Je binadamu ulizaliwa hapa duniani ili utafute pesa?

Je binadamu ulizaliwa hapa duniani ili utafute pesa?

mr pipa

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2021
Posts
4,287
Reaction score
9,162
Vijana wajinga wajinga utawakuta wanasema "tafuta hela"
Hivi huu mfumo ni nani aliuanzisha na madhumuni yake ni nini?

Ni kweli kwa akili zako timamu umezaliwa ili uje utafute hela ujenge sijui ununue kagar then uzeeke ufee

Asubuh kazini wiki miez miaka umezeeka

Na wewe unapita mbele ya watoto zako na kusema nimepambana kuwajengea maisha mazuri, na watoto wanangoja ufe siku ya pili mali zinauzwa, kuna maana gani sasa?
Eti maendeleo! Unafanya maendeleo gani kama si upungufu wa akili, wewe na kichaa nani mwenye kichaa

Kengine utakakuta kanajitutumua kanakopa na kukopa kananunua gari, na kamapita mitaani kanaona kametoboa kimaisha kanaona wenzake wapumbavu

Kabisa gari ni kakitu ka kujivunia binadamu
asee huyo aliebuni huu mfumo kawaweza sana

Wewe binadam hivi ushawahi kukaa kuusumbua ubongo wako japo kwa dakika moja
Kujiuliza kwanini?na kwa faida ipi?

Kama hujanielewa pole sana

NB: binadam msio na kitu msipanic hakuna cha maana huko ni upumbavu mtupu maisha ni haya haya relax
 
Lengo la kuzaliwa ni ili uje pia uzaliane. Sasa njia unazotumia ili uishi zinakufanya uangukie katika matumizi ya hela.
 
Tatizo mfumo sahihi wa maisha umemezwa na mfumo wa kundi la wahuni wakiongozwa na shetani, hapo ndiyo wengi tumekwama.

Mfumo umebaki wa zaliwa, nenda shule, oa/olewa, jenga nyumba, nunua gari, kibiashara/ajira then zeeka au ugua mwisho kufa. Kisha waliobaki wapite humo humo.
 
Back
Top Bottom