

Shellukindo aligusia pia suala la baadhi ya watumishi wa taasisi hiyo kutokuwa na sifa na kueleza kuwa, jambo hilo linaweza kuwa chanzo cha matatizo ya kifedha yaliyolikumba Bunge kwa sasa.

Alisema, tume yake inazo taarifa kuwa Mhasibu Mkuu wa Bunge (jina tunalihifadhi) amekuwa akionekana hawezi kuendelea kuwa mtumishi wa Bunge kwa wadhifa huo kwa sababu ya kuwa na kiwango kidogo cha elimu.

"Haiwezekani yeye awe analipa tu, tumempa muda wa kusoma ili awe na sifa za uhasibu. Kwa sasa hana sifa zinazokubalika kuendesha taasisi kama Bunge. Yeye ana vyeti vya chini chini, lakini mhasibu anatakiwa kuwa na CPA," alisema Shellukindo.

Alisitiza kuwa upo uwezekano wa mahesabu katika taasisi hiyo kuwa ni yenye utata kutokana na udhaifu wa mhasibu huyo.

Hata hivyo alisema, awali kabla ya kufanyika kwa mabadiliko ya sasa hivi, tume yake ilikuwa haina uwezo wa kuchukua hatua zozote za kikazi kwa mhasibu huyo kwa sababu Idara ya Uhasibu ya Bunge ilikuwa ikiripoti moja kwa moja Hazina. Alieleza zaidi kuwa hivi sasa tume yake imepewa meno na iko kwenye mkakati wa kuhahakisha kila senti ya Bunge inafahamika ilivyotumika kwa vile wahasibu wote sasa wanaripoti katika tume hiyo baada ya kufanyika mabadiliko katika muundo wa utumishi kwa wafanyakazi wa Bunge. Shellukindo alisema kwa kuanza, tume yake imepanga kuanza kupokea ripoti za Idara ya Uhasibu ya Bunge kila baada ya miezi mitatu ili kudhibiti ufujaji wa fedha wa aina yoyote katika taasisi hiyo.

Chanzo: Tanzania Daima
 
Last edited by a moderator:
Mhhhh. Aisee. Hapa patamu enh!. Milion 10 kwa mwezi hiyo nyumba iko dodoma au sayari gani?
 
Hivyo ndivyo MAPESA ya UMMA yanavyopenyezwa na kuwarudia wahusika. Dola elfu 8 kwa mwezi! Hata Ikulu ya Chamwino ingepangishwa isingelipiwa hivyo?
 
Yesu mungu na mariaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.......................hapa lazima tume iundwe............ikulu anayolala jk tukiamua kumcharge aifiki million 6...jamani hivi hawa watu wanatuona vipi sana ama .....kumbe kuna mambo makubwa sana yamefichwa umo ndani ya bunge hatujui...kama haya machache tumeyanyaka.....jk...mmmmhhh.......,kazi ipo mashehe wachungaji mapadre kwa style hii....wabwatukien tu....kuna wakati lazima tuchoke
 
8,000 x 12 x 5 = usd 480,000 in five years only housing; kweli masikini hajijui kuwa ni masikini; hata akili haifanyi kazi. Hata Raisi hana akili!
 
Duh huo ndo utawala bora wa sheria.
Hapo bado masulufu,posho,mshahara utaona mzee 6 anaondoka na kama zaidi ya 20M.
Wkt amount hiyo sidhani kama waziri wa UK analipwa.
 
Kweli hawa viongozi wetu hawana uchungu na kodi zetu, hiyo nyumba ina nini hasa? Na kama unaworthy 10ml kwa nini wanunue na thamani tena za ml 200!?
Namna hii hatuendi popote
 
Nyumba za serikali si wameshajiuzia sasa wanabaki kupangisha.. hii akili ya viongozi wetu sijui imekaaje. chunguzeni vizuri utakuta hiyo nyumbani aliyopangishiwa ni ya hao hao tu hakuna kitu hapo ni mchezo tu wanatuchezea watanzania.
Inamaana hiyo hadhi anayotaka spika kwa kuhamishiwa nyumba ambayo alikuwa anakaa tayari na kupangishiwa nyingine hiyo ya mamilioni ni hadhi gani huyu jamaa ataitaka.
Waafrika kweli akili hatuna.. mbona mtoni kiongizo wa juu tu anakaa kwenye nyumba kama raia tu mwingine. Hiyo ni "game" tu wamecheza.. hizo hela wanajilipa wenyewe hakuna kitu hapo.. no body can agree kulipa mtu kiasi chote hicho kwa pango.. imekuwa ikulu hiyo..????
 
