Ni nini sababu ya binadamu kuletwa Duniani?

Ni nini sababu ya binadamu kuletwa Duniani?

Hivi tunaposema katuumba kwa mfano wake inamaanisha sifa hizi tulizonazo binadamu yeye si anazo kama ukatiri, jeuri, chuki, dharau, wema, furaha n.k?
Aliyeweka mema na mabaya ni yeye mwenyewe Muumbaji ili ladha halisi ya maisha isomeke.

Wema unaonekana zaidi kwenye ubaya. Kama mwanga kwenye giza
Maana utajuaje Upendo kama hamna chuki?
Kwa maana hiyo sasa mabaya yapo ili yadhihirishe mema lasivyo maisha yasingekuwa na ladha.

Mungu alituumba na uwezo wa kubalance mema katikati ya mabaya na hayo ndio maisha. Unapo amua kuchagua mabaya, shida ni wewe sasa wala sio uumbaji.
 
Ukisoma kitabu cha Mwanzo kwenye Biblia utagundua kuwa alitupenda sana,na akatupa vitu vyote vizuri bali dhambi zetu ndio zilisababisha leo tunapitia tabu na haya mateso,lkn bado anatuwazia mema,something good is yet to come,keep on living the promises of God hautajutia kamwe...
Kama alitupenda kwanini alituwekea dhambi, mateso na shida?
 
Kama alitupenda kwanini alituwekea dhambi, mateso na shida?
Najua unataka majibu mepesi kwa mtindo wa kudandia,soma Biblia vizuri na uielewe,utapata majibu ya mswali yako yote...
 
Hakuna, ila bado najiuliza wanawake wanafaidi nini zaidi ya pombe huko peponi
Kwani si nimesikia mtakuwa na mabwana huko wa kuwakula? Vipi hamtafaidi
 
Najua unataka majibu mepesi kwa mtindo wa kudandia,soma Biblia vizuri na uielewe,utapata majibu ya mswali yako yote...
Hayo majibu mepesi yanaweza yakawa ni njia ya kunipa maana kubwa sana na kuuza kbsa hoja yangu
 
Ndo sisi tutabadilika na kuwa mabikra?
Niliwahi kusikia hivyo kwasababu mwili uliochezewa si umeshaharibika kule unakuwa na mwili mwingine mpya 😂😂
 
Niliwahi kusikia hivyo kwasababu mwili uliochezewa si umeshaharibika kule unakuwa na mwili mwingine mpya 😂😂
Mi nikifika huko sitaki kuliwa, ningependa nipumzike kwa kunywa pombe tu
 
Mi nikifika huko sitaki kuliwa, ningependa nipumzike kwa kunywa pombe tu
😅😅😅 inawezekanaje usiwe ili bwana wako apate wapi raha
 
Ule 🔥 moto aliumbiwa ibilisi/shetani na malaika zake waovu ila mwanadamu ataenda motoni kwasababu anafanya mambo yale yale aliyoyafanya shetani na malaika zake ambayo yalikuwa chukizo kwa Mungu.
 
Maisha ni fumbo.
Maisha ya duniani yalikuwa ni zawadi na sio adhabu, changamoto ni binadamu kutaka kuishi against nature, hapo ndipo mateso yanapo anzia.

Swali: Unauhakika gani kwamba upo duniani?
Umeshawahi kuota ndoto na ukajiona upo huko ndotoni? What if na hapa upo ndotoni na pengine ukifa hapa ndo unaamka kutoka usingizi uliokuwapo?
Hii ndo maana halisi ya Great thinker, lazima kichwa kifanye kazi!
 
Kuna wengine hapa hatukua na umuhimu wa kuzaliwa sema ni vile tu Mungu aliamua tuje kuwa wafariji watu anaowapenda hata kama sisi wenyewe hatuna furaha.
Unaambiwa ukijiua ni dhambi ila maisha yote tunaishi ukiteseka na huku unaona wengine wakiyafurahia maisha.
Not fare kabisa . Kulikua hakuna umuhimu wa sisi wote kuwepo hapa tulipo
 
Back
Top Bottom