Lighton
JF-Expert Member
- Aug 5, 2019
- 2,020
- 3,372
Hatujawekewa nafasi ya kupokea chuki, tumepewa nafasi ya kuchagua kati ya upendo na chuki. Ninaamini katika kitabu cha mwanzo, MUNGU alipomuumba mwanadamu na kumuweka katika bustani ya amani.Kwanini hatukuumbwa na upendo tu maana ndiyo unasisitizwa hata kwenye vitabu vyake...
Kulikuwa na haja gani tukawekewa nafasi ya kupokea chuki, hila na fitina wakati vitu vyote hivyo havimpendezi Mungu
Ni baada ya binadamu kujua kwamba Kuna mabaya na mema tayari alikuwa uchi, mema na mabaya yalipokuwa mbele zake, alifanya yale yaliyompendeza. Baya hupandwa moyoni kwasababu ya madhaifu na kwasababu ya asili zetu.
Wapo ambao walizaliwa Ili waende motoni. Utajiuliza kwanini MUNGU aliruhusu zipotee, Ni kwasababu hizo Roho MUNGU alijua haziwezi kubadilika kwasababu ya asili zao usaliti. Mfano mzuri ni shetani, ni kiumbe aliyeumbwa katika Hali ya kipekee lakini mwishowe alikuwa msaliti.
Unaweza kujiuliza MUNGU hakujuwa kwamba shetani atakuja kuwa msaliti? Na Kama alijua kwanini alimuumba? Kwanini MUNGU alifanya hayo yote? MUNGU pekee ndiye anayejua.
Binadamu alichagua kuishi Kwa uhuru, Binadamu aliamua kubadilika kwasababu ya tamaa zake. MUNGU habadiliki na Wala Sheria yake habadiliki.
Umepewa uhuru utachagua uutumieje!