Nyumba za serikali si wameshajiuzia sasa wanabaki kupangisha.. hii akili ya viongozi wetu sijui imekaaje. chunguzeni vizuri utakuta hiyo nyumbani aliyopangishiwa ni ya hao hao tu hakuna kitu hapo ni mchezo tu wanatuchezea watanzania.
Inamaana hiyo hadhi anayotaka spika kwa kuhamishiwa nyumba ambayo alikuwa anakaa tayari na kupangishiwa nyingine hiyo ya mamilioni ni hadhi gani huyu jamaa ataitaka.
Waafrika kweli akili hatuna.. mbona mtoni kiongizo wa juu tu anakaa kwenye nyumba kama raia tu mwingine. Hiyo ni "game" tu wamecheza.. hizo hela wanajilipa wenyewe hakuna kitu hapo.. no body can agree kulipa mtu kiasi chote hicho kwa pango.. imekuwa ikulu hiyo..????


Si ajabu ni nyumba yake, au ya mkuu fulani huko juu, Tanzania lazima tuanze upya waliopo madarakani ni watumiaji kuliko viongozi walioko nchi zilizoendelea, kaaaaaazi kwelekweli
 
Wakuu sasa hapana tunamlaumu Sitta as a person au systme inayomruhusu Spika hata ukiwa wewe au mimi kukaa kwenye nyumba ya gharama hiyo. Kuna institutional corruption lazima tuikemee pia. Tatizo hakuna mwenye uwezo na hakuna mechanism ya kupambana na bunge as institution.
 
viongozi wa hovyo huwekwa na wananchi wa hovyo
 
kitu kinachoendelea katika serikali ya nchi hii ni upumbavu tu,
hamna lolote lile..
hela zote hizo eti ni matumizi ya spika..huu si ni ushenzi huu!
lakini sishangai wala nn kwa kuwa najua matumizi ya katibu mmoja wa wizara yanaweza kuwa ni mara dufu ya haya..
this country is fucked up,its all i can tell!
 
Naweza pata wapi audited reports za bunge kwa miaka 5 iliyopita?
 
Mwenda-pole umesema ukweli. Jamani wana JF ambao mpo huko nyumba ilipo chunguzeni hiyo nyumba ni ya nani ikiwezekana na tilte deed yake tuwe na uhakika. Naamini huu ni mchezo mchafu tu. Halafu eti Shelukindo na Spika mnasema mnapambana na Mafisadi! Hata nyie ni kundi hilo tu, TOA KWANZA BORITI KWENYE JICHO LAKO NDIO UONE KIBANZI KWA MWENZIO. Kwa jinsi hii kamwe hatutafika. Msafi ni Nani na mweye kudhubutu kukemea ili tumweke madarakani 2010?
 
Habari wanabodi,

Ni muda sijaingia humu sababu ya majukumu makubwa niliyokabidhiwa miezi mitatu iliyopita,Muda wa kupitia humu unakuwa mdogo sana.

Hii ya spiika kutumia zaidi ya milion 700 kwa muda wa miaka matano kwa malazi tu ni jambo la kupigwa vita.

Nchi ya mandondocha..sijui tumerogwa!

Mwanakijiji fuatilia hili,hiyo nyumba inamilikiwa na nani na je tender ilitangazwa kupata mzabuni.Unawez akuta hiyo ni nyumba ya kigogo wa serikali..tayari dar sasa hivi kuna nyumba za dola 8000??aisee..
 
Back
Top Bottom