Ndugai: Wabunge ishaurini Serikali, iendelee kununua ndege au isitishe

Sasa hao wanaotaka kuanza kujadili; wanao huo uelewa wa jinsi gani mashirika ya ndege yanaendeshwa? Kuendesha shirika la ndege sio sawa sawa na biashara ya kuuza nyanya, ambayo unanunua "stock ya nyanya" asubuhi, baada ya siku mbili au tatu unaweza kupiga hesabu umepata faida kiasi gani.

Ndege ni tofauti; unanunua ndege leo - inabidi uanzishe route mpya; uwe na mikakati ya bei, masoko ili kuweza kupata abiria. Na tatizo hao abiria ni lazima wakuamini pia kama hilo shilika liko reliable; kabla hawajaanza kulitumia. Hiyo yote inachukua muda. Ndio maana mashirika ya ndege huwa yanakuwa na muda waliojiwekea "PLANNED LOSSES". Kipindi ambacho wanategemea watakuwa wanapata hasara kuelekea kwenye faida.

Hivyo kutegemea ATCL iwe imepata faida ndani ya miaka 3 au 4 ya kujiendesha, hiyo sio sawa. Muhimu ni kuangalia hiyo hasara wanayoipata; inapungua??? Inaleta matumaini kuelekea kwenye faida kwenye miaka ijayo??? Na hiyo pia iangaliwe kwa pamoja na contribution yake kwenye maeneo mengine ya uchumi; ikiwemo utalii.

Kuhusu kubinafsihwa kwa TRC - hapo watuambie tu kama kuna janja janja za kuanza kutaka kujiuzia hilo shirika jipya na SGR yake. TRC ilishabinafsishwa wakati fulani; kwa wale wahindi; sijui walikuwa wanaitwa RITES???? Nini kilitokea???? Nina hakika Spika wa sasa nae alishakuwa Mbunge wakati ule?? TRC si ilikwisha kabisa mpaka serikali ikaamua kulichukua tena kwa asilimia 100??? Mbona hao RITES hawakujenga SGR??????

Mwekezaji Binafsi yeyote anakuja kwa kuangalia kwa upana maslahi yake binafsi. Hiyo ni hatari kwa hii miundombinu mikubwa ambayo inategemewa kuwa ndio "lifeline" ya Uchumi wetu. Ndio maana nchi zilizoendelea; miundo mbinu mikubwa ambayo ndio inachochea kukua kwa uchumi; inamilikiwa na serikali mpaka sasa. Na hiyo ikiwemo Bandari; Reli na Mashirika ya Ndege.
Mbona USA watengeneza ndege hawamiliki ndege kama tumeshindwa biashara ya korosho, madini na utalii huko kunakohitaji utaalamu sio siasa hatuwezi kufanikisha msijidanganye ..
 
Mbona USA watengeneza ndege hawamiliki ndege kama tumeshindwa biashara ya korosho, madini na utalii huko kunakohitaji utaalamu sio siasa hatuwezi kufanikisha msijidanganye ..
mkuu ni kweli ulichosema kwamba US haimiliki ndege ? mbona kuna mashirika kadhaa ya ndege huko je unataka kusema zote ni za private sector ? naomba ufafanuzi wako
 
Hivyo kutegemea ATCL iwe imepata faida ndani ya miaka 3 au 4 ya kujiendesha, hiyo sio sawa. Muhimu ni kuangalia hiyo hasara wanayoipata; inapungua??? Inaleta matumaini kuelekea kwenye faida kwenye miaka ijayo??? Na hiyo pia iangaliwe kwa pamoja na contribution yake kwenye maeneo mengine ya uchumi; ikiwemo utalii.
Mkuu mbona Msemaji mkuu wa serikali ya Awamu ya Tano, Alisema tumepata faida ya takriban 28 bilion.....

Na hao hao ATCL walitoa gawio kwa serikali...ina maana yote hayo yalikuwa changa la macho
 
Alafu kinachonichanganya...

