Ndugu yangu kakamatwa kwa simu ya wizi, Nawasihi sana tuchukue tahadhari tunaponunua simu 'used'

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Tamaa ni moja ya sifa kuu inayowatafuna vijana wengi sana hasa wenye kupenda vitu vyenye gharama kuzidi uwezo wao.

Sikuhizi kwenye makundi mengi ya vijana ili uonekane kijana wa kisasa inaaminika inabidi uwe na simu nzuri zenye brand kubwa kama iphone, Samsung, Google pixel, Nokia, n.k.

Kijana wetu kadakwa kwa kununua simu ya wizi na sasa yupo Polisi.

simu aliinunua mwezi wa pili kwa bei mteremko laki 4 , dukani ilikuwa laki 9,

Kwa bahati nzuri mwenye simu hataki mambo yafike mbali, yeye anachotaka ni pesa tu kesi inaisha.

Shilingi milioni 1 ndio inahitajika kumnasua huyu ndugu na hapo tunashukuru mwenye simu anahisi aliibiwa kwa kuisahau simu mahala, Ingekua vinginevyo kwamba aliibiwa na vitu vingine, kujeruhiwa au hata angeamua tu kudanganya ili kumtia adabu huyu ndugu yangu basi si ajabu angehitaji pesa nyingi ama ndugu kwenda jela miaka 20.

Siku hizi kuna ofisi zimejazana kibao za wanasheria / attorneys, ni hawa ndio tunaowatumia kutuandalia mikataba ya kisheria tunapouziana magari, mashamba, nyumba, n.k. hivyo kama unataka kununua simu iliyotumika hata kama ni ya mjomba wako hakikisha mnauziana kwa mkataba.

Wanasheria watawaandalia mkataba wa mauziano wenye taarifa za simu muhimu kama Imei, taarifa za muuzaji na mnunuzi, malipo, n.k. baada ya hapo kila moja atasaini na kupewa nakala ya mkataba, lolote likitokea jua kwamba sheria inakulinda kupitia mkataba.


ni heri umpe attorney elf 30 kwajili ya mkataba kuliko kukamatwa uchi huna nyaraka yoyote ya kuthibitisha unamiliki simu kihalali, utaingia gharama kubwa sana ama kwenda kuozea jela.


Mchango wa wadau, rafiki yake kafungwa miaka 30 kuuziwa simu iliyoporwa na kumuua mmliliki

Rafiki yangu mmoja yupo jela baada ya kuhukumiwa miaka 30 tokea 2020. Alinunua simu ambayo baada tu ya kuanza kuitumia ilikuja kufahamika iliporwa pamoja na vitu vingine na wakati wa uporaji mwenye mali alipigwa na kufariki wiki moja baadae.
Bahati mbaya sana hakumfahamu vyema aliyemuuzia maana alidakishwa tu kijiweni na mtu asiyemjua na yeye akapachika line yake. Hivyo alituhumiwa kwa mauaji ya kukusudia na uporaji.
 
Tamaa ni moja ya sifa kuu inayowatafuna vijana wengi sana hasa wenye kupenda vitu vyenye gharama kuzidi uwezo wao.

Sikuhizi kwenye makundi mengi ya vijana ili uonekane kijana wa kisasa inaaminika inabidi uwe na simu nzuri zenye brand kubwa kama iphone, Samsung, Google pixel, Nokia, n.k.

.
Kila simu, hata unayonunua dukani inaweza kufanywa iwe ya wizi.
Kwa sababu huyo anayosema ni simu yake, ametumia kigezo gani?
 
Pole sana kwake, nina rafiki alitoa hela nyingi kununua Samsung akashangaa baada ya miezi miwili anapigiwa simu na Askari wa Oysterbay kuwa simu ni ya wizi

Alichukulia masihara labda matapeli mpaka siku alivyoona kero ya kupigiwa imezidi na kuamua kwenda Polisi, akakuta kweli na simu kwa mujibu wao, ni ya mdogo wa kiongozi mkubwa sana nchini

Ilibidi aitoe bila masharti ya ziada maana walimtaiti kwa maelezo tu akaona hana pa kutokea na aliinunua kwa raia aliyeipost kwenye mtandao

Tuweni makini sana na simu hasa hizi Samsung either nunua dukani ama hakikisha anakupa risiti halali, vinginevyo nunua kwa unaemuamini
 
Tamaa ni moja ya sifa kuu inayowatafuna vijana wengi sana hasa wenye kupenda vitu vyenye gharama kuzidi uwezo wao.

