Kiuhalisia hakuna hata haja ya binadamu kuja duniani...

Kiuhalisia hakuna hata haja ya binadamu kuja duniani...

SankaraBoukaka

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2019
Posts
3,214
Reaction score
5,011
Binadamu tunajiona viumbe waliobarikiwa kwa akili na maarifa. Tumegundua teknolojia, tumeandika vitabu, tumejenga miji mikubwa, na tumeunda tamaduni nyingi. Lakini tukichunguza kwa undani, yote haya hayajabadilisha ukweli wa msingi,,,, binadamu hakuja duniani kufaidika kwa namna ya kudumu.

Kwa sababu matukio makuu ya binadamu ni mawili tu .... ni kuzaliwa na kufa. mwisho wa yote bado ni uleule. Hakuna ugunduzi wa kisayansi, hakuna teknolojia ya kisasa, wala falsafa ya kina inayoweza kubadilisha ukweli huu wa kimsingi.
Binadamu tunaishi kwa muda mfupi, tukijidanganya kuwa tuna faida kubwa, lakini dunia yenyewe haijabadilika kwa ajili yetu.

Miti bado inakua bila kujali nani yupo, bahari bado inacheza mawimbi yake bila kuuliza ruhusa, na jua bado linazunguka ratiba yake bila msaada wa binadamu.
Hata ugunduzi mkubwa kama ndege au smartphone za mkopo, havibadilishi ukweli kwamba wateja wa watu credit tutaondoka duniani bila kujua siri kamili ya maisha.

Sisi ni kama mgeni tuliovamia tamasha bila tiketi. Tunafurahia muziki, tunacheza kidogo, tunabishana na wenzetu, lakini mwisho wa siku tunatolewa nje kwa lazima.
Dunia haikuwahi kutuomba tuje, na haitulili tubaki.

Kiuhalisia, binadamu hakuja duniani kwa faida yake. Yote tunayofanya ni michezo ya muda mfupi, tamthilia ya kujipa matumaini.
Mwisho wake unabaki pale pale: kuzaliwa na kufa.
Dunia inaendelea bila sisi, na sisi tunaondoka bila kubadilisha chochote cha msingi kwa nafsi zetu.

Usijipe stress, kumbuka kuna maisha hata bila hela za kausha damu na simu za watu credit
 
Mimi najiuliza mbona hata maisha ya miaka hiyo ,karne za zamani huko enzi za utumwa kabisa ,mbona watu walikuwa wanavaa mavazi yale yale kama "Suti" ina maana bado hakuna mageuzi makubwa .

Inakuwaje tutumie mfumo wa computer ,ambao umegunduliwa miaka mingi sana huko nyima , zaidi tunafanya mabadiliko madogo madogo...Kwa nn iwe kila kitu cha kisasa kitumie mifumo ile ya programming ,na computer application.
 
Ila haya mambo yote ukishakuwa na pesa za kutosha hauwezi kujiuliza maswali kama haya😁

A human mind is a mystery.
Sio kwel mkuu Dunia ni kiumbe ambacho kimekamilika na Mungu alikipenda ndo maana hata sisi hatuna umuhimu kwa Mungu kushinda Dunia sema watu wanahisi wao ni bora kuliko Dunia lakini Kwa Mungu sisi ni nothing
 
Binadamu tunajiona viumbe waliobarikiwa kwa akili na maarifa. Tumegundua teknolojia, tumeandika vitabu, tumejenga miji mikubwa, na tumeunda tamaduni nyingi. Lakini tukichunguza kwa undani, yote haya hayajabadilisha ukweli wa msingi,,,, binadamu hakuja duniani kufaidika kwa namna ya kudumu.

Kwa sababu matukio makuu ya binadamu ni mawili tu .... ni kuzaliwa na kufa. mwisho wa yote bado ni uleule. Hakuna ugunduzi wa kisayansi, hakuna teknolojia ya kisasa, wala falsafa ya kina inayoweza kubadilisha ukweli huu wa kimsingi.
Binadamu tunaishi kwa muda mfupi, tukijidanganya kuwa tuna faida kubwa, lakini dunia yenyewe haijabadilika kwa ajili yetu.

Miti bado inakua bila kujali nani yupo, bahari bado inacheza mawimbi yake bila kuuliza ruhusa, na jua bado linazunguka ratiba yake bila msaada wa binadamu.
Hata ugunduzi mkubwa kama ndege au smartphone za mkopo, havibadilishi ukweli kwamba wateja wa watu credit tutaondoka duniani bila kujua siri kamili ya maisha.