Bunge la Kikwete si lililaumu sana kwa Shirika kubwa la ndege kama la kwetu halina ndege?

Kwa hiyo leo hii tunazipinga tena?

Kenya walipata hasara ya 800b..ila bado wanachapa kazi
hii nayo ni hoja kwa kiasi fulani, wasiponunua sasa hivi hawatonunua tena, alafu ndege haziozi pia
 
Mkuu mbona Msemaji mkuu wa serikali ya Awamu ya Tano, Alisema tumepata faida ya takriban 28 bilion.....

Na hao hao ATCL walitoa gawio kwa serikali...ina maana yote hayo yalikuwa changa la macho
huwenda hilo gawio ndio part of loss😂 yani unapata faida 5000, unaipa serikali 3000 alafu unabaki na buku mbili kwa ajili ya ku oparate biashara ambapo haitoshi inabidi ukope tena
 
Mwendazake angekusikia unampinga ungeshughulikiwa na vyombo vyote vya ulinzi na usalama.
 
hilo ndilo kosa kubwa sana alilofanya na mbaya zaidi walimuuza akiwa bado hajafa kwa kutoa taarifa zake za ndani huko
iseee...

taarifa isitoshe wakaamua kumpost akiwa amerest kabisa kwenye jeneza.

Balaa kabisa...tuwe makini na waliotuzunguka.

Nilichogundua ukiyagusa maslahi ya mtu atakufanya kitu hamna!
 
Nami naomba nichangie kidogo kuhusu ununuzi wa ndege ingawa mimi sio mbunge lakini kama raia wa Tanzania.
1. Ndege moja ya rais
2. Ndege moja ya viongozi wa juu (makamu wa rais na waziri mkuu e.t.c)
3. Ndege mbili ndogo za abiria 70, kwa ajili ya safari za ndani.
5. Ndege ya tano kubwa kwa ajili ya route muhimu kama kwenda China/India washirika wa kibiashara.
Hizo nyingine ziuzwe fedha tupeleke kwenye miradi ya maendeleo.
Kama taifa bado hatuwezi kubeba hasara ya ndege 11 kwa sasa.
"KAZI IENDELEE"
 
Nami naomba nichangie kidogo kuhusu ununuzi wa ndege ingawa mimi sio mbunge lakini kama raia wa Tanzania.
1. Ndege moja ya rais
2. Ndege moja ya viongozi wa juu (makamu wa rais na waziri mkuu e.t.c)
3. Ndege mbili ndogo za abiria 70, kwa ajili ya safari za ndani.
5. Ndege ya tano kubwa kwa ajili ya route muhimu kama kwenda China/India washirika wa kibiashara.
Hizo nyingine ziuzwe fedha tupeleke kwenye miradi ya maendeleo.
Kama taifa bado hatuwezi kubeba hasara ya ndege 11 kwa sasa.
"KAZI IENDELEE"
Na nje hakuna itakayokwenda, maana zitadakwa jukwaju..!!! Mahusiano na wengine ni muhimu
 
Wamuuzie , anatafta ya kutumia kuzurura ....!!!hata akiwa anawalipa mdogo mdogo sio mbaya ...
Litamfilisi trust me... Lile moja bado linataga pale airport mpaka leo halijatotoa kifaranga hata kimoja licha ya ripoti kuonesha lililishwa bilion 4 kasoro mia
 
ile picha ukiiangalia hata kama humpendi jamaa utamuonea huruma fulani utajikuta unaona anakosewa
Hakika Chief..

Binadamu kazi sana,aliyeipiga hiyo picha huyo huyo ndo Magu alikuwa anampa ugali.

tuchague marafiki + watu sahihi

Ikibidi ni kuwa kivyako tuu ngumu ngumu....saa zingine washkaji ni masnitch tuu

Nimeanza kuamini ule msemo wa (be yourself + private)
 
Back
Top Bottom