Sikuhizi kwenye makundi mengi ya vijana ili uonekane kijana wa kisasa inaaminika inabidi uwe na simu nzuri zenye brand kubwa kama iphone, Samsung, Google pixel, Nokia, n.k.

Kijana wetu kadakwa kwa kununua simu ya wizi na sasa yupo Polisi.

simu aliinunua mwezi wa pili kwa bei mteremko laki 4 , dukani ilikuwa laki 9,

Kufupisha story ni kwamba kiasi cha shilingi milioni 1 kinahitajika ili atoke, na hapo tunashukuru mwenye simu anahisi aliibiwa kwa kuisahau simu mahala, ila ingekua vinginevyo kwamba aliibiwa na vitu vingine au hata angesingizia kuwa aliibiwa na vitu vingine ili kumtia adabu huyu ndugu yangu basi si ajabu dau lingefika mpaka milioni 5+.

Bila hivyo anahamishiwa mahabusu anakoweza kukaa hata miaka mitano bila kusomewa kesi na hata akisomewa mashtaka kesi ya wizi ni mvua ya kutosha.

Nawaasa sana ndugu zangu humu hasa vijana ama wenye vijana, Simu mnaponunua hakikisha unanunua dukani, ikitokea unanua simu mtaani nenda kwa wanasheria waliojaa tele mjini kwenye ofisi zao za attorneys, ukifika hapo watakuandalia mkataba wa mauziano huku wao wakiwa mashahidi, watachukua kila taarifa ya simu na kuambatanisha utambulisho wenu wa namba za simu na vitambulisho vyenu, kila moja wenu atasaini na kupewa nakala ya mkataba. Binafsi niliwahi kununua simu ya laki 2 hapo zamani na niliandaliwa mkataba kwa shilingi elf 20.
Acha uoga. kwani mtu akienda polisi ndo nini
 
utajuaje kua ni ya wizi?
aiseeeee somo la hekima liwepo mitaani
Hakikisha unaponunua simu mtaani muuziane kwa mkataba ulioandaliwa na wanasheria.

Bila hivyo jiandae kwa lolote, simu waweza nunua leo ila ukakamatwa 2025
 
Kama hujawahi kuibiwa simu huwezi kujua uzito wa hili suala.
Mimi yeyote anayenunua simu ya wizi either kwa kujua au kutokujua lolote limkute tu.
hawa vijana wengi wadogo vitu vingi wanafanya bila kuwa na experience ya maisha kama sisi watu wazima.

Kesho anaweza kuwa mtoto wako kanunua bila kujua ni ya wizi akikutana na mtu mwenye mawazo kama yako ataozea jela.

careful what you wish for !!
 
Pole sana kwake, nina rafiki alitoa hela nyingi kununua Samsung akashangaa baada ya miezi miwili anapigiwa simu na Askari wa Oysterbay kuwa simu ni ya wizi

Alichukulia masihara labda matapeli mpaka siku alivyoona kero ya kupigiwa imezidi na kuamua kwenda Polisi, akakuta kweli na simu kwa mujibu wao, ni ya mdogo wa kiongozi mkubwa sana nchini

Ilibidi aitoe bila masharti ya ziada maana walimtaiti kwa maelezo tu akaona hana pa kutokea na aliinunua kwa raia aliyeipost kwenye mtandao

Tuweni makini sana na simu hasa hizi Samsung either nunua dukani ama hakikisha anakupa risiti halali, vinginevyo nunua kwa unaemuamini
Mambo ya kununua kwa unaemwamini kwa kauli mali pekee haitoshi kwa ulomwengu wa sasa, kesho mwaweza kupishana kauli akakuchoma ama nae aliinunua ya wizi likakukuta wewe.