Sisi ni kama mgeni tuliovamia tamasha bila tiketi. Tunafurahia muziki, tunacheza kidogo, tunabishana na wenzetu, lakini mwisho wa siku tunatolewa nje kwa lazima.
Dunia haikuwahi kutuomba tuje, na haitulili tubaki.

Kiuhalisia, binadamu hakuja duniani kwa faida yake. Yote tunayofanya ni michezo ya muda mfupi, tamthilia ya kujipa matumaini.
Mwisho wake unabaki pale pale: kuzaliwa na kufa.
Dunia inaendelea bila sisi, na sisi tunaondoka bila kubadilisha chochote cha msingi kwa nafsi zetu.

Usijipe stress, kumbuka kuna maisha hata bila hela za kausha damu na simu za watu credit
Imemchukua binadamu mabilioni ya miaka tangu kutokea kwenye uso wa Dunia na kuwa kama alivyo leo. Haikuwa bahati nzuri au mbaya. Hata kama matofali ya nyumba hayaoni kwanini yapo pale, mmiliki wa nyumba anaona umuhimu wa kila tofali na anajali sana.
 
Kuna watu wapo maabara wanapambana kutafuta dawa ya kuishi milele
 
Binadamu tunajiona viumbe waliobarikiwa kwa akili na maarifa. Tumegundua teknolojia, tumeandika vitabu, tumejenga miji mikubwa, na tumeunda tamaduni nyingi. Lakini tukichunguza kwa undani, yote haya hayajabadilisha ukweli wa msingi,,,, binadamu hakuja duniani kufaidika kwa namna ya kudumu.

Kwa sababu matukio makuu ya binadamu ni mawili tu .... ni kuzaliwa na kufa. mwisho wa yote bado ni uleule. Hakuna ugunduzi wa kisayansi, hakuna teknolojia ya kisasa, wala falsafa ya kina inayoweza kubadilisha ukweli huu wa kimsingi.
Binadamu tunaishi kwa muda mfupi, tukijidanganya kuwa tuna faida kubwa, lakini dunia yenyewe haijabadilika kwa ajili yetu.

Miti bado inakua bila kujali nani yupo, bahari bado inacheza mawimbi yake bila kuuliza ruhusa, na jua bado linazunguka ratiba yake bila msaada wa binadamu.
Hata ugunduzi mkubwa kama ndege au smartphone za mkopo, havibadilishi ukweli kwamba wateja wa watu credit tutaondoka duniani bila kujua siri kamili ya maisha.

Sisi ni kama mgeni tuliovamia tamasha bila tiketi. Tunafurahia muziki, tunacheza kidogo, tunabishana na wenzetu, lakini mwisho wa siku tunatolewa nje kwa lazima.
Dunia haikuwahi kutuomba tuje, na haitulili tubaki.

Kiuhalisia, binadamu hakuja duniani kwa faida yake. Yote tunayofanya ni michezo ya muda mfupi, tamthilia ya kujipa matumaini.
Mwisho wake unabaki pale pale: kuzaliwa na kufa.
Dunia inaendelea bila sisi, na sisi tunaondoka bila kubadilisha chochote cha msingi kwa nafsi zetu.

Usijipe stress, kumbuka kuna maisha hata bila hela za kausha damu na simu za watu credit
Mada nzuri sana.

Upekee wa binadamu ni mifumo, Mfano mifumo ya urithi wa Tech. Binadamu anayezaliwa leo hataanza mwanzo kuvumbua ndege, anaendeleza walipoishia wengine.

Ni kweli bado matukio muhimu ni kuzaliwa na kufa but hatujui kama itabaki hivi nyakati zote sababu wanaozaliwa hawaanzi mwanzo, wanaendeleza walipoishia wengine.

Leo binadamu ana Ai, baada ya miaka 1000 Atakuwa na nini? Hatujui atakuwa na nini. Labda ataweza kubadili ufahamu kutoka kwenye mwili huu kwenda digitali.

Au, inawezekana dunia ina mfumo wake wa kujisafisha anapotokea kiumbe mwenye akili kuweza kubend forces of nature sababu kwanini bado tupo hapa Kwenye kuzaliwa na kufa?

All in all, linapokuja suala la mifumo na future, sisi ni wa kipekee.
 
Maisha hayana maana kwa maana ipi unajaribu kufikiri kwa mtazamo upi
Si kwamba unajaribu kifikiri nje ya uwezo asilia wa binadamu kiasi ukose maana
 
Maisha yana maana na pia hayana maana wakati mwengine.
Don’t stress, And take it easy.
 
Back
Top Bottom