Ni nini sababu ya binadamu kuletwa Duniani?

Ni nini sababu ya binadamu kuletwa Duniani?

Hukutengenezewa kama upungufu, ni zawadi, kwamba uwe na free will. changamoto tu ni kuwa will power haina mipaka, na unaweza ukafanya jambo hata kinyume na aliyekupa huo uwezo wa kuchagua. Hasa ndo kinachokutesa.

Hasira ya Mungu ipo kwasababu uliumbwa ukiwa mkamilifu. Kwa hiyo mapungufu uliyonayo ni ya kujitakia tu, ni kama unavyolea mtoto wako alaf afanye kitu tofauti na unavyo mwelekeza utakasirika
Freewill ni utapeli mkuu
 
Kwa Jamii za kiafrica kuwaambia kuwa hicho wanachoamini na kuabudu ni watu walikaa na kupanga mipango ya jinsi ya kuiitawala Dunia wanaanza kukukemea kuwa ni pepo🤣🤣
Na wanaamini kabisa hicho kitu ni kikuu kuliko wao na bila hicho kitu hawawezi kabisa .

Kufuli na kitasa la kwenye sanduku walilopo ni AHADI NA KITISHO.
 
Hivi ni raha gani hizo ambazo mwanadamu anazikosa kama akiamua kuishi maisha ya utakatifu kiasi cha kuona maisha ni mabaya kama akizikosa?
Ni tamaa mbaya? ulevi? Uchawi? Uzinzi? Ufiraji? Wizi? Kutokuheshimu wazazi? Mbona ni ubatili tu huu.
Mtu yeyote aliyepevuka hata kama hamuamini Mungu anaelewa kabisa hapo ni kujilisha upepo tu wala hayana faida ila hasara.
Kula raha ni dhambi?
 
Na wanaamini kabisa hicho kitu ni kikuu kuliko wao na bila hicho kitu hawawezi kabisa .

Kufuli na kitasa la kwenye sanduku walilopo ni AHADI NA KITISHO.
Hapa umenena mkuu! Yaani unakwambia mtu ata asome satanic bible Ili alinganishe ukweli wa anayofundishwa, anaruka futi 100 yote hiyo ameshapigwa pin, kuwa hata kusoma hiyo biblia ni dhambi, 🙌 sa sijui tutaamka lini
 
Freewill ni utapeli mkuu
Alie kupa freewill anajua kabisa mwishoni lazima uzingue ili akuchome bila kusamehe , halafu yeye anakutaka wewe ukikosewa usamehe , na papo hapo ana dai ana upendo, na hapo hapo anadai upendo huvumilia ,husamehe wala hauhesabu mabaya , na papo hapo yeye anahesabu mabaya kwa kuandika dhambi zetu na wino wa chuma🤔
 
Hapa umenena mkuu! Yaani unakwambia mtu ata asome satanic bible Ili alinganishe ukweli wa anayofundishwa, anaruka futi 100 yote hiyo ameshapigwa pin, kuwa hata kusoma hiyo biblia ni dhambi, 🙌 sa sijui tutaamka lini
Kuna wale wanafunzi wanajua umuhimu wa elimu wao husoma kwa bidii bila hata fimbo wala ahadi, na kuna wale wanafunzi wao mpaka bakora na vitisho ili wasome ,hivyo yote haya yanahitajika ili mambo yaende.
 
Habari wanaJf
Nimekuwa nikijiuliza swali moja la msingi sana lakini majibu thabiti nimekuwa nikikosa kabisa...

Kwa wale wanaoamini kuhusu uwepo wa Mungu naomba wanijuze kwanini tumeletwa hapa duniani ambako tunaishi maisha mafupi na kupita, je Mungu hakuona namna nyingine ya kutufanya tufike huko kwenye maisha ya milele kunakosemwa na vitabu vyake bila kupitia hapa duniani kwenye shida na karaha?
Kulikuwa na haja ipi kutupitisha kwenye mateso hali ya kuwa ipo sehemu salama tunaelekea? ( Kwanini alitupitisha duniani?)

Hata wale wasioamini uwepo wa Mungu nao naomba wanisaidie kujua juu ya hili swali langu...kama hakuna maisha baada ya haya kwanini tupitishwe hii sehemu yenye taabu na mateso mengi tena kwenye maisha mafupi..kwanini tumetolewa huko tulikokuwa na kuletwa hapa duniani ambako kuishi kwetu ni muda mfupi na tisingebaki huko huko kama tulikuwa na maisha kabla?

Nini sababu ya sisi binadamu kuletwa/kupitishwa hapa duniani?
Dunia ni darasa, la kutuwezesha kuishi na Mungu milele. Kama tukiamua kumpa Yesu maisha yetu tutapokea wokovu.
 
Habari wanaJf
Nimekuwa nikijiuliza swali moja la msingi sana lakini majibu thabiti nimekuwa nikikosa kabisa...

Kwa wale wanaoamini kuhusu uwepo wa Mungu naomba wanijuze kwanini tumeletwa hapa duniani ambako tunaishi maisha mafupi na kupita, je Mungu hakuona namna nyingine ya kutufanya tufike huko kwenye maisha ya milele kunakosemwa na vitabu vyake bila kupitia hapa duniani kwenye shida na karaha?
Kulikuwa na haja ipi kutupitisha kwenye mateso hali ya kuwa ipo sehemu salama tunaelekea? ( Kwanini alitupitisha duniani?)

