Taadhari Kuna Wizi wa pesa katika Baadhi ya benki zetu kupitia huduma za Kibenki kwa njia ya simu. Wateja wa benki tuchukue taadhari. Mamlaka Ziamke!

Mawimba

Senior Member
Apr 29, 2013
155
158
Habari zenu wanaJf, poleni na miangahiko yakusukuma gurudumu la maisha. Napenda nitangulize radhi kwenu kwa matatizo ya kiuandishi yatakayo jitokeza katika uandishi wangu.

Ndugu zangu kama nilivyo taadharisha hapo juu. kunawizi unaendelea Na Ndugu yangu kakutana na hii adha.

Tukio lenyewe lilivyokuwa...

siku ya tukio Jamaa yangu akiwa katika shughuri zake za kila siku majira ya saa 8 mchana akakutana na vijana wasajiri laini. Wakamueleza wanasajiri laini na wanabadilisha mfumo kutoka 3G kwenda 4G, kutokana na changamoto ya mtandao wa kijiji anachoishi akavutiwa na huduma ya Kuamishwa kwenye 3G Kwenda 4G.

Akawaomba wasaidie kwa hilo. Wakachukua simu yake wakatoa laini wakaiweka kwenye simu yao wakafanya yakufanya Wakamwambia tumemaliza teyari umeshahamishwa hivyo Hakikisha huduma zako za kifedha ambazo zipo kwenye hii laini. Akachukua simu Akaingia kwenye menyu ya tigo Pesa ilipofunguka Hakuangalia hata salio akakata kisha akaingia kwenye menyu ya benki akaingiza namba ya siri Ilipofunguka hakufanya chochote akakata akawaambia nimejiridhisha teyari (kipindi anafanya hizo shughuri alijitenga nao akawa peke yake) wakachukua hile simu yao wakatoa laini wakamkabidhi mwenye akairudisha kwenye simu yake, akaachana nao akaenda kuendelea na shughuri zake za kila siku.

saa 2 usiku akapata mesegi kutoka benki ikionesha ametuma pesa Milioni mbili na laki tano kwenda kwenye namba ya simu.

kipindi anatafakari mesegi zikaingia mesegi zingine zikiwa na miamala mingine, Akashtuka akapiga simu Tigo wakamwambia awapigie wabenki husika Akafanya hivyo lakini hakuwapata Ikabidi aende benki kuzuia huduma kwenye ATM.

Siku iliofatia akaenda Benki kufuatilia na kulalamika Akapatiwa barua aende polisi lakini nao wanafutilia kwenye kitengo cha Fraud.

lakini polisi waliomba taarifa ya IMEI namba ya kifaa kilichowezesha muamala Hile benki wakakataa kutoa.
Mteja akalalamika kwenye Benki wanampa maneno yakusubiri Hadi sasa miezi minne Dana dana tu zimekuwa.

hili tatizo ni wazi hizi baadhi ya benki zetu katika mifumo ya huduma za kibenk Mkononi Usalama wake ni mdogo.

au ni wafanyakazi wa hizi benki wanahusika kuwezesha huu uhuni.
 
Mbona ukibadilisha line ambayo unaitumia nmb mobile ni mpaka uende kwenye atm uka update taarifa zako hapo ilikuwaje wakubadilishie line hapo hapo ifanye kazi nmb mobile?

Kitendo cha kutoa au line yako kuwekwa kwenye simu ya mtu mwingine halafu ukabonyeza menyu za nmb mobile na tigopesa hapo ndio ulifanya makosa watakuwa walikuwa na app ya kukamata hizo password.

Siku nyingine mwambie ndugu yako huduma zinazohusu kubadili line au za kifedha aende kwa mawakala wanaotambulika na sio hawa wasajili line mtaani baadhi yao ni wezi.

Pole
 
Hata mawakala nao vimeo....kuna siku nimetoa pesa kwa wakala nikapata meseji kwa simu baada ya dakika chache ikaingia msg nyingine kuwa hela imetoka, nikamuuliza mbona hela imetoka mara mbili akajifanya eti network akairudisha....ningekua sipati meseji ndio ingekua imeenda hivyo
 
Benk wamekua majambazi kuna fwala alikula 400k yangu ya bure hivihivi pale NMB mbezi Beach nilitaman nimwendee kwa bibi nikampotezea. Ila namwandalia mtego atanasa siku.
 
Hata mawakala nao vimeo....kuna siku nimetoa pesa kwa wakala nikapata meseji kwa simu baada ya dakika chache ikaingia msg nyingine kuwa hela imetoka, nikamuuliza mbona hela imetoka mara mbili akajifanya eti network akairudisha....ningekua sipati meseji ndio ingekua imeenda hivyo

Wanatoa mara 2 ndomana mimi miamala yangu nafanyia kwa sim banking tu kwa wakala nampa code tu
 
Mbona ukibadilisha line ambayo unaitumia nmb mobile ni mpaka uende kwenye atm uka update taarifa zako hapo ilikuwaje wakubadilishie line hapo hapo ifanye kazi nmb mobile?

Kitendo cha kutoa au line yako kuwekwa kwenye simu ya mtu mwingine halafu ukabonyeza menyu za nmb mobile na tigopesa hapo ndio ulifanya makosa watakuwa walikuwa na app ya kukamata hizo password.

Siku nyingine mwambie ndugu yako huduma zinazohusu kubadili line au za kifedha aende kwa mawakala wanaotambulika na sio hawa wasajili line mtaani baadhi yao ni wezi.

Pole
sawa ndugu Ila hata kama walikopi password swali linakuja waliwezaje? maana Kifaa kilipoteza sifa ya kuingia kwenye mfumo kwa kuwa Hile App haikubali kufanya kazi kama laini usika haipo kwenye hicho kifaa

kama jibu waliudanganya mfumo (ku hack) basi mtoa huduma awajibike kwa uzembe.... halafu mtoa huduma kagoma kutoa taarifa za muhimu kwa jeshi la polisi kuna jambo kama linaendelea hivi juu ya wezi na watoa huduma
 
Hata mawakala nao vimeo....kuna siku nimetoa pesa kwa wakala nikapata meseji kwa simu baada ya dakika chache ikaingia msg nyingine kuwa hela imetoka, nikamuuliza mbona hela imetoka mara mbili akajifanya eti network akairudisha....ningekua sipati meseji ndio ingekua imeenda hivyo
Mie niliacha kabisa kutumia mawakala iliponikuta hiyo. Nilitoa laki 3 na nusu..akaita mara 2. Ndo nikashtuka msg zinakuja 2 eti akaja na maelezo ya kipumbavu ku8nyesha kuwa lile tatizo mie ndo nimelisababisha. So ikabidi anipe hela zote. Ila aisee sikuamini mpaka nikaomba tena bank statement kujilidhisha kwamba hajatoa tena zingine. Toka hapo mie na mawakala mbalimbali kabisa
 
Back
Top Bottom