Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ndo tatizo la kuchagua uongozi wa hovyo maana na matendo yao yanakuwa ya hovyo hovyo..
 
enzi za mwalimu unakaa kwenye nyumba ya serikali na hakuna kuwa na double standard hata kama wewe ni spika unatumia samani zilizopo, who are you uishi kama upo peponi.

kama kweli ni kwanini basi isijengwe nyumba nyingine huku kupanga ni ufujaji mkubwa wa jasho langu mlipa kodi, nakumbuka mwalimu aliwahi kusema mnanijengea nyumba kubwa kwani mimi tembo...kwa life style hii ya viongozi wetu nachelea kusema tuna MATEMBO WENGI
 
Dola elfu nane sio nyingi ila umasikini ndio umewadumaza na kuona ni ela kubwa ,hivi mnaelewa kuwa kwa kila Mtz anaemiliki simu ya mkononi (mobile phone au cellular phone) anaweza kumiliki honda pikipiki au gari ndogo ? Mmewahi hata kulifikiria ? AU just mnaona watu wakiagizia vocha ,na kutwa yupo na simu sikioni ?

Kwa hili naona itakuwa mnamuonea tu ,kuna aina mbili za fedha ,inawezekana mtu akasema apewe fedha cash na atajihudumikia mwenyewe na inawezekana serikali inamlipia ,sasa spika analipa mwenyewe au analipiwa ?

Nitaona spika anenda kinyume ikiwa hawatumikii wananchi vile inavyotakiwa,anaelemea upande mmoja ,anawalinda mafisadi na kuwakingia kifua watu wanaohojiwa hoja za maana ,hapo nitaweza kabisa kusema kuwa spika analiibia Taifa hili na hawatumikii wananchi ,hivyo hela yote anayopokea iwe mshahara,malipo ya anapoishi na posho ,hizo zote zitakuwa sio haki yake kwa kuwa hatimizi wajibu wake ,yupo hapo kwa kuwalinda wafuasi wa Sultani CCM tu.
 
dola elfu nane sio nyingi ila umasikini ndio umewadumaza na kuona ni ela kubwa ,hivi mnaelewa kuwa kwa kila mtz anaemiliki simu ya mkononi (mobile phone au cellular phone) anaweza kumiliki honda pikipiki au gari ndogo ? Mmewahi hata kulifikiria ? Au just mnaona watu wakiagizia vocha ,na kutwa yupo na simu sikioni ?

Kwa hili naona itakuwa mnamuonea tu ,kuna aina mbili za fedha ,inawezekana mtu akasema apewe fedha cash na atajihudumikia mwenyewe na inawezekana serikali inamlipia ,sasa spika analipa mwenyewe au analipiwa ?
aaaahhh!!!....🙁
 
hivi mshaona ile ofisi yake au mnalalama tuuu?

Reception peke yake ina furnitures na vikolombwezo vinavyoworth 20 million

then kuna receprtion ya pili ndio hatari zaidi maana sidhani hata kama Obama na executive reception kama ile

then kuna ile conference room no1 haina mfano na ile conference room no 2 ndio kufuru

then kuna hiyo Ofisi yenyewe ...ofisini kwa JK ni taka taka kulinganisha na ofisi ya Spika wa nchi maskini kama Tanzania...na kama hiyo haitoshi yule mheshimiwa ile bedroom ya kulala pale ndio utafikiri jamaa anakaa kwenye penthouse

Kwa mbali inaelekea kukaribiana na ile ya Gavana Balali...ambayo nduli hataki kuitumia kisa iko too lavish...na wakija mawaziri na wanasiasa basi huwapeleka ofisi ambayo iko moderate

of course hapo bado hatujaongelea Spika alivyolazimisha apewe escort kuliko ya Vice President au Rais wa Zanzibar
 
Ikiwa analipiwa au analipwa wa kumlaumu na kuilaumu ni serikali ,sio spika wala mic. Yeye ameajiriwa na analipwa na muajiri wake sasa makelele ipigieni serikali ya CCM kuwa ndio inayoimaliza nchi hii,vinginevyo itakuwa choyo tu.Sasa kama hajalipwa hizo hela hapa kwao Tz akalipwe wapi, China ? Halafu hiki cheo ni dhamana kubwa sana ,lazima kiwe na hadhi ya aina yake ,kwa mnavoonyesha hata akilipwa dola 1000 mtaziona nyingi.
 