Kama ilivyo kwa gari, kwenye simu pia hakikisha hata ukinunua kwa rafiki yako kuwe na mkataba ulioandaliwa na attorneys waliojaa kama utitiri mjini, ni heri umpe attorney elf 50 kwajili ya mkataba kuliko kukamatwa na huna nyaraka yoyotr ya usbahidi.
 
Tamaa ni moja ya sifa kuu inayowatafuna vijana wengi sana hasa wenye kupenda vitu vyenye gharama kuzidi uwezo wao.

Sikuhizi kwenye makundi mengi ya vijana ili uonekane kijana wa kisasa inaaminika inabidi uwe na simu nzuri zenye brand kubwa kama iphone, Samsung, Google pixel, Nokia, n.k.

Kijana wetu kadakwa kwa kununua simu ya wizi na sasa yupo Polisi.

simu aliinunua mwezi wa pili kwa bei mteremko laki 4 , dukani ilikuwa laki 9,

Kufupisha story ni kwamba kiasi cha shilingi milioni 1 kinahitajika ili atoke, na hapo tunashukuru mwenye simu anahisi aliibiwa kwa kuisahau simu mahala, ila ingekua vinginevyo kwamba aliibiwa na vitu vingine au hata angesingizia kuwa aliibiwa na vitu vingine ili kumtia adabu huyu ndugu yangu basi si ajabu dau lingefika mpaka milioni 5+.

Bila hivyo anahamishiwa mahabusu anakoweza kukaa hata miaka mitano bila kusomewa kesi na hata akisomewa mashtaka kesi ya wizi ni mvua ya kutosha.

Nawaasa sana ndugu zangu humu hasa vijana ama wenye vijana, Simu mnaponunua hakikisha unanunua dukani, ikitokea unanua simu mtaani nenda kwa wanasheria waliojaa tele mjini kwenye ofisi zao za attorneys, ukifika hapo watakuandalia mkataba wa mauziano huku wao wakiwa mashahidi, watachukua kila taarifa ya simu na kuambatanisha utambulisho wenu wa namba za simu na vitambulisho vyenu, kila moja wenu atasaini na kupewa nakala ya mkataba. Binafsi niliwahi kununua simu ya laki 2 hapo zamani na niliandaliwa mkataba kwa shilingi elf 20.
Rafiki yangu mmoja yupo jela baada ya kuhukumiwa miaka 30 tokea 2020. Alinunua simu ambayo baada tu ya kuanza kuitumia ilikuja kufahamika iliporwa pamoja na vitu vingine na wakati wa uporaji mwenye mali alipigwa na kufariki wiki moja baadae.
Bahati mbaya sana hakumfahamu vyema aliyemuuzia maana alidakishwa tu kijiweni na mtu asiyemjua na yeye akapachika line yake. Hivyo alituhumiwa kwa mauaji ya kukusudia na uporaji.

Katika hili tuwe waangalifu sana.
 
Wewe unanunuaje simu mkononi pasipo na uthibitisho anayekuuzia ndiye mmiliki halali?
Simu yoyote iliyonunuliwa kihalali ina vithibitisho vikiwemo risiti halali na mkataba wa mauziano.

Kama hivyo hakuna basi endelea kununua simu kiholela ukisubiri somo la hekima.
Mimi sinunui simu used nanunua brand new ila pia baada ya muda hata ukiniuliza risiti iko wapi siwez kukwambia maana napoteza. So, watu wengi wakifika muda wa kuuza simu huwa risiti unakuta hana tena ishapotea. Sema mimi simu huwa siuzi natumia nikiichoka nagawa kwa ndugu au inakuwa imeharibika natupa kule.
 
Eti mwenye simu ana roho nzuri 😭😭😭😭
Hiyo ni michezo ya polisi wahuni .
Wanauza simu then wanakuja wanakukamata kwa mlango wa pili. Simu unanyang'anywa anakwenda kuuziwa mjinga mwingine na pesa unatoa
Aise sijawahi kuwaza hiko kitu ingawa kununua simu mkononi ni risk kubwa unaweza kukuta unauziwa simu ya mtu aliuliwa ukapata msala wa murder case
 
Back
Top Bottom