Hata wale wasioamini uwepo wa Mungu nao naomba wanisaidie kujua juu ya hili swali langu...kama hakuna maisha baada ya haya kwanini tupitishwe hii sehemu yenye taabu na mateso mengi tena kwenye maisha mafupi..kwanini tumetolewa huko tulikokuwa na kuletwa hapa duniani ambako kuishi kwetu ni muda mfupi na tisingebaki huko huko kama tulikuwa na maisha kabla?

Nini sababu ya sisi binadamu kuletwa/kupitishwa hapa duniani?

Tumeletwa duniani ili tupitie mtihani wa imani utiifu na matendo mema na ni Uhuru kila mtu achague atamtii nani Mwenyezi Mungu au matamanio ya nafsi

Kama tungeliumbwa moja kwa moja kwa ajili ya Pepo bila uchaguzi, hilo lingekuwa sawa na malaika lakini wanadamu tumepewa hiari ya kuchagua ndiyo maana kuna ujira kwa wema na adhabu kwa uovu Allah anasema katika Qur'an 👇🏽


Surat Al-Mulk (67:2)
"Ambaye ameumba mauti na uhai ili akujaribuni, ni nani miongoni mwenu mzuri zaidi wa vitendo. Naye ni Mwenye nguvu, Mwenye kughufuria".



Maisha haya si lengo lenyewe ni darajatu la kuelekea kwenye maisha ya milele.

Surat Al-Ankabut (29:64)
"Na haya maisha ya dunia si chochote ila ni pumbao na mchezo. Na hakika makaazi ya mwisho ndiyo maisha hasa laiti wangekuwa wanajua."


Surat An-Nisa (4:40)
"Hakika Mwenyezi Mungu hadhulumu hata chembe ya udongo..."

Surat Taha (20:123-124)
"...Hapo utakapokujieni uwongofu kutoka Kwangu, basi atakayeufuata uwongofu Wangu hatapotea wala hatataabika. Na atakaye puuza maonyo Yangu, basi bila shaka atakuwa na maisha ya dhiki..."

Surat Al-Mu’minun (23:115)
"Je, mlidhani kwamba tumewaumba kwa bure tu, na ya kwamba hamtarudishwa kwetu?"


Mwenyezi Mungu alituumba kwa lengo gani

Surat Adh-Dhariyat (51:56)
"Sikuwaumba majini na watu ila waniabudu."

Surat Al-Baqara (2:286)
"Mwenyezi Mungu hamkalifishi mtu yeyote ila kwa kadiri ya uwezo wake..."
 
Alie kupa freewill anajua kabisa mwishoni lazima uzingue ili akuchome bila kusamehe , halafu yeye anakutaka wewe ukikosewa usamehe , na papo hapo ana dai ana upendo, na hapo hapo anadai upendo huvumilia ,husamehe wala hauesabu mabaya , na papo hapo yeye anahesabu mabaya kwa kuandika dhambi zetu na wino wa chuma🤔
naam mkuu dhana ya freewill inakinzana na hizo sifa, kuna maswali uki-reason unaona kabisa freewill haifit
 
Je unachokiona kiko sawa, umewahi kufikiri kinaweza kuwa na madhara kiasi gani kwa wengine?
Kwa mazingira je?

Hapo ndo amri zinaanza sasa, maana binadamu wakikosa mipaka ni disaster.
Kwani huko peponi kutakuwaje?
Kwanini asingeumba pepo akatupeleka moja kwa moja maana huko ni hakuna dhambi watu wanakula bata mwanzo mwisho
 
Kwani huko peponi kutakuwaje?
Kwanini asingeumba pepo akatupeleka moja kwa moja maana huko ni hakuna dhambi watu wanakula bata mwanzo mwisho
Bata ipi ya peponi unayoizungumzia hapa? Huko ni kuimba mapambio na kunywa juice. Mambo yote mazuri na matamu ni dhambi, hayatakuwepo peponi.
Labda kule upande wa pili ndo watapewa mabikra na mito ya pombe, nafikoria hukamia huko maana pepo yao inavutia
 
Bata ipi ya peponi unayoizungumzia hapa? Huko ni kuimba mapambio na kunywa juzi. Mambo yote mazuri na matamu ni dhambi, hayatakuwepo peponi.
Labda kule upande wa pili ndo watapewa mabikra na mito ya pombe, nafikoria hukamia huko maana pepo yao inavutia
Nilimsikia Shekh Kipozeo anasema Peponi kuna mito ya pombe, mabikra 72 wabiiiichi…… kuna starehe zaidi ya hiyo kweli? 😂
 
Nilimsikia Shekh Kipozeo anasema Peponi kuna mito ya pombe, mabikra 72 wabiiiichi…… kuna starehe zaidi ya hiyo kweli? 😂
Hakuna, ila bado najiuliza wanawake wanafaidi nini zaidi ya pombe huko peponi
 
🤣🤣 mulemule Sema baadhi yao wanachanganya na ushirikina wakusema YESU ni Mungu sasa Mungu anapakwaje Mafuta hapo ndiyo kuna mpaka mkubwa.
Ikawaje mungu wao awe na ahadi tofauti na Mungu wako, huku hakuna kula wala kunywa ni harusi moja tu ya mwana kondoo , na kwenu ni bikra 72 na mito ya faru john?
 
Back
Top Bottom