Natafuta mganga wa kienyeji konki
HUJAMBO KAKA NAOMBA MSAADA TAFADHALI NATESEKA UZI HUU UNA MDA MREFU SASA HAUKUANZA LEO JUZI WALA JANA YANI DAH USISEME HAKUNA UCHAWI SEMA HUJAROGWA KWAKWELI
Salama Kaka, habari za kwako?

Dunia ina mengi ambayo hatuyafahamu, ndiyo maana Wazee walipata kusema tembea uone
 
Poleni na majukumu ya kila siku, nimekuja na ID yangu hii sina haja ya kujificha.

Moja kwa moja kwenye mada, nahitaji msaada kama kuna mtu anamjua mganga wa uhakika anifanyie kazi yangu, kuna waganga huwa nasikia wanatoa watu mabusha, wanatuma majini au kumpa mtu ugonjwa nahitaji mganga wa hivyo.

Hii Dunia ina mengi, na ikifika kipindi cha vita unaambiwa usichague silaha, nahitaji jambo langu likamilike kwasababu kuna watu wanaweza kukukosea heshima mpaka wakapitiliza. Ukimya na subira ni muhimu lakini kuna watu huwa wanaona kama umezubaa.

Nikifanikiwa kazi yangu nitakupa ya shukrani sina hiyana. Watu wa mahubiri hapa sio sehemu yake.

Nawashukuruni naamini nitapata msaada wenu.
Karibu mbeya kama upo serious lakini
 
Back
Top Bottom