...na kama hiyo haitoshi yule mheshimiwa ile bedroom ya kulala pale ndio utafikiri jamaa anakaa kwenye penthouse

Duh mkuu GT umeniacha hoi huo usingizi anapumbunzika na maiwaifu wake? Au kila kimada cha Kinondoni kinachotumia gari la ofisi za bunge kama sikosei au cha Upanga?
Bado tunasafari ndefu sana tena mno.
 
 
Ikiwa analipiwa au analipwa wa kumlaumu na kuilaumu ni serikali ,sio spika wala mic. Yeye ameajiriwa na analipwa na muajiri wake sasa makelele ipigieni serikali ya CCM kuwa ndio inayoimaliza nchi hii,vinginevyo itakuwa choyo tu.Sasa kama hajalipwa hizo hela hapa kwao Tz akalipwe wapi, China ? Halafu hiki cheo ni dhamana kubwa sana ,lazima kiwe na hadhi ya aina yake ,kwa mnavoonyesha hata akilipwa dola 1000 mtaziona nyingi.


Mkuu Mwiba hapa nadhani ndo hoja ilipo, ni tatizo la kimfumo, na mtu anaweza kutoa hoja kwamba anapewa vikolombwezo hivo vote na serikali ili pia asiwe na nguvu za kuibana serikali au miswada mbali mbali hata yenye utata ipitishwe au hoja za kuzima zizimwe, maadamu ssipika kasema kuwa hii sio hoja. au imecheleweshwa au ni ya hovyo hovyo, na hayo tumeshayaona tayari yakitokea

Kinyume na hapo, kwa nini aache nyumba ya serikali akapangishe, eti kuwa sio ya hadhi yake?

Kesho tutamsikia raisi kapanga kule Tabata kwa sababu Ikulu sio ya hadhi yake si imejengwa tangu enzi za mjeremani? sasa hapo tutakuwa tumefikishana wapi?
 
"Watanzania wana wivu wa kike" B.W Mkapa

Mlitaka akaishi Manzese? mlipokuwa mkiuza nyumba za serikali mlitegemea nini?

"Miafrica ndivyo ilivyo" Nyani Ngabu
 
Mkuu Mwiba hapa nadhani ndo hoja ilipo, ni tatizo la kimfumo, na mtu anaweza kutoa hoja kwamba anapewa vikolombwezo hivo vote na serikali ili pia asiwe na nguvu za kuibana serikali au miswada mbali mbali hata yenye utata ipitishwe au hoja za kuzima zizimwe, maadamu ssipika kasema kuwa hii sio hoja. au imecheleweshwa au ni ya hovyo hovyo, na hayo tumeshayaona tayari yakitokea

Kinyume na hapo, kwa nini aache nyumba ya serikali akapangishe, eti kuwa sio ya hadhi yake?

Kesho tutamsikia raisi kapanga kule Tabata kwa sababu Ikulu sio ya hadhi yake si imejengwa tangu enzi za mjeremani? sasa hapo tutakuwa tumefikishana wapi?

Hatukuletei Machine gun yako wala nini! (Lol). Ila una point kaka.
 
Vyovyote vile hiyo nyumba ni ghali sana hata mkiitetea.

kama inalipwa na serikali basi kwa uhakika watu wamekula 10% kama ilivyo jadi. huhitaji phd kupata hisia ya bei za nyumba za kuishi TZ, labda iwe ranchi kama ya Michael jackson ndio itakaribia but nyumba tuu. mhh
 
Vyovyote vile hiyo nyumba ni ghali sana hata mkiitetea.

kama inalipwa na serikali basi kwa uhakika watu wamekula 10% kama ilivyo jadi. huhitaji phd kupata hisia ya bei za nyumba za kuishi TZ, labda iwe ranchi kama ya Michael jackson ndio itakaribia but nyumba tuu. mhh


Umeshaiona au?, nenda ukaitembelee ndani kisha njoo upinge!
 
Ndio maana wanazuoni wa kanisa katoliki Tanzania wameamua kutoa elimu ya uraia, haki za binadamu, democrasia na jinsi ya kumtambua mtu muadirifu anayestahili kupewa uongozi, namna ya kuhakikisha watu waadilifu wanaotaka nafasi za uongozi wanasaidiwa kuzipata na kadhalika.

Katika mpango huo pia wameelezea umuhimu wa wananchi kujua mafao na malupulupo ya viongozi wao na ikibidi wawe na uwezo wa kuamua kuapunguzia malupulupu hayo.
 
Dola elfu nane sio nyingi ila umasikini ndio umewadumaza na kuona ni ela kubwa ,hivi mnaelewa kuwa kwa kila Mtz anaemiliki simu ya mkononi (mobile phone au cellular phone) anaweza kumiliki honda pikipiki au gari ndogo ? Mmewahi hata kulifikiria ? AU just mnaona watu wakiagizia vocha ,na kutwa yupo na simu sikioni ?

Wewe Mwiba huu utafiti umeufanya lini? Au data hizi umezipata wapi? Mimi kiwango cha juu cha matumizi yangu ya simu ni sh. 10,000 kwa kwezi ina maana kwa mwaka natumia si zaidi ya sh. 120,000. Sasa hii pesa inaweza kununua pikipiki au gari? Wengine hawazidishi sh. 5000 kwa mwezi. Sasa ni miaka mingapi atakusanya mpaka anunue pikipiki au gari?

Nyumba ya dola 8,000 kwa kwa mwezi kwa Tanzania ni nyingi sana. Huu ni ufisadi kabisa.
 
Wakuu sasa hapana tunamlaumu Sitta as a person au systme inayomruhusu Spika hata ukiwa wewe au mimi kukaa kwenye nyumba ya gharama hiyo. Kuna institutional corruption lazima tuikemee pia. Tatizo hakuna mwenye uwezo na hakuna mechanism ya kupambana na bunge as institution.

Well, yeye ni kiongozi na alipaswa kuona kwamba kupangisha nyumba ya milioni 10 na kutumia milioni zaidi ya 200 kununua thamani ni tatizo kubwa katika nchi maskini kama Tanzania. Sasa kama yeye haoni kuwa hilo ni tatizo ili aweze kubadilisha, then he is a problem as an individual. Remember, institutional problems are caused by individuals and it is individuals who work in those institutions who should fix them.
 
Wewe Mwiba huu utafiti umeufanya lini? Au data hizi umezipata wapi? Mimi kiwango cha juu cha matumizi yangu ya simu ni sh. 10,000 kwa kwezi ina maana kwa mwaka natumia si zaidi ya sh. 120,000. Sasa hii pesa inaweza kununua pikipiki au gari? Wengine hawazidishi sh. 5000 kwa mwezi. Sasa ni miaka mingapi atakusanya mpaka anunue pikipiki au gari?

Nyumba ya dola 8,000 kwa kwa mwezi kwa Tanzania ni nyingi sana. Huu ni ufisadi kabisa.
.

Umesema kweli kabisa, kwa vigezo vyovyote kwa mazingira ya Tanzania pango la dola 8000 bila kusahau dola 200000 na 300000 kwa samani na gari ni KUFURU
 
Well, yeye ni kiongozi na alipaswa kuona kwamba kupangisha nyumba ya milioni 10 na kutumia milioni zaidi ya 200 kununua thamani ni tatizo kubwa katika nchi maskini kama Tanzania. Sasa kama yeye haoni kuwa hilo ni tatizo ili aweze kubadilisha, then he is a problem as an individual. Remember, institutional problems are caused by individuals and it is individuals who work in those institutions who should fix them.

Give me a second,

Wajameni, spika ni mtu anaye-report kwa jamhuri ni mtu mkubwa sana, dola 8000 is nothing kwa cheo chake, lazima spika awe sehemu ambayo hatapenda kuhemea kwa kwenda visafari visivyokuwa na maana.

Tumeona watu wengi nyumba za pango ya dola 5000, ni za kawaida sana maeneo ya oysterbay...
 
Back
Top